Changamoto kubwa ya Kiusalama kwa Urusi na hatma ya Usalama barani Ulaya

Changamoto kubwa ya Kiusalama kwa Urusi na hatma ya Usalama barani Ulaya

Si kwa ubaya lakin MWAKA 2025 utachangamka sana kimatukio, kuanzia huko duniani(developed Countries) mpaka huku bara la kiza(developing Countries).

mambo ya chaguzi, kupinduana, visasi, kusalitiana, chokochoko na vitisho, kiufupi mambo yatachangamka sana, kuanzia kisiasa, kijamii mpaka kiimani na kiuchumi kiujumla tujipange na yajayo, Kila mtu akae upande sahihi.

Natia nukta.
 
Kuanguka kwa Syria hakuwezi kuifanya Russia kuwa dhaifa, japo italeta changamoto kubwa sana kwake..........

USSR na China waligombana baada ya Iosiph Stalin kufa. Ugomvi wao uliitwa Sino-Soviet Split, na uliisha miaka ya 90's ambapo walipatana tena.......
Kuanguka kwa Assad na kuondoka kwa mshirika wa Urusi hapo Syria ni hasara kubwa kwa Urusi kwani haiwezi project power Middle East na Africa kisawasawa.

Urusi inaitaka Syria kama transit, airlifters za Urusi zote haziwezi toka Urusi zikafika Afrika bila kufanya refuering. Huwa zinatua Latakia pale Khmeimim airbase kwanza kisha ndio zinapeleka mizigo Libya kwa Khalifa Haftar, au zinapeleka mizigo Sudan vitani, au zinaenda Algeria au hizi military junta mpya za West Africa. Ikiwa Syria itaangukia mikononi mwa waasi basi Urusi itakosa access ya kutua Latakia labda wapate access ndani ya Iran.
Sasa sera za kimataifa za Urusi na Iran sio sawa kwa kila kitu, lakini kwa upande wa Syria ya Assad pale Latakia, Urusi ilikuwa ni kama inajitawala. Hivyo kuna limitations ya kipi Urusi atapitisha na kipi hawezi.

Pia Urusi kuikosa Tartus naval base ni hasara kubwa zaidi. Urusi mpaka sasa Afrika haina mshirika ambaye anampa access ya base, mazungumzo na Eritrea au Sudan bado yanaendelea na hayatimii hivi karibuni. Kwahiyo meli za Urusi zitakosa makazi Middle East nzima na Afrika endapo Tartus itaanguka.

Washirika wa kijeshi wa Urusi waliopo Afrika watapata hasara. Sina imani kama waasi wa Syria watakubaliana na Urusi kuipa access ya hizo bases sababu Urusi ilizitumia hizohizo kuwashambulia. Kwa hili labda kwa mbali Urusi inaweza pata temporary access pale Libya upande wa Haftar endapo watafanya makubaliano, ingawa Haftar ni very opportunist and very demanding.

Na kwa namna nyingine, Syria inaungana na Armenia kama nchi zilizopotezwa na ushawishi wa Russia kwenye hii 2020s. Assad alikuwa ni mtu pekee ambaye amekingiwa kifua na Urusi na akabaki anasimama, kuondoka kwake kutapunguza imani kwa strongman mwingine atakayeta kuitegemea Urusi.

Najibu hivi nikiwa na imani Assad anaanguka within few days.
 
Sasa Mkuu, watu wameshuhudia Russia imepoteza kwenye Collective Security Treaty Organisation (CSTO).

Washuhudie tena iipoteze Syria, kiushawishi itashuka pakubwa na hili nalo ni pigo katika sura ya kimataifa.
SOMO KUTOKA LIBYA: Kuangusha serikali ni jambo moja, na kuanzisha utawala wa kiraia ambao unakubalika ndani na nje ya mipaka ya nchi ni jambo jingine kabisa. Syria ni taifa gumu sana kuliko hata Lebanon ukizingatia kuna jamii kama za kishia, kisuni, kikristo, kikurdi na kiarabu. Unadhani HTS wanaweza kutawala nchi ya namna hii ndani ya usiku mmoja kwa kutumia mabomu ya NATO peke yake ???

You may win the war but lose the peace!

KUHUSU CSTO: Nakupa mfano mmoja tu. Baada ya miaka 20 nchini Afghanistan Marekani iliamua kuondoka kwa aibu mwaka 2020-2021 na Taliban wakarudi. Lengo lilikuwa siyo kushindwa peke yake, bali Marekani ilibidi ajikite na kuidhibiti China kupitia mkakati wake The Pivot to Asia.

Ni suala la vipaumbele, japo nadhani changamoto kubwa kwa Syria siyo HTS bali Israel na Turkey ambao wanataka kuimega Syria kwa kisingizio cha kutengeneza Buffer Zones. Sasa Mrusi atafanyaje, nadhani muda ndiyo utasema.
 
Sasa Mkuu, watu wameshuhudia Russia imepoteza kwenye Collective Security Treaty Organisation (CSTO).

Washuhudie tena iipoteze Syria, kiushawishi itashuka pakubwa na hili nalo ni pigo katika sura ya kimataifa. Atakuwa haaminiki!
Hivi karibuni Uturuki ana mafanikio kidiplomasia kuliko Urusi.

