Bush Dokta
JF-Expert Member
- Apr 11, 2023
- 24,831
- 45,154
😀😀😀Wasira akisikia CDM wanaongea huwa hasinzii kabisa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
😀😀😀Wasira akisikia CDM wanaongea huwa hasinzii kabisa
Balile naye anaogopa jamani.Huyu balile analeta mambo ya kishamba, afadhali Ndugu Pascal Mayalla umempa za uso kwamba hamuwezi lissu na wakati mwingine awe makini anapo deal na watu wagumu aina hiyo.
sidhani........ yafute matumaini hayo....tafuta njia sahihi za kuzuia uchaguzi na si watanzania waoga kama tulivyo wewe na mimi......Wasira akisikia CDM wanaongea huwa hasinzii kabisa
😀sidhani........ yafute matumaini hayo....tafuta njia sahihi za kuzuia uchaguzi na si watanzania waoga kama tulivyo wewe na mimi......
Kama anaogopa basi atulie aache watu watoe hoja zao.Balile naye anaogopa jamani.
Watabadilika tu shida huleta akilisidhani........ yafute matumaini hayo....tafuta njia sahihi za kuzuia uchaguzi na si watanzania waoga kama tulivyo wewe na mimi......
wana shida sana tena sana, lakini bado ni class ile ile ya Lumpen proletariat! They resist changes as long as wanapata bamia na mlenda wanakula na jioni wanapata K kwa wake zao...all is over!Watabadilika tu shida huleta akili
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile, ametoa maoni yake kuhusu hali ya ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), akisisitiza kuwa chama hicho kilikumbwa na majeraha makubwa wakati wa kampeni za uchaguzi uliopita na sasa kinahitaji kujenga umoja na mwelekeo mpya wa kisera.
"Siku moja nilisema wakati mnafanya kampeni zenu za uchaguzi CHADEMA, mlijeruhiana sana na sisi tunajua kazi yetu ni kama fundi nyundo, ukiwa unaezeka bati huangalii kwamba ni saa sita mchana huwezi kupanda juu kugonga msumari. Kufikisha ujumbe ndilo jukumu letu la msingi," amesema Balile.
"Mpaka ikafika hatua nikasema ama Tundu Lissu ama Mbowe atakayeshinda baada ya uchaguzi huu ninaamini ataanza kuzungumza kama Mwenyekiti. Wakati ule mlikuwa hamzungumzi kama Mwenyekiti bali kama wagombea."
"Nimeona CHADEMA ya Wenyeviti wote waliotangulia na sasa Tundu Lissu, mlikuwa na sera yenu ya majimbo, lakini haizungumzwi sana siku hizi," amesema Balile, akitaka kufahamu ikiwa sera hiyo bado ni nguzo muhimu kwa chama hicho.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) taifa Tundu Lissu akizungumza wakati wa mkutano kati ya CHADEMA na Jukwaa la Wahariri (TEF)
"Hapa hatutazungumza sera zingine tutazungumza habari ya uchaguzi kwasababu tunatekeleza maamuzi ya chama chetu (CHADEMA), tunataka (Wahariri) mtuelewe, tunataka mkituelewa kama mnakubaliana na sisi na nyinyi muwe sehemu ya mapambano haya,"
"Vyombo vya habari ni sehemu muhimu sana ya mapambano haya na ni sehemu muhimu vilevile ya ukandamizaji, kwasababu wanaokandamiza si tu wanakandamiza vyombo vya habari lakini vilevile wanataka kuweka vyombo vya habari viwasaidie katika ukandamizaji wao. Vyombo vya habari vinaweza kutumika kama daraja la ukombozi na vinaweza kutumika na vimetumika katika historia kama vyombo vya ukandamizaji. Tunataka vyombo vya habari vya Tanzania vichague upande wa kuwa vyombo vya ukombozi, vyombo vya kuleta demokrasia katika nchi ya Tanzania."
"Sasa shida iko wapi? Kwanini kila tume inayoteuliwa (Ikiwamo Tume ya Jaji Warioba) inasema tufanye mabadiliko kwenye mfumo wa uchaguzi? Huu mfumo wa uchaguzi una shida gani hasa? Na hii shida hii ndiyo inayoelezea sababu ya bila mabadiliko hakuna uchaguzi."
"Hiyo shida ndiyo tunayosema isipotatuliwa hakutakuwa na uchaguzi. Mheshimiwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, lugha yangu ilikuwa bayana kabisa, tumesema siyo hatutasusia uchaguzi, tutazuia uchaguzi, lugha siyo kususia uchaguzi lugha ni kuzuia uchaguzi, na tumesema tutazuia uchaguzi kwa nguvu ya umma, tutawaalika Watanzania wahakikishe uchaguzi huu haufanyiki."
