johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 97,869
- 171,716
CAG Kicheere anaongea na waandishi wa habari muda huu.
Updates;
========
CAG: NILIBAINI WAKALA NNE ZA SERIKALI ZILIKUWA ZINADAIWA BILIONI 783.39
TANROADS ilikuwa na deni kubwa lenye thamani ya bilioni 770.1 kutoka kwa wakandarasi na wahandisi washauri kutokana na kuchelewa kupata fedha za kutekeleza miradi kutoka hazina, wakala wa majengo bilioni 1, RUWASA bilioni 12 na TARURA milioni 125
-Ni madeni ya wakandarasi, watoa huduma na washauri katika hizo taasisi nne
CAG: MIRADI INAYOTEKELEZWA INA TOZO YA RIBA YA BILIONI 14.9
Mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali(CAG) amesema miradi mbalimbali inayotekelezwa nchini ina riba ya bilioni 14.9 kama adhabu ya kuchelewesha kulipa hati za madai ya wakandarasi kinyume na masharti ya mikataba
-CAG amesema malipo hayo hayana tija kwani yangeweza kuepukika kwani baadhi ya pesa ni za wafadhili ambazo zipo lakini mlolongo mrefu wa malipo kwa serikali unakwamisha
MALIASILI NA UTALII
CAG: Nilifanya ukaguzi maalum wizara ya maliasili na utalii, nilibaini bilioni 6.8 zililipwa kutoka kwenye mfuko wa tozo ya maendeleo ya utalii bila idhini ya afisa masuuli kinyume na kanuni ya fedha. Pamoja na haya nilibaini matumizi ya jumla ya bilioni 16 yalifanyika bila kuwa na hati za malipo pia yalibainika matumizi ya bilioni 11 ambayo hayakuwa na nyaraka toshelezi na milioni 89 zilizotumiwa na makumbusho ya Taifa kwa matumizi yasiyoendana na shughuli za utalii.
Kwa maoni yangu mkurugenzi wa utalii na mhasibu waliokuwa wanahusika walitumia vibaya fedha za tozo ya utalii jumla ya Tshs Bilioni 34
CAG: BODI YA WAKURUGENZI YA ATCL HAINA MJUMBE MWENYE UZOEFU NA MASUALA YA ANGA
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali amesema hayo na pia kuongeza kuwa Shirika linadaiwa hivyo inakuwa changamoto kuruka kwenye baadhi ya maeneo
Pia Viwanja vya Ndege vimetajwa kuwa na changamoto
Updates;
========
CAG: NILIBAINI WAKALA NNE ZA SERIKALI ZILIKUWA ZINADAIWA BILIONI 783.39
TANROADS ilikuwa na deni kubwa lenye thamani ya bilioni 770.1 kutoka kwa wakandarasi na wahandisi washauri kutokana na kuchelewa kupata fedha za kutekeleza miradi kutoka hazina, wakala wa majengo bilioni 1, RUWASA bilioni 12 na TARURA milioni 125
-Ni madeni ya wakandarasi, watoa huduma na washauri katika hizo taasisi nne
CAG: MIRADI INAYOTEKELEZWA INA TOZO YA RIBA YA BILIONI 14.9
Mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali(CAG) amesema miradi mbalimbali inayotekelezwa nchini ina riba ya bilioni 14.9 kama adhabu ya kuchelewesha kulipa hati za madai ya wakandarasi kinyume na masharti ya mikataba
-CAG amesema malipo hayo hayana tija kwani yangeweza kuepukika kwani baadhi ya pesa ni za wafadhili ambazo zipo lakini mlolongo mrefu wa malipo kwa serikali unakwamisha
MALIASILI NA UTALII
CAG: Nilifanya ukaguzi maalum wizara ya maliasili na utalii, nilibaini bilioni 6.8 zililipwa kutoka kwenye mfuko wa tozo ya maendeleo ya utalii bila idhini ya afisa masuuli kinyume na kanuni ya fedha. Pamoja na haya nilibaini matumizi ya jumla ya bilioni 16 yalifanyika bila kuwa na hati za malipo pia yalibainika matumizi ya bilioni 11 ambayo hayakuwa na nyaraka toshelezi na milioni 89 zilizotumiwa na makumbusho ya Taifa kwa matumizi yasiyoendana na shughuli za utalii.
Kwa maoni yangu mkurugenzi wa utalii na mhasibu waliokuwa wanahusika walitumia vibaya fedha za tozo ya utalii jumla ya Tshs Bilioni 34
CAG: BODI YA WAKURUGENZI YA ATCL HAINA MJUMBE MWENYE UZOEFU NA MASUALA YA ANGA
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali amesema hayo na pia kuongeza kuwa Shirika linadaiwa hivyo inakuwa changamoto kuruka kwenye baadhi ya maeneo
Pia Viwanja vya Ndege vimetajwa kuwa na changamoto