Bunda: Auawa na mkewe kwa kuchomwa kisu, kung'atwa sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo sehemu za siri pamoja na ulimi

Bunda: Auawa na mkewe kwa kuchomwa kisu, kung'atwa sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo sehemu za siri pamoja na ulimi

Julius Rubambi (38), ambaye ni Ofisa wa Kilimo katika Kata ya Neruma wilayani Bunda mkoani Mara, amefariki dunia baada ya kuchomwa kisu pamoja na kung'atwa katika sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo sehemu za siri pamoja na ulimi, na mkewe aitwaye Elizabeth Stephen (30), ambaye naye amejeruhiwa vibaya hali iliyosababishwa alazwe katika hospitali ya Kibara, baada ya kutokea kwa ugomvi wa kifamilia kati yao.
.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Salim Morcase pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Bunda Dkt.Vicent Naano, wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba tayari mwanamke huyo anashikiliwa na Jeshi la Polisi huku uchunguzi ukiendelea


View: https://www.instagram.com/p/C5Q-MmTsEUy/?igsh=eXZ3bTl6eGVxbHRu
 
Ofisa kilimo katika kata ya Neruma wilayani Bunda Mkoani mara anadaiwa kufariki dunia baada ya kuchomwa kisu na mke wake katika ugomvi uliohusishwa na wivu wa mapenzi.

Ofisa Kilimo wa Kata ya Neruma wilayani Bunda Mkoa wa Mara, Julius Rubambi (38) amefariki dunia baada ya kudaiwa kuchomwa na kisu na mke wake baada ya kutokea ugomvi baina yao.

Akizungumza kwanjia ya Simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Salim Morcase amesema tukio hilo limetokea leo Jumanne Aprili 2,2024 katika eneo la Kibara wilayani Bunda majira ya saa 4 asubuhi.

Kamanda Morcase amemtaja mtuhukiwa wa mauaji hayo kuwa ni Elizabeth Steven ( 30) ambaye tayari anashikiliwa na jeshi hilo kwa uchunguzi zaidi.

"Ni kweli tukio lipo,mke wa marehemu naye amejeruhiwa na tunavyoongea amelazwa katika hospitali ya Kibara huku akiwa chini ya ulinzi wa polisi kwaajili ya taratibu zingine," amesema

Amesea taarifa za awali zinadai wanandoa hao walikuwa na ugomvi ambapo mume alimtuhumu mke wake kuwa na mahusiano nje ya ndoa hali iliyoplekea kuwepo na majibizano kisha kuibuka kwa ugomvi.

Amefafanua kuwa kufuatia ugomvi huo mke huyo alimchoma kisu mume wake kifuani ndipo mume naye alipompiga na kupelekea mke kupoteza fahamu kabla ya wote kukimbizwa hospitalini kwaajili ya matibabu.

Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Dk Vicent Naano amesema,marehemu mbali na kuchomwa na kisu lakini pia amekutwa na majeraha ya kung'atwa sehemu mbalimbali za mwili wake na kwamba amefariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Kibara.

"Amejeruhiwa sehemu mbakimbali hadi sehemu za siri na taarifa zinasema ugomvi wao ulianza tangu usiku wa kuamkia leo ila hadi sasa bado sijajua chanzo cha ugomvi ni nini," amesema Dk Naano

Amesema baada ya kufikishwa hospitalini hapo hali ya ofisa kilimo huyo ilionekana kuwa mbaya hivyo uongozi wa hospitali ukiwa unafanya maandalizi ya rufaa kwaajili ya kupelekwa katika hospitali ya rufaa ya Kanda Bugando kwaajili ya matibabu zaidi ofisa kilimo huyo alifariki dunia.
Ooh Nifah is sad and am sad too 😭😭
 
Sijui kwann kukitokea kifo/vifo vya wanandoa, afu viwe vinahusu wivu wa mapenzii, bas mie furaha na roho kwatuu.

Nasema bado wauane tena na tena afu zaidi.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mungu asimame na hizo ndoa zenu,
Maana hali ni tete kwa upande huo mumshinde sheitwain ibilis
 

Attachments

  • Screenshot_20240402-195435~2.png
    Screenshot_20240402-195435~2.png
    108 KB · Views: 5
Back
Top Bottom