"Bila mabadiliko hakuna uchaguzi na siyo bila mabadiliko hatutashiriki uchaguzi, hiyo siyo lugha yetu, lugha yetu ni bila mabadiliko uchaguzi hautafanyika, ndiyo lengo letu. Sasa ni kwanini, hii lugha mbona kali sana, ni kwanini? Mfumo wetu wa uchaguzi una shida gani? na kwanini wazee waliopendekeza ubadilishwe kwanini walipendekeza hivyo? Una shida gani? Shida ya kwanza kabisa, mfumo wetu wa uchaguzi ni mfumo wa Rais, ambao unadhibitiwa kutoka juu mpaka chini ya Rais na mnafahamu Rais wa nchi hii ni Mwenyekiti wa CCM, na Marais wa CCM wametumia udhibiti wao wa mfumo wa uchaguzi kuhakikisha kwamba CCM inabaki madarakani kwa njia zozote, nyingi haramu"
"Majimbo haya yametengenezwa kwa upendeleo mkubwa sana – upendeleo kati ya Tanganyika na Zanzibar, kati ya miji na vijijini, na kati ya mikoa na mikoa. Matokeo yake, dhana ya usawa wa uwakilishi wa umma imevurugwa kabisa,"
"Jiulize, haya majimbo ni kwa ajili ya uchaguzi wa binadamu au kwa ajili ya kuangalia wapi tutaweka barabara na umeme? Kwa nini idadi ya watu haizingatiwi?"
"Katika Uchaguzi Mkuu uliopita, Jimbo la Temeke lilikuwa na wapiga kura 478,000 waliomsimamisha mbunge mmoja. Lakini kwa upande wa Zanzibar, majimbo yote 50 yalikuwa na wapiga kura 566,000 tu, ambao waliwachagua wabunge 50. Hii ina maana kwamba mbunge mmoja wa Temeke anawakilisha watu wengi zaidi kuliko wabunge wote wa Zanzibar kwa pamoja, lakini bado wote wanalipwa mshahara sawa na posho sawa."
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
😀😀😀we jamaawana shida sana tena sana, lakini bado ni class ile ile ya Lumpen proletariat! They resist changes as long as wanapata bamia na mlenda wanakula na jioni wanapata K kwa wake zao...all is over!
Sawa. Wahariri hawapaswi kuwa na upande japo ni binaadamu. Ila wewe una upande japo tulikuheshimu sana.Asante kwa taarifa, wahariri tupo na hatuna hofu.
P
Kama wameanza kudai ajira wameanza kutambua kuwa ajira siyo hisani ni sehemu ya haki za msingiwana shida sana tena sana, lakini bado ni class ile ile ya Lumpen proletariat! They resist changes as long as wanapata bamia na mlenda wanakula na jioni wanapata K kwa wake zao...all is over!
Leo mada waliyoandaa ni Uchaguzi tuAkifika kwenye kujadili muungano naomba mnijuze..
Antipasu ni Project!! Tumeishaona projects kadhaa za namna hii . Nyingi zilikuja kuishia kuwa Ndovu weupe!Lissu yupo mbele ya muda sana,
Mkuu mi nadhani kwa maoni yangu na mtazamo ninavyouona, mbinu pekee ambayo Chadema wanaweza kuzuia uchaguzi ni kutengeneza "unrest" situation. Napata mashaka hayo baada ya kuanza kuona tuvikundi kundi kama hawa vijana wanaoibuka hivi sasa wa NATO sijui. Maana narejea hali kama hii kipindi cha JK mara usikie sijui CWT wana hili mara kule kuna hili.sidhani........ yafute matumaini hayo....tafuta njia sahihi za kuzuia uchaguzi na si watanzania waoga kama tulivyo wewe na mimi......
basi ni project nzuri maana anapigania mamabo ya msingi kwa taifa letu, tui support project isife kama hizo nyingine.Antipasu ni Project!! Tumeishaona projects kadhaa za namna hii . Nyingi zilikuja kuishia kuwa Ndovu
Ballile ni kirusiHuyu balile analeta mambo ya kishamba, afadhali Ndugu Pascal Mayalla umempa za uso kwamba hamuwezi lissu na wakati mwingine awe makini anapo deal na watu wagumu aina hiyo.
1. CCM will never heed to majadiliano. Forget about that, CCM acknowledging "defeat" in the sense that, to them, accepting free and fair elections is a defeat jeopardizing their grip of power!Mkuu mi nadhani kwa maoni yangu na mtazamo ninavyouona, mbinu pekee ambayo Chadema wanaweza kuzuia uchaguzi ni kutengeneza "unrest" situation. Napata mashaka hayo baada ya kuanza kuona tuvikundi kundi kama hawa vijana wanaoibuka hivi sasa wa NATO sijui. Maana narejea hali kama hii kipindi cha JK mara usikie sijui CWT wana hili mara kule kuna hili.
Lakini kwa yote hayo binafsi siyaungi mkono. Chadema ingeshiriki uchaguzi na kutumia namna zote kulinda kura. No Reform No Election I don't think if it will work out.
TANZANIA KWANZA!
MAJADILIANO NDIO SULUHU
MUNGU TUSAIDIE..
Hatujasema bila Reforms tutasusia, tumesema bila reforms tutahakikisha Uchaguzi haufanyiki kabisa.Asante kwa taarifa, wahariri tupo na hatuna hofu.
P
Sahivi kaambiwa maswali yake ni NONSENSE....Ballile ni kirusi