CHADEMA sasa hivi wanashikiwa akili na Lissu, Lema na Wanaharakati

Ritz

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2011
Posts
51,303
Reaction score
40,190
Wanaukumbi,

Tatizo kubwa la vijana wa Chadema na wafuasi wao karibia wote sasa hivi wanameshikiwa akili na Lissu, Lema na wanaharakati huko Team Space kila siku mnajikuaanya na kulishwa pumba mnameza tu.

Hakuna taifa duniani ukigusa mambo yanayohatarisha ‘National Security’ serikali ikakuchekea. HAKUNA. Maslahi ya Taifa ni makubwa zaidi ya mtu au chama.

Kipindi Rais Samia ameingia madarakani tulisihi tumpe MUDA aweze kuweka uchumi na nchi katika mstari.

CHADEMA wakajazwa upepo na ‘Team Space’ kuanzisha vuguvugu la Katiba Mpya.

Kosa ni kujaribu ku-Sabotage Rais Samia ashindwe ku-control na kuendesha nchi.
Tuliwaonya mkakaidi.

Endeleeni tu kujazwa upepo na “Team Space wenzenu wanapiga pesa wakati nyie mnabatizwa kwa moto cha kushangaza anachoongea Lema na Lissu marufuku kupinga.
 
Kama ambavyo bunge limeshikiwa akili na Samia? amewaaminisha Spika ni mteule wa rais
Wewe ulitakaje kwa mfano Spika awe Lema yaani wewe upo Chadema unataka kuwapangia cha kufanya chama kingine akili za Bavicha wanazijua wenyewe.
 
Mbona nyasi za hapo mtaa wa kijani zinakukoma wenzio hatikuonei wivu.
 

Hoja yako ni nini hapa?
 
Wewe ulitakaje kwa mfano Spika awe Lema yaani wewe upo Chadema unataka kuwapangia cha kufanya chama kingine akili za Bavicha wanazijua wenyewe.

Lema na Lisu wako cdm, na wanapangia chama chako cha kufanya, halafu unalalamika. Unapinga nini na unashauri nini?
 
Kama ambavyo CCM wanashikiwa akili na machifu.
 
Iviii kumbe kudai katiba mpya ni kushikiliwa akilii??? Ile tume ya warioba wao walishikiliwa akili na nanii mkuuuu?
 
Ingekuwa jambo la busara ulete Post tuijadili badala ya kuhitimisha mada ambayo tayari umeamua msimamo wako, members tujifunze jinsi ya kuweka mada zinazojadilika.
 
Na bado mpaka mnye kabisa. Mmeshindwa kutumia intelinsia kuzia mitandao ili kuwadhibiti CHADEMA na wanaharakati.. mammae zenu MaCCM.
 
Huna hoja! Hivyo ni vizuri ukakaa tu kimya. Ndani ya nchi yetu hakuna National security kama unavyotaka kuwaaminisha watu hapa.

Badala yake kuna nguvu kubwa inayotumika kulinda maslahi ya ccm na viongozi wake. Dhambi iko wapi kwa Watanzania kudai Katiba Mpya?
 
Hivi chadema bado ipo tu , Si walisema Magufuli ameiiteketeza ?
 
Mzee umerudi kwa kasi sana [emoji41]
Za siku nyingi mkuu.

Cc. D. Chongolo
 
Uwendawazimu ndivyo unavyoanza. Unaanza kuona hata vitu ambavyo havipo.

Tanzania hatuna kitu chochote ambacho kinahatarisha usalama na umoja wetu, zaidi ya mifumo mibaya ya utawala. Lakini mwendawazimu anaona kuna watu wanatishia usalama wa Taifa.

Ritz, muda mrefu ulipotea. Kama ulikuwa unapata matibabu Mirembe hospital, hakika wamekuruhusu kutoka hospitali kabla hujapona. Rudi tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…