Uturuki kaiunga mkono Azerbaijan dhidi ya Armenia iliyoungwa mkono na Urusi na Iran, akashinda.

Uturuki ndio aliiokoa serikali ya Libya ile Government of National Accord kwa kuipa silaha na mafunzo na baadad kafanikisha kuiunganisha na kundi wakaunda Government of National Unity. Turkey ndio sponsor wao na mlinzi wao mkubwa.
Urusi pale Libya inashirikiana hasa na UAE kuunga mkono na Misri kuunga mkono serikali ya kundi la Khalifa Haftar. Bado Uturuki inashinda.

Uturuki anaelekea kuishinda influence ya Urusi na Iran hapo Syria.

Kiufupi calculations za Uturuki zinaleta majibu positive kila ikijipa majukumu magumu.
 
Kuanguka kwa Assad na kuondoka kwa mshirika wa Urusi hapo Syria ni hasara kubwa kwa Urusi kwani haiwezi project power Middle East na Africa kisawasawa.

Urusi inaitaka Syria kama transit, airlifters za Urusi zote haziwezi toka Urusi zikafika Afrika bila kufanya refuering. Huwa zinatua Latakia pale Khmeimim airbase kwanza kisha ndio zinapeleka mizigo Libya kwa Khalifa Haftar, au zinapeleka mizigo Sudan vitani, au zinaenda Algeria au hizi military junta mpya za West Africa. Ikiwa Syria itaangukia mikononi mwa waasi basi Urusi itakosa access ya kutua Latakia labda wapate access ndani ya Iran.
Sasa sera za kimataifa za Urusi na Iran sio sawa kwa kila kitu, lakini kwa upande wa Syria ya Assad pale Latakia, Urusi ilikuwa ni kama inajitawala. Hivyo kuna limitations ya kipi Urusi atapitisha na kipi hawezi.

Pia Urusi kuikosa Tartus naval base ni hasara kubwa zaidi. Urusi mpaka sasa Afrika haina mshirika ambaye anampa access ya base, mazungumzo na Eritrea au Sudan bado yanaendelea na hayatimii hivi karibuni. Kwahiyo meli za Urusi zitakosa makazi Middle East nzima na Afrika endapo Tartus itaanguka.

Washirika wa kijeshi wa Urusi waliopo Afrika watapata hasara. Sina imani kama waasi wa Syria watakubaliana na Urusi kuipa access ya hizo bases sababu Urusi ilizitumia hizohizo kuwashambulia. Kwa hili labda kwa mbali Urusi inaweza pata temporary access pale Libya upande wa Haftar endapo watafanya makubaliano, ingawa Haftar ni very opportunist and very demanding.

Na kwa namna nyingine, Syria inaungana na Armenia kama nchi zilizopotezwa na ushawishi wa Russia kwenye hii 2020s. Assad alikuwa ni mtu pekee ambaye amekingiwa kifua na Urusi na akabaki anasimama, kuondoka kwake kutapunguza imani kwa strongman mwingine atakayeta kuitegemea Urusi.

Najibu hivi nikiwa na imani Assad anaanguka within few days.
North South Corridor AJ Graphic.jpg

Mwaka huu 2024, Mrusi katengeneza The North-South Corridor, inayopotia Russia-Iran-India, hivyo kumfanya Mrusi kuwa moja ya mataifa wadau wa The Persian Gulf. Sasa Mrusi ataweka kambi yake Iran au India ili kufika Afrika na Mashariki ya kati, sifahamu.

Ukisoma historia utafahamu kwamba hii njia, The Persian Route, ndiyo ilitumika sana kipindi cha WW2 na USA, Britain na USSR kuunganisha Asia-Europe-Afrika. Hii njia iliwahi kusababisha ugomvi mkubwa baina ya USSR na USA hadi kupeleka Truman kuwatisha USSR waondoke Iran ndani ya masaa 48, ili kuwazuia wasiweze kupata sehemu ya kimkakati ambayo itawapa uraisi wa kufika Middle East-Central Asia-Far East-Afrika.

Sasa kipindi hiki kina Mullah wa Iran wanawaogopa NATO, unadhani nini kitawazuia kuwaruhusu Warusi wasiweke kambi kwenye The Persian Gulf, jambo ambalo litakuwa na hatari zaidi ukizingatia ni World's Oil Choke Point.

What a Time To Be Alive......
 
View attachment 3171657
Mwaka huu 2024, Mrusi katengeneza The North-South Corridor, inayopotia Russia-Iran-India, hivyo kumfanya Mrusi kuwa moja ya mataifa wadau wa The Persian Gulf. Sasa Mrusi ataweka kambi yake Iran au India ili kufika Afrika na Mashariki ya kati, sifahamu.

Ukisoma historia utafahamu kwamba hii njia, The Persian Route, ndiyo ilitumika sana kipindi cha WW2 na USA, Britain na USSR kuunganisha Asia-Europe-Afrika. Hii njia iliwahi kusababisha ugomvi mkubwa baina ya USSR na USA hadi kupeleka Truman kuwatisha USSR waondoke Iran ndani ya masaa 48, ili kuwazuia wasiweze kupata sehemu ya kimkakati ambayo itawapa uraisi wa kufika Middle East-Central Asia-Far East-Afrika.

