Uchaguzi 2020 CASE STUDY - Jimbo la Hai - Walitumia teknolojia gani kupata matokeo sahihi ya kila kituo ndani ya saa 8?

Uchaguzi 2020 CASE STUDY - Jimbo la Hai - Walitumia teknolojia gani kupata matokeo sahihi ya kila kituo ndani ya saa 8?

Maoni yangu nazani umeyaona kuhusiana na hili swala la mahakama na jumuiya za kimataifa....
Nimeyaona na nimekujibu kwa ulivyoona hapo juu.

Kwa sasa huwezi kupeleka tena kesi kwenye hiyo mahakama kama mtu binafsi au taasisi binafsi kwa sababu nchi imeshawithdraw declaration ya kuruhusu kesi zipelekwe mahakama hiyo na taasisi binafsi au mtu.
 
Mkuu nilidhani ungeleta hoja ambayo ni very objective kwa kutuambia jiografia ya Hai ipoje? Kuna umbali gani kutoka vituo vya kupigia kura na sehemu ya majumuisho, kwa kumbukumbu zangu wakati wa kusubiri matokeo msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Hai alisema kata ambayo ipo mbali kuliko zote jimboni hapo haizidi kilomita 30 umbali ambao hauzidi lisaa limoja mpaka kufika kituo cha majumuisho.

Halikadhalika, ilibidi utuambie mathematically (kwa takwimu zenu siyo za Tume) hali ya uhesabuji kura ilikuaje? Waliojiandikisha walikua wangapi, waliopiga kura wangapi, kura za Mbowe kwa kila kituo zilikua ngapi? Na za mpinzani wake zilikua ngapi? ili tujue hizo kura feki zilizoongezwa zilikua ngapi
Hapo mwisho umemaliza kabisa, huwezi kusema kulikuwa na kura feki wakazi hakuna kura zilizozidi idadi ya wapiga kura.
 
Hongera mkuu, wewe ni hodari wa matusi. Mimi si fani yangu hii, kwa hio kwa hili nakupa ushindi kama mlivopata ushindi wa kupora haki za watu hongereni mabingwa wa wizi!
Tatizo lenu ndio hilo, mnadhani kila mtu anayetoa mawazo yake tofauti na unavyotaka wewe kuwa ni ccm. Mimi ni mmoja wal wale wasio na vyama vya kushabikia ila kwenye haki nasema.
Utofauti wetu mkubwa ni kuwa wengine tunafikiria kwa akili zetu na sio maneno ya kujazana upepo.
Kama uliona wazo langu si zuri ungesma lako. Hadi sasa nashindwa kuelewa ni lipi ambalo nilili andika linaonyesha nimewapendelea ccm. Procedures za kupata haki kwa njia ya sheria zina eleweka na ndizo nilizo mshauri mtoa mada.
 
Hivi unajua kuwa waangalizi wa uchaguzi EAC wamesema ulikuwa huru na wa haki ?

Hivi unajua SADC pia wamesema uchaguzi ulikuwa huru na wa haki ?

Hivi unajua Tanzania pamoja na kesi ya Mtikila kuamuriwa kuwa Tanzania iruhusu mgombea binafsi mpaka sasa Tanzania haijatekeleza uamuzi huo ?

Hivi unajua Tanzania mpaka imeshajitoa law taasisi binafsi na mtu mmoja mmoja kupeleka kesi mahakama ya Africa ya haki za binadamu?

Hivi unajua sasa hivi Tanzania imetunga sheria inayozuia mtu kufungua shauri la katiba katika mahakama za ndani hapa nchini ?
Hao waangalizi kama tungekuwa tumeenda mahakama ya africa zingelazimika kufuata maamuzi yake
Serikali yetu ilikuwa one step ahead maan walikuwa wanajua kuwa mahakama za ndani zipo chini yake.ila mahakama za nje bado
Hapa kesi zingefunguliwa kwa kuangalia mikataba ya kimataifa ya haki za binadamu na demokrasia....
kwa mtazamo wangu kufika mahakama za kimataifa kuna njia nyingi na sio moja kama tungeamua .... mfano kwa petition
 
Hao waangalizi kama tungekuwa tumeenda mahakama ya africa zingelazimika kufuata maamuzi yake
Serikali yetu ilikuwa one step ahead maan walikuwa wanajua kuwa mahakama za ndani zipo chini yake.ila mahakama za nje bado
Hapa kesi zingefunguliwa kwa kuangalia mikataba ya kimataifa ya haki za binadamu na demokrasia....
kwa mtazamo wangu kufika mahakama za kimataifa kuna njia nyingi na sio moja kama tungeamua .... mfano kwa petition
Mkuu hivi unaufahamu walau kidogo wa sheria na katiba ?
 
Tusiwalaumu viongozi wa upinzani these guys are heroes beyond imagination
Ni kwel Mkuu ila muda mwingine ni kama hizi drama tumezichoka za tume huru tumezichoka...
 
