Bwawa la Mwalimu Nyerere kuanza kujazwa maji Desemba 22, 2022

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Ujenzi wa Bwawa hilo (JNHPP) ambao hadi Novemba 2022 ulikuwa umefikia 77.15%, unatazamiwa kufikia 80% wakati mchakato wa kujazwa maji utakapoanza.

Meneja Mawasiliano wa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO, Elihuruma Ngowi amesema “Ujazaji maji utaanza wiki ijayo Desemba 22, 2022 na siyo leo (Desemba 15) kama ilivyoelezwa awali.”

Pia Soma: KUMEKUCHA! JNHPP Kuanza kujazwa maji Disemba 15, 2022
 
Wafanya kazi 1108 wote ni wakigeni kweli mbona wengi hivo, wanafanya kazi gani hizo ambazo watanzania hawaziwezi? Taifa watu 60m wakati tuna wataalamu wa kila nyanja.
 
Yale yale ya SGR Dar-Moro. Hapa wamekalia kuongelea wazawa ni 90.99% ya waajiriwa wote badala ya kuonesha hatua ujenzi ulipofikia na nini kimepekea ujazaji maji katika bwawa hilo usianze leo December 15 kama walivyoahidi wenyewe bila shuruti.
Kwahiyo kusema mradi umefika 80% siyo hatua!?...ungetafuta habari yenyewe,labda mleta mada kaleta kwa ufupi,watu mna chuki Sana na serikali yenu, yakitokea matatizo mnaitazana mkitaraji utatuzi. Be positive sister!
 
Ujenzi wa Bwawa hilo (JNHPP) ambao hadi Novemba 2022 ulikuwa umefikia 77.15%, unatazamiwa kufikia 80% wakati mchakato wa kujazwa maji utakapoanza.

Meneja Mawasiliano wa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO, Elihuruma Ngowi amesema “Ujazaji maji utaanza wiki ijayo Desemba 22, 2022 na siyo leo (Desemba 15) kama ilivyoelezwa awali.”

Mradi umeajiri watu 12,298 huku 11,190 sawa na 90.99% wakiwa ni wazawa wakati 1,108 sawa na 11.01% wakiwa ni raia wa kigeni.

Pia Soma: KUMEKUCHA! JNHPP Kuanza kujazwa maji Disemba 15, 2022
Maji yanayoka wapi, majumbani hatuna maji mpaka siku 3 mfululizo!
 
Wafanya kazi 1108 wote ni wakigeni kweli mbona wengi hivo, wanafanya kazi gani hizo ambazo watanzania hawaziwezi? Taifa watu 60m wakati tuna wataalamu wa kila nyanja.
Kuajiri kampuni ya nje kujenga hilo bwawa, ni dhahiri wasomi wetu wako chini ya viwango. Na simaanishi juu ya utaalamu tu, bali hata mtaji na vitendea kazi!
 
Kwa hiyo kusema mradi umefika 80% siyo hatua!?...ungetafuta habari yenyewe,labda mleta mada kaleta kwa ufupi,watu mna chuki Sana na serikali yenu,yakitokea matatizo mnaitazana mkitaraji utatuzi,be positive sister!!
Ushauri siyo chuki bwashee.

Serikali ikifanya vizuri kwa mtu kama mimi huwa naipongeza hata kama ni kimoyomoyo mfano awamu ya tano ilijitahidi sana katika suala la kusambaza umeme vijijini-niliipongeza kwa hilo. Awamu ya sita imefanikisha kuchepusha maji kwenda Tinde toka bomba kuu la Mwanza-Tabora/Shelui ikiwa ni ahadi ya awamu ya tano-nimeipongeza serikali.

Awamu ya sita imeleta kata kata ya umeme nchini-nimeisema.

Imechelewesha kukamilika kwa bwawa la Nyerere-tumeisema.

Iliahidi kuanza ujazaji wa maji katika bwawa hilo hii leo December 15 lakini imekuja na excuse tena kana kwamba aliyeahidi ni taasisi nyingine-wewe unataka niendelee kupiga mapambio kuwa imefanya vizuri. Hii siyo praise team.
 