Sasa kipindi hiki kina Mullah wa Iran wanawaogopa NATO, unadhani nini kitawazuia kuwaruhusu Warusi wasiweke kambi kwenye The Persian Gulf, jambo ambalo litakuwa na hatari zaidi ukizingatia ni World's Oil Choke Point.

What a Time To Be Alive......
Kuhusu India hiyo option tuiondoe mkuu.
India nayo itataka kuwa superpower muda si mrefu ujao hivyo haitaki kuwa subjugated kwenye maamuzi ya superpower mwingine. Power dynamics za India ni kuwachanganya washirika wake na isitegemee nchi moja kwa wingi lakini pia isinunue ugomvi. Iliweza kununua mafuta ya Urusi akiwa na vikwazo, hapohapo ni adui na China, hapohapo inanunua silaha Urusi lakini pia na Marekani.

Tubaki na Iran, ndio maana pale nikaandika endapo Khmeimin airbase itaponyoka mikononi mwa Urusi, basi Iran ndio inaweza kuwa suluhisho. Hata hivyo Urusi haitokuwa na autonomy kama ilivokuwa Syria.

Kwanza, Urusi ina mahusiano mazuri na Israel, kuweka kambi Iran watapishana.

Pili, Iran na Urusi sio kila sehemu ya kiusalama wanakubaliana.

Tatu, Iran itataka benefits kubwa kwenye makubaliano ya kuweka base ya Urusi kwao. Kwa Assad yeye Urusi ilikuwa inatumia kisingizio cha kumlinda, Iran haihitaji kulindwa na Urusi hivyo lazima kuna kitu kikubwa kiwekwe mezani na Urusi ndio Iran iingie risk ya kuweka airbase ya Urusi. Pia hata bandari inaweza kaa Iran, changamoto ibaki Bosphorus.

Hasara nyingine ni kuwa Iran inatafutwa. Urusi ingepata nchi yenye mgogoro uliojifia kama ilivyokuwa Syria ingekuwa bora zaidi kuliko Iran ambako pako very active.

Au basi Urusi iunde "People's Repuplic" hapo Syria jambo ambalo ni gumu mno kwa sasa.
 
Nafikiri wakimbizi huwa hawachagui mahali pa kwenda na kujihifadhi. Wanajibanza popote pale penye usalama kuliko kule walikokuwa.

Labda wahamiaji (immigrants) ndio ambao huwa wanachagua mahali au nchi ya kukimbilia.
Utakuwa mjinga, utoke bongo nchi yenye asili ya Oligarchy uende ugenini kwenye Oligarchy tena? Tofauti ya urusi na bongo ni maendeleo tu ila mikandamizo inayoendelea kule na hapa bongo ni sawa tu. Ukiisema CCM ya urusi umeisha.
 
NATO wamecheza mchazo mkali sana wa kisiasa dhidi ya MRUSI.

Mosi, wameanzisha mtafaruku Lebanon kwa kumtumia mshirika wao mkubwa Israel, jambo ambalo limepelekea vikosi vingi vya Hizbullah kuondolewa nchini Syria na kurudishwa Lebanon kuzuia uvamizi wa Israel. Jambo hili limechangia kwa kiasi kikubwa Syria kukosa ulinzi katika eneo la Aleppo.

Pili, NATO kutumia mwanachama wake Turkey wamefanya shambulio zito dhidi ya Syria kwa kutumia mgongo wa makundi ya waasi na makundi mengina ya kigaidi. Jambo hili limewaweka Warusi na Wairani njia panda kwasababu kwasasa Iran anasaidia washirika wake Hizbullah kupambana nchini Lebanon, hivyo ni ngumu kurudisha au kuvigawanya vikosi vya Hizbullah baina Syria na Lebanon kama ilivyokuwa mwaka 2015 ambapo vikosi vya Hizbullah vilijazana nchini Syria.

Tatu, Urusi ndiye aliyetoa mchango mkubwa kwa Syria mwaka 2015 ili Assad asipinduliwe. Kipindi hiki yuko kwenye wakati mgumu kwasababu hawezi kutuma vikosi vyake ilhali yuko anapambana na Ukraine na NATO kule Donbass. Mwaka 2015 alitumia vikosi vyenye wanajeshi wasiopungua 60,000 hadi kukamilisha ile vita dhidi ya waasi na magaidi. Kipindi hiki kupeleka wanajeshi 60,000 siyo jambo rahisi.

Nne, NATO na EU wameanzisha chokochoko nyingine nchini Georgia kama zile za Maidan nchini Ukraine mwaka 2014 ambazo ndiyo chanzo kikubwa cha uvamizi wa Urusi nchini Ukraine. Serikali iliyopo Georgia ina mahaba na Moscow, EU, Ukraine na NATO hawataki hili litokee kabisa. Upande mwingine Urusi hataki kabisa Georgia igeuke Ukraine nyingine. Hivyo kama mambo yakiwa mabaya na serikali ikapinduliwa itabidi avamie kijeshi. Mwaka 2008 alivyovamia Georgia alitumia vikosi vyenye wanajeshi 75,000. Kipindi hiki sidhani kama itakuwa rahisi.

