CAG aongea na waandishi wa habari - Aprili 8, 2021

CAG aongea na waandishi wa habari - Aprili 8, 2021

Tamasha la utalii pana upigaji wa takribani 1.5 B maana tamasha hili halikuwemo ktk bajeti za wizara ila iliamuliwa kila mamlaka chini ya wizara kutoa 250m kufanikisha na fedha hizi matumizi yake CAG hakupata vielelezo, ambapo Clouds walilipwa 600+m na TBC 200+m lakini malipo haya hayakuwa na uthibitisho maana risiti za kielektroniki hazikutolewa
 
Tamasha la utalii pana upigaji wa takribani 1.5 B maana tamasha hili halikuwemo ktk bajeti za wizara ila iliamuliwa kila mamlaka chini ya wizara kutoa 250m kufanikisha ila fedha hizi CAG hakupata vielelezo, ambapo Clouds walilipwa 600+m na TBC 250+m lakini malipo haya hayakuwa na uthibitisho maana risiti za kielektroniki hazikutolewa
Unasikilizia wapi mkuu??
 
... unapenda kweli kuwahi kuleta habari but with no details or very shallow. Usiwe unakimbilia ku-post; unaziba nafasi ya mwenye nia ya kutuletea habari kwa ukamilifu! Hata hizo UPDATES zako zitakuwa very shallow I guess!

😂 😂
 
Kwakweli, yule mwendazake anatakiwa afufuliwe, ili aje atupe maelezo mazuri, tena atupe maelezo ya kunyooka sawa sawa sisi raia kuhusu huu upuuzi (Ufisadi) aliokua akifanya yeye na wateule wake.

Na atueleze kwanini alitufanya sisi raia wajinga kwa kutuaminisha hakuna ufisadi nchi hii katika awamu yake, wakati katika awamu zilizoongoza kwa ufisadi hakuna kama ya kwake.

Sasa majibu yanaanza kupatikana kwanini;

1) Bunge lilipitisha sheria ya kosa la jinai kutangaza takwimu za serikali.

2) Serikali kukamata na kufunga watu waliohoji matumizi ya fedha za umma.

3) Serikali ilitumia nguvu nyingi sana kuaminisha raia maendeleo ya nchi kwa kutumia flyover mbili na ndege (Kuwapumbaza raia).

4) Vyombo vya habari kufungiwa.
 
Huu upigaji unaosemwa na CAG tena katika awamu iliyojinasibu kupambana na ubadhirifu unaweza kuhitimisha kwa maneno machache kuwa Pamoja na simba kuwa mkali lakini anazaa

Kazi ya CAG ni kusema

Wanaopokea report zao ni kama vile wanafunzi wanavyopokea majibu ya mtihani wao wa mwisho wa mwaka. Wapo wa kupata A, B, C, D......
 
CAG Kicheere anaongea na waandishi wa habari muda huu.

Updates;
========

CAG: NILIBAINI WAKALA NNE ZA SERIKALI ZILIKUWA ZINADAIWA BILIONI 783.39

TANROADS ilikuwa na deni kubwa lenye thamani ya bilioni 770.1 kutoka kwa wakandarasi na wahandisi washauri kutokana na kuchelewa kupata fedha za kutekeleza miradi kutoka hazina, wakala wa majengo bilioni 1, RUWASA bilioni 12 na TARURA milioni 125

-Ni madeni ya wakandarasi, watoa huduma na washauri katika hizo taasisi nne

CAG: MIRADI INAYOTEKELEZWA INA TOZO YA RIBA YA BILIONI 14.9

Mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali(CAG) amesema miradi mbalimbali inayotekelezwa nchini ina riba ya bilioni 14.9 kama adhabu ya kuchelewesha kulipa hati za madai ya wakandarasi kinyume na masharti ya mikataba

-CAG amesema malipo hayo hayana tija kwani yangeweza kuepukika kwani baadhi ya pesa ni za wafadhili ambazo zipo lakini mlolongo mrefu wa malipo kwa serikali unakwamisha

MALIASILI NA UTALII

CAG: Nilifanya ukaguzi maalum wizara ya maliasili na utalii, nilibaini bilioni 6.8 zililipwa kutoka kwenye mfuko wa tozo ya maendeleo ya utalii bila idhini ya afisa masuuli kinyume na kanuni ya fedha. Pamoja na haya nilibaini matumizi ya jumla ya bilioni 16 yalifanyika bila kuwa na hati za malipo pia yalibainika matumizi ya bilioni 11 ambayo hayakuwa na nyaraka toshelezi na milioni 89 zilizotumiwa na makumbusho ya Taifa kwa matumizi yasiyoendana na shughuli za utalii.

Kwa maoni yangu mkurugenzi wa utalii na mhasibu waliokuwa wanahusika walitumia vibaya fedha za tozo ya utalii jumla ya Tshs Bilioni 34
Sijui yule rais wa wanyonge alikuwa anafanya nini na mtandao wake wa wasukuma nchi nzima.
 
Kazi ya CAG ni kusema

Wanaopokea report zao ni kama vile wanafunzi wanavyopokea majibu ya mtihani wao wa mwisho wa mwaka. Wapo wa kupata A, B, C, D......
Na wapo wakupata Z sio F ........ Afanaleki nipo kwenye taharuki kubwa yaani 18Bn zinakusanywa then hazipelekwi benki doooh!
 
Kazi ya CAG ni kusema

Wanaopokea report zao ni kama vile wanafunzi wanavyopokea majibu ya mtihani wao wa mwisho wa mwaka. Wapo wa kupata A, B, C, D......
Tatizo ni kwamba either alikatazwa au alisahau kusema, na aliyejaribu kusema alijikuta hana huo U-CAG

Ndio maana jamaa akauliza haya yanayosemwa leo yalitokea lini (sababu kwa alivyokuwa kimya majuzi unaweza ukasema yametokea jana)
 
Back
Top Bottom