Tetesi: CCM wanapita vyuoni kuorodhesha UVCCM waliokosa mkopo

Tetesi: CCM wanapita vyuoni kuorodhesha UVCCM waliokosa mkopo

Mwisho wa siku mtasema kwamba CCM imetoea maagizo kuhakikisha wanafunzi wote walio wanachama wa CCM hawatakiwi kupata supp..
Hahahaa sasa watoke vipi...maana agenda ya ufisadi waliizika siku nyingi...
 
Viongozi wa UVCCM wameagizwa na viongozi wa CCM kupita kila chuo kuorodhesha wanachuo waliokosa mkopo ambao ni wana chama wa CCM

Zoezi hili linafanyika kwa siri, ili wanafunzi wasio wanachama wa CCM wasijue kinachoendelea

Ili uorodheshwe unatakiwa uonyeshe kadi ya CCM na registration number ya chuo

Zoezi hili limeanza wiki iliyopita mpaka mwishoni mwa juma
Rafiki yangu wakaribu ambaye ni UVCCM ameniambia wamehakikishiwa watapata mkopo

Nikarejea waziri wa elimu alisema atatoa mkopo kwa mwanafunzi wasiozid 25, 000 na hadi sasa wametoa kwa wanachuo 20, 000 tu

Ndio nchi yetu ilipofikia hapa, licha ya bwana mkubwa kuhubiri usawa but he doesn't walk his talk

Vijana wenzangu ambao sio makaada wa CCM wakipolisikia hili walitaharuki na kuanza kutafuta kadi za CCM ilimradi tu wawepo kwenye orodha ya CCM inayoratibiwa Lumumba

Poleni ndugu wanachuo msio CCM...

uhalali wa hii serikali ya awamu ya tano unatia mashaka. Sina hakika kama CCM walishinda kwa kura halali mwaka 2015
 
Ukawa nunueni tu hizo kadi halafu mkiwa ndani ya uvccm ndiyo tutaimaliza vizuri ccm kwa kutengeneza migogoro isiyoisha
What is UKAWA? It not legally existent neither valid! Stop using that bad name!!
 
huyu je?
Habari hii ni kweli ila pia chumvi imejazwa uvccm wanaandikisha majina kwa watoto wenye kundi maalum waliokosa mkopo tena napinga kabsa swala la eti ili uandikwe lazima uwe na kadi ya ccm kuna vijana wameandika majina yao ni yatima tena hawajaulizwa suala la kadi
msikie huyu
Vijana wa Ufipa hv mbowe anawalipa shilingi ngapi kwa uongo wa namna hii hv leo ukipelekwa mahakamani unao ushahidi wa upuuzi ulioandika hapa ???? au unadhani kutumia fake id hapa unaweza kuandika chochote tu ukitakacho?? na siku msitu huu ukifyekwa sijuh mtajificha wapi tena.
jibu utapata. But kwenye bodi ya mikopo who is UVCCM?
 
Hakuna uhusiano katika kupata Mkopo na itikadi za kisiasa, Mkopo ni haki ya mhitaji anayestahili kulingana na vigezo.
 
Vijana wa Ufipa hv mbowe anawalipa shilingi ngapi kwa uongo wa namna hii hv leo ukipelekwa mahakamani unao ushahidi wa upuuzi ulioandika hapa ???? au unadhani kutumia fake id hapa unaweza kuandika chochote tu ukitakacho?? na siku msitu huu ukifyekwa sijuh mtajificha wapi tena.

Ebu taja jambo moja ccm waliwahi kukubali hata kama wangeshikwa red handed just one. Epa, Kagoda, Escrow, Meremeta, Buzwagi Safari za viongozi nje ya nchi n.k wewe kukataa kwamba siyo kweli na wewe unao ushahidi?
 
Wawaajiri kwanza UVCCM wanaosota mtaani tangu mwaka jana kwa kukosa ajira
 
Haiwezekani. Ni uongo mkubwa. Mimi niko ccm lakini sikupataga udhamimi enzi za Sumaye akiwa waziri mkuu.

Wakati huo utawala ulikuwa unaheshimu haki na sheria.

Sio utawala huu wa kibabaishaji.

Ngoja nami niende nikanunue kadi ya hili lichama naweza kupata mkopo, ili niweze kusoma degree yangu ya sociology.
 
Ccm Itashindwa Acha Ijichanganye Watu Wana Hasira Sana
 
Siamini uzi huu kama ni wa kweli.
Ni serikali gani ulimwenguni ambayo yaweza kuwabagua wananchi (wanafunzi) wake katika misingi ya vyama?Unapoenda Hospitali na kumkuta bwana mganga ama Daktari hakuulizi wewe ni wa chama gani kabla hajakutibu?
Huwa anatibu watu WOTE na wa vyama vyote.Maana alisomeshwa na SERKALI si CHAMA!
Labda ni Korea Kaskazini peke yake kuliko na ujinga huo!
Maana hili laweza kuwagawa watanzania VIBAYA SANA!
Siaamini kuwa Rais Magufuli anaweza kuinama (THAT LOW) yaani chini kiasi hicho na ATOE AGIZO ABAGUE na kusema wanafunzi wasio wana CCM WASIPATE mikopo.
Hapo sikubali!
Maana atakuwa amepoteza dira kabisa!
Ndiyo maana siamini.
Na kama wanafanya hivyo labda basi ni BEHIND his BACK yaani nyuma ya MGONGO wake ili kumpaka matope na kumchonganisha kati ya serikali yake na wananchi.
Huko ni kufikiria kwangu!
 
Back
Top Bottom