Ushauri siyo chuki bwashee.
Serikali ikifanya vizuri kwa mtu kama mimi huwa naipongeza hata kama ni kimoyomoyo mfano awamu ya tano ilijitahidi sana katika suala la kusambaza umeme vijijini-niliipongeza kwa hilo...
We jamaa huna details kabisa halafu upo Frontline kulalama,maji toka Viktoria kwenda mkoa wa tabora jakaya alisaini na wahindi 2014/15 na ndiyo waliotoa hela na ndiyo waliofanya kazi,bwawa la nyerere awamu ya tano iliishia 30%+ awamu ya SITA ipo 80% na ni mwaka na miezi Tisa tu,

Umeme vijijini ni mpango wa mzee mkapa,alifanya akaishia alipoishia, kikwete akafanya akaishia alipoishia,awamu yako ikafanya ikaishia ilipoishia, iliyopo inatarajiwa kumalizia, mgao wa umeme maji hakuna,awamu ya tano aliachiwa amalizie kinyerezi projects, umeme wa uhakika wa gesi akarukia mradi ghali wa maji uliomshinda,angemalizia kinyerezi pasingekua na kilio Cha maji ya kuzalishia umeme
 
We jamaa huna details kabisa halafu upo Frontline kulalama,maji toka Viktoria kwenda mkoa wa tabora jakaya alisaini na wahindi 2014/15 na ndiyo waliotoa hela na ndiyo waliofanya kazi,bwawa la nyerere awamu ya tano iliishia 30%+ awamu ya SITA ipo 80% na ni mwaka na miezi Tisa tu,

Umeme vijijini ni mpango wa mzee mkapa,alifanya akaishia alipoishia, kikwete akafanya akaishia alipoishia,awamu yako ikafanya ikaishia ilipoishia, iliyopo inatarajiwa kumalizia, mgao wa umeme maji hakuna,awamu ya tano aliachiwa amalizie kinyerezi projects, umeme wa uhakika wa gesi akarukia mradi ghali wa maji uliomshinda,angemalizia kinyerezi pasingekua na kilio Cha maji ya kuzalishia umeme
Kasome uelewe nilichoandika. Nimeongelea bomba la maji kwende Tinde toka bomba kuu la maji Mwanza-Tabora halafu ndio uje na uPraise team wako.

Unaposema awamu ya 5 iliishia 30% tu, je, unajua bwawa hilo lilitakiwa liwe tayari hadi kufikia lini kwa mujibu wa awamu ya 5?

Kuhusu umeme wa REA ni kweli ulianza na Mkapa lakini kati ya Mkapa, Kikwete na Magufuli nani alisambaza umeme kwa kiwango kikubwa nchini? Pia ni nani anayefanya zoezi la kusambaza umeme vijijini liende kwa mwendo wa konokono tangu kufariki kwa Magufuli?
 
Wafanya kazi 1108 wote ni wakigeni kweli mbona wengi hivo, wanafanya kazi gani hizo ambazo watanzania hawaziwezi? Taifa watu 60m wakati tuna wataalamu wa kila nyanja.
Si kazi ya kujaza maji ktk Hilo bwawa[emoji16][emoji849]

Kazi za kitaalamu hizo
 
Kasome uelewe nilichoandika. Nimeongelea bomba la maji kwende Tinde toka bomba kuu la maji Mwanza-Tabora halafu ndio uje na uPraise team wako.

Unaposema awamu ya 5 iliishia 30% tu, je, unajua bwawa hilo lilitakiwa liwe tayari hadi kufikia lini kwa mujibu wa awamu ya 5?

Kuhusu umeme wa REA ni kweli ulianza na Mkapa lakini kati ya Mkapa, Kikwete na Magufuli nani alisambaza umeme kwa kiwango kikubwa nchini? Pia ni nani anayefanya zoezi la kusambaza umeme vijijini liende kwa mwendo wa konokono tangu kufariki kwa Magufuli?
Kama 80% Leo unadai limechelewa,hiyo awamu ya 5 ambao waliishia 30+% walipanga %ngapi ifikiwe lini!?
 
Ujenzi wa Bwawa hilo (JNHPP) ambao hadi Novemba 2022 ulikuwa umefikia 77.15%, unatazamiwa kufikia 80% wakati mchakato wa kujazwa maji utakapoanza.

Meneja Mawasiliano wa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO, Elihuruma Ngowi amesema “Ujazaji maji utaanza wiki ijayo Desemba 22, 2022 na siyo leo (Desemba 15) kama ilivyoelezwa awali.”

Pia Soma: KUMEKUCHA! JNHPP Kuanza kujazwa maji Disemba 15, 2022
ngoja nijizuie kutukana. maji kutoka wapi? mto upi? mvua zipi? Bladf
 
Back
Top Bottom