CAG: Uwanja wa Ndege Chato ni mradi usio na faida

CAG: Uwanja wa Ndege Chato ni mradi usio na faida

Kipindi kile alisemaje ?

Kama kipindi kile alikaa kimya kwa kuogopa Mamlaka tunajuaje kama kipindi hiki asemi kila anachotakiwa kusema ili mradi tu kuridhisha mamlaka ?

Hii nchi unafiki mwingi sana kwamba ingebidi aombe wananchi msamaha na ajiondoe kwenye hio kazi sababu inaonyesha ni bendera fuata upepo
CAG aliwekwa afiche ukweli
 
Hiyo ni imani yako hakuna mtu mwenye haki ya kukufanya usiamni unacho kiamini.

Ila ukweli jiwe aliharibu sana maisha ya watanzania na kutumia hivyo fedha za umma.
Jiwe ni Rais wa nchi gani sasa hivi..., takuwa chizi kupigana na Mizimu au kutetea mizumi au kusema kwamba ni sawa upuuzi sasa ufanyike sababu marehemu fulani alifanya...., keeping in mind anayetetewa alikuwa ni part ya huo huo so called uharibifu uliofanyika huko nyuma...

Hence narudia ninachosema mimi sio mfuasi wa binadamu yoyote bali ni mtu mwenye fikra huru na raia wa hii nchi, na kama mlipa kodi nina stake katika matumizi ya hio kodi.... (sishambulii personalities bali issues)
 
Tulisema tukaitwa wapinzani tuna wivu.

Sasa wenye mamlaka wa kusema wamesema.

.https://www.instagram.com/p/CcUyVOhtBIe/?igshid=YmMyMTA2M2Y=
Screenshot_20220414-145349.jpg
 
Tulisema tukaitwa wapinzani tuna wivu.

Sasa wenye mamlaka wa kusema wamesema.

.https://www.instagram.com/p/CcUyVOhtBIe/?igshid=YmMyMTA2M2Y=
Legacy ya dikteta inazidi kuyeyuka!!

Sukuma gang Kwisha habari yao
 
Hivi uwanja wa ndege wa Chato unatofauti gani na Uwanja wa Ndege wa Musoma unaojengwa? Au wa Mtwara? Hizo faida anazotaka CAG ni zipi? Zionekane baada ya mda fani? Maana nina hakika ata ujenzi wa terminal 3 Mwaimu Nyerere bado hatujaanza kupata faida

Sent using Jamii Forums mobile app
Wazee wakutetea mfu mshafika
 
Waliambiwa wakawa wanakomaa vichwa ooh mwacheni afanye kazi sasa mikazi yenyewe ndio hiyoooo ya hovyo, walikua wakiambiwa kitu wanakua wakali kweli kweli kuliko pili pili kichaa. Sasa wanaanza tarrrrrrrrrrtiiiiibuuuuu kuukubali ukweli.
 
Afadhali uwanja upo hata mkisema mpaka mapovu yawatoke ni sawa tu maana Geita utabaki uwanja wao! Ile sehemu mmepora madini sasa hivi kumebaki maandaki maana hata mchanga umabebwa, no replacement!
Madini mliobebea yakiisha siku moja tutapata watalii watakaokuja kutembelea mashimo waliochimba Geita!
Madini yameporwa na Nani? Kuwa muwazi tu kuwa CCM ndo waporaji, kwa nini uzunguke mbuyu?
 
Bomoeni mpeleke nyumbani kwenu kupiga kelele hakuwasaudii .
Wajinga ni watu na watu ni ninyi.
Mjinga anayeenda kuweka kitu mahali kisipohitajika wakati kulikuwa na mambo msululu ambayo yangewasaidia watu wa Chato.
 
Pendezesha kwenu kwa kujenga vitu vitakavyo tumika na watu wote, pia vitakavyo kuwa na faida. Sasa huo uwanja wa ndege una faida gani ikiwa kwa mwezi unaingiza watu wachache hivyo? Angejenga barabara labda. Sasa ona hasara hiyo kubwa
Sasa hivi uwanja wa ndege kila inapofika July, August, September, tunautumia kuanikia mpunga na mihogo.
 
CAG kwa hili sijui kama yuko sahihi Mapori yaliyoko Kule mijambazi ya Rwanda na Burundi ilikuwa inasumbua sana

Magufuli akatangaza kuwa yale maeneo ni mbuga za taifa sababu kuonekana mbugani kama sio mtalii unapigwa risasi .umefuata nini mbugani

Kwa kuanzisha mbuga akawa kakomesha utekwaji magari na mabasi kwenye yale Mapori sababu majambazi wanyarwanda na warundi walijikatia mapori yale wengine wakaanzisha hadi mashule na vituo vya ujambazi .Tatizo hilolimekuweko Serikali zote Magufuli Ndie alibadilisha hiyo hali

Tatizo Serikalini coordination hamna kilichotakiwa ni wizara zote kushirikiana ku push agenda ya utalii kule ili uwanja uwe active
Lakini pia Jeshi huo uwanja ungewasaidia!!

Sasa tuchukulie mfano Serikali iseme hauna faida ufungwe wanatakaje na zile mbuga zifungwe wanyama warudishwe walikotoka na mapori yale waachiwe Majambazi wa kinyarwanda na kirundi waendelee kuteka mabasi na magari na Kuua raia?

Anyway huo ni uamuzi wa Serikali

Ila Nadhani siku ingine CAG akifanya ukaguzi ni vizuri kupata information za kutosha zaidi ya hizo za profit and loss
Yaan wewe kil.AZA huwe na akili kuliko CAG?! kumbuka pia huyo CAG Ni chaguo la Jiwe
 
Kwa elimu kidodo tu kuhusu uwanja wa choto ni kwamba kama ukikamilika kwa aslimia [emoji817] basi ndo utakua uwanja mkubwa na borq kuliko viwanja vyote vya ndege Tanzania ,Uwanja wa ndege was Mwalimu Nyerere upo nyuma kwa ubora ,Ndege kubwa yoyote kutoka popote Duniani kwenye huo uwanja inatua.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilicheka sana siku ambapo Prof. Mussa Assad alipoulizwa ghafla kama kweli kuna upotevu wa ile Trillion 1.5! Kiufupi
alijibu kwa wepesi tu "Hapana Mweshimiwa Rais" [emoji51][emoji51][emoji51]

Na hapo hapo kwenye mitandao habari ndiyo ilikuwa inazunguzwa kweli kweli! Hakika yule Mzee alikuwa anaogopwa na wasaidizi wake mpaka basi.
Nakumbuka swali lilikuwa "Kuna trilioni 1.5 iliyo ibiwa,CAG akajibu hapana"hii ilikuwa "technical question and technical answer"
CAG hakuwahi kusema zimeibiwa 1.5trn bali hakuna viambatanisho vya matumizi ili ajiridhishe zilitumika kufanyia kitu gani!Raisi anaulizia pesa zilizoibiwa!
 
Back
Top Bottom