Bukoba: Ndege ya Precision Air yapata ajali Ziwa Victoria, watu 19 wafariki dunia

Bukoba: Ndege ya Precision Air yapata ajali Ziwa Victoria, watu 19 wafariki dunia

Issue hali ya anga ilikua mbaya anarudije mwanza wakati anga ndio limechafuka?
Anarudi. Hali ya hewa kuwa mbaya inayoongelewa ni kwenye kutua asingeweza kuona alama za uwanja tangia juu. Ujue huo uwanja hauna taa za kuongoza utuaji ni rangi pekee kama za kwenye barabara za lami. Kwahiyo kukiwa na ukungu, mawingu mazito au mvua kubwa hawezi kuona sehemu sahihi ya kutua sembuse mwisho wa sehemu ya kutembelea ndege.

Ilishawahi kututokea Bukoba hapo awali na vile vindege vya watu 10 (Auric Air), kufika Bukoba ruban anasema hatuwezi kutua haoni hali, ya hewa mbaya. Tukarudi Mwanza na kukaa saa 1 kisha tukaondoka na kutua salama vizuri kabisa.
 
Serikali pia hiangalie huduma la shirika hili wana route nyingi kuliko idadi ya ndege, mara nyingi ndege ikitoka mbeya iyo iyo inaenda mwanza tena ndege iyo iyo jioni inaenda kilimanjalo hii hali inafanya shirika kuangalia pesa zaidi kuliko usalama wa ndege zao.

Sent from my Nokia G10 using JamiiForums mobile app
Daah, mkuu. Hii ni ndege ujue na sio Marcopolo au Yutong🤣🤣

Uendeshaji wa ndege na mabasi ni tofauti. Ina muda wa kutembea na muda wa service
 
Ukuu wake na uponyaji unafeli kwenye barabara ?
Hakuna mahali Ukuu wa Mungu unafeli, isipokuwa Barabarani uzembe huwa mkubwa kuliko Angani.

Imagine ili uwe Rubani wa ndege unahitaji si Chini ya miaka 5 kuweza kufuzu, na Dereva anahitaji skills kidogo na Leseni ambayo anaipata hata bila kuingia darasani.

Kwa route za ndani ya Nchi nyingi Rubani anarusha ndege Kwa muda wa masaa 1.5 (Mbeya - DSM) hadi 2 ( DSM - Mwanza) kuweza kutua wakati Kwa umbali huo Dereva wa basi anahitaji zaidi ya masaa 12 kuweza kufika.

Angalia mwenyewe wapi Pana risks zaidi
 
Daah, mkuu. Hii ni ndege ujue na sio Marcopolo au Yutong🤣🤣

Uendeshaji wa ndege na mabasi ni tofauti. Ina muda wa kutembea na muda wa service
Na muda mwingi inatakiwa iwe angani ndio inakuwa salama zaidi wanasemaga wajuzi !
 
Anarudi. Hali ya hewa kuwa mbaya inayoongelewa ni kwenye kutua asingeweza kuona alama za uwanja tangia juu. Ujue huo uwanja hauna taa za kuongoza utuaji ni rangi pekee kama za kwenye barabara za lami. Kwahiyo kukiwa na ukungu, mawingu mazito au mvua kubwa hawezi kuona sehemu sahihi ya kutua sembuse mwisho wa sehemu ya kutembelea ndege.

Ilishawahi kututokea Bukoba hapo awali na vile vindege vya watu 10, kufika Bukoba ruban anasema hatuwezi kutua haoni hali ya hewa mbaya. Tukarudi Mwanza na kukaa saa 1 kisha tukaondoka na kutua salama vizuri kabisa.
upo mkuui most wanted
 
Dar es Salaam. Abiria watano kati ya watu 19 waliofariki katika Ajali ya ndege ya shirika la ndege la Precision Air iliyotokea leo Novemba 6 Bukoba mkoani Kagera, ni watumishi wa Menejimenti na Maendeleo ya Afya (MDH).
Ajali hiyo imetokea leo Novemba 6 wakati ndege hiyo ikijaribu kutua katika uwanja wa ndege wa Bukoba, lakini kutokana hali ya hewa kuwa mbaya, ilipoteza mwelekeo na kutumbukia katika ziwa Victoria.
Mkurugenzi Mtendaji wa MDH, Dk David Sando amelithibitishia Mwananchi kuwa watumishi hao watano ni miongoni mwa wengine wanane wa ofisi hiyo waliokuwa safarini kwenda Bukoba.
Watumishi wetu jumla walikuwa wanane na awali walitolewa watatu ambao hali zao hazikuwa nzuri wakapelekwa hospitali lakini baadaye waliweza kutolewa watano ambao hawakuweza kuishi, wamefariki,” ameelezea Dk Sando kwa masikitiko.
Ametaja majina ya watumishi waliopoteza maisha kuwa ni pamoja na watafiti watatu wakiwemo Dk Boniface Jullu, Dk Neema Faraja na Dk Alice Simwinga pamoja na Sauli Happymark pamoja na Mkuu wa kitengo cha mawasiliano MDH ZarchariaMlacha.
Amewataja watumishi watatu waliofanikiwa kuokolewa kuwa ni pamoja na Nickson Jackson, Dk Josephine Mwakisambwe na Dk Felix Otieno.
Dk Sando amesema wataalamu hao wa afya ya jamii walikuwa wakielekea Tabora wakipitia Mwanza na kwamba lengo la safari hiyo ilikuwa ni mkutano wa mwaka kwenda kuangalia maendeleo ya miradi.
 