Tano, NATO wanamtumia Turkey kwasababu wanafahamu fika kwamba, ili Urusi afanye oparesheni zake za kijeshi za anga ni lazima atumie anga la Turkey. Lakini pia, Turkey ni nchi jirani na Georgia, hivyo Urusi akivutana Turkey ina maana NATO wataitumia nchi hiyo kama njia ya kufanya vurugu dhidi ya Urusi kupitia Georgia.

Kubwa zaidi na hatari, ili manowari za kijeshi za Urusi zitoke Black Sea na kufika kwenye kambi ya kijeshi ya Urusi iliyoko Syria, ni lazima wapite nchini Uturuki kwenye mfereji wa The Bosphorous. Wakivutana Urusi atazuiwa kupita kama ambavyo mwaka 2015 nchi ya Malta ilizikataa manowari za Urusi kupita kwenye mipaka yake. Kazi ngumu.

Sita, kama Iran ataingilia moja kwa moja basi lazima Israel na Turkey wataingia kwenye vita dhidi ya Syria moja kwa moja kwasababu nchi zote hizi hazimpendi Iran. Israel na Turkey wakiungana madhara makubwa sana yatatokea nchini Syria na Israel hasahasa ukizingatia uwezo wa kijeshi ambao Iran kauonesha hivi karibuni.

Saba, Urusi na Iran wanaweza kutumia mgambo wa Houthis, japo hili nalo ni changamoto kwasababu tayari baadhi ya mgambo wako Urusi wanapambana kule Donbass, lakini pia Houthis wamekabwa koo hivi karibuni baada ya UK, USA na ISRAEL kuongeza nguvu ya mashambulizi dhidi yao kuvisaidia vikosi vya serikali.

MRUSI ATAFANYA NINI SASA ????

Anaweza kuhusika moja kwa moja kwa kupeleka vikosi vyake, japo hili ni jambo la hatari mno hata kama mpaka sasa ana vikosi vya wanajeshi milioni 1.15 (Active Personnel), hili litasababisha nguvu zake kule Ulaya kupungua.

Mchezo kama huu USSR alichezewa mwaka 1969 na NATO, baada ya kuona vikosi vyake vizito viko Eastern Europe, waliamua kuitumia China kuvamia mpaka wa kusini wa USSR ambao haukuwa na wanajeshi wengi. Ilikuwa ngumu kwa USSR kupeleka vikosi mpaka wa kusini kupambana na CHINA ndani ya usiku mmoja ilhali kule Ulaya kuna vikosi vizito vya NATO.

AU, Mrusi anaweza kufanya jambo la hatari zaidi ambalo wazungu hawawezi kulipenda. Kukodi maelfu ya mamluki kutoka Asia na Afrika wajazane Ulaya kuua maelfu ya Wazungu, jambo ambalo litakuwa ni hatari mno kwa bara la Ulaya.

Ila kubwa zaidi ni kwamba vita ikiendelea basi, UE itaendelea kupokea wimbi kubwa mno la wakimbizi kama ilivyokuwa 2011-2016, jambo ambalo litakuwa siyo zuri hasa kwa kipindi hiki ambacho uchumi wa mataifa ya UE umegubikwa na mfumuko mkubwa wa bei.

ENDAPO MATAIFA YATAHUSIKA MOJA KWA MOJA: Mfano Iran aende Syria basi lazima The Persian Gulf yote itahusika kwasababu hakuna taifa linaloweza kupambana na Iran bila kutumia korido za nchi kama Qatar, Saudi Arabia na Bahrain. Nchi hizi ambazo zina kambi za jeshi za Marekani zikitumika kuishambulia Iran, lazima nazo zitashambuliwa vibaya.

NB: Mpaka sasa, kwenye huu mchezo mwenye THE UPPER HAND ni Benjamin Netanyahu na Israel yake. Akizichanga karata zake vizuri (Jambo ambalo sidhani kama ataweza) basi anaweza kupata suluhu kubwa kabisa ya kidiplomasia hasa kule GAZA na WEST BANK, lakini pia kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kumtenga IRAN kutoka Lebanon na Syria.

SWALI: Je, Mrusi anaweza kukubali kupoteza kambi zake muhimu za kijeshi kule Tartus na kukubali maslahi yake mengine ya kiusalama yapotee kwa kukubali kuachia serikali ya Assad ianguke ???
Waache wachezeane draft sisi tuendelee kushangaa
 
Perfomance ya HTS imekuwa nzuri sana hasahasa kwenye matumizi ya teknolojia na uwezo wa kutengeneza silaha zao wenyewe. Wataalamu wanasema wanatumia mbinu za jeshi la Uingereza hivyo tunafahamu kwamba British SAS ndiyo wamekuwa wakiwafundisha tokea 2020 baada ya mkataba wa Astana. Changamoto zinazowakumba HTS ni ileile ambayo iliwakumba Ukraine baada ya 2022.

Mosi, wameanza vizuri na kwa haraka mno. Inabidi wafanikishe kuitoa serikali ya Assad kipindi hikihiki ambacho upepo uko upande wao, na wakishindwa walau wailazimishe serikali hiyo kukaa mezani na kufanya makubaliano maana kwasasa wana The Upper Hand. Wakishindwa kuitoa serikali ya Assad hii vita itageuka kuwa A War of Attrition kama Ukraine.

