LGE2024 CCM: TAMISEMI itambue demokrasia yetu ni changa, ipuuze makosa madogomadogo katika hatua ya rufaa uchaguzi Serikali za mitaa

LGE2024 CCM: TAMISEMI itambue demokrasia yetu ni changa, ipuuze makosa madogomadogo katika hatua ya rufaa uchaguzi Serikali za mitaa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
1731040513589.jpg
 
Wanajifanya hawahusiki,mbona hawajiulizi kwa nini wagombea wa CCM hakuna aliyekatwa?au wanamaanisha kuwa CCM ni Mungu asiyekosea?.
 
Sheria gani boss, au unadhani bado watu wako usingizini? Unataka kusema hizo hujuma za dhahiri ndio hizo sheria. Hivi huwa hambadiliki wakati watu wameshastuka nyie bado mnatumia mbinu za kizee kunajisi uchaguzi?
Sidhani kama kuna mbinu zaidi ya chadema kutafuta sababu na maigizo je wangesimama na mpango wao wa kususia uchaguzi mpaka katiba mpya unafikiri Ccm wangefanya uchaguzi bila kukaa na chadema ila ndani ya chadena kuna wenye chama ndio wanaamua na kifupi ccm itaendelea kuongoza kwa kura za chadema!
 
Hivi wale vijana wa ufipa waliokuwa wana shupaza shingo na hash tag ya "SAMIA YUKO WAPI" bado wanasikika huko mtaani kwako?
 
CCM: TAMISEMI IPUUZE MAKOSA MADOGO MADOGO, KUKUZA DEMOKRASIA .


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeiomba Wizara ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), kuwaelekeza wasimamizi Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kupuuza makosa madogo madogo yaliyotokea, ili kuruhusu wagombea wengi kushiriki uchaguzi huo.

Akizungumza na wahariri na waandishi waandamizi wa vyombo vya hahari nchini, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ametoa mfano wa makosa hayo yanayostahili kupuuzwa ni pamoja na wagombea kukosea herufi.

Kupitia mkutano huo uliofanyika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, leo Novemba 12, 2024, Balozi Nchimbi amesema ni vyema TAMISEMI ikaangalia uwezekano wa kuwarudisha wagombea wote walioenguliwa kutokana na makosa hayo madogo madogo ili kuhamasisha ukuaji wa demokrasia kwenye uchaguzi huo.

Aidha, kuhusu sehemu kubwa ya malalamiko mengi ya kuenguliwa kuonekana ni ya wagombea wa vyama vya upinzani, Balozi Nchimbi amewatoa shaka Watanzania kuwa, si kweli kwamba wagombea walioenguliwa ni wale wa vyama vya upinzani pekee, bali pia hata wagombea wa CCM wapo waliowekewa mapingamizi ya kugombea.

“Waziri wa TAMISEMI tunajua anafuata sheria, lakini ni muhimu kutambua demokrasia yetu hii bado ni changa hivyo tunahitaji muda wa kuendelea kujiífunza…tunaziomba mamlaka hasa TAMISEMI katika nyakati za mwisho za rufaa kuyapuuza makosa madogo madogo ili watu wengi wapate nafasi ya kugombea", alisema Dkt. Nchimbi.

#Ends
 

Attachments

  • VID-20241112-WA0309.mp4
    21.8 MB
CCM: TAMISEMI IPUUZE MAKOSA MADOGO MADOGO, KUKUZA DEMOKRASIA


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeiomba Wizara ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), kuwaelekeza wasimamizi Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kupuuza makosa madogo madogo yaliyotokea, ili kuruhusu wagombea wengi kushiriki uchaguzi huo.

Akizungumza na wahariri na waandishi waandamizi wa vyombo vya hahari nchini, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ametoa mfano wa makosa hayo yanayostahili kupuuzwa ni pamoja na wagombea kukosea herufi.

Kupitia mkutano huo uliofanyika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, leo Novemba 12, 2024, Balozi Nchimbi amesema ni vyema TAMISEMI ikaangalia uwezekano wa kuwarudisha wagombea wote walioenguliwa kutokana na makosa hayo madogo madogo ili kuhamasisha ukuaji wa demokrasia kwenye uchaguzi huo.

