Elections 2015 CHADEMA ikipewa Nchi, Oktoba 2015, Hakuna Hatari Kugeuka Utawala wa Kidikteta? Nauliza Tuu!


Mwanangu Paskali, poleni sana kwa kifo cha mpambanaji mwenzenu na hasa ambaye angekuwa ngome yenu kuu kwa Mzee wetu Lowasa ambaye wewe ni kambi yake ange wawezesha kuufikia ukuu wa nchi mliotamani sana mzee wetu Edo aupate, sinashaka nyuma ya kifo hiki kuna wachawi ambao wanaendelea kuwa loga. Kifo hiki cha kapteni wetu Komba kwa kweli ni pigo kuu kwa kambi yenu. Tangu Kapten aseme kama Edo anafaa zaidi aliandamwa na mikosi na hatimaye waxhawi walifanikiwa.
Pili mwanangu Je bado kambi yenu ina nguvu na hizo ndoto zitafikiwa? Naona kambi inayoungwa na mfalme na wengineo wanazidi kuwaporomosha, sasa inaonekana hakuna jiwe litakao salia juu ya lingine.
Au kwa maelezo niliyonukulu hapo juu na wewe umemtema? naomba nifahamishe hata kama siyo juu ya mada yako. Na kwa mada yako naona kama unampango wa kujiunga na CDM, binti mwanana ambaye wenye gere wamekuambia hafai lakini rohoni unapenda sana.
 
PASCO NI MFUASI WA LOWASSA ZITTO NI MFUASI WA LOWASSA ZITTO kaachwa na CCM aadhibike kwa kuwa ni mfuasi wa lowassa
Haha...wanajifanya kutamani kuwa wacheza chess kwa akili za kasuku za kurudia kila sauti.Ndio maana wanarudia matusi.Ndivyo inavyokuwa kambi ya wapiga dili kichaa.Anytime wanaweza thurika kwa ukubwa wa dili wanazoziingia.
 
Pasco umetoka povu sana nchi yetu inhitaji viongozi wenye element za udiketa tusingwe wahi kusikia milion kumi za kununua mboga wala nyoka mwenye makengez wat cdm did whether is unconstitutional or nt let them do tanzania inahitaji viongozi kama haw wanareact mapema then it's over tuko nyuma sana hizi porojo za watu kama pasco ndo zinaidumaza hii nchi
 
Pasco
Kwa jinsi unavyojikanyaga, inaonekana umechomwa moyoni kwa uamuzi huu wa mahakama; na hitimisho lake kutoka CDM. Pole sana.
 
Mkuu MwanaHaki, kwanza asante kwa post hii, uzi huu unaelekea post 100, hii ndio posti ya kwanza kuijibu kwa sababu ndio post pekee iliyojikita kwenye subject matter!, na kufuatia post hii, nimeipeleka kule juu ili wenye kuhitaji kuujua ukweli, waujue ukweli, tuwaache hawa wajinga wajinga waendelee kupiga porojo!.

Asante.

Pasco
 
Pasco
ccm ipo madarakani na sasa ni zaidi ya miaka 30 je huu si udikteta????
 
Last edited by a moderator:
ITAUWA WATU WENGI SANA.
just imagine uwe na waziri kama sugu halafu ujifanye kumchimbachimba,kama hajatuma watu wakakunyonga ama kukupiga shaba.
lema awe waziri umletee vyoko,utaokotwa mtaloni minus your head.

Ulimboka, Mvungi, Prof. Mwaikusa, Kubenea, Abisolom, Mwangosi, Kombe, Muuza magazeti Morogoro, Mauwaji ya Arusha, Oparesheni Tokomeza watu badala ya Majangili ambao wengine ni viongozi ndani ya ccm na mengine mengi. Je Lema na Rais wa Mbeya (Sugu) ni mawaziri? Kenge we!
 

Sijasoma Katiba ya CHADEMA, ila nitaisoma. Tuwekee version zote mbili, ile ya awali, na hiyo mpya. Nataka kujua iwapo kweli usemayo yametokea, ili iwe changamoto kwetu sote!
 
You're killing me Pasco!

Kama unalala na kuamka ukidhani CHADEMA watakabidhiwa nchi hapo October 2015, utakuwa ni kati ya watu wenye daydream.

Kwa CHADEMA hii, haitatokea.

Sasa huu ndiyo udictator ............ Kwa hiyo CCM ikishindwa haitakabidhi nchi siyo? It will happen, whether this year, next year or 2020, it will happen!! The history never lied before!!
 

We Pasco utakuwa ni mburula mshika pembe!!!! Chama hakijakataa kuutambua uwepo wa mahakama na ndio sababu mzito kabwela akaacha kwanza aitafute haki mahakamani, baada ya mahakama kumpatia haki aliyostahili ndio na ufafanuzi juu ya katiba ya chama inavyoelekeza au kuagiza ulipotolewa na mwanasheria mkuu wa chama sasa huo udikteta uko wapi? Au unakumbusha Makonde alivyomzuia mzee Waryoba kutoa yake ya moyoni? Aibu kwenu msiokuwa na haya
 
Pamoja na wengi kucoment hakuna aliyejibu kwa hoja
ktk kile kilichoandikwa na Pasco mpaka sasa.
Ni dalili kilichowasilishwa kipo sahihi.
Badala ya kujibu hoja anashambuliwa aliyeleta hoja.
 