Pili, A War of Attrition inategemea vitu vikubwa viwili, Ability to Produce Artillery at an industrial scale na Ability to mass mobilise personnel. Mpaka sasa, HTS wana wanajeshi wasiopungua 30,000, huku Syria ina wanajeshi 170000 na ina uwezo wa kukusanya wanajeshi wengi zaidi kupitia Conscription. HTS wameonesha uwezo mkubwa mno wa kutengeneza Drones na silaha za kisasa, lakini sidhani kama wana uwezo wa kuwashinda Iran na Urusi katika kuzalisha silaha za kijeshi.

Changamoto kubwa ambayo imewakuta NATO kule Ukraine ni ability to supply Ukraine with armaments on time. NATO wamesema kwasasa Russian Arms Industry is on full capacity na imeajiri watu milioni 3 wanaofanya kazi kubwa kulisaidia jeshi la Mrusi kule Ukraine. Inakadiriwa Mrusi anazilisha silahaa mara 10 zaidi ya NATO kwa kipindi hiki. Ukizingatia na anavyosaidiwa na Arms Industry za China, Iran na North Korea ndiyo tatizo zaidi.

HTS watapambana, lakini itafika kipindi watahitaji silaha kutoka nchi za Magharibi. Israel mwenyewe wakati anapambana na Hamas na Hizbullah aliishiwa na silaha akaenda kwenye Congress kuomba, sembuse HTS. Hivyo wasipoweza kumtoa Assad kwasasa au kumlazimisha kukaa meza ya makubalioni kipindi hiki na washirika wake kama Iran, Russia, China na North Korean wakaanza kumpa silaha, sidhani kama NATO wataweza kuwapa silaha Israel, Ukraine na HTS kwa pamoja, kwasababu ni jambo la gharama mno.

Kubwa zaidi ni kwamba ili HTS wazalishe silaha zao itabidi wategemee supply lines ambazo China na Japan hawawezi kwepeka. Sasa, jiulize itakuwa rahisi kama China ataweka ugumu ?

War is just boring!
Mkuu kiaje?

Sasa kinotokea Syria ni mpango wa kuwatanua Russia na mgogoro wake na Ukraine jambo ambalo Russia limestukia.

Russia walikuwa wameleke vikosi vya Wagner pale lakini wamebadili mawazo na wataendelea kulinda base yao hiyo ya Turtus. Pia wameona SMO yakaribia kuchukua Donbass yote hivyo kasi yake isipungue.

Hivyo kilibakia na hao HTS na wakurdi na Sunni kuingia Damascus kisha kuwafungulia mlango Israeli ambao siku zote wamekuwa wakisema wataka kuhakikisha Hezbollah hawapati silaha kutoka Iran kupitia Syria.

Kwahiyo Russia, Iran na China wameona wamwachie Erdogan aende Damscus na kundi lake huku wao wakiangalia tu maana walimwonya Assad kuhusu Cells zilizokuwa zikiandalwia na Mossad.

Syria haina tofauti sana na Lebanon kwani ni nchi ambazo kwa jina zajulikana hivo lakini kiuhalisia hazina nguvu yoyote ile na mwisho wake ndo kama unavyouona.

Israeli anaingia hapo Syria na IDF watakuwa wakiangalia pande hiyo kutokea milima ya Golan ambayo tayari wameichukua na kuanzia hapo Syiria hadi Palestione upande wa kaskazini itakuwa yatawaliwa na Israeli na hakutakuwa na shida yoyote kwake.

Lakini bado vita kubwa imepangwa kutokea mjini Damascus na Assad alionywa na Russia walipomsaidia 2015 lakini hakutaka kufuata ushauri wao wa kuhakikisha ajijenga na kujenga Syria mpya.
 
Kuhusu India hiyo option tuiondoe mkuu.
India nayo itataka kuwa superpower muda si mrefu ujao hivyo haitaki kuwa subjugated kwenye maamuzi ya superpower mwingine. Power dynamics za India ni kuwachanganya washirika wake na isitegemee nchi moja kwa wingi lakini pia isinunue ugomvi. Iliweza kununua mafuta ya Urusi akiwa na vikwazo, hapohapo ni adui na China, hapohapo inanunua silaha Urusi lakini pia na Marekani.

Tubaki na Iran, ndio maana pale nikaandika endapo Khmeimin airbase itaponyoka mikononi mwa Urusi, basi Iran ndio inaweza kuwa suluhisho. Hata hivyo Urusi haitokuwa na autonomy kama ilivokuwa Syria.

Kwanza, Urusi ina mahusiano mazuri na Israel, kuweka kambi Iran watapishana.

Pili, Iran na Urusi sio kila sehemu ya kiusalama wanakubaliana.

Tatu, Iran itataka benefits kubwa kwenye makubaliano ya kuweka base ya Urusi kwao. Kwa Assad yeye Urusi ilikuwa inatumia kisingizio cha kumlinda, Iran haihitaji kulindwa na Urusi hivyo lazima kuna kitu kikubwa kiwekwe mezani na Urusi ndio Iran iingie risk ya kuweka airbase ya Urusi. Pia hata bandari inaweza kaa Iran, changamoto ibaki Bosphorus.

