Uchaguzi 2020 CHADEMA, Tundu Lissu kuwa mgombea wenu mtapoteza muda wenu

Kwa wanasiasa waliopo Zitto is the best,,ingawa mara chache ana jaziba lakini ni mtu makini,anajua kujieleza kwa lugha rahisi na kueleweka.Ni aina ya mwanasiasa mwenye maarifa ya kutosha.

Both Tundu & Zito are best....

Lakini, Kila mmoja wa hawa ana "strengths" na "weaknesses"kama tu ambavyo hakuna binadamu katika dunia hii aliye totally hana uzuri ama ubaya....

Tukiwalinganisha hawa kwa "possibilities" za kupeperusha bendera kwenye nafasi kuu, Tundu Lissu ana nafasi kubwa zaidi....

Sababu ni hizi;

1. Tundu anatoka chama kikuu cha upinzani.....

Kwa vyovyote hawawezi kuacha kusimamisha mgombea Urais ili wamuunge wa chama kingine kidogo....!!

2. Anauzika kisiasa na majukwaani. Tukio la mwaka 2017 pekee ni nyundo ya kumpondea mpinzani wake Magufuli - CCM iwapo watamsimamisha tena....

LAST BUT NOT LEAST;

Zitto is good, ni mdogo kiumri kwa Tundu kwa takribani miaka 7 au 8, ana nafasi siku za usoni kuwania kiti cha Urais....

Hivyo naamini kabisa ACT Wazalendo ktk nafasi ya Urais, watamuunga mkono Tundu Lissu na CHADEMA....
 
Vipi wawe? Ni mpiga kura wa kihistoria,? Yaani ulikuja Duniani kupigia kusifia wanaume wenzako
Chadema wangemuunga mkono Zitto ndiye mwenye sifa si Lissu. Lissu ni mwanasheria wa kihistoria hapa Tanzania lakini si presidential material.
 
Kama wanapoteza muda wewe kinakuwasha nini? kila siku Chadema, Chadema, waacheni
 
Mkuu washauri, mi naona na wenyewe waunge juhudi kama NCCR na TLP?
 
Kwani nyie mgombea wenu ni good listener? Yeye kwa matusi ndo nje nje na huwa anakiri mwenyewe.
 
Kama wanafanana is shear coincidence, lakini Lissu hana vision wala qualities za kuongoza nchi
Ndiyo nikakuambiaje? Kama ni mambo ya vision na qualities mbona huyu aliyepo ndiye hana? Na zaidi nimekuambia kuwa hizo sifa siyo za Lissu bali ni za Magufuli, hawafanani kwa namna yoyote.
 
Ndiyo nikakuambiaje? Kama ni mambo ya vision na qualities mbona huyu aliyepo ndiye hana? Na zaidi nimekuambia kuwa hizo sifa siyo za Lissu bali ni za Magufuli, hawafanani kwa namna yoyote.
Anxisha mada yako mkuu hapa tunamuongelea Lissu.
 

Mwenyekiti wako anatumia bilioni 1.2 kila mwezi kwa matumizi gani wakati kila kitu analipiwa kupitia kodi zetu?
 
Tangu lini uliona binadamu anakubali ushauri wa shetani au ibilisi??
 
Chadema wangemuunga mkono Zitto ndiye mwenye sifa si Lissu. Lissu ni mwanasheria wa kihistoria hapa Tanzania lakini si presidential material.
Tanzania inaweza kuongozwa na mtu yoyote tu hata kichaa.

Imagine sasa hivi inaongozwa na jiwe na watu wako comfortable tu atashindwa vipi binadamu mwenzetu?
 

Binafsi namkubali sana Lissu.

Ila nafasi ya Ikulu ni kubwa sana kwake. Lissu hapaswi kuwa mwamuzi mkuu. Ingawa ni mzuri wa kujenga hoja na kutaka haki, sio mazingira yote haki inakuwa haki, haki inaweza kuwa na mtizamo tofauti, hivyo kwa muumini mkubwa wa haki kama Lissu akiwa na mamlaka makubwa atataka haki itafsiriwe sawa na mtazamo na imani yake.

Niseme tu Lissu na Mh. wa sasa hawajatofautiana sana. Lissu anafaa sana kuwa waziri mkuu, mtendaji mkuu wa serikali...ili awe na mtu wa kumfunga speed governor.

Ni mtizamo wangu tu, na haundoi uthamani wa Lissu kama kiongozi muhimu na mashuhuri ktk taifa letu. Lissu ni asset muhimu sana.

Kuishi kwake ni muujiza, ikiwa ni muujiza basi lipo kusudi ambalo anapaswa kulitimiza. Shime, tumuombee siha njema, tuwe wa kwanza kutaka ulinzi na usalama wake dhidi ya adui aliye kizani na mwenye fundo la chuki.
 
Good analysis.
 
Bora wamsimamishe mtani wangu kingwendu atakuwa anachekesha majukwaani kuliko hawa makanjanja wa kisiasa waongo waongo tu.
 
Jamani naomba october ifike mapema ili kelele za chadema ziongezeke
Najua watapigwa kipigo kibaya sana kwenye kisanduku cha kura.
Walitengeneza mbwembwe zakutaka mabeberu waikwamishe nchi naona wameshindwa.

Wakahamia kwenye korona napo wameshindwa.
Haki zabinadam saivi napo hawaongei baada ya baba yao kutaka waandamanaji wapigwe risasi huko marekani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…