Carol Ndosi: Rais Samia aache kusisitiza kila mara kuwa yeye ni Rais mwanamke, haipendezi

Carol Ndosi: Rais Samia aache kusisitiza kila mara kuwa yeye ni Rais mwanamke, haipendezi

Leak

JF-Expert Member
Joined
Feb 22, 2012
Posts
52,916
Reaction score
43,505
Mwana harakati na Mjasiriamali carol Ndosi kupitia kipindi cha Joto Kali la Asubuhi TV-E ameweka wazi kukerwa kwake na kitendo cha Rais Samia kila anapopata nafasi kuongea na Watanzania basi lazima aseme kuwa yeye ni Rais mwanamke na yeye ni mwanamke. Amesema kuwa amekuwa akirudia mara kwa mara kila apatapo nafasi kuwa yeye ni mwanamke wakati kila mtanzania anajua kuwa yeye ni mwanamke.

Carol Ndosi anasema kuwa Rais Samia yeye ni Rais hapaswi kuendelea kujificha nyuma ya kimvuli cha uanamke kwani hilo si jambo zuri na haipendezi kwa Rais kuwa na hofu ya uanamke wake bali anatakiwa ajue watu wanamuamini kama Rais si kama mwanamke.

Amesema pengine Rais Samia anapitia mambo mengi kwenye chama chake au kwa watu wanaomzunguka kwa sababu ya uanamke wake lakini yeye kama Rais hatakiwi kuitumia kama ngao kwani yeye ni Rais na watu wanajua ni mwanamke hatakiwi kuwakumbusha watu, haipendezi.

Chanzo: TV-E/E-FM
 
Huyu mama iko wazi uwezo wa kuwa kiongozi wa nchi hana.

Kila hotuba yake yeye anatanguliza jinsia yake, kila hotuba atatangazia watu jinsia yake.

Miezi 7 sasa mila hotuba ni jinsia yake, kila akisimama lazima ataje jinsia yake. Hii ni ile kitaalam tunaita inferiority complex disorder, ni ugonjwa wa akili.

Huyu mama uwezo wa kua raia hana. Hilo liko wazi. Kuna mataahira yake yanataka apewe hadi 2030, tatizo uwezo hana.

Ukitaka kujua huyu mama hakuna kitu, ahutubie bila kusoma hutuba, unaweza kulia, vyote atakavyoviongea havina maana yoyote.

Hii nchi ina safari ndefu ya maendeleo.
 
Huku ndo Ku enjoy uhuru wa kukosoa.

Tumetoka mbali sana.

Samia anaweza kukosolewa na Carol Ndosi.

Wakati Magufuli hata Ayubu Rioba asingeweza kukosoa.

Great ..
Tujivunie nchi yetu kwa kweli..
Tumerudi kuwa civilised nation
 
Hata yeye hajui kitu,mwanamke hakuumbwa aongoze watu hata angekuwa yeye huyo Ndosi lazima angekuwa na wenge.miezi saba sasa inakatika still anathibitisha jinsia yake kwa wananchi kwani wao hao wananchi hawamjui mwanamke kwa kumtizama?avue nguo basi ili tufunge hesabu!!!

Hakuna mwanamke anayeweza kufanya kitu kwa 100% akaweza bila kumshirikisha mtu hii yote inatokana na uwezo wao mdogo wa kuhakiki mambo that's why anajificha nyuma ya pazia la jinsia yake.
 
Mwana harakati na Mjasiriamali carol Ndosi kupitia kipindi cha Joto Kali la Asubuhi TV-E ameweka wazi kukerwa kwake na kitendo cha Rais...
Inategemea context. Rais ameongea katika muktadha gani? Hata Sisi wanaume huwa tunapenda kuzungumzia jinsia zetu katika utendaji. Kwa mfano, mimi ni mwanaume siwezi.

Yote kwa yote, wanaume na wanawake tumeumbwa na Mungu kama binadamu sawa. Utofauti wa nafsi moja na nyingine upo hata miongoni mwa wanaume. Kuna wanaume hopeless kabisa na kuna wanaume vichwa. As well as wanawake wapo vichwa. Tuna Rais jasiri na imara. SHH.

Cc CarolNdosi.
 
Huku ndo Ku enjoy uhuru wa kukosoa.

Tumetoka mbali sana.

Samia anaweza kukosolewa na Carol Ndosi.

Wakati Magufuli hata Ayubu Rioba asingeweza kukosoa.

Great ..
Tujivunie nchi yetu kwa kweli..
Tumerudi kuwa civilised nation
Am i the only one feeling this is a lil harsh..

Sijui yani..

Mbona kama anamfokea Mama yetu?.
 
Back
Top Bottom