Hasara nyingine ni kuwa Iran inatafutwa. Urusi ingepata nchi yenye mgogoro uliojifia kama ilivyokuwa Syria ingekuwa bora zaidi kuliko Iran ambako pako very active.

Au basi Urusi iunde "People's Repuplic" hapo Syria jambo ambalo ni gumu mno kwa sasa.
Syria, Lebanon na Iraq zimeshaanguka unadhani Iran atakuwa na nguvu kubwa ya kupambana na NATO na Israel peke yake hali wamemzunguka pande zote kuanzia Saudi Arabia, Bahrain, Qatar na Pakistan ???

Huu ni ushindi mkubwa mno kwa Israel na Netanyahu. Binafsi naamini Iran inaweza kujilinda japo bila kushirikiana na mataifa kama Russia na China, ni suala la muda tu nayeye. Hivyo kama Russia wataweka kambi nchini Iran, jambo ambalo naamani linawezekana sana hasa kipindi hiki, litakuwa A Desperate Move & An Alliance of Convenience.

Kuhusu India, nakubaliana kabisa na wewe, kutakuwa na bandari peke yake ambayo inaweza kuwa na Dual-Use, japo kambi ya jeshi ni ngumu kama ulivyosema.

Either Way, Syria has fallen,
Another Major Win for the Empire.
 
Kuhusu India hiyo option tuiondoe mkuu.
India nayo itataka kuwa superpower muda si mrefu ujao hivyo haitaki kuwa subjugated kwenye maamuzi ya superpower mwingine. Power dynamics za India ni kuwachanganya washirika wake na isitegemee nchi moja kwa wingi lakini pia isinunue ugomvi. Iliweza kununua mafuta ya Urusi akiwa na vikwazo, hapohapo ni adui na China, hapohapo inanunua silaha Urusi lakini pia na Marekani.

Tubaki na Iran, ndio maana pale nikaandika endapo Khmeimin airbase itaponyoka mikononi mwa Urusi, basi Iran ndio inaweza kuwa suluhisho. Hata hivyo Urusi haitokuwa na autonomy kama ilivokuwa Syria.

Kwanza, Urusi ina mahusiano mazuri na Israel, kuweka kambi Iran watapishana.

Pili, Iran na Urusi sio kila sehemu ya kiusalama wanakubaliana.

Tatu, Iran itataka benefits kubwa kwenye makubaliano ya kuweka base ya Urusi kwao. Kwa Assad yeye Urusi ilikuwa inatumia kisingizio cha kumlinda, Iran haihitaji kulindwa na Urusi hivyo lazima kuna kitu kikubwa kiwekwe mezani na Urusi ndio Iran iingie risk ya kuweka airbase ya Urusi. Pia hata bandari inaweza kaa Iran, changamoto ibaki Bosphorus.

Hasara nyingine ni kuwa Iran inatafutwa. Urusi ingepata nchi yenye mgogoro uliojifia kama ilivyokuwa Syria ingekuwa bora zaidi kuliko Iran ambako pako very active.

Au basi Urusi iunde "People's Repuplic" hapo Syria jambo ambalo ni gumu mno kwa sasa.
Uko sawa kabisa anetafutwa hapo ni Iran.

Israeli keshafanikisha kuwamaliza nguvu Hezbollah na uwezo wao wa kujigroup na kupata silaha kutoka Iran.

Pili, Israeli akiwa hapo Syria ataweza kabisa kuingalia Iran kwa karibu zaidi kwa kuweka Buffer zone.
 
Assad ameshapinduliwa Mrusi amedhalilika sana kwa hili. KAMA mshirika wako mhimu anaangushwa kwa vita ya week moja huwezi kuwa na maana kujiita Super Power ni hovyo tu..

Putin kumbe hana lolote ni mbabaishaji tu Syria pale Urusi ana kambi zake 2 kama Waasi wamechukua na wamesaidiwa na Israel na UK basi ni aibu kubwa
 
Kwa ufupi Russia ipo kwenye wakati mgumu.

Syria ni eneo ambalo ana air base yake ya Khmeimim na naval facility huko Tartus.

Mbali na hilo Syria kwa Russia ni eneo muhimu kwa energy strategy.

Ikiwa akiruhusu kupoteza Syria, ukizingatia ameshapoteza allies kwenye mkataba wa CSTO, ushawishi wake kimataifa utapungua sana!

Russia ana wakati mgumu sana! Sijui hata akili gani itakayotumika ila ngoja tuone itakuwaje!
inaelekea tunafikiri tofauti,mimi nafikiri hasira za mataifa ya ulaya kwa russia kama ufaransa,ni kupoteza ushawishi wao kwa makoloni yao africa magharibi,na kufungwa kambi zao,kisha kuwaalika wagner ili washirikiane nao,
Vita vya ukraine,vinamnufaisha USA,lakini sio mataifa ya ulaya,ambayo hutegemea gas ya urusi kuendesha mitambo yao ya udhalishaji viwandani na matumizi mengine
Pia chakula kwa sehemu kubwa ulaya inategemea urusi na ukraine,na kwa sasa mifumuko ya bei ni mikubwa sana huko ulaya kama sio duniani.
Urusi ni taifa kubwa,likitikisika hata wale wanaompinga,kwa namna moja nao wataathirika tu.
 
