Tetesi: CCM kufukuza Wanachama 11 wakiwemo Vigogo hawa 3

Tetesi: CCM kufukuza Wanachama 11 wakiwemo Vigogo hawa 3

Ukitaka kujua upinzani upo au haupo waambie ccm wawafukuze uanachama msukuma na bashe halafu uchaguzi uanze upya nakuhakikishia LUMUMBA WATAJAA
 
Taarifa kutoka chanzo cha ndani kabisa ndani ya CCM zinasema kwamba kuna uwezekano mkubwa katika Kikao kijacho cha CCM takribani Wanachama 11 wakafutiwa Uanachama ambapo ndani yao wapo Vigogo Watatu ambao ni Nape Nauye, Hussein Bashe na Msukuma.

Nape na Bashe wanafukuzwa baada ya kugundulika kuwa wanatumika na Chama cha Upinzani CHADEMA huku Msukuma anafukuzwa kwa kosa la kuwa mropokaji, mweneza chuki na mtu asiye mkweli kwa Wanachama wenzie.
Team Edo hao isipokuwa Nape......
 
Samahani brother naomba unisaidie ku share...!! naomba unisaidie ku share....
 
Magu asipoangalia atafukuza wanachama wote kisha atajifukuza na yeye mwenyewe. Kwa ambao hamjanielewa ni kwamba, chama ni wanachama. Sasa ukifukuza wanachama wote kutakuwa hakuna chama. Kwahiyo naye atakuwa amejifukuza toka ccm.
Wakati mnawafukuza Zitto, Arfi na wenzao wanachadema wote waliondoka? Mbowe alijifukuza?
 
Tunataka ccm mpya na Tanzania mpya! Ukweli kati hao aliowataja mtoa post ni wawili wako kundi la Lowasa, ila Nnape ni kuukosa uwaziri tu unamuuma sana. Napendekeza wawili watimuliwe mara moja!
 
Hivi nyakati hizi kuna upinzani mkubwa au kelele tu?
Ukiitishwa uchaguzi leo kubenea atarudi kweli?
Wanaofahamu maana ya upinzani wanajitahidi kuwabana wasipumue ili wananchi wasisikie ya upande wa pili. Kwa uwezo wako wa kufikiri omba tu utokee uchaguzi wa mjini kwa watu wanaojitambua ndio utaona nguvu ya pinzani.
 
Wanaofahamu maana ya upinzani wanajitahidi kuwabana wasipumue ili wananchi wasisikie ya upande wa pili. Kwa uwezo wako wa kufikiri omba tu utokee uchaguzi wa mjini kwa watu wanaojitambua ndio utaona nguvu ya pinzani.
wenzako wanaomba uchaguzi usitokee leo,wapo taabani mno
 
Natamani utokee uchaguzi wapambanishwe Kubenea Vs Paul tuone jinsi aibu itakavyofichwa bila mafanikio
 
Wakati mnawafukuza Zitto, Arfi na wenzao wanachadema wote waliondoka? Mbowe alijifukuza?
Yale yalikuwa maamuzi ya chama siyo ya mtu mmoja kama magu anavyofanya. Analeta chuki binafsi ndani ya chama chetu kikongwe. Kisa tu kwasabb hakupata uungwaji mkono ndani ya chama wakati wa uchaguzi
 
Back
Top Bottom