Nimeyaona na nimekujibu kwa ulivyoona hapo juu.

Kwa sasa huwezi kupeleka tena kesi kwenye hiyo mahakama kama mtu binafsi au taasisi binafsi kwa sababu nchi imeshawithdraw declaration ya kuruhusu kesi zipelekwe mahakama hiyo na taasisi binafsi au mtu.
Serikali yetu ilitupiga changara macho...
Kupitishwa kwa hii sheria ni moja ya viashiria kwamba uchaguzi usingekuwa wa huru na haki...
 
Serikali yetu ilitupiga changara macho...
Kupitishwa kwa hii sheria ni moja ya viashiria kwamba uchaguzi usingekuwa wa huru na haki...
Serikali hii ni ya kidikteta siyo sheria hiyo tu karibu sheria zote zilizotungwa na bunge la 11 ni sheria kandamizi
 
Serikali hii ni ya kidikteta siyo sheria hiyo tu karibu sheria zote zilizotungwa na bunge la 11 ni sheria kandamizi
Na unakutana na mtu anasema anakwambia Serikali ya watu wanyonge...
 
Tusiwalaumu viongozi wa upinzani vita wanayoipigana ni nzito sana.

Hakuna mtanzania yoyote anaweza kuipigana ndiyo maana Lowassa na Sumaye walitepeta mapema tu.
Ni kweli kabisa Mkuu. Wamepitia misukosuko mingi sana. Bungeni, Kupigwa risasi mchana kweupe, Uraiani, Jimboni na hata kwenye Mahakama zetu.

Lakini bado wamesimama imara kututetea sisi Watz. Niwatie Moyo Ndugu zetu hawa kuwa Mungu wetu ni Mwaminifu na Hakika hatawacha hivi hivi. Iko Siku Mungu atawainua tu. Na Baraka za Mungu zitawale Kwao na Vizazi Vyao.
 
Ni kweli kabisa Mkuu. Wamepitia misukosuko mingi sana. Bungeni, Kupigwa risasi mchana kweupe, Uraiani, Jimboni na hata kwenye Mahakama zetu.

Lakini bado wamesimama imara kututetea sisi Watz. Niwatie Moyo Ndugu zetu hawa kuwa Mungu wetu ni Mwaminifu na Hakika hatawacha hivi hivi. Iko Siku Mungu atawainua tu. Na Baraka za Mungu zitawale Kwao na Vizazi Vyao.
Mungu atawainua pale wananchi tutakapoamua kuwatetea.

Uchaguzi huu wanafanyiwa ushenzi mkubwa na ni tusi kubwa sana kwa wananchi kuchagua mtu halafu anatangazwa mwingine.
 
Tusiwalaumu viongozi wa upinzani these guys are heroes beyond imagination
Heroes wakati wanatumia 330million *12 =3,960 million anakula mlevi wa konyagi na genge lake la wahuni. Kafanya nini kuendeleza chama? Mafisadi wakubwa.
 
Umeharibu pale ulipojitangaza kuwa Ni mwajiriwa wa Serikali. Acha kutuona wajinga.
 
Huyu ni mfanyakazi wa serikali aliye mzalendo! uzalendo wake uishie hapa kwa wengine kufuatilia na kuchukua hatua. Madracula wanyonya damu wakiongozwa na lile lizee la chato na kuratibiwa na kidracula kidogo chenye njaa ya damu kasabaya kanavizia kamfahamu kamtafune mzima mzima. Wee ndugu umemaliza kazi yako pumzika! wengine wafanye upande wao!

Duuu jamaa unajifariji sana mpaka unakuwa mjinga. Sasa uzalendo Wake Hapo uko wapi JF. Are you serious. Kama ndo aina ya wanachama hao walioshindwA ndo kama wewe Basi hata nyumba yako sijui inasalimikaje.
 
Duuu jamaa unajifariji sana mpaka unakuwa mjinga. Sasa uzalendo Wake Hapo uko wapi JF. Are you serious. Kama ndo aina ya wanachama hao walioshindwA ndo kama wewe Basi hata nyumba yako sijui inasalimikaje.
Niliwahi kujihusisha na opposition politics kuanzia mwaka 1995 hadi 2015 na nilikuwa natumia pesa sana kuhakikisha napiga kura na kushiriki kampeini kabla vitambulisho hivi havijaja ambavyo sikupata kwa vile ninaishi nje ya nchi. Kila wakati wa uchaguzi nilikuwa nakwenda nyumbani kupiga kura. Ila malalamiko yetu yote yalikuwa ni yale yale hata pale ilipokuwa wazi kuwa hatukuwa na reach kubwa tulikuwa tulidai tumeiwbiwa kura. Tulikuwa tunapata kure nyingi mijini lakini siyo vijijini
 
Back
Top Bottom