Aidha, kuhusu sehemu kubwa ya malalamiko mengi ya kuenguliwa kuonekana ni ya wagombea wa vyama vya upinzani, Balozi Nchimbi amewatoa shaka Watanzania kuwa, si kweli kwamba wagombea walioenguliwa ni wale wa vyama vya upinzani pekee, bali pia hata wagombea wa CCM wapo waliowekewa mapingamizi ya kugombea.

“Waziri wa TAMISEMI tunajua anafuata sheria, lakini ni muhimu kutambua demokrasia yetu hii bado ni changa hivyo tunahitaji muda wa kuendelea kujiífunza…tunaziomba mamlaka hasa TAMISEMI katika nyakati za mwisho za rufaa kuyapuuza makosa madogo madogo ili watu wengi wapate nafasi ya kugombea", alisema Dkt. Nchimbi.

#Ends
 

CCM: TAMISEMI IPUUZE MAKOSA MADOGO MADOGO, KUKUZA DEMOKRASIA

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeiomba Wizara ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), kuwaelekeza wasimamizi Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kupuuza makosa madogo madogo yaliyotokea, ili kuruhusu wagombea wengi kushiriki uchaguzi huo.

Akizungumza na wahariri na waandishi waandamizi wa vyombo vya hahari nchini, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ametoa mfano wa makosa hayo yanayostahili kupuuzwa ni pamoja na wagombea kukosea herufi.

Kupitia mkutano huo uliofanyika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, leo Novemba 12, 2024, Balozi Nchimbi amesema ni vyema TAMISEMI ikaangalia uwezekano wa kuwarudisha wagombea wote walioenguliwa kutokana na makosa hayo madogo madogo ili kuhamasisha ukuaji wa demokrasia kwenye uchaguzi huo.

Aidha, kuhusu sehemu kubwa ya malalamiko mengi ya kuenguliwa kuonekana ni ya wagombea wa vyama vya upinzani, Balozi Nchimbi amewatoa shaka Watanzania kuwa, si kweli kwamba wagombea walioenguliwa ni wale wa vyama vya upinzani pekee, bali pia hata wagombea wa CCM wapo waliowekewa mapingamizi ya kugombea.

“Waziri wa TAMISEMI tunajua anafuata sheria, lakini ni muhimu kutambua demokrasia yetu hii bado ni changa hivyo tunahitaji muda wa kuendelea kujiífunza…tunaziomba mamlaka hasa TAMISEMI katika nyakati za mwisho za rufaa kuyapuuza makosa madogo madogo ili watu wengi wapate nafasi ya kugombea", alisema Dkt. Nchimbi.
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2024-11-12 at 19.23.11.mp4
    21.8 MB
  • WhatsApp Image 2024-11-12 at 19.23.12.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-12 at 19.23.12.jpeg
    73.1 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2024-11-12 at 19.23.13.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-12 at 19.23.13.jpeg
    71.5 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2024-11-12 at 19.23.13 (1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-12 at 19.23.13 (1).jpeg
    90.6 KB · Views: 1
Sasa mtu anakosea herufi atawezaje kusaini nyaraka muhimu? Hao ndiyo wanatuletea wahamiaji haramu nchini .....anasain document bila kuisoma.
 
View attachment 3150555Ni Samia Tena na Demokrasia, Aagiza Wagombea Walioenguliwa kwa Makosa Madogomadogo Majina yao Yarudishwe

Na Joseph Bulebe, Dar es salaam

Rais Samia Suhuhu Hassan ameendelea kuonesha ulimwengu na watanzania kwa ujumla kuwa demokrasia ndo kitu cha msingi katika uongozi wake unaofuata utawala bora na demokrasia.

Katika hali ambayo haikutegemewa na wagombea wote waliokuwa wameenguliwa kisheria na wasimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa kwa makosa madogomadogo, Rais Samia ameamuagiza Waziri wa TAMISEMI, Mohammed Mchengelwa kuwarudisha wagombea wote walioenguliwa kwa makosa madogo madogo kama kukosea mwaka wa kuzaliwa, eneo analotoka, tarehe nk.

