Catherine Ruge: Rais Samia anawanyima Wazanzibar wenzake fursa ya kuwa nchi yenye Mamlaka kamili

Catherine Ruge: Rais Samia anawanyima Wazanzibar wenzake fursa ya kuwa nchi yenye Mamlaka kamili

Historia hata iweje.....

Suala ni je TANZANIA YA MUUNGANO haina faida kwa WATU WA BARA NA ZANZIBAR?!!!!

Ukitaka kufukua makaburi utayafukua mpaka ya wahindi wekundu kuidai AMERIKA YAO.....
Muungano umepitwa na wakati. Tanganyika irudi na Zanzibar ijitegemee na mambo yake
 
Muungano umepitwa na wakati. Tanganyika irudi na Zanzibar ijitegemee na mambo yake
Muungano ni kama NDOA YA WAZAZI WAKO iliyofungwa kabla ya wewe kuzaliwa.....

Hauhojiki KUPITILIZA....
Hauvunjwi......
Hauvunjiki......

Hapa "UAMSHO" wanaweza kutupa funzo kubwa......

#KaziIendelee
 
"Niko Unguja na Wazanzibari wanamwambia Mama Samia "Kitendo cha yeye Kuzuia madai ya Katiba Mpya ni kuwanyima Wazanzibari fursa ya kuwa nchi yenye Mamlaka kamili, wanamkumbusha kuwa yeye kama mzanzibari anatakiwa alinde Maslahi ya Zanzibar asilewe Madaraka"-CPA Catherine Ruge

Na huyu ni kiongozi? Kwa hiyo kila anayepata nafasi badala ya kuangalia maslahi ya nchi angalie maslahi ya alikotoka! Hii inajikumbusha kisa kimoja; Kuna watu walitaka kutandaza lami Butiama yote Mwalimu Nyerere alipokuwa Rais, akawauliiza, "Mkiweka lami hadi kijijini kwangu na vijiji vingine vya Watanzania mtaweka?" Kimya! Lami haikuwekwa.

Sasa kuna katabia kamejitokeza kwa baadhi ya viongozi wa MWENDOKASI hawajui integrity katka uongozi hupimwa kwa kuangalia vitu vingi. Kwa hiyo tunataka Rais Samia aangalie maslahi ya Zanzibar badala ya Tanzania? Tutafika kweli kwa fikra hizi? Hawa ndiyo vijana wenzetu wanaotaka kuongoza nchi? Hivi kina Mwalimu Nyerere wangekuwa wabinafsi enzi za ujana wao tungeikuta Tanzania moja au tungekuta tuna Marais hadi wa Ukoo kama Somalia?Tuache hizi fikra za aibu.
 
Mwafrica mbele ya maslahi yake yupo tayari kuua hata ndugu zake ili yeye aendelee kufaidi keki ya taifa.
 
"Niko Unguja na Wazanzibari wanamwambia Mama Samia "Kitendo cha yeye Kuzuia madai ya Katiba Mpya ni kuwanyima Wazanzibari fursa ya kuwa nchi yenye Mamlaka kamili, wanamkumbusha kuwa yeye kama mzanzibari anatakiwa alinde Maslahi ya Zanzibar asilewe Madaraka"-CPA Catherine Ruge

Kwa sababu ni Mzizibar basi hawapendelee Wazanzibar wenzake Pro-Chadema mnaona sawa sababu atakuwa anawafurahisha. Sasa kwa nini mlikuwa mnapiga kelele kuwa Chato inapendelewa.
 
Mama Samia asipokuwa mwangalifu hao CCMwanaweza kumshinikiza aanze kurithi mienendo ya mtangulizi wake.
 
Huyo pimbi aambiwe Rais hayupo hapa kugawanyisha fito,asubirie TL na Mbowe wakiwa Marais ndio wafanye huo ujinga wake.
 
Halafu akilinda maslahi ya Zanzibar atalaumiwa kama JPM kwa "ukanda/ukabila."

Dear Chadema, jitahidini kufahamu vipaumbele vya Watanzania kisha muwe kipazasauti cha vipaumbele hivyo. Kadhalika, jibidiisheni kusoma upepo wa kisiasa ulivyo. Mama Samia anapendwa na Watanzania, pengine kutokana na kuwa Rais wa kwanza mwanamke. Lakini pia anaongea lugha ya kistaarabu. Sasa mkicheza ovyo karata zenu, mtaishia kuonekana mnam-bully.

Mwisho, mjibidiishe kuwa proactive. Anzisheni mijadala itakayowafanya Watanzania wafanye tafakuri badala ya sasa ambapo mnaendeshwa kwa matukio. Mnasubiri Mama Samia atamke hili au lile mpate cha kuongea.

Povu ruksa [emoji4]
Wewe ni takataka tu

Ajenda zote anazosimamia Samia ni za chadema ufahamu ilo?

Kama ufahamu tafuta clip za lissu akigombea urais 2020.

Tatizo unajifanya mpumbavu wakati ni mjinga!!

Hoja ya katiba pia sio ya watanzania?

Mwaka 2013 wakati wanachi wanataka katiba walikuwa ni waburundi au wakenya?

Acha utoto hoja zote wanazosimamia chadema ni hoja za watanzania!!
 
Huu unzanzibari na utanganyika huu jmn, tukisema rais Samia ni mtanzania inatosha sio mambo ya muunguja sio mnini
 
Wazazibar tena wanabahati sana, washukuru hata kwa hii katiba, Mzanzibar anakuja kutawala wabara wala hakuna chokochoko, ila wa bara akienda kutawala huko hapo hapakaliki.

Hapalaliki
 
Haya ndio madhara ya kuokoteza watu barabarani na kuwapa Mic.

She does not have a clue about our country.

Jinge.r kabisa.
 
Historia hata iweje.....

Suala ni je TANZANIA YA MUUNGANO haina faida kwa WATU WA BARA NA ZANZIBAR?!!!!

Ukitaka kufukua makaburi utayafukua mpaka ya wahindi wekundu kuidai AMERIKA YAO.....
Umekua msemaji wa wahindi wekundu kuanzia lini?.
 
Wazazibar tena wanabahati sana, washukuru hata kwa hii katiba, Mzanzibar anakuja kutawala wabara wala hakuna chokochoko, ila wa bara akienda kutawala huko hapo hapakaliki.
Mbona Mh kule wanasema kazaliwa Bara huku ama?.
Si tumebadilishana😅
 
Back
Top Bottom