Maneno ya huyu ni kwamba walijiokoa wenyewe.

View attachment 2408639
Kwa haraka ukisikiliza maelezo ya huyu abiria na manusura wa ajali kuna points muhimu kaziongea zinatoa picha ya nini kimejiri.

1. Kutoka Dar hadi Mwanza.
Hali ya hewa ilikuwa nzuri na wamesafiri vizuri. Hii inathibitisha ndege haikuwa na tatizo.

2. Kutoka Mwanza hadi Bukoba.
Hali ya hewa ziwani haikuwa nzuri kwani kulikuwa na mawingu na mvua. Hadi Bukoba hali ilikuwa sio nzuri. Walishindwa kutua wakazunguka Misenyi huku Rubani akiwajulisha atajaribu tena kutua akishindwa watarudi Mwanza. Hii inaondoa dhania kwamba ndege haikuwa na mafuta ya kufika Mwanza. Baada ya kutoka Misenyi abiria anasema waliambiwa wajiandae ndege inatua na ghafla wakajikuta wapo majini na mbele maji yameanza kuingia. Hapa unaona ni kwa nini hakuna rubani aliepona na wengi waliofariki ni waliokuwa mbele. Ni milango ya nyuma pekee ilifunguliwa na wengi waliokuwa nyuma walitoka.

3. Ruban alishusha ndege.
Uwanja wa ndege Bukoba hauna taa za kuongoza ndege wakati wa giza, ukungu au mawingu. Ukitafakri maelezo ya huyu abiria rubani atakuwa ameshusha ndege sehemu isiyo sahihi kutokana na hali isiyo nzuri ya hewa (kutoona) hivyo kusababisha kujikita kwenye maji. Tambua unamaliza ziwa unaanza uwanja wa ndege Bukoba, Mwanza na Entebbe Uganda.

Kwa ufupi.
1. Ndege ya PA iliyopata ajali haikuwa mbovu wala kuwa na tatizo.
2. Ndege ya PA haikuwa na upungufu wa ziada ya mafuta kwani ruban alitangaza kurudi Mwanza akishindwa kutua mara ya pili.
3. Hali ya hewa kutokuwa rafiki kwa zoezi la kutua.
4. Rubani kudhani anaweza kutua katika hali hiyo ya hewani kitu ambacho hakikuwezekana na ikawa kinyume na matarajio yake.
5. Maji yalianza kuingia mbele ndio maana haikuwa rahis marubani kusalimika
6.nk...... nisimalize yote niachie wengine waendelee kuchambua maelezo ya abiria
 
Ulishamsikia Heche kapanda Precision pamoja na kila siku kulalama kuhusu Air Tanzania? Lini ulisikia Zitto kapanda Precision? Kwa nini Mbowe anasafiri na Air Tanzania siku zote? Akili kichwani
Sema kipindi kile air Tanzania walikuwa hawana ndege,ilibidi tu kupanda PA. Ila kwa sasa big no.
 
Kwa maelezo hayo, unahitajika uchunguzi wa kina sana
Kwa haraka ukisikiliza maelezo ya huyu abiria na manusura wa ajali kuna points muhimu kaziongea zinatoa picha ya nini kimejiri.

1. Kutoka Dar hadi Mwanza.
Hali ya hewa ilikuwa nzuri na wamesafiri vizuri. Hii inathibitisha ndege haikuwa na tatizo.

2. Kutoka Mwanza hadi Bukoba.
Hali ya hewa ziwani haikuwa nzuri kwani kulikuwa na mawingu na mvua. Hadi Bukoba hali ilikuwa sio nzuri. Walishindwa kutua wakazunguka Misenyi huku Rubani akiwajulisha atajaribu tena kutua akishindwa watarudi Mwanza. Hii inaondoa dhania kwamba ndege haikuwa na mafuta ya kufika Mwanza. Baada ya kutoka Misenyi abiria anasema waliambiwa wajiandae ndege inatua na ghafla wakajikuta wapo majini na mbele maji yameanza kuingia. Hapa unaona ni kwa nini hakuna rubani aliepona na wengi waliofariki ni waliokuwa mbele. Ni milango ya nyuma pekee ilifunguliwa na wengi waliokuwa nyuma walitoka.

