Abu Ubaidah Commando
JF-Expert Member
- Sep 8, 2016
- 7,591
- 6,946
..fikiria kwa mfano Waisraeli walivyoandika kuhusu Entebe Raid.
..Watanzania tunaweza kuandika kuhusu mapigano ya Lukaya. Bila kuwapiga vibaya Walibya pale Lukaya huenda historia yetu, na matokeo ya vita vya Uganda, ingekuwa tofauti.
..Pia kuna mapigano ya Sembabule ambayo yalikuwa ya muda mrefu, wiki tatu, na kuna wakati Jwtz walikuwa wameelemewa, but somehow they pulled through.
..hiyo ni kwa upande wa vita vya Uganda. Sasa kuna vita vya Msumbiji, operation za Comoro I & II, na operation ya Seychelles.
Sio hizi za wababaishaji wa leo wanatuchanganya tu🤣🤣🤣🤣Hizi ndio historia watoto wetu wanapaswa kuzijua, na ikiwezekana zichapishwe kwenye vitabu vya shule itapendeza, acha zile historia za kutengenezwa na western na mipicha yao ya kuchora eti mtu amefungwa minyororo na waarabu kisha anateswa. Akili zingine bwana, unabakia kucheka tu 🤣🤣🤣🤣
Hapa akili naona zimeanza kujirudi. Mzungu sio mtu ila wachache tu wenye kujitambua.
Kwenye mahojiano na Raia Mwema, Kiwelu anaweka wazi, alifanya survey ya kuvuka, akaongoza kuvuka na hata kutoa operation order. Baada ya hapo aliripoti kwa amir Jeshi mkuu kwamba kazi ya kwanza imekwisha...tunapotofautina mimi na wewe ni kuhusu kubadilishana majukumu kati ya Tumainieli Kiwelu na David Musuguri.
Kwenye mahojiano na Raia Mwema, Kiwelu anaweka wazi, alifanya survey ya kuvuka, akaongoza kuvuka na hata kutoa operation order. Baada ya hapo aliripoti kwa amir Jeshi mkuu kwamba kazi ya kwanza imekwisha.
Halafu anasema, akamkabidhi Musuguri kuendesha kazi ya kuingia Uganda yeye akirudi makao makuu kwa ajili ya kutafuta nguvu ikiwemo vifaa kutoka kwa nchi marafiki, kazitaja.
Hadi hapo Kiwelu anatueleza vita ilikuwa na hatua mbili. Demarcation inaweza isionekane kirahisi kwani pande zote mbili zilikuwa vitani tena mpakani. Hata hivyo, mipango ya vita kwa mujibu wa Kiwelu inaeleza wazi uwepo wa awamu mbili, kukomboa mipaka na kuingia Uganda.
Katika vitabu vya vita ya Kagera na kama ukimsikiliza Kiwelu, kazi kubwa ilikuwa kuvuka daraja.
Ukubwa wa kazi ile unatokana na aliyosema Kiwelu, kwamba, kuna askari ambao hawakuwahi kupigana vita.
Kwahiyo ile ilikuwa 'firsthand experience'
Pili, hakukuwepo matarajio ya kuvunjwa kwa daraja
Tatu, hawakuelewa ukubwa na kujizatiti kwa jeshi la adui
Nne, kipigo cha kwanza walichopata kiliondoa morali
Ukimsoma Kiwelu katika mahojiano na Raia mwema, kuna sehemu anasema '' nikarudi makao makuu Dar es salaam kuendelea na CoS''. Kwa mantiki alikuwa 'siyo' na Mwakalindile alikuwa Acting.
Hata hivyo, kuna mkanganyiko kidogo. Kwamba, alikataa kumpa habari Sokoine inaonyesha ni katika capacity ya CoS akijua aliye juu yake ni CDF. Pili, alidhibiti habari na kueleza kuwa ikibidi habari ziende atapeleka mwenye Ikulu inaeleza ukuu wake na hasa CoS. Lakini pia yeye ndiye aliyetangaza 'operation order'' usiku ule. Kwa maana hiyo ni CoS, CDF na Amir Jeshi mkuu waliojua mpango.
Kwa mtazamo wangu hapa palihitajika maelezo mengine na ndiyo maana tunashauri kuwatumia washiriki kama Meja jenerali Msuya ambaye ni mmoja wa watu walio hai na walioshiriki kwa ukaribu sana.
