Uchaguzi 2020 CHADEMA na ACT-Wazalendo kufanya maandamano ya amani Nov 2, 2020 kupinga kuvurugwa kwa Uchaguzi Mkuu

Uchaguzi 2020 CHADEMA na ACT-Wazalendo kufanya maandamano ya amani Nov 2, 2020 kupinga kuvurugwa kwa Uchaguzi Mkuu

Victorie mama huwa sikuelewi kabisa unasimama upande gani? Ila kwa hili la maandamano tuko pamoja hawa viongozi baada ya kuona hawatopata posho za bunge wanadai haki, binafsi ningependa kesho wawe pamoja na watoto na wake zao barabarani tofouti na hapo waache sinema za ajabu kwa watanzania...

Jana mchana nimekutana na viongozi hawa maeneo ya Rose Garden, sugu a.k.a jongwe kachoka naona haamini kama hatokalia kiti chekundu

Unataka haya yaendelee?

IMG-20201022-WA0001.jpg
 
Chadema na ACT wanatakiwa kujua kuwa watanzania sio wapumbavu kiasi hicho kwamba waende barabarani kuandamana kwasababu ya kutetea ulaji wa wanasiasa.

Miaka yote chaguzi zinapo fanyika wapinzani hulalamika kuibiwa Kura lakini kwa kuwa walikuwa wanashinda ubunge na kuwa na uhakika na shibe ya matumbo yao walikuwa hawaoni umuhimu wa kuandamana na kudai haki.

Uchaguzi wa 2020 umekuwa tofauti kwao baada ya watanzania kuwanyima nafasi za kuingia bungeni kunufaika na Kodi zetu huku wakishinda kutwa kutukana na kususia vikao vya bunge na wakiti mwingine wakijifunga midomo ili wasichangie chochote bungeni ama kuanzisha fujo kwa makusudi(mkasahau kuwa wananchi ndio waajiri wenu). Leo ndio mmeona umuhimu wa kuandamana baada ya kukosa ajira ?

Ukweli ni kwamba watanzania hatuta andamana na hatuto tii amri zenu zozote.
Kumbukeni jinsi tulivyo kataa amri yenu ya kukaa kwenye vituo kulinda Kura basi mjue kuwa hata hili la kuandamana halito fanikiwa pia.

Kesho tutakwenda kwenye shughuli zetu za kutafuta ugali kwaajili ya watoto wetu na si kupigania ulaji wenu huku mkijificha kwenye kivuli Cha Demokrasia.

Demokrasia ni pamoja na kuheshimu maamuzi ya wapiga kura, hiyo Demokrasia mnayo itaka nyinyi ya lazima upinzani washinde kamwe haiwezi kukubalika kwetu.

Mwisho niseme tu kuwa tunawapuuza Kama tulivyopuuza agizo la kulinda Kura .

Andamaneni wenyewe na familia zenu zinazonufaika na mishara yenu ya kibunge Ila sisi msituhusishe.

Mwlm Nyerere alikuwa sahihi alipo sema hutuwezi kuwapa nchi CHADEMA
View attachment 1617409
Nmeupenda tu ushauri wa mzee, kuna maeneo vyama vya upinzani vinafeli. Ni kama mbwa flani mwenye njaa anabweka sana ila akishashiba analala tu asubiri njaa iume tena aanze kelele
 
Rafiki zangu wakubwa kutoka upinzani nilioongea nao wanasema kuandamana ni upuuzi na haitabadili chochote. Wanasema hawashiriki. Wanadai kuwa ushauri mwingi waliokuwa wanatoa kwa vyama vyao kuhusu masuala ya uchaguzi ulipuuzwa na kushindwa huku vibaya ni matokeo ya kupuuzwa kwa ushauri wao. Pengine huu ni muda wa vyama vya upinzani kujitathmini zaidi wapi walikosea.
 
Madelo ga wiza

Napenda kuwasihi watanzania wote hasa wana jf kutijihusisha na maandamano ambayo kumsingi na batili na ni uchu wa madaraka kwa viongozi wetu.

Sitafurahi kuona wanabodi wenzetu wakisota rumande bila sababu yenye tija kwa taifa letu hili lililobarikiwa amani

Tanzania ni nchi inayo pokea wakimbizi ba sisi hatutaki kuwa hao wakimbizi abadani.

Ni wengi wameonya juu ha hatari hii lakini nimeona nitumie elimu yangu kwa faida yako wewe unayepanga kuandamana,fikiria kuna maisha baada ya hapa.

Usikubali kamwe kutumika kisiasa!!

Kumbuka akili ni nywele ........!

Asiye sikia la mkuu......!

Then poleni sana kwa kupoteza mjipange tena 2025

#magema jr
 
Ni upuuzi kushabikia raia wasio na hatia wakipigwa kisa kudai haki zao.

Mbona Lissu alipotua Dar watu walifanya maandamano ya amani na hakuna vurugu ilitokea? Kwani mkiacha waandamanaji wakusanyike kwa amani mnakosa nini?

Hili bara kweli lina laana
Vyama vipo 21
hapo vimeandikwa ACT na CHADEMA
Vyama vingine sisi atuandamani tunasubiri wenzetu wenye uchungu zaidi na nchi wafe ili sisi tukombolewe..
 
Sawa
Si wengine umri mdogo
Bado hatujala mema ya nchi
 
shughuli ya kesho ni nzito saa moja nitapata supu na chapati tatu pale kimboka bar buguruni.
 
Nafurahi kusikia ushahidi upo, na ni matumaini yangu makubwa kwamba utatumika barabara wakati utakapohitajika.
Kuhusu hili la "... uchaguzi huu ulikuwa tayari na matokeo...", swali ni kwa nini mliruhusu uchafuzi huo uendelee huku mkiwa mnajua ulikuwa umeandaliwa?

Huoni kwamba fursa nzuri ilikuwa ni kuuzuia uchafuzi huo mara moja huko huko kwenye vituo vya kupigia kura? Ingekuwa rahisi zaidi na salama zaidi kama zoezi zima la kupiga kura lingesitishwa wakati mawakala wenu wanazuiwa kufanya kazi mliyowatuma waifanye.

Na hata hiyo mikoba ya kura zilizoingizwa, hapo hapo ndipo zingeonyeshwa kwa wananchi nchi nzima.

Kwa nini mlikubali uchaguzi uendelee? Hilo ndilo swali.
Sidhani kama CDM na ACT wangekua na uwezo wa kuzuia uchaguzi...hapo unawalaumu bure tu.
 
Nmeupenda tu ushauri wa mzee, kuna maeneo vyama vya upinzani vinafeli. Ni kama mbwa flani mwenye njaa anabweka sana ila akishashiba analala tu asubiri njaa iume tena aanze kelele
Ajabu Sana.
 
Mkuu ingia barabarani kesho. Kwangu mimi maandamano ni kupotezeana muda tu. Wacha tukatafute riziki za kula familia zetu..

Kwa vizazi vijavyo huu ni wakati wa kuwatengenezea njia. Maisha ni mafupi ,dunia ni mtihani tu . Kila mtu atakufa . Starehe zina mwisho.
Future kwa vizazi vijavyo
 
Back
Top Bottom