Busara kidogo inahitajika katika hili

Busara kidogo inahitajika katika hili

Sasa hajam-deny haki zake? Ukatae mtoto ila jina ung'ang'anie alitumie la kwako? Ili baadaye akishapiganiwa amekua vizuri ndiyo uje uanze kumganda. What if ulivyokataa mimba mama yake angeamua kuitoa?
Jina ni sahihi its her biological father, labda mambo mengine ila hilo hata ukisema umpe jina lako wewe mtoto haibaidilishi ukweli. Utajifurahisha tu
 
Jina ni sahihi its her biological father, labda mambo mengine ila hilo hata ukisema umpe jina lako wewe mtoto haibaidilishi ukweli. Utajifurahisha tu
Eeh hata akitumia jina la baba mlezi au la ujombani haitobadili kuwa baba mzazi ni mwingine. Tunampa heshima mtu aliyejitoa sadaka kuwa baba kwako wakati baba halisi amekukataa.
 
Lil sis don't stress yourself; Wala hata usiwaze huyo baba yako anajisikiaje; sio shida zako hata kama umemsamehe.

Baba yako ni mtu selfish; wakati wewe unamuhitaji kwenye maisha yako; yeye hakuwa tayari. Muda huu yeye anakuhitaji wewe na anakulazimishia; sio sawa.

Ukweli ni kwamba sio kila mwanaume ni baba. Kuna watu wengi waliolelewa na baba zao; lakini hicho alicho/anachokupa baba yako mlezi; kuna millions of people hawajawahi kuki_experience. Mshukuru huyo baba yako mlezi sanaaaaa. Hujapata ombwe/ trauma kwa sababu ya kutokulelewa na baba; kwa sababu yeye aliamua kuwa baba ambaye hukuwa naye. Mimi ninajua umuhimu wa uwepo wa baba kwenye maisha ya mtoto wa kike; kwa kukukubali wewe na kukufanya mtoto wake uuuh; kitu kikubwa mnoooo, ni neema.

Tena mama yako mmmh basi tu; mimi binafsi ningekupa na surname ya huyo baba mlezi period; ingebaki tu damu yake kwako maana haiwezi kutolewa. Ubaba sio tu kumwaga mbegu; ubaba ni malezi. Baba ni yule anayejua umekula nini, umevaa nini, umelala wapi; anakupenda, anakujali, anakufundisha, anakuoyna, anakuwa concerned na wewe kwa Kila hali. Ukiumwa, ukiwa na changamoto yoyote; he is always there you. Huyo ndiyo baba na hicho kinacho-form bond kati ya mtoto na mzazi. You are an absentee parent; don't expect any bond with your child

Huyo baba yako mzazi; kaa naye kwa kina mwambie tu you are at peace with him, unamtambua kama baba yako mzazi; ila huwezi kuwa karibu naye kama anavyotamani. Ni mtoto wake kwa kukuzaa; but alishauza hiyo haki kwa mwanaume mwingine.

Nenda kamwambie baba yako mlezi ukweli wote; asije akakuona you are an ingrate. Naamini amefanya Kila kitu kwenye maisha yako kwa sababu ya upendo na sio kungoja shukrani. But kiubinadamu tu; mpe tu shukrani zake; una deni juu yake. Mpe na msimamo wako juu ya huyo baba yako mzazi. Hakikisha baba yako mlezi ana amani juu yako. Don't lose than man, don't hurt him, don't disappoint him. Make him proud; isije siku akasema "mtoto wa watu ni wa watu tu".
Umetisha saaaaana Mkuu.
 
Sasa hajam-deny haki zake? Ukatae mtoto ila jina ung'ang'anie alitumie la kwako? Ili baadaye akishapiganiwa amekua vizuri ndiyo uje uanze kumganda. What if ulivyokataa mimba mama yake angeamua kuitoa?
Alimtelekeza kipindi ambacho anamhitaji tena ,kipindi ambacho kuzaa out of wedlock ilikua ni dhambi sana,baba wa watu akakubali kumfichia aibu mama wa watu na good enough anamlea kwa upendo 100%
Leo kwa kua hana binti ktk uzao mwingine ndo amerudi...hana mapenzi na Carleen isipokua anataka tu binti amuoze atoe mkono siku ya harusi thats all!!

