pye Chang shen
JF-Expert Member
- Jul 11, 2016
- 11,422
- 6,108
Kilaza mamakoAcha kutuletea utopolo wako wa Buguruni, kilaza mkubwa
Mimi napenda kukosoa pande zote bila kujali nakosoa CCM au upinzani. Kwa kuangalia mantiki na ukweli.Chanjo za COVID19 ni jambo la hiari duniani kote. Serikali haiwezi lazimisha wananchi kuchomwa chanjo kama hawataki. Wakifanya hivyo watakuwa wanakiuka na kuvunja haki za binadamu na dunia nzima itawageukia. Huyu ni mshauri mbaya na haufai.
Mbowe na elimu zake amefika wakati amepwaya sababu yeye asichukulie Ni mwelewa kuliko watanzania tulio baki. Akachanje familia yake ndipo aje kusema kwa niaba ya walio tayari na siyo wananchi. Akanywe mifaru John yake huko.Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeomba huduma ya utoaji chanjo ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19), iwe ya lazima badala ya hiari kama ilivyotangazwa na Serikali...
Wewe sio mtu wa kuandika sentence mbili kwenye jambo nyeti kama hili......hebu dadavua mwenyekiti ameharibu wapi......??Hapo wanaharibu.
Ni kweli. Siyo safari tu ila hata kadiri siku zinavyosonga mbele watu wataelewa somo. Kuna wengine mpaka waone mtu wa karibu kafa ndiyo wanajua hatari ya ugonjwa. Lakini kusema watu wachanjwe kwa lazima sio.Mdogo mdogo watazikubali tu, mtu akiwa na safari hapa hawezi kukwepa
Wee mzee umejitokeza tena kwa ile ID yako siyo? Udini utaakuua wewe mzee mzima hovyo!Chanjo za Corona zinaweza kuwa lazima kwa Chadema kwa sababu ni mwiko kuhoji wazo la Mwenyekiti ila sio watanzania wote.
Ukisoma huko mitandaoni, Hakuna anayemuunga mkono Mbowe......suala la Chanjo kila mtu afanye kwa utashi wake tu,ukipata dili kwenda nje utalazimika kuchanja tu,ila kama ni mtu wa Mwanza, Mbeya,Dodoma itakuwa ngumu, labda na private sector baadhi ya makampuni yaseme lazima kwa wafanyakaziTusubiri mwitikio wa wananchi
VIONGOZI WA CHADEMA TAIFA WAWE WA KWANZA KUPATA CHANJO NA TUONE PICHA ZAO NA VIDEO WAKICHOMWA.MBOWE AWE MSTARI WA MBELEChama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeomba huduma ya utoaji chanjo ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19), iwe ya lazima badala ya hiari kama ilivyotangazwa na Serikali..
Hapo wanaharibu.
Wakati chanjo hizi zinadaiwa kuleta madhara, si vema kulazimisha watu wachanje kwani usalama wa hizi chanjo teyari umeonyesha utata hata huko nje.Wewe sio mtu wa kuandika sentence mbili kwenye jambo nyeti kama hili......hebu dadavua mwenyekiti ameharibu wapi......??
Mbona WHO inainisha kuwa chanjo ni lazima na sio hiari....sasa kama rais Samia ameamua kufuata muongozo wa WHO kwanini anapingana na utaratibu huu......??
Wakati chanjo hizi zinadaiwa kuleta madhara, si vema kulazimisha watu wachanje kwani usalama wa hizi chanjo teyari umeonyesha utata hata huko nje.
Kweli kuna baadhi ya nchi chanjo imeleta madhara.....lakini uhiari wa kutoa chanjo hauoni kama itarudisha nyuma juhudi za serikali na umoja wa mataifa kupambana na janga hili....pamoja na kuitia hasara serikali kutokana ughali wa gharama za uagizaji hizo dawa.......???Wakati chanjo hizi zinadaiwa kuleta madhara, si vema kulazimisha watu wachanje kwani usalama wa hizi chanjo teyari umeonyesha utata hata huko nje.
Huyu ana zeeka vibaya sasaChama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeomba huduma ya utoaji chanjo ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19), iwe ya lazima badala ya hiari kama ilivyotangazwa na Serikali.
Wito huo umetolewa leo Jumatatu, tarehe 19 Julai 2021 na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe, akizungumza na wanahabari jijini Mwanza.
“Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, iweke utaratibu mzuri wa chanjo kuwa ya lazima kwa Watanzania,” amesema Mbowe.
Aidha, Mbowe ameitaka Serikali iongeze juhudi katika kutoa elimu kwa wananchi juu ya kujikinga na maambukizi ya COVID-19, kwa kuwa wengi hawachukui tahadhari dhidi ya janga hilo.
“Lakini public awareness (uelewa kwa umma) haiko, wala usifikiri Watanzania hawana akili, wamedanganywa hawajui washike la rais au la nani,” amesema Mbowe.
Mbowe ameongeza “ wameweka usugu hawaogopi Corona, wanafikiri ugonjwa huu wanaambukiza wachache.”
Wakati huo huo, Mbowe ameiomba Serikali iweke mkakati wa kutoa matibabu ya COVID-19 bure kwa wananchi, kwa kuwa wengi hawana uwezo wa kumudu gharama za matibabu.
“Kitu kikubwa hatujakijua ni gharama za matibabu, kimsingi gharama za COVID-19 ilipaswa kusimamiwa na Serikali kwa asilimia 100,” amesema Mbowe na kuongeza:
“Sababu janga limetengazwa la kidunia na Shirika la Afya Duniani (WHO). Serikali na nchi zake zinawajibika kuwatibu na kuwakinga wananchi.”
Serikali ya Tanzania, imesema imekamilisha muongozo wa kuingiza na kutoa chanjo ya COVID-19, na kwamba zitaingizwa nchini hivi karibuni.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi, alisema chanjo hiyo itatolewa bure kwa Wananchi watakaohitaji.
Mwanahalisi
Mbowe kapotoka hapa kuna makundi ya kuchanja binafsi na familia yangu hatupo
Wakawachanje wabibi na wababu huko na watu wenye Ukimwi na kisukari