Changamoto ya ulevi: Jinsi inavyoumiza familia na jamii

Changamoto ya ulevi: Jinsi inavyoumiza familia na jamii

Usibishane na bible ....Wapeni pombe maskini wasahau shida zao,.......
Usibishane na koroani tukufu....mbiguni kuna mito ya pombe........mixer skin girl
Usibishane na jesus ......water to change kua vodka..........We nan.....
Kama kansa hata ukutumia koriea, kuku broira,kulamba papachu ect unapata y pombe
Kwahiyo Mungu mwenye enzi anatuhimiza tuwe walevi na mazezeta sio?
 
sasa unataka watu wote wawe walokole? Halafu serikali ipate wapi kodi na ajira?
Prague (Check)- wakati walunchi karibu kila mtu hupata bia mbili- ndi anarudi job- halafi life expectance ni miaka 85! achane hizo tafuteni pesa- na pata mvyunyoe kwa ajili ya tumbo lako! kwanza sijawahi ona watu wachoyo kama wanaokunywa soda- matajiri wengi hupata pombe! swala no moderation na sii kuacha! Mbona serikali imepiga marufuku gongo tangu uhuru na bado hawajafanikiwa! Na divai safi alitengeneza Yesu mwenyewe katika bibilia sasa hii ni kitu cha enzi na enzi watu wanaachaje? Ulanzi, mnazi, mbege, kilimanjaro, henenkeen, windhoeek... n. k vina ubaya gani? Achani roho mbaya acheni watu wafurahie maisha ni matam sana na pia ni mafupi ukupata nafasi furahia?

Je nimeeleweka? Ngoja nitafute windhoek baridi na pembeni makange safi ya samaki... tafuteni pesa!!!
Jitathimini vizuri kabla ya kujibu hoja zangu nilizoandika katika hii thread,usituonyeshe kiasi gani una umbumbu katika akili yako.
 
Safari lager ladha inayoridhisha
Screenshot_20230419-102528.png
 
Hawa watu wapo kifungoni na ukweli ni kwamba wanaona wako sawa na hawataki kusikia wakiambiwa ukweli yaani ni kifungo kikali cha nguvu.Yaani huwezi amini yupo mzee hapa jirani anakaribia kwenye miaka 70 hivi nilikua napewa habari zake amepata kansa ya koo na alikua mlevi wa kupindukia.Athari ni kubwa, mtu anakua mbishi anapoa ambiwa lakini janga analokuja kuvuna nila aibu na kamwe hatosahau maishani shuhuda walioshia huko ni nyingi mno ndugu.
Mtu kaishi mpaka miaka 70 unasingizia pombe nini sasa
 
Usibishane na bible ....Wapeni pombe maskini wasahau shida zao,.......
Usibishane na koroani tukufu....mbiguni kuna mito ya pombe........mixer skin girl
Usibishane na jesus ......water to change kua vodka..........We nan.....
Kama kansa hata ukutumia koriea, kuku broira,kulamba papachu ect unapata y pombe
Najibu reply hii ya pili kukusaidia.Kutoka katika kitabu cha nabii Isaya 5:11-12,Ole wao waamkao asubuhi na mapema,wapate kufuata kileo;wakishinda sana hata usiku wa manane mpaka mvinyo imewaka kama moto ndani yao! Na kinubi, na zeze,na matari, na filimbi, na mvinyo, zote ziko katika karamu zao;lakini hawaiangalii kazi ya BWANA wala kuyafikiri matendo ya mikono yake.
 
Kuna wanaoshauriwa kupata beer kidogo ili kuongeza damu, hapo imekaaje? Kuna daktari akipata kilevi kidogo upasuaji anafanya vizuri kabisa, vipi hapo? Wewe sema pombe ya kipimo haina madhara.
Ndugu daktari anashauri pombe kama kitendea kazi cha kumsaidia kufanya kazi? Lahasha ndugu huo ni upotoshaji mkubwa.Pombe yoyote ile unapotumia inaondoa utimamu na ubongo unashindwa kuratibu matendo ya mwili kwa usahihi,huo ndio ukweli.
 
Habari wapendwa,

Leo napenda tuzungumzie hili suala la ulevi na athari zake na jinsi linavyoumiza familia na jamii kwa ujumla.
Wapendwa ulevi ni tabia mbaya ambayo mtu hujijengea taratibu akizani ya kua yupo sawa kumbe anajimaliza siku hadi siku.

Kwa mfano ulevi wa pombe tuache bangi na sigara hivi pia nitavizungumzia mwishoni,sio siri madhara ni makubwa watu hujidangaya kunywa kwa kujilinda na kujipa matumaini kua mfano bia mbili tatu hazitanidhuru lakini ukweli ni kua unapokua katika utumwa huo jua fika unaharibu mwili wako mpendwa, akili zako utajidanganya kua zitakuwa salama zaidi unavyotumia pombe lakini ukweli wa kisayansi ni kua unapelekea kemikali aina ya dopamain kuzalishwa kwa wingi katika ubongo na kupelekea ubongo kuratibu matendo ya mwili vibaya, yaani kupungukiwa utimamu, huu ndio ukweli na uache ukuingie vizuri na uelewe na kubadilika wewe kama mtumiaji

Achilia mbali hizo athari za ubongo lakini ukweli ambao unauma