CHADEMA mkitaka kupata kura 2025 acheni kauli za chuki kwa JPM

CHADEMA mkitaka kupata kura 2025 acheni kauli za chuki kwa JPM

Sikumpa Lowassa kwa kumuamini, bali nilitoa kura kwa nafasi ya urais kwa mgombea wa upinzani ili kuifanya CDM kuwa na kura nyingi. Lakini ningesikitika sana kama kura yangu ndio ingeamua Lowassa kubwa rais.
Jibu ni Ndiyo ulimpa Lowasa! Kwanini kura yako uliipereka kwa mtu ambae humuamini? Unaamini sanduku la kura ni la majaribio?
 
Na ndio rais anayependwa na wananchi wake,ukibisha nenda kasome andiko la jamii forum Instagram kuhusu mbowe kumsema Vibaya JPM alafu usome moment za WANANCHI utajua nini ninachokimaanisha.
Kumbe Mitandao inatoa picha Sasa mbona awamu ya tano ilikua inashambuliwa Mitandaoni mkadai wananchi wapo field sio Twitter Wala Facebook!! Acheni unafiki.
 
Na ndio rais anayependwa na wananchi wake,ukibisha nenda kasome andiko la jamii forum Instagram kuhusu mbowe kumsema Vibaya JPM alafu usome moment za WANANCHI utajua nini ninachokimaanisha.
nani alimua ben sanane, anzory gwanda na wenzake ?
 
Nadhani CHADEMA kwa sasa wangeweka nguvu kwenye kupata madiwani wengi. Kwa nafasi ya urais wasisimamishe mgombea maana tayari mmiliki wa chama (Mbowe) anamuunga mkono mgombea urais wa CCM 2025, Mama Samia.
 
Sikumpa Lowassa kwa kumuamini, bali nilitoa kura kwa nafasi ya urais kwa mgombea wa upinzani ili kuifanya CDM kuwa na kura nyingi. Lakini ningesikitika sana kama kura yangu ndio ingeamua Lowassa kubwa rais.
Mkuu unacheza ngoma ya chawa wa Magufuli. They are enjoying that. Sure, Lowassa was a bad gamble for CHADEMA morally, but not “that bad” in TZ’s realpolitiks.

Acha chawa wa Magufuli na CCM waendelee kunadi hiyo karata ya Lowassa kinafiki. Hii ni nchi ya mafisadi na Lowassa siye mkuu wa mashetani.
 
Wewe si lolote kwa chadema mkuu hauna athari yeyote, jaribu kutenganisha chadema na mitazamo yako binafsi wewe kama wewe. Nakwambia hivyo kwa sababu kuna wakati mtu anapozungumzia jambo kuhusu Chadema kwamba imefanya hiki na kile ajabu unakuja wewe kusema mie sikutaka hivyo sijui sikuunga mkono, sasa inahusiana vp kwani wewe ni nani kwa Chadema?

Huenda hujui unachoongea, CDM sio robot, ni chama chenye watu. Sio lazima kila kinachopotishwa na chama kila mtu aridhie. Sasa unaponichanganya ukataka nitetee jambo nisikikubaliana nalo sijui unamaanisha nini?

Na kwa kukusaidia hapa ni kwenye mtandao wa kijamii na sio ofisi ya CDM au ndani ya vikao. Hivyo naweza kusema hivyo maana hapa niko kama mimi. Ukitaka utetezi wa aina hiyo usije hapa, nenda kwenye ofisi au vikao vya CDM ukapate majibu ya kitaasisi.
 
Wewe mmoja unamkata wenzio million 50 wanamkubali sasa ujioni kama ni tahira.

..hapana.

..madikteta hu-invest kwa kiwango kikubwa kwenye uongo na ulaghai na kuweza kuwachota akili wananchi wengi.

..kilichotokea ni kwamba uongo wa Jpm ulipewa nafasi kubwa ya kusikika na kutetewa kuliko ukweli.
 
Hao chadema washapigwa hadi bomu huko Arusha, huko Zanzibar cuf waliuliwa kama kuku hadi wakakimbilia huku. Unataka kutuaminisha upinzani umeanza kupata mateso kipindi cha Magufuli tu?

..je, ulisikia Jk au Bm wakijiweka karibu na matukio hayo? Au wateule wao wakiwakashifu na kuwazodoa wahanga wa matukio hayo?

..pia unyama na ukatili dhidi ya wapinzani chanzo chake kilikuwa amri ya Jpm kuzuia wapinzani kufanya shughuli zao.

..Na mambo hayo mabaya yalifanyika kwa kipindi kirefu bila Jpm kuchukua hatua kuyakomesha.
 
Kumbe Mitandao inatoa picha Sasa mbona awamu ya tano ilikua inashambuliwa Mitandaoni mkadai wananchi wapo field sio Twitter Wala Facebook!! Acheni unafiki.
Kwahiyo kwa kutizama mitaani na mitandaoni unaonaje mitazamo ya watu kuhusu Magufuli?
 