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 
Mie simtetei in a way kwamba kafanya jambo sahihi but anastahili Tag ya kuwa biological father. Hakuweza kuwa social father kwa binti thus why bint ana bond na baba mlezi.
Biological father bila huduma ni zero tu,kubwa amefata jinsia ya mtoto maana angekua na mabinti asingemtafuta

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 
Nikitoa ushauri kama wa wale mabraza wa miaka 40 nasema hivi...

Mheshimu sana huyo Baba mlezi,,, na hata Baba mzazi pia mpe heshima yake kwa kadri nafsi yako inavoshawishika...

Sometimes behind the scene za migogoro ya wazazi ni nzito sana....

Enjoy life na baba mlezi But mzazi pia usimkatae kiiivo coz safari bado ni ndefu duniani..
 
Mungu akubariki, utakuja shukuru kwa hayo maamuzi baadaye..
Ila Ninamshukuru na Mama yake pia.
Huwa anajitahidi binti yangu aone mchango wangu.

Kila ninalofanya kwa ajili yake huwa anamwambia.

Kuna kipindi nilikaa miaka 4 bila kumwona ila siku tunaonana she always hugs me na huwa analia kwa furaha.

Namshukuru sana Mama yake kwa hilo tu! Japo alinirubuni sana.
 
All included!!

Hii Task itakuwa nyepesi kama Baba Mzazi
Atakaa mezani na Baba Mlezi, wayajenge. Sisi Wanaume ni rahisi sana kuelewana
 
Una kesi kama ya shosti angu mmoja ila yeye aliamua kusimama upande wa Mama yake na Baba mlezi. Huyo Baba mzazi muache alalamike weee atachoka mwenyewe kamwe usije umiza waliokua nawe kipindi kigumu na cha furaha.

Hawa jamaa wa hit and run ndo kawaida zao hizo. Anakimbia huku akijua kuna mimba au mtoto katelekeza anabaki kujipa matumaini atanitafuta akikua.

Ukisogeza ukaribu zaidi kituo cha pili kitakua kutembeleana,leo atataka uende huku kesho kule kesho kutwa pale.

Muheshimu tu kama mmoja wa wazazi wako.
That is all
 
Lil sis don't stress yourself; Wala hata usiwaze huyo baba yako anajisikiaje; sio shida zako hata kama umemsamehe.

Baba yako ni mtu selfish; wakati wewe unamuhitaji kwenye maisha yako; yeye hakuwa tayari. Muda huu yeye anakuhitaji wewe na anakulazimishia; sio sawa.

Ukweli ni kwamba sio kila mwanaume ni baba. Kuna watu wengi waliolelewa na baba zao; lakini hicho alicho/anachokupa baba yako mlezi; kuna millions of people hawajawahi kuki_experience. Mshukuru huyo baba yako mlezi sanaaaaa. Hujapata ombwe/ trauma kwa sababu ya kutokulelewa na baba; kwa sababu yeye aliamua kuwa baba ambaye hukuwa naye. Mimi ninajua umuhimu wa uwepo wa baba kwenye maisha ya mtoto wa kike; kwa kukukubali wewe na kukufanya mtoto wake uuuh; kitu kikubwa mnoooo, ni neema.

Tena mama yako mmmh basi tu; mimi binafsi ningekupa na surname ya huyo baba mlezi period; ingebaki tu damu yake kwako maana haiwezi kutolewa. Ubaba sio tu kumwaga mbegu; ubaba ni malezi. Baba ni yule anayejua umekula nini, umevaa nini, umelala wapi; anakupenda, anakujali, anakufundisha, anakuoyna, anakuwa concerned na wewe kwa Kila hali. Ukiumwa, ukiwa na changamoto yoyote; he is always there you. Huyo ndiyo baba na hicho kinacho-form bond kati ya mtoto na mzazi. You are an absentee parent; don't expect any bond with your child

Huyo baba yako mzazi; kaa naye kwa kina mwambie tu you are at peace with him, unamtambua kama baba yako mzazi; ila huwezi kuwa karibu naye kama anavyotamani. Ni mtoto wake kwa kukuzaa; but alishauza hiyo haki kwa mwanaume mwingine.

