Bunge Primary School, Uchafu mwingine city center unaofumbiwa macho na vigogo

Bunge Primary School, Uchafu mwingine city center unaofumbiwa macho na vigogo

Eti wakuu, kwa Karne ya sasa kuna umuhimu gani wa kuendelea kuwa na Primary Schools kama Bunge pale kati kati kabisa ya Mji?? Lengo ni nini?? Tena shule ya serikali, shule zinazofahamika kwa kuwa na wanafunzi wachafu wasio na maadili hakuna mfano.

Eneo potential la kuweka investments za maana, wewe unaweka shule ya msingi? Hata kama ilijengwa zamani, Je, bado kuna uhalali wa kuendelea kuwepo pale?

Ni mtoto yupi anayesoma primary ya Bunge ni mkazi wa eneo lile lililojaa ofisi za serikali?

Uwepo wa shule kama Bunge huleta msuguano tu wa kimaslahi kwa maana ikifika December, kila mzazi anayefanya kazi Posta, mwenye IST anataka mwanae akasome Bunge. What for.

Hata kama ni shule, basi mpeni muwekezaji binafsi atakayeweza kumaintain mazingira pamoja na usafi wa wanafunzi kama zilivyo shule zingine za private za English Medium lakini sio kuweka shule uchafu katika eneo potential kama Posta Mpya (A few kilometers from the state house)

Vp kuhusu usalama wa watoto wadogo?? Yale mazingira gani ya shule watoto wanachangamana na wababa watu wazima wanaenda kupata lunch pale. Wakibakwa je (Sexual Harassment)??

Kwa zile movements za Magari binafsi kwanza ni hatari hata kwa usalama wa wanafunzi wa Darasa la kwanza..

SHULE YA BUNGE CITY CENTER NI UCHAFU MWINGINE UNAOFUMBIWA MACHO NA VIGOGO..
Umetumwa kuchokoza mada ili uone reactions za wadau ama nini, kwanini unaita shule ya serikali uchafu, au umetumwa uje uchokonoe mada na wanaotamani eneo Hilo?
 
Somehow ulikuwa na hoja ila lugha ulotumia si nzuri, let's say ungeshauri mamlaka husika zikafanyia marekebisho hiyo shule lakini kuhitimisha iondoke wewe upo nyuma ya keyboard ila kuna watu pasipo kutarajia inawasaidia ile shule.
 
Vp kuhusu usalama wa watoto wadogo?? Yale mazingira gani ya shule watoto wanachangamana na wababa watu wazima wanaenda kupata lunch pale. Wakibakwa je (Sexual Harassment)??

Kwa zile movements za Magari kwanza ni hatari hata kwa usalama wa wanafunzi wa Darasa la kwanza..

Kwamba Tanzania nzima shule iliyo kwenye mzunguko wa watu ni bunge tu???
Nyingine zimetengwa na wababa watu wazima?? 😁😁😁
Shule nyingine ni porini hakuna magari
 
Serikali ni hao hao unaotarajia wafanyie kazi maoni yako.
Wafanyie kazi maoni yangu kwani mimi ni mwana CCM?? Au mimi ni mtoto wa Samia/JK/JPM??

Sijaandika kwa lengo la mada hii kufanyiwa kazi, I just wrote it..
 
Restaurant sio kwa ajili ya watoto ni watu wa nje wengi wakiwa ni wanafunz wa IFM...... wafanyakazi baadhi wa ofisi za posta!!

wanafunz pia canteen Kuna Sheria za kuingia pale ko siwezi ku judge directly najua maake nimekuwa mteja wa restaurant iliyopo ndani ya shule ya msingi bunge,
Vp kuhusu rush hours asubuhi na jioni kwa usalama wa watoto na private cars??

For so long as kuna movement ya watu wazima na watoto katika compounds za shule kwa kisingizio cha lunch, kuna risks kubwa sana ya sexual harassment pale..
 
Back
Top Bottom