CCM, kwa mtaji wa ukakasi wa suala la Bandari, kaeni mguu sawa kung'olewa!

Kuna jamaa mmoja ni pro_Ccm ni mzee mtu mzima alituambia tutakufa wote hii Karne

CCM haito Toka madarakani hayo sio maneno yangu ni ya mzee mmoja Mwana CCM kindaki ndaki....
 
Tanzania ni nchi yetu, Watanzania ni watu wetu, CCM ni chama chetu, na wapiga kura ni kura zetu, huwezi kuiba kitu ambacho ni chako, ni unachukua tuu.
P
Uongoo wanaiba, na wanatangaza ushindi kwa CCM, usidanganye hapa akati iko wazi kabisaa.
 
Kuing'oa ccm madarakani ni ndoto za mchana ama ni kauli za kujipa moyo tu.

Kama kweli suala la DP World limewagusa njia sahihi ya kupambana na Hilo ni kutunga katiba mpya. Vinginevyo ccm itaendelea kuwepo.
Suala, ndugu yangu, siyo Katiba. Funguka. Kwani Katiba na sheria zilizopo zinafuatwa na Serikali iliyopo madarakani? Mwamko wa wananchi wa Tanzania kwa kiasi kikubwa ni duni. Hakuna mwanasiasa ambaye ameweza kuwaamsha ndiyo maana kura zao zinaibiwa, vyombo vya usalama vinawanyanyasa wao wanaridhika.Je huu ndiyo uhuru tuliodai? Waliodai Uhuru wamezeeka. Wengi vijana waliopo sasa hawana habari, wanajali kutesa kwa zamu na siyo mstakabali wa Tanzania! Hilo ndiyo tatizo enyi wanasheria mnaopotezea hoja kwenye Katiba.
 
Ukakasi ni mkubwa sana...

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Ni kweli kuna msemo kuwa ukubwa na nguvu za tembo pia ndiyo udhaifu wake ulipo. Shuhudia tembo akizama kwenye matope. Kila akitumia nguvu zake kujikwamua ndivyo anavyodidimia. CCM ichukue hadhari.
Umenena mkuu!
 
Mkuu Jidu, Jidu La Mabambasi , usiwe na shaka yoyote na Watanzania ni watu poa, hata uwafanyie nini, ukifika muda wa kuchagua ni kile kile chetu chama numberi uno!.
P
Mkuu Pascal Mayalla hili suala la Bandari limeibua hisia tofauti.
Kwa mara ya kwanza wapinzani wa kisiasa vyama tofauti pamoja na walio chama tawala wenye kupinga mkataba huu usioeleweka wameungana kuwa kitu kimoja-kupinga huu mkatba.
Shida kubwa waliondani ya chama tawala hawalioni hili kuwa ni basis ya kukingoa cham kwenye uchaguzi wa 2025.
 
Kuing'oa ccm madarakani ni ndoto za mchana ama ni kauli za kujipa moyo tu.

Kama kweli suala la DP World limewagusa njia sahihi ya kupambana na Hilo ni kutunga katiba mpya. Vinginevyo ccm itaendelea kuwepo.
Bahati mbaya iliyoje ni kwamba maamuzi ya either katiba mpya itungwe ama isitungwe yako mikononi mwa hao hao wafanya madudu
 
Hapa CCM iisaidie nchi, maama naliona kama suala ambalo pia limeamsha U Tanganyika na U Zanzibar, jambo hili nalo ni hatari.
 
Uing'oe CCM, umlete nani?.
P
 
Vijana kama mnabeti endeleeni kubeti, kama mnashabikia Simba na Yanga endeleeni, kama ni kuchakata papuchi endeleeni, kama ni stori za kwenye vijiwe vya kahawa endeleeni lakini ndoto ya kuitoa ccm madarakani bado sana. Kuitoa ccm madarakani inahitaji michakato mingi,mirefu na migumu sana. Lamda Msaidiwe na walinda mipaka na wao watakapo wachoka
 
Pengine inawezekana hujasoma political science.
Chama huwa ni cha watu, na chama hicho kama kinatawala, ndio kinawapa serikali nini kifanyike kimipango na kiutekelezaji ili chama na nchi inufaike.

Sasa chama kikijialienate, kikawa chama dola, kinatekeleza matakwa ya dola, kiuhalisia chama kinakuwa hakina tofauti na idara ya serikali.

Hapo kama wananchi wanajielewa na kuna demokraia, kuanguka is a matter of time.

Wapi KANU ya Kenya, UNIP ya Zambia, MCP ya Malawi?

Bottom line, CCM ina mtaji gani kisiasa katika ukodishaji wa Bandari?
 
Time and generation can sort out everything chukua vijana wenye miaka 30 kurudi chini waulize ccm na andazi unachagua nini atakujibu ngoja hichi kizazi cha kina wasira na warioba kiishe kuna siku tutaongea lugha moja.
 
Idadi ya watu wenye akili nzuri na safi ya kuweza kuing'oa CCM madarakani hapa Tz bado haitoshi, kwa hiyo usijidanganye.
 
Wang'olewe na chama gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…