Nenda kamwambie baba yako mlezi ukweli wote; asije akakuona you are an ingrate. Naamini amefanya Kila kitu kwenye maisha yako kwa sababu ya upendo na sio kungoja shukrani. But kiubinadamu tu; mpe tu shukrani zake; una deni juu yake. Mpe na msimamo wako juu ya huyo baba yako mzazi. Hakikisha baba yako mlezi ana amani juu yako. Don't lose than man, don't hurt him, don't disappoint him. Make him proud; isije siku akasema "mtoto wa watu ni wa watu tu".
Aah hayaa..twende kazi washauri...who is next??
 
Hoping....!
Okeee. Iko hivi, mama mzazi alijua ipo siku utahitaji kujua asili ya baba yako na hakutaka kukuuza kwenye ukoo mwingine na ndio maana licha ya kuingia kwenye mahusiano na mtu mwingine bado alikuandika kwa jina la ukoo wa baba yako. Pia kwa kuwa alimuambia mimba ni yake, alijua ipo siku baba yako angekutafuta umri wa ujana ukimtoka Hakutaka kukunyang'anya haki ya msingi inayohusu utambulisho wako. Your mother ni zaidi ya binadamu na anastahili pongezi kwenye hili.

Na kwa upande mwingine baba mlezi aliafiki wewe kuitwa kwa jina la baba yako mzazi na kuwa tayari kukulea kama mwanaye wa kumzaa. Anajua ipo siku utakutana na baba yako mzazi na maamuzi yako mikononi mwako yeye ametimiza sehemu yake kama mzazi.

Nini cha kufanya? Endelea kumpenda baba mlezi kama mwanzo lakini baba yako mzazi usimpuuze, forgive. You never know ni nini kilimfanya akatae na huenda hiyo sababu hapendi uisikie huenda ikakuumiza au ikakufanya uhamishie hasira kwa mama. Kuna baadhi ya mambo wanaume huwa tunayapa muda hatukubali kirahisi. What if mama alikuwa na mahusiano na mwanaume mwingine at the same time yuko kwenye mahusiano na baba yako? Unafikiri ni rahisi kukubali kirahisi. Wanaume huwa tunajipa muda mtoto azaliwe. Sisemi mama alikuwa hivyo ila najaribu kufikiri kwa kina as a man. Na mara nyingine mtoto akizaliwa akina mama huwa wakali kutokana na waliyopitia baada ya kukataliwa. Na Unafikiri kama sababu inaweza kuwa kama hizo na wakati huu baba ako ameshakuwa mtu mzima atakuwa tayari kumkosea heshima mama yako aliyekulea? Sidhani !

Mpe nafasi kabla hajafa akutambulishe kwa ndugu zako na sio lazima uhitaji kitu kutoka kwake. Isijetokea mbeleni ukaolewa na kaka yako au watoto wenu wakaja kuoana. Na ndio sababu mojawapo ya msingi ambayo mama yako alikuandika jina la ukoo la baba yako mzazi. Utajisikiaje hayo mambo yakija kutokea kwenye maisha yako? Kujua identify yako na wanaohusika nawe ni jambo la msingi katika mambo mengi.

Kaa na baba mlezi mweleze juu ya ujio wa huyo baba mzazi kwenye maisha yako. Lakini usisahau kumtambua na kumuambia baba mlezi kuwa ana nafasi kubwa katika maisha yako ila unahitaji kujua ndugu zako kwa sababu mojawapo ya hizo nilizotaja zisijetokea. Kuna wakati utatamani kumjua baba yako vizuri pamoja na ndugu zako wengine lakini atakuwa hayupo wamebaki wasiokutambua.

Usiangalie sana mambo ya nyuma ambayo huyajui. Kwa kuwa mama hakuzuii fanya kukutana naye na kuwa na mawasiliano naye ya kawaida. Kuna mengi lakini hayo yanatosha kiutu uzima.
 
Back
Top Bottom