..je, ulisikia Jk au Bm wakijiweka karibu na matukio hayo? Au wateule wao wakiwakashifu na kuwazodoa wahanga wa matukio hayo?

..pia unyama na ukatili dhidi ya wapinzani chanzo chake kilikuwa amri ya Jpm kuzuia wapinzani kufanya shughuli zao.

..Na mambo hayo mabaya yalifanyika kwa kipindi kirefu bila Jpm kuchukua hatua kuyakomesha.
Sijui hata unaongea nini? Unakubali ni kweli kwamba wapinzani walipitia mateso toka hata awamu ya JK halafu unamsifia JK kwa kufanya huo unyama lakini hakuuzungumzia sijui kutokuonyesha kuhusika, sasa ndio nini?
 
Nimekuwa nikifuatilia posti nyingi hapa jamii forums zinazomuhusu aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, pia hata mitaani na kwenye vyanzo vingi vya habari ikitokea magufuli ametajwa na kiongozi yeyote kwa lengo la kumfedhehesha basi 90% ya watoa maoni watakuwa upande wa JPM.

Sasa rahi yangu kwa CHADEMA ni kwamba wanapaswa waelewe kwamba wananchi wa kawaida wao shida yao haikuwa demokrasia ila ni unafuu wa maisha, hivyo unaposimama jukwaani kumponda Magufuli na kumsifia Samia ukidhani unawafuraisha ni kujichimbia kaburi.

Nimefuatilia hotuba ya Mbowe ni wazi watu hawana imani nae tena si mtetezi wa wananchi tena na mbaya zaidi alipomsema vibaya JPM na kumsifia Samia wengi waliguna na kuonyesha wazi kuwa kalamba asali ya ikulu.

Tulishakubaliana mikutano ya siasa sio takwa la Rais lipo kikatiba inakuwaje tena mwenyekiti wa chama anamsifia Rais kuwa anamshukuru kwa kuruhusu, haki inadaiwa na haiombwi sasa wamekuwaje tena.

Nawasisitiza Magufuli mkimtumia vizuri kwenye sera zenu ndiye anaweza kuwapeleka Ikulu kwa sababu yeye alikuwa kipenzi cha wananchi.
nchi washike wasishike Yaani atatajwa sana hadi mpasuke,ndo kasababisha majanga yote haya lazima atumike kama reference
 
Huenda hujui unachoongea, CDM sio robot, ni chama chenye watu. Sio lazima kila kinachopotishwa na chama kila mtu aridhie. Sasa unaponichanganya ukataka nitetee jambo nisikikubaliana nalo sijui unamaanisha nini?

Na kwa kukusaidia hapa ni kwenye mtandao wa kijamii na sio ofisi ya CDM au ndani ya vikao. Hivyo naweza kusema hivyo maana hapa niko kama mimi. Ukitaka utetezi wa aina hiyo usije hapa, nenda kwenye ofisi au vikao vya CDM ukapate majibu ya kitaasisi.
Bado haujaelewa, hakuna mwenye kutaka ufafanuzi wa masuala ya kuhusu Chadema kutoka kwako. Kikubwa ni kwamba unataka kutetea maujinga ya chadema kwa kutumia misimamo yako binafsi, mtu akizungumzia issue ya Chadema na Lowassa wewe unakuja kusema haukukubaliana na ujio wa Lowassa Chadema, sasa nani kakuuliza kama ulikubali au haukukubali na hata usipokubali we ndio nani?
 
Sijui hata unaongea nini? Unakubali ni kweli kwamba wapinzani walipitia mateso toka hata awamu ya JK halafu unamsifia JK kwa kufanya huo unyama lakini hakuuzungumzia sijui kutokuonyesha kuhusika, sasa ndio nini?

..matukio wakati wa Bm na Jk yalikuwa machache kuliko ya wakati wa Jpm.

..matukio wakati wa Jpm yaliendelea kwa muda mrefu huku yakitetewa na watendaji wa Ccm, serikali, na Jpm mwenyewe.

..waliokuwa wakitenda matukio mabaya wakati wa Jpm walikuwa wakidai ni " amri kutoka juu " maana yake yaliyokuwa yakifanyika yalikuwa maelekezo ya Jpm.

..Jpm mwenyewe alitoka public na kumuelekeza Spika afukuze wabunge toka bungeni ili waje mtaani awashughulikie.

..Kama Jpm alikuwa haungi mkono dhuluma na ukatili dhidi ya wapinzani basi angekomesha mambo haya mara moja. Jpm alikuwa mtu wa kuchukua hatua za haraka.
 
Kwa Akili yako unaamini kuwa magufuli alimfuata azory Kumuua au unaishi kinadharia,taifa lolote lenye watu wanafiki hawawezi kupiga hatua, magufuli amuue azory Kwa lipi alilomkosea na lililokuwa linamadhara Kwa JPM.

..Na jaribio la kumuua Lissu una utetezi gani?
 
Back
Top Bottom