Akiongea leo na waadishi wa Habari, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Balozi Emmanuel Nchimbi amesema Rais Samia amemugiza kumwambia waziri wa TAMISEMI wagombea wenye makosa hayo warudishwe katika kinyanganyilo cha uchaguzi ili kulinda demokrasia changa inayokuwa katika nchi yetu.

Hii sio mara ya kwanza Mh Rais anaonesha ukomavu wa demokrasia nchini katika mambo ya siasa.

Mara tu baada ya kuingia madarakani Mh Rais aliruhusu mikutano ya siasa ya wazi iliyokuwa imekatazwa na mtangulizi wake.

Hakuishia hapo Mh Rais aliunda tume ambayo pamoja na mengine ilipendekeza kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi ambayo tayari imeundwa, kuondoa pingamizi ya zuio ya mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa ambalo nalo limeondolewa.

Mh Rais katika kuonesha demokrasia zaidi aliwaondolea kesi mbalimbali wapinzani mahakamani kama vile Mwenyekiti wa CHADEMA na makamu wake pamoja na kuwarudisha nchini wapinzani wote waliokuwa wamekimbia nchi kipindi cha awamu ya tano.

Kama hiyo haitoshi Rais amewakaribisha Ikulu Wapinzani na kuongea nao na chini ya utawala wake wapinzani wanaalikwa karibia kila tukio la kitaifa na dhifa mbalimbali za kitaifa.

Huyu ndo Rais Samia, Mwanamama wa kwanza katika nchi ya Tanzania na ukanda wa Afrika Mashariki anayeipeleka nchi ya Tanzania katika kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa kidemokrasia zaidi.

Kongole kwako Rais Samia kwa kulinda demokrasia nchini kwa hali na Mali sasa wagombea waliokuwa mmeenguliwa mkutane katika kampeini tarehe 20/11/2024.
Katafuteni wajinga wa hivyo. Mtengeneze tatizo wenyewe kisha mjifanye kulitatua wenyewe? Kujitekenya na kucheka wenyewe!
 

"Wapo Wanaccm waliowekewa mapingamizi, wapo wa ACT, wapo wa CHADEMA, na majibu ya mapingamizi yalitoka, lakini kwa hatua za rufaa kwa maelekezo ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi ambaye ni Rais wa Tanzania nilipofanya naye mazungumzo, ambacho tumekiona wapo wagombea wengi sana wa vyama mbalimbali ambao waliwekewa mapingamizi katika hatua za awali.

Katika maelekezo ya Mwenyekiti wa CCM, tumeelezana kuwa ni vizuri watu wapate nafasi, hivyo nitumie nafasi hii kutoa wito kwa waziri mwenye dhamana ya serikali za mitaa, tunatambua umefuata sheria lakini ni muhimu kukumbuka kwamba demokrasia yetu bado ni changa, ni muhimu tuzidi kukua.

Soma Pia:
Tunaziomba mamlaka hasa TAMISEMI, katika hatua ya mwisho za rufaa kuyapuuza makosa madogomadogo ili Watanzania wengi zaidi wapate nafasi ya kugombea. Yapo makosa makubwa, kwa mfano nafasi ni maalumu kwa wanawake lakini amejaza mwanaume"
Wote lao ni moja,hapo ni kutuhadaa tu wananchi,baba moya mama moya,.
 
CCM chama bora sana, kina usikivu na kinatatua changamoto za watu nchini.

Asante kwa kusikiliza na kutatua changamoto hii, haya hima tarehe 27 tukapige kura
 
Eti mwenyekiti wa ccm anaiomba wizara ya Tamisemi

...Tamisemi ni wizara iliyoko ndani ya Ofisi ya Raisi.

..sio wizara kamili kama Wizara ya Fedha, Mambo ya ndani, etc.

..kilichotokea ni Waziri wa Tamisemi kuiomba Tamisemi ....

..Nadhani MAKELELE yamekuwa mengi wanaona haya kuendelea na uchaguzi waliokuwa wamepanga.
 
Back
Top Bottom