Unapokataa kuongea na waziri wa ulinzi na waziri mkuu, unawezaje kuendelea kukaa mstari wa mbele? I think alirudishwa kwenye madawati ili asifanye mambo ya kiutawala kuwa magumu
yote ni kwa sababu ya kutojua tafsiri sahihi ya uongozi wa kijeshi. Wakati. wa vita Ile ya siku sita Kati ya Israel na nchi za kiarabu jukumu la kuandaa jeshi LA Israel lilikuwa mikononi mwa Yizhak Rabin Chini ya Moshe dayan, lakini makamanda waliopigana ni akina ariel shalon na wengineo. hata wakati wa Israel kukomboa raia wake kutoka Entebbe, jukumu lilikuwa chini ya
brigadier general dan shomron lakini operation yenyewe iiendeshswa na na lt col. Netanyahu.
unatafsiri vibaya hayo unayosoma
Hawakupigania dini , walipigania heshima na utu wa mwafrika.Wewe weka hata na donkey wacha mapunda, mradi kuna "Ahmed' huyo hafai kabisa, atakuwa ni "mfia dini" tu huyo.
Hata Mkwawa alikuwa ni Abdallah, ndiyo wale wale.
Brig Gen Kabunda yupo, ni mstaafu.Brigadier General Lupembe ameshatangulia mbele ya haki. Brigadia Gen. Kabunda niliwahi kusikia kwenye banda la sabasaba la jeshi, wamba ndio waliovuka mto kwenda upande wa pili ili daraja liweze kujenga. Naamini inawezekana alikuwa ni special force operator.
All in all, hizi zisiwe hadithi za kusimuliwa tena. Ziandikwe ili watu wengi wazisome na kuelewa. Uzalendo unajengwa. Most of them would be the future role models
Ngwilizi amewahi kuwa de facto RAIS wa Seychelles.Seychelles, Meja Jenerali Ngwilizi ndio aliongoza mapambano? Na msumbiji he?
Usiponielewa utaona kuwa ni mbishi; ukweli ni kuwa jukumu la kusimamia vita ile lilipewa CoS wa wakati huo, lakini yeye kusimamia vita haina maana kuwa ndiye aliyeingia vitani na wapiganaji. Makamanda wote walioingia vitani na vikosi vyao wanajulikana. Lakini makamanda hao wasingechukua vikosi na kuvipeleka vitani bila ridhaa ya uongozi wa juu wa jeshi ambao ulikuwa unatoka kwa CoS wakati huo, siyo kwa CDF. Hiyo ni tofauti na wanaoamini kuwa kwa vile CoS ndiye aliyekuwa amepewa jukumu la kusimamia vita ile basi yeye ndiye aliyepigana; hicho ndicho ninatofautiana nyie wote. Kwa level ya juu ni sawa kuwa ndiye aliyengoza vikosi vyote vya vita, lakini kwenye microlevel siyo sawa kabisa kwani yeye hakuingia kwenye thiata kabisa-ambayo ndiyo mimi naongelea; ukishahema kuwa yeye ndiye aliyepigana, basi unaweza kusema pia kuwa Nyerere ndiye aliyepigana kwa vile ndiye aliyekuwa amiri jeshi mkuu na ndiye aliyetangaza vita ile, jambo ambalo wapiganaji hawatakubaliana nawe.We jamaa nnimekusoma kwenye nyuzi 2 tofauti kuhusu vita y kagera, nimegundua Ni mbishi tu na unalazimisha watu waelewe kile unachoamini. Sometimes unaharibu radha ya uzi kwa ubishi wako wa kimaandazi
Ngwilizi amewahi kuwa de facto RAIS wa Seychelles.