Assad ameshapinduliwa Mrusi amedhalilika sana kwa hili. KAMA mshirika wako mhimu anaangushwa kwa vita ya week moja huwezi kuwa na maana kujiita Super Power ni hovyo tu
Unataka warusi wafanyaje kam askari wa assad hawatak kupigana hao waasi wana silaha duni jeshi lina kila kitu then wanaachia tu maeneo hio imewakatisha tamaa urusi na irani. Urusi pia ana vita kwake.
 
1.Nafikiri warusi sio wajinga kiasi hicho - haya mambo lazima waliishayaona na wamecalculate risk na maamuzi bila shaka wazee wa wazee wa SVRna GRU waliishafanyia kazi kitambo sana.
2.Urusi katulia tuliii hapo Syria. Hatujaona akiangaika sana au kupanick kisa hao waasi wanaingia..na kitu cha ajabu - HATUJASKIA mpaka sasa hao waasi wakitamka RUSSIA MUST GO- Wote wapo kimya kabisa.
3.Behind the scene hii awamu ya pili ya movement ya waasi ni muendelezo wa vita kati ya Hezbollal na Israel.Syria imekuwa ikiwapatia silaha Hezbollah - kupitia Damascus na kwingineko. Ili kuimaliza kabisa Hezbollah ni lazima njia za panya zote zizibwe.- Ndo hapo Damascus kwa Assad - So Russia hajihusishi na migogoro ya Syria na Israel..hili aliweka wazi kitambo sana na ndo maana ingawa Russia yupo Syria bado aliwapa Israel waendelee na operation zao hapo.
4.Hii operation watu wengi watakua wamehusika au kuna makubaliano yamewekwa kati ya ISRAEL,TURKEY, IRAN, RUSSIA. Ndo maana husikii kelele kote huko.
HIvyo sioni Urusi akiwa kwenye hatari yoyote zaidi hatujaona wala jusikia viashiria vyovyote kutoka kwa waasi vikisema Russia waondoke.
Ikumbukwe kuwa hawa waasi wanapiga mpaka interview na tv za Israel na wanawashukuru Wayahudi - Wayahudi na Warussi hata kama wanautofauti but wapo wanawasiliana at least for now : Putin & Netanyahu wako karibu sana - so Israel will not do kitu ambacho kitamuumiza Russia maximumly...
 
Syria, Lebanon na Iraq zimeshaanguka unadhani Iran atakuwa na nguvu kubwa ya kupambana na NATO na Israel peke yake hali wamemzunguka pande zote kuanzia Saudi Arabia, Bahrain, Qatar na Pakistan ???

Huu ni ushindi mkubwa mno kwa Israel na Netanyahu. Binafsi naamini Iran inaweza kujilinda japo bila kushirikiana na mataifa kama Russia na China, ni suala la muda tu nayeye. Hivyo kama Russia wataweka kambi nchini Iran, jambo ambalo naamani linawezekana sana hasa kipindi hiki, litakuwa A Desperate Move & An Alliance of Convenience.

Kuhusu India, nakubaliana kabisa na wewe, kutakuwa na bandari peke yake ambayo inaweza kuwa na Dual-Use, japo kambi ya jeshi ni ngumu kama ulivyosema.

Either Way, Syria has fallen,
Another Major Win for the Empire.
Mkuu, hii vita ni ya Marekani/ Israeli dhidi ya Russia, Iran na China ambapo Marekani yataka kuhodhi vyanzo vya mafuta katika eneo lote la ghuba.

Lakini pia naona wasahau Uturuki na nafasi yake katika vita hivi vya sasa na harakati za Israeli dhidi ya Syria na Assda.

Wiki ilopita (jummane) Benjamini Netanyahu alisema Syria yacheza na moto pale alipomshutumu Assad kwamba awasaidia Hezbollah kupitisha silaha hapo Damascus.

All in all ni kwamba hii yatuonyesha udhaifu mkubwa wa Syria na Lebanon kwamba zimekuwa pale kama nchi waangalizi. Pia idara zao za ujasusi zimekuwa dhaifu mno kiasi cha kuweza kupenyezewa majasusi kutoka pande zote Israeli, Uturuki na CIA.

Iran nayo imeonyesha udhaifu mkubwa kwenye medani za ujasusi khasa baada ya raisi wao Raisi kuuawa huko milimani chopa lake lilipodunguliwa na pia kabla ya hapo yule Sulemani kudunguliwa, kushindwa na kumlinda Naslallah kutokana na mfumo mzima wa Ujasusi kuingiliwa na Mossad.

Pia Hezbollah kuanza kudunguliwa kwa zile pagers na baadae kiongozi mmoja baada ya mwingine hiyo ni ishara ya ujasusi ulokomaa wa Mossad.

Wakati huohuo kwa mara ingine tena hii yatuonyesha uwezo mkubwa wa Idara za usalama za Mossad na ile ya CIA kwa kazi zao nje ya mataifa yao ambazo ni pamoja na kushirikiana kupalilia vitalu vya magaidi mseto.

