Pasco.
NB. Kwa msisitizo: Pasco wa jf, sio mwanachama wa chama chochote cha siasa!, hajawahi kujiunga na chama chochote cha siasa, wala hana mpango wowote wa kujiunga na chama chochote, kwa lengo la lolote, bali ni political commentator, ambaye anazungumzia jambo lolote, kuhusu chama chochote. Sio mfuasi, mshabiki, wa kambi yoyote, au kiongozi yoyote, bali kama Mtanzania mwingine yoyote, kuna watu anaowakubali kijamii, kiuchumi na kisiasa, na siku ya kupiga kura, atapiga kura kuchagua kiongozi.
Mwanangu Paskali, poleni sana kwa kifo cha mpambanaji mwenzenu na hasa ambaye angekuwa ngome yenu kuu kwa Mzee wetu Lowasa ambaye wewe ni kambi yake ange wawezesha kuufikia ukuu wa nchi mliotamani sana mzee wetu Edo aupate, sinashaka nyuma ya kifo hiki kuna wachawi ambao wanaendelea kuwa loga. Kifo hiki cha kapteni wetu Komba kwa kweli ni pigo kuu kwa kambi yenu. Tangu Kapten aseme kama Edo anafaa zaidi aliandamwa na mikosi na hatimaye waxhawi walifanikiwa.
Pili mwanangu Je bado kambi yenu ina nguvu na hizo ndoto zitafikiwa? Naona kambi inayoungwa na mfalme na wengineo wanazidi kuwaporomosha, sasa inaonekana hakuna jiwe litakao salia juu ya lingine.
Au kwa maelezo niliyonukulu hapo juu na wewe umemtema? naomba nifahamishe hata kama siyo juu ya mada yako. Na kwa mada yako naona kama unampango wa kujiunga na CDM, binti mwanana ambaye wenye gere wamekuambia hafai lakini rohoni unapenda sana.