Usiponielewa utaona kuwa ni mbishi; ukweli ni kuwa jukumu la kusimamia vita ile lilipewa CoS wa wakati huo, lakini yeye kusimamia vita haina maana kuwa ndiye aliyeingia vitani na wapiganaji. Makamanda wote walioingia vitani na vikosi vyao wanajulikana. Lakini makamanda hao wasingechukua vikosi na kuvipeleka vitani bila ridhaa ya uongozi wa juu wa jeshi ambao ulikuwa unatoka kwa CoS wakati huo, siyo kwa CDF. Hiyo ni tofauti na wanaoamini kuwa kwa vile CoS ndiye aliyekuwa amepewa jukumu la kusimamia vita ile basi yeye ndiye aliyepigana; hicho ndicho ninatofautiana nyie wote. Kwa level ya juu ni sawa kuwa ndiye aliyengoza vikosi vyote vya vita, lakini kwenye microlevel siyo sawa kabisa kwani yeye hakuingia kwenye thiata kabisa-ambayo ndiyo mimi naongelea; ukishahema kuwa yeye ndiye aliyepigana, basi unaweza kusema pia kuwa Nyerere ndiye aliyepigana kwa vile ndiye aliyekuwa amiri jeshi mkuu na ndiye aliyetangaza vita ile, jambo ambalo wapiganaji hawatakubaliana nawe.
Jibu simple ni kuwa kuna makamanda wanaopanga mezani na kuna makamanda wanaotekeleza mipango iliyopangwa mezani kwa vitendo.Hizo reference unazoleta zote nadhani ziko sahihi kwa sababu zile ambazo nimesoma sijaona makosa yoyote, tatizo ni jinsi mnavyozitafsiri. Tafsiri zenu ni kinyume na ujumbe uliomo kwenye references hizo. Unaposoma kuwa jukumu la kuongoza vita lilikuwa mikononi mwa Kiwelu, haina maana ya kuwa yeye ndiye aliyekwenda akapanga vita na kuongoza vikosi kuingia msituni. Yeye ndiye aliyekuwa top commander wa kuratibu vita ile, lakini makamanda walioingia nsituni ni wengine na kamanda aliyepanga plani ya vita ni mwingine.
Comment yako imejaa kusema vita ilipangwa na kuongozwa na Kiwelu, lakini unasahau kuwa yeye alikuwa Chief of staftt na kamanda wa pili juu ya mabrigedia na majenerali wote. Ni kweli ilikuwa jukumu lake kuwasimamia hao makamanda waliokuwa chini yake, lakini siyo yeye aliyekwenda kwenye thieta. Nimetoa mifano mizuri inayojulikana kutoka isareli kuwa kamanda wa operation siyo siyo anayepigana kwenye operation hiyo.
Jibu simple ni kuwa kuna makamanda wanaopanga mezani na kuna makamanda wanaotekeleza mipango iliyopangwa mezani kwa vitendo.
Jibu simple ni kuwa kuna makamanda wanaopanga mezani na kuna makamanda wanaotekeleza mipango iliyopangwa mezani kwa vitendo.
Kipi ambacho hujaelewa kwenye post yangu!?Basi kwa jibu simple hilo ni kuwa kamanda aliyepanga vita yote mezani alikuwa kanali Kitete siyo Kiwelu; ukisoma mahojiano hayo anaeleza alivyokuwa akizunguka naye kuvinjari lile eneo la mto ambapo kanali kKitete ndiye aliyeweka mkakakati wa kuwazunguka askari wa Amini kutokea Magharibi. Wakati huo kanali Kitete ndiye aliyekuwa Chief Tactician wa Ngome kabla hajapandishwa cheo kuwa Brigedia na yeye pia kupewa brigedi ya kuongoza ndani ya uganda.
Huyo imrani Kombe, ndio huyu aliekua mkuu wa TIS, alieuwawa Moshi?Huyu ni mmoja kati ya makamanda walioongoza vita vya Kagera lakini siyo maarufu ktk vyombo vyetu vya habari, lakini ukisoma VITABU mbalimbali vinavyohusu VITA VYA KAGERA utagundua kwamba alikuwa na mchango mkubwa toka mwanzo mpaka mwisho wa vita, yaani toka Mutukula/Kagera mpaka Koboko kijiji alikozaliwa Iddi Amin Dada.
Baada ya majeshi ya Uganda kuvamia ardhi ya Tanzania na kuikalia, Tumainieli Kiwelu [ meja jenerali wakati huo] ambaye alikuwa Chief of Staff JWTZ alipewa jukumu la kuandaa majeshi yetu na kuongoza mapigano ya kukomboa ardhi yetu.