Russia na China wao wataendelea kuangalia hali yaendaje lakini Russia wao wana uhakika na kuchukua Donbass na hapo Syria au mashariki ya kati walikuwa ni kama vile wapo sokoni wakiangalia nyanya ipi ni bora.
 
Syria, Lebanon na Iraq zimeshaanguka unadhani Iran atakuwa na nguvu kubwa ya kupambana na NATO na Israel peke yake hali wamemzunguka pande zote kuanzia Saudi Arabia, Bahrain, Qatar na Pakistan ???

Huu ni ushindi mkubwa mno kwa Israel na Netanyahu. Binafsi naamini Iran inaweza kujilinda japo bila kushirikiana na mataifa kama Russia na China, ni suala la muda tu nayeye. Hivyo kama Russia wataweka kambi nchini Iran, jambo ambalo naamani linawezekana sana hasa kipindi hiki, litakuwa A Desperate Move & An Alliance of Convenience.

Kuhusu India, nakubaliana kabisa na wewe, kutakuwa na bandari peke yake ambayo inaweza kuwa na Dual-Use, japo kambi ya jeshi ni ngumu kama ulivyosema.

Either Way, Syria has fallen,
Another Major Win for the Empire.
Syria Wasuni ni majority, Iraq uko wako almost nusu kwa nusu Wasuni na Washia ila kwa sasa wenye mamlaka ni Wasuni na Washia wana wanamgambo wanaoungwa mkono na Iran, Saudi Arabia Wasuni ni wengi zaidi, Yemen Washia hao Houthi ndio wana madaraka.

Mpaka sasa Iran imebaki na Iraq kwa uchache na Yemen ambayo haina faida kiuchumi labda kiusalama pale ghuba. Iran huwa inapenda kuitumia Iraq kama corridor endapo itawekewa vikwazo vya kiuchumi, Iran haitokubali kuipoteza Iraq na huwa inaitia hasara sana hata former PM wa Iraq niliona anapambana mno na Iranian influence.
Ukichunguza hata Assad hakuwa anataka silaha za Iran zipite kwenda Lebanon na Israel ilikuwa ikimuonya azuie au atalipa usumbufu. Tatizo la Iran akikusaidia unakuwa mtumwa wake.

Iran inasponsor makundi ya Kishia hapo Middle East ndio sababu nchi nyingi zinaungana kuihofia. Israel na NATO zamani hawakuwa na kauli dhidi ya umoja wa Kiarabu, enzi za kina Hafez al Assad.

Tatizo lilikuja kwa ME wenyewe kupigana, Saddam kawapiga Kuwait na akatishia kuivamia Saudi Arabia. Saddam kaivamia Iran. Mara Muslim Brotherhood ina wadhamini Uarabuni na wakati huo bado ni kundi la kigaidi kwa serikali nyingine za Kiarabu.

Kujiimarisha kwa NATO na Israel lawama ziende kwa Middle East wenyewe kutoaminiana na kutunishiana mabavu. Wakishindwana watakuja North Afrika kama ambavyo UAE imeanza kila mgogoro ipo.
 
Mkuu, hii vita ni ya Marekani/ Israeli dhidi ya Russia, Iran na China ambapo Marekani yataka kuhodhi vyanzo vya mafuta katika eneo lote la ghuba.

Lakini pia naona wasahau Uturuki na nafasi yake katika vita hivi vya sasa na harakati za Israeli dhidi ya Syria na Assda.

Wiki ilopita (jummane) Benjamini Netanyahu alisema Syria yacheza na moto pale alipomshutumu Assad kwamba awasaidia Hezbollah kupitisha silaha hapo Damascus.

All in all ni kwamba hii yatuonyesha udhaifu mkubwa wa Syria na Lebanon kwamba zimekuwa pale kama nchi waangalizi. Pia idara zao za ujasusi zimekuwa dhaifu mno kiasi cha kuweza kupenyezewa majasusi kutoka pande zote Israeli, Uturuki na CIA.

Iran nayo imeonyesha udhaifu mkubwa kwenye medani za ujasusi khasa baada ya raisi wao Raisi kuuawa huko milimani chopa lake lilipodunguliwa na pia kabla ya hapo yule Sulemani kudunguliwa, kushindwa na kumlinda Naslallah kutokana na mfumo mzima wa Ujasusi kuingiliwa na Mossad.

Pia Hezbollah kuanza kudunguliwa kwa zile pagers na baadae kiongozi mmoja baada ya mwingine hiyo ni ishara ya ujasusi ulokomaa wa Mossad.

Wakati huohuo kwa mara ingine tena hii yatuonyesha uwezo mkubwa wa Idara za usalama za Mossad na ile ya CIA kwa kazi zao nje ya mataifa yao ambazo ni pamoja na kushirikiana kupalilia vitalu vya magaidi mseto.

Russia na China wao wataendelea kuangalia hali yaendaje lakini Russia wao wana uhakika na kuchukua Donbass na hapo Syria au mashariki ya kati walikuwa ni kama vile wapo sokoni wakiangalia nyanya ipi ni bora.
Russia ya Putin kwa sasa unaionaje Mkuu?
 
Back
Top Bottom