CCM sasa tunaelewana, Chongolo amekubali mkataba DP World ulikuwa na makosa! Sasa tusonge mbele!

Nakubaliana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Chongolo kuwa Mkataba wa Bandari siyo MSAHAFU na ikiwezekana kama kuna mapungufu yasahihishwe.

Mimi nawashauri CCM wasione aibu hata kama mkataba ulikwisha sainiwa warudi kwa hao Waarabu na kuwapigia magoti kuhusu dosari zilizopo kwenye mkatabana zisahihishwe.

Suala hili la Bandari litakuja kuigharimu CCM wasipochukua tahadhari mapema. Ni jambo lisilopingika kuwa Mkataba una dosari na ni vema hizo dosari zikarekebishwa mapema.
 
Tupo Dubai tunatekeleza ushauri wako
 
Mkuu nipo huku namanyere,mwimbi,ulumi ndani huku nlishangaa watu wanasema huyu mama ameuza bandari zote

Nikaona nguvu ya social media coz hii issue haitangazwi kwenye redio kabsaa
 
Upo kazini kulaza akili za watu?

Huu ujinga wa CCM sasa umefikia mwisho

Mmeburuza watu muda mrefu sasa, hatimaye muda wenu umefikia kikomo.

Hata mfanye nini, safari hii hamponi na kubaki na uozo uleule uliomo ndani ya chama hiki.
Dawa pekee inayoweza kuwaponya ni kuitikisa CCM ndani kwa ndani na kutupilia mbali uozo uliomo ndani ya chama.
Hii ni kazi kubwa a ngumu, lakini bila kuifanya, mwisho wenu umewadia.
 
Dhamira ya mkataba haikuwa nzuri na hilo lipo wazi,
Kulekebisha ili kuendelea na muwekezaji huyo huyo si jambo zuri pia,
Mkataba usiwepo kabisaaa kama ni muwekezaji awe mwingine..
Unarekebisha kitu/jambo lililokosewa kwa bahati mbaya au kwa kutojua.

Utarekebishaje kitu ambacho kilifanywa kwa udanganyifu toka mwanzo?

Utaondoa vipi dhamira ya udanganyifu iliyokusudiwa toka mwanzo?
 
etc na si kina MSANDO wachumia Tumbo ambaye amezoea kusaini mikataba ya kupiga show za giggy money na Mapromota mkataba wa page moja tu.

Halafu Afrika aisee hakunaga scandal, ndio maana hatupati viongozi bora

Unafanya uchafu kesho kutwa watu wamesahau. Mtu ambae jina lake linakukumbusha clip ya kumchoma vidole Giggy Money ndani ya kibasi

RAIS unaejiheshimu na unaeheshimu Wananchi wako unampaje mtu kama huyu taadhima ya kuongoza wananchi kama Mkuu wa Wilaya ? Keshokutwa utasikia Mkuu wa Mkoa

Kijamaa nacho kinadhani wote tumesahau kwamba ni kichafu na kijinga, kinapata ujasiri wa kusimama mbele ya Watanzania kuongelea issue ya kitaifa ya bandari
 
Wishful thinking. Pipedreaming. Ni hadithi ya fisi kunyemelea mkono wa binadamu akifikiri utadondoka. The cup is half full tuendelee unaweza lusema pia the cup is half empty tuache.
 
Jidu la Mabambasi,
CCM walipoteza nafasi adhimu Tangu day one. Walichokomalia mpaka wakakataa kukiri kosa ni kudhani Kwa vile kulikuwa na saini ya Mwenyekiti wao akimwamuru Waziri Mbarawa asaini mkataba basi ingeonekana Mwenyekiti ni dhaifu. Kwa hiyo wakaamua kujitosa kama walivyo bila tahadhari yoyote. Miongoni mwa watu waliokuwa na hofu ya kasoro zilizomo kwenye mkataba ni Wasira, lakini Kwa unafiki akaahidiwa posho akasaliti nafsi yake na Watanganyika wenzake.
 
Kwa sasa nafikiri CCM wameona hofu ya wananchi.
 
Sijui kama huko CCM kwa sasa hivi kuna yeyote anayelitambua hili.
Nashangaa kidogo, sijui wewe hili umeliokota wapi mkuu, 'Jidu'?

Nina mashaka makubwa kama kweli unayaamini maneno yako hayo!
Mkuu soma tu alama za nyakati.
CCM na serikali kisiasa iko katika panic mode.
Ni vyema wakajisahihisha, kama Katibu Mkuu Chongolo anavyosema.
 
Wanatengeneza tatizo alafu Wanalitatua!Nyuma ya pazia hili lilipangwa wala si bahati mbaya!!
 
Na kama kutakuwa na mabadiliko kwenye huo mkataba ni lazima yawekwe wazi ili wananchi wakubaliane nayo na sio kufanya kisirisiri kama safari za nje anazofanya Samia!
Kweli kabisa maana hatuna wataalamu wazuri
 
Suala la bandari lingewekwa wazi tangu mwanzo na wananchi wakaelezwa juu ya faida ya kubinafsisha bandari na baadaye kikaundwa jopo la wataalam kujadiliana na Waarabu na tukatoka na mkataba mzuri na unaoeleweka.
 
Tutaendelea kubisha hivyohivyo hadi Mwenyekiti aongee. Sisi huwa tunasikiliza neno la Mwenyekiti.
 
Tanzania imeshindwa kesi ya makinikia yapigwa faini ya TShs Billion 800
Daadeki! Shamba la bibi kizee hili! Tusipokuwa waangalifu na kufuata utaratibu tutashtwakiwa; haya sasa.
bila kuwa na sheria inayoadhibu wanaosaini mikataba ya hovyo au kuisaini bila kuisoma kwanza, wachkliwe hatua za kisheria/nidhamu, itabidi bajeti za kila mwk ziwe na fungu la fidia ya mamikataba mabovu. mm naamini wanaosaini wanajua athari za hizo saini zao lakini tamaa za fedha zimetamalaki. ungeweza kupata a/c zao za mabenki ungejua kw nn nchi imefkishwa hapo na kw nn wazalendo wanateseka. mafixadi wanatutesa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…