Ahmed Takadiri Kitete[ kanali wakati huo] ametambulishwa ktk kitabu cha " Vita vya Kagera -- 'kagera hadi arua' " kama mkuu wa mipango ya uamrishaji kivita ktk operesheni ya kuyaondoa majeshi ya Uganda ktk ardhi ya Tanzania.
Ahmed Kitete alipandishwa cheo na kuteuliwa kuongoza Brigade ya Minziro ambayo ilipigana maeneo ya Bushenyi, Kasese, Fort Portal, Hoima, Masindi, Karuma Falls, Pakwach, Bondo, Arua, Yumbe, na Moyo mpakani na Sudan [ sasa hivi South Sudan].
Brigade ya Minziro ndiyo iliyohitimisha vita vya Uganda na Brigadier.Kitete ndiye kamanda wa Tanzania aliyefika mpaka kijiji cha Koboko alipozaliwa alipozaliwa Iddi Amin Dada.
Makamanda wote wakuu waliopiganisha vita vya Kagera walikuwa na majina yao ya kimapigano au nom de guerre, kwa mfano Major General Kimario alijulikana kama " kamanda mbogo." Major General Imran Kombe alijulikana kama "kamanda ngono" kwasababu aliongoza mapigano kuvuka mto ngono. Colonel Tumbi ambaye alikuwa mkuu wa vikosi vya mizinga aliitwa "kamanda radi."Ahmed Takadiri Kitete alipewa jina la " kamanda supersonic. "
Baada ya vita vya Kagera Ahmed Kitete alikuwa mkuu wa operesheni na mafunzo wa Jwtz. Kwa bahati mbaya alifariki kwa ajali ya gari jijini D'salaam.
Nakaribisha michango ya wengine wenye taarifa za Ahmed Takadiri Kitete shujaa na kamanda mahiri wa jeshi la wananchi wa tanzania
cc Echolima, Manyerere Jackton , gobore, Mohamed Said, Nguruvi3, gobore, The only
Huyo imrani Kombe, ndio huyu aliekua mkuu wa TIS, alieuwawa Moshi?
Hivi vitabu vinapatikana wapi?..Kitabu cha "Vita vya Kagera" kilichoandikwa na Lt.Col.Ngatuni, Maj.Kigadye, na Capt.Ghahae kinasema hivi, ktk picha mbalimbali:
Ukurasa wa 40.
.." Meja Jenerali T.N.Kiwelu, kamanda wa kwanza kupewa jukumu la kumsukuma nyuma na kuyafyeka majeshi haramu ya nduli Idi Amin.."
Ukurasa wa 43.
"..Baada ya Brigedi mbalimbali kufanya matayarisho yao ya mwisho, Kamanda Mkuu aliyepewa dhima ya kuyaongoza mapambano ya kumtoa nyoka pangoni mwetu, Meja Jenerali Kiwelu, alikutana nao kupeana ushauri wa mwisho. Kutoka kushoto waliokaa ni Brigedia Musuguri, Meja Jenerali Kiwelu, na Brigedia Mayunga. "
Ukurasa wa 49.
"Kamanda Mkuu aliyeamrisha mapambano ya kumng'oa adui katika eneo la Kagera, Meja Jenerali Kiwelu, akiwa na mkuu wa mipango ya uamrishaji Kivita, Kanali Kitete, wakiwa katika hali ya kubadilishana mawazo na mbinu baada ya kutembelea sehemu za muhimu za mbele. Mawazo na maelekezo yao yaliwezesha wapiganaji shupavu kumng'oa adui katika eneo la Kagera."
Ukurasa wa 35.
"...Meja Jenerali David Musuguri, Kamanda wa Majeshi ya Tanzania yaliyokuwa Uganda.."
Kitabu cha " War in Uganda" kilichoandikwa na Tony Avirgan na Martha Honey kinasema hivi:
Ukurasa wa 79.
" As the preparation for phase two began, Tanzanian forces underwent an important command change, Kiwelu, who had been working twenty hours a day for three months organizing an army and lines of supply and directing the retaking of occupied lands, went back to Dar Es Salaam to resume his duties as Chief of Staff. The new commander of what was now the 20th Division wa Major General David Musuguri. "
Hivi vitabu vinapatikana wapi?
Unaweza kutusaidia
Sent from my Redmi 8A using JamiiForums mobile app