Bunda: Auawa na mkewe kwa kuchomwa kisu, kung'atwa sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo sehemu za siri pamoja na ulimi

Bunda: Auawa na mkewe kwa kuchomwa kisu, kung'atwa sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo sehemu za siri pamoja na ulimi

Kei ina nguvu sana, vijana acheni kushindana na mlipotoka. Ukiona umeoa JIKE SHUPA na uwezo wako wa kumdhibiti mdogo muache aende, hakunaga tuzo ya uvumilivu ni kifo tu utaambulia..!!!
 
20240402_215834.jpg


20240402_215837.jpg


20240402_215840.jpg
 
Tunatofautiana akili kwa kweli hivi kitu cha kuingia ukakojoa ukaendelea na mishe zako zinatoa mtu roho! Hivi kuna watu wapo serious na mpz kiasi hiki?

Jitu hujazaliwa nalo mumekutana ukubwani umelioa au kukuoa hujalikuta bikira unalikuta lilishatumika hadi basi kulifanyia wivu hadi kukutoa roho inatoka wapi?
Umeongea kwa hisia sana.
 
Ofisa Kilimo katika kata ya Neruma wilaya ya Bunda mkoani Mara anayefahamika kwa jina la Julius Rubambi ameuawa kwa kuchomwa kisu na kung'atwa ulimi na mkewe kutokana na wivu wa kimapenzi huku mkewe Elizabeth Stephen akijeruhiwa vibaya na kulazwa hospitali ya Kibara.

Inasadikika kuwa chanzo cha ugomvi huo ni mwanaume kumtuhumu mke wake kuwa ameanzisha mahusiano mengine nje ya ndoa.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa jeshi la Polisi mkoani Mara ACP Salim Morcas na amesema tayari mwanamke huyo anashikiliwa na Jeshi hilo na kwamba uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.

YAKOBO 4:1,2, INASEMA; 1 Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu? 2 Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi! 3 Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.

Mungu amesupply kwetu kila remedy ya maisha yetu ya kila siku. Tungalimpa Yesu Maisha yetu na kujazwa Roho Mtakatifu atakayekuwa anatuongoza, hakika hapangekuwa na mapigano wala mauaji wala magomvi, wala wivu wala chochote. haya yote yanatokana na kwamba wakati mwingine tunakuwa mbali na uso wa Mungu, hivyo tunampa adui shetani nafasi, na anaweza kukufanya chochote. kama hamjui, hao hata sio wa kuwacheka kama wewe haujaokoka, kama hujaokoka shetani anaweza kukugeuza na kukufanya chochote apendavyo kwasababu hauna uwezo wa kushinda dhambi.

kabla sijaokoka, nilikuwa nagombana mno na mke wangu, nilishampiga sana pia, nilikuwa na hasira sana, nilikuwa katili sana, nilipookoka, kila kitu kilibadilika, ninaishi nikiwa a living testimony kwamba ukiokoka Mungu huwa anakubadilisha kabisa.

enyi waume, nanyi wake, mkitaka ndoa yenu iwe salama, pambaneni ninyi kwa ninyi mmpe Yesu Maisha, kama mwenzako bado, omba na msaidie aokoke, mkiokoka nyote mtakuwa mmeziba mlango wa shetani pakubwa sana. ama la, shetani atakua anaingia na kutoka kwenu, anaweza kuleta magonjwa apendavyo kupitia mwenza wako, kwasababu mmemkataa Yesu na mmempa yeye shetani nafasi. mwenye masikio na asikie, usisubiri hadi shetani akuteketeze katika dakika za mwisho ndio umtafute Mungu, wahi mapema kabla hajakusambaratisheni.
 
Ofisa kilimo katika kata ya Neruma wilayani Bunda Mkoani mara anadaiwa kufariki dunia baada ya kuchomwa kisu na mke wake katika ugomvi uliohusishwa na wivu wa mapenzi.

Ofisa Kilimo wa Kata ya Neruma wilayani Bunda Mkoa wa Mara, Julius Rubambi (38) amefariki dunia baada ya kudaiwa kuchomwa na kisu na mke wake baada ya kutokea ugomvi baina yao.

Akizungumza kwanjia ya Simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Salim Morcase amesema tukio hilo limetokea leo Jumanne Aprili 2,2024 katika eneo la Kibara wilayani Bunda majira ya saa 4 asubuhi.

Kamanda Morcase amemtaja mtuhukiwa wa mauaji hayo kuwa ni Elizabeth Steven ( 30) ambaye tayari anashikiliwa na jeshi hilo kwa uchunguzi zaidi.

"Ni kweli tukio lipo,mke wa marehemu naye amejeruhiwa na tunavyoongea amelazwa katika hospitali ya Kibara huku akiwa chini ya ulinzi wa polisi kwaajili ya taratibu zingine," amesema

Amesea taarifa za awali zinadai wanandoa hao walikuwa na ugomvi ambapo mume alimtuhumu mke wake kuwa na mahusiano nje ya ndoa hali iliyoplekea kuwepo na majibizano kisha kuibuka kwa ugomvi.

Amefafanua kuwa kufuatia ugomvi huo mke huyo alimchoma kisu mume wake kifuani ndipo mume naye alipompiga na kupelekea mke kupoteza fahamu kabla ya wote kukimbizwa hospitalini kwaajili ya matibabu.

Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Dk Vicent Naano amesema,marehemu mbali na kuchomwa na kisu lakini pia amekutwa na majeraha ya kung'atwa sehemu mbalimbali za mwili wake na kwamba amefariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Kibara.

"Amejeruhiwa sehemu mbakimbali hadi sehemu za siri na taarifa zinasema ugomvi wao ulianza tangu usiku wa kuamkia leo ila hadi sasa bado sijajua chanzo cha ugomvi ni nini," amesema Dk Naano

Amesema baada ya kufikishwa hospitalini hapo hali ya ofisa kilimo huyo ilionekana kuwa mbaya hivyo uongozi wa hospitali ukiwa unafanya maandalizi ya rufaa kwaajili ya kupelekwa katika hospitali ya rufaa ya Kanda Bugando kwaajili ya matibabu zaidi ofisa kilimo huyo alifariki dunia.
na kwa wasio wanasheria, nikiwadokeza tu, hii kesi hawezi kunyongwa, ni manslaughter kwasababu kifo kimetokea wakati wa ugomvi, malice aforethought inaweza kuwa ya kutafuta. soon dada atakuwa mtaani, na ataolewa tena. ila mwenzake ndo kafa, na siajabu kafa katika dhambi. ndo maana tunasema okokeni, shetani yupo ili kuangamiza maisha ya wanadamu kabla hawajarudi kwa Mungu. shetani hua anagombanisha wanadoa,wanapigana, wanachinjana yeye kakaa pembeni, ikiwezekana wote wauane ili wote waende motoni. kuweni makini, kuishi nje ya Mungu hakuna mwisho mwema.
 
Back
Top Bottom