CCM ikiendelea kupuuza misingi ya uongozi ya Hayati Dkt. Magufuli, ni dhahiri watakosa kura 2025

Unaongelea slogan ya kutia watu kwenye viroba na kupoteza watu na kuwabambikizia kesi au ipi ?
Hapana mkuu, kuuwa, kudhurumu watu ni kosa kubwa mbele za Mungu na kwa watu wenye mfano wako, ila kuacha wezi na mafisadi yakiendelea kutesa maisha ya wengi ndio dhambi kubwa
 

 
Kalale naye kaburini, mpuuzi mkubwa.
Kwa mf, kwa tusi kubwa kama hili, mkuu umepata faida gani hapo??

Punguza ujinga kidogo kidogo ili ujione udhaifu wako mbele ya Kifo na roho ya mauti isivyokuwa na rafiki wala adui wote ni wa kwake, hata wewe ni rafiki mkubwa wa roho hiyo maiti
 
Ukiulizwa hao uliowataja wana kosa gani utaishia kujichomeka tu vidole puani...
Mfano mnyeti mko bize eti haiwezekani akawa tajiri ndani ya muda mfupi, mkibiwa oke thibitisheni kwa nini haiwezekani hamna ushahidi...
Ni chuki tu za wivu...
 
Mama kisiasa anacheza kwenye mikono hatari. Mswahili akiahidiwa fedha ya msaada na wazungu anaona hapo chini tu haoni mbali. Kwao maisha ni sasa hivi.
 
Mkuu unatok dunia gani?
Mwendazake ameondoka na hatarudi, mliofaidika pamoja na kina Polepole na Bashiru, enzi zenu ndo kalas.
Watu wameteswa
Watu wamedhulumiwa
Watu wamefukuzwa kazi eti vyeti feki(wakati mwenyewe ana Phd yenye utata)
Watu wamenyang'anywa mali zao
Watu wamebobolewa nyumba zao Kimara
Watu wamebambikwa kesi za uhujumu uchumi
Watu wameuwawa
Watu..........jaza mwenyewe!

Hizo ndo sera za CCM zilizo enziwa na Mwendazake!
Heri sasa tunapumua kama binadamu, siyo kuishi kama mashetani aliyoyashabikia Mwendazake.
 
Kuuwa na kuumiza watu bila kosa, ni upumbavu, ila kuacha wezi na mafisadi, wauza ngada wakiendelea kuuwa watu, kunyanyasa wajane ndio upumbavu zaidi
 
Mkuu, ni kweli usemacho, Kuuwa na kutesa watu bila kosa, ni jambo lisilovumilika kokote kule

Lakini kuacha majambazi, mafisadi, majizi na wauza ngada wakiendelea kutesa wengi, ni jambo lisilovumilka zaidi na ni kosa kubwa zaidi
 
Hatutaki kusikia habari za shetani
Tena ukimwita shetani ndio kabisaa hutaacha kumkumbuka, ni heri umwite binadamu

maana shetani amekuwepo duniani kabla ta mababu zako wote we pimbi
 
Onywanebhe
 
Shetani tunamkumbuka kila siku kama usemavyo lakini kwa kumlaani na kumuomba Mungu amuangamize kwenye moto wa jehanamu.
wewe ni duni mno
 
Mkuu, ni kweli usemacho, Kuuwa na kutesa watu bila kosa, ni jambo lisilovumilika kokote kule

Lakini kuacha majambazi, mafisadi, majizi na wauza ngada wakiendelea kutesa wengi, ni jambo lisilovumilka zaidi na ni kosa kubwa zaidi
Hizo side show za Mwendazake ndio zilimuondolea kabisa uhalalil wa kuwa Rais Bora nchini Tanzania.
Na hili tayari limeshaandikwa kwenye histiria.
Walioteswa, kudhulumiwa, kuuwawa, kubambikwa kesi, kutesa watu. kamwe HAWAWEZI kumsamehe Mwendazake hata kama kuna negative elements katika Taifa, elements ambazo watashughulikiwa kwa nguvu ya sheria.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…