Tetesi: CHADEMA kufutwa?

Tetesi: CHADEMA kufutwa?

Actually mfumo wa vyama vingi Africa upo kwa nguvu ya wahisani/mabeberu tu.

Hata mchakato halali ukifuatwa wa kufuta upinzani kwa maana ya bill bungeni hamuwezi hata kuzuia chochote.

You’re very right. Leo muswada wa kufuta vyama vingi ukipelekwa bungeni utapita kwa nderemo na vifijo. Ndipo Tanzania ilipofikia. Watanzania/Waafrika wamezoea kutawaliwa kidikteta. Nyerere na Mobutu katika enzi zao, kwa nyakati tofauti walilifafanua hili kwa media za Ulaya. Kwamba: “sisi Waafrika asili yetu ni kutawaliwa na chifu mmoja tu anayekabidhiwa dhamana kamili juu ya usalama na ustawi wa jamii. Sasa hii vyama vingi ni kama kuleta machifu wengi na kuwakanganya wananchi”!

Lakini 1992, Nyerere, akiwa nje ya madaraka ya urais na uenyekiti wa CCM, alikuwa mkweli na mhalisia (honest and realist) kwamba Watanzania wengi elimu na uelewa wao uko chini sana kiasi cha kutotanabahi umuhimu wa demokrasia na mfumo wa vyama vingi. Hivyo akaipiku (overrule) Tume ya Nyalali na kuwapa ushindi 20% waliotaka mfumo wa vyama vingi. Hii ni moja ya nyakati Nyerere alipoonyesha “statesmanship” ya hadhi yake. Ni wakati alipowakosoa viongozi wa CCM na serikali yake kwa kukumbatia “mabaya” ya utawala wake na kutupilia mbali “mazuri”.

Leo hii CCM na serikali yake wanaona ufahari kuongoza taifa lililojaa watu wenye uelewa finyu wa demokrasia, mfumo wa vyama vingi, utawala bora, na haki za binadamu. Watu waliojaa hofu kuhusu mustakabali wao kiuchumi na tishio la kunyanyaswa na vyombo vya dola. Lugha iliyoenea nchini ni kama ya North Korea. “Rais wetu mpendwa/kipenzi”; “kwa busara kuu za mheshimiwa ...”; Hata kurekebisha mitaro ya barabara za mitaani watu wanamlilia “Rais mpendwa”! Rais ndio anashukuriwa kwa kutoa pesa za miradi ya kitaifa na ya vitongoji. Bizarre! Bora tuachane na vyama vingi.

Hata upinzani nako hivyohivyo. Viongozi wanatajwa kwa namna ya kuabudiwa. Natambua mchango mkubwa na mhanga unaotolewa na CHADEMA kusimamia demokrasia Tanzania. Sina tatizo kabisa na Mbowe kuongoza muda mrefu. He has earned it. Aina ya siasa zinazofanywa nchini zinahitaji mtu aina ya Mbowe kuongoza upinzani. Lakini CHADEMA nao wazungumzie utekelezaji wa mipango na maamuzi ya taasisi zao kuliko kurejea maagizo na busara za mwenyekiti hata kama ni kitu kilekile. Mtindo wa kauli ni muhimu sana.
 
Ni kweli kabisa boss, ila ukweli tunaujua japo inatumika nguvu nje ya uhalisia kufikia hilo hitimisho lako.
Nashukuru sana kama mnaujua ukweli. Lakini Kumbuka hata CCM hapa ilipofika ilitumika nguvu kubwa sana kuibadilisha. Ni vigumu sana kubadilisha mazoea na imani ya mtu ambayo ameiwekeza sehemu kwa miaka, halfu utake kuibadilisha kwa siku moja. Ila taratibu tutaelewana tu.
 
Kuna taarifa zinasambaa kwenye magroup ya whatApp ya kuwepo mkakati wa kuifuta CHADEMA kabla ya uchaguzi mkuu mwaka huu.

Je, hizi taarifa ni kweli? Kama ni kweli nini malengo ya watu waliopanga ili jambo? hawaoni wanaiweka amani yetu mashakani?
Hata vikifutwa vyama vyote vya siasa , upinzani upo palepale.

Msitutishe
 
Mbona Chadema imeshajifuta yenyewe tu boss?
Sasa kama haipo hicho kihoro mlicho nacho chatoka wapi? Hao akina Lijualikali wanakisemaje chama ambacho hakipo. Huyo Mbatia mnayemtumia atawafikisha wapi? Kila siku mnasema Chadema kimekufa halafu kesho mnatuletea majina ya waliohama chadema kwenda CCM.
 
Hamna siku nitafurahi kama chadema ikifia mbali,nita nunua mbuzi utengenezwe mchemsho wa mombo na vinywaji vikali vyakutosha bila kusahau muziki mkubwa vijana wafurahi Hadi asubui.
 
Hapa dawa ni kurudi kwenye siasa ya Chama kimoja hakuna namna..ikiwa chadema haipo means upinzani haupo...
 
Mbona Chadema imeshajifuta yenyewe tu boss?
[/QUO
Lakini mbona inaandamwa sana? Kama CDM inajichimbia kaburi lake yenyewe, mbona CCM na dola wanang'ang'ania kuwanyang'anya CDM jembe/chepe wanalojichimbia nalo? Si waachwe mpaka wajifukie?
 
Kuna taarifa zinasambaa kwenye magroup ya whatApp ya kuwepo mkakati wa kuifuta CHADEMA kabla ya uchaguzi mkuu mwaka huu.

Je, hizi taarifa ni kweli? Kama ni kweli nini malengo ya watu waliopanga ili jambo? hawaoni wanaiweka amani yetu mashakani?
"Kikinuka, mtanitafuta sana na hamtanipata" - mwamba Mbowe.
 
CCM PEKEYAKE ISINGEWEZA MZIKI WA CHADEMA. NDIOMAANA WAMEIKOD NCCR. JE UONGO?
 
Msajili wa vyama anaweza asikifute kwenye usajili wa kisheria. Lakini wananchi wakakifuta kwenye mioyo yao. Na tayari wananchi hawana imani nacho.
Ulikaa wapi na wananchi wa nchi hii nzima walikokwambia wameichoka CDM? Ni ukweli usiopingika kwamba kuna shida ndani ya CDM lakino si ya kufikia kuchokwa na wananchi wenye ufahamu. CDM haikuwa makini kwenye kufanya vetting ya wagombea wao toka mwanzo ndio maana hatusikii makundi ya wanachama wakihama na hawa mamluki waliopenya ndani ya Chadema huko nyuma. CCM wasimame wao bila dola waone cha moto, kwani upinzani uko mioyoni mwa wananchi. Ndio maana leo CUF ikatekwa na CCM na ndani ya siku mbili tuu wanacuf wakaamka kuwa ACT Wazalendo na wala hawakurudi au kwenda CCM - jiulize ni kwa nini?
 
Back
Top Bottom