Last edited by a moderator:
wafuasi wa chadema wengi wao hawajitegemei kiakili,jambo ata liwe LA ukweli,ila kama linamuhusu Mbowe au Slaa wao mahaba mbele,Mbowe kadanga taifa kuwa anamkanda wa Bomu LA arusha kimya mpaka Leo,Mnyika nae ameacha kutumia akili,anawaza ataishi VP kwa anaojipendekeza
 
Udikteta una advantages zake pia. Kama umesoma histry vizuri ukiangalia mafanikio yaliyoletwa na Mussolin akiwa na Fascists, Hitler na Nazis wake. Only if ukipata patriotic leaders (dictator).
 
Msingi wa hoja yako Pasco kwamba Chadema ni chama cha kidikteta ni dhaifu kwasababu sababu zote unazotoa hujazitetea vizuri kuthibitisha ukweli wake.

Kwamba Chadema walibadilisha katiba pasipo maamuzi ya vikao halali vya chama, tukuulize wewe na msajili wa vyama mabadiliko hayo au katiba hiyo mpya ya Chadema ilikubaliwa vipi na ofisi ya msajili wa vyama. Mjadala wako juu ya hii hoja ungeonekana uko balanced kama ungejadili "role" ya ofisi ya msajili katika "uchakachuaji" huo wa katiba ya Chadema. Vinginevyo hoja yako inaonekana ina msukumo mkubwa wa hisia kuliko "facts".

Kwamba Chadema wanavunja katiba ya nchi kwa kukataza wanachama wake wasikishitaki chama, wewe mwenyewe kwenye hili andiko lako unaonekana unaelewa kwamba si kweli; maana umegusia kwamba wanachama wa Chadema wanaruhusiwa kukishtaki mahakamani chama. Habari ya mwanachama kufukuzwa kwa kukishtaki chama ina ukweli pale tu mwanachama anapokuwa ameshindwa katika hiyo kesi yake dhidi ya chama. Binafsi hapo sioni kama mtu unahitaji elimu ya sheria kuona kwamba katiba ya nchi haijavunjwa.

Hitimisho: kwenye kujadili hizi hoja Pasco "emotions" zako zimeonekana wazi zikizidiwa na "logic". Hasa leo; sijui matokeo ya mahakama hukuyapenda? Otherwise I still respect your ability to discuss issues. You are among the minority who often present "substance" here at JF. The gaffe didn't hurt too much, IN MY OPINION.
 
Mkuu ycam, kwanza asante kwa objectivity yako katika bandiko lako hili. Chama kikishapata usajili wa kudumu, kiko huru kubadilisha katiba yake wakati wowote kitakapotaka, Chadema hakikumweleza Msajili kuwa kinabadilisha katiba kuunda katiba mpya, bali kilitoa taarifa ya kufanya mabadiliko ya katiba yake. Kwa vile katiba ndio roho ya chama, kila kipengele kilichomo kwenye katiba husika, kiliwekwa kwa sababu. Logic ya kuwepo kwa kipengele kile ni kuzua usultani na uongozi wa kifalme ndani ya Chadema na kwa maoni yangu this is the essence ya jina la Chadema kuwa ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo.

Katika mabadiliko hayo ya 2006, kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Chadema, kwangu alikanusha kuwepo kwa kipengele hicho cha ukomo wa madaraka, rejea hapa Soma hapo kwenye bold. Kisha msome JJ. Mnyika hapa.
Nadhani unaweza ku compare na ku contrast.

Kwamba Chadema wanavunja katiba ya nchi kwa kukataza wanachama wake wasikishitaki chama, wewe mwenyewe kwenye hili andiko lako unaonekana unaelewa kwamba si kweli; maana umegusia kwamba wanachama wa Chadema wanaruhusiwa kukishtaki mahakamani chama. Habari ya mwanachama kufukuzwa kwa kukishtaki chama ina ukweli pale tu mwanachama anapokuwa ameshindwa katika hiyo kesi yake dhidi ya chama. Binafsi hapo sioni kama mtu unahitaji elimu ya sheria kuona kwamba katiba ya nchi haijavunjwa.

Hitimisho: kwenye kujadili hizi hoja Pasco "emotions" zako zimeonekana wazi zikizidiwa na "logic". Hasa leo; sijui matokeo ya mahakama hukuyapenda? Otherwise I still respect your ability to discuss issues. You are among the minority who often present "substance" here at JF. The gaffe didn't hurt too much, IN MY OPINION.[/QUOTE]
Demokrasia ndio msingi mkuu wa Chadema, ikiwa na maana pana zaidi ya kuheshimu haki na uhuru wa kutafuta haki popote kwa mujibu wa katiba!. Zuio hili ni la nini haswa?!.

Pasco.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…