3. Ruban alishusha ndege.
Uwanja wa ndege Bukoba hauna taa za kuongoza ndege wakati wa giza, ukungu au mawingu. Ukitafakri maelezo ya huyu abiria rubani atakuwa ameshusha ndege sehemu isiyo sahihi kutokana na hali isiyo nzuri ya hewa (kutoona) hivyo kusababisha kujikita kwenye maji. Tambua unamaliza ziwa unaanza uwanja wa ndege Bukoba, Mwanza na Entebbe Uganda.

Kwa ufupi.
1. Ndege ya PA iliyopata ajali haikuwa mbovu wala kuwa na tatizo.
2. Ndege ya PA haikuwa na upungufu wa ziada ya mafuta kwani ruban alitangaza kurudi Mwanza akishindwa kutua mara ya pili.
3. Hali ya hewa kutokuwa rafiki kwa zoezi la kutua.
4. Rubani kudhani anaweza kutua katika hali hiyo ya hewani kitu ambacho hakikuwezekana na ikawa kinyume na matarajio yake.
5. Maji yalianza kuingia mbele ndio maana haikuwa rahis marubani kusalimika
6.nk...... nisimalize yote niachie wengine waendelee kuchambua maelezo ya abiria
 
Dar es Salaam. Abiria watano kati ya watu 19 waliofariki katika Ajali ya ndege ya shirika la ndege la Precision Air iliyotokea leo Novemba 6 Bukoba mkoani Kagera, ni watumishi wa Menejimenti na Maendeleo ya Afya (MDH).
Ajali hiyo imetokea leo Novemba 6 wakati ndege hiyo ikijaribu kutua katika uwanja wa ndege wa Bukoba, lakini kutokana hali ya hewa kuwa mbaya, ilipoteza mwelekeo na kutumbukia katika ziwa Victoria.
Mkurugenzi Mtendaji wa MDH, Dk David Sando amelithibitishia Mwananchi kuwa watumishi hao watano ni miongoni mwa wengine wanane wa ofisi hiyo waliokuwa safarini kwenda Bukoba.
Watumishi wetu jumla walikuwa wanane na awali walitolewa watatu ambao hali zao hazikuwa nzuri wakapelekwa hospitali lakini baadaye waliweza kutolewa watano ambao hawakuweza kuishi, wamefariki,” ameelezea Dk Sando kwa masikitiko.
Ametaja majina ya watumishi waliopoteza maisha kuwa ni pamoja na watafiti watatu wakiwemo Dk Boniface Jullu, Dk Neema Faraja na Dk Alice Simwinga pamoja na Sauli Happymark pamoja na Mkuu wa kitengo cha mawasiliano MDH ZarchariaMlacha.
Amewataja watumishi watatu waliofanikiwa kuokolewa kuwa ni pamoja na Nickson Jackson, Dk Josephine Mwakisambwe na Dk Felix Otieno.
Dk Sando amesema wataalamu hao wa afya ya jamii walikuwa wakielekea Tabora wakipitia Mwanza na kwamba lengo la safari hiyo ilikuwa ni mkutano wa mwaka kwenda kuangalia maendeleo ya miradi.
So ndege ilikuwa itoke Bukoba iende mwanza then Tabora. Too sad. Maana hawa watumishi hawakuwa na haja ya kwenda Bukoba. Mzunguko usio na Maana na umecost maisha yao.
 
Kikosi cha zima moto na uokoaji , kinatakiwa kutafakari katika haya hivi karibuni moto uliwaka kule mlina Kilimanjaro lakini jitihada za kuuzima moto zilikuwa siyo effective sana ikichangizwa na vifaa vilivyokuwa vikitumika, leo tena Ndege imedondoka lakini pia tumeendelea kushuhudia bado kikosi hiki hakijajipanga kisawasawa kukabiliana na matukio ya dharula katika maeneo tofauti tofauti.

Serikali ione umuhimu wa kukiwezesha kikosi hiki ili kifanye wajibu wake kisheria kikamilifu... Roho za watu hazina spare...Mlima Kilimanjaro unaiingiza serikali fedha nyingii sanaaa. Basi upewe kipaumbele maalumu.

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
Kulingana na UN majanga yote yanatikiwa kupewa kipaumbele. Na kuna miongozo kabisa inatolewa kwa kipindi Fulani fulani.
Kuanzia 2015 hadi 2030 tunapaswa kuongozwa na SENDAI FRAMEWORKS for Disaster Risks Reduction.
Kama mwanachama wa UN serikali ya URT iliridhia na kupitisha!
Tatizo lipo kwenye utekelezaji. Tunapenda vitu kuliko usalama wa watu wetu!
Ukiangalia idadi ya ma V8, mausafiri ya maana, viongozi na vyeo vilivyofika eneo la tukio viliishia kuwa mashuhuda bila msaada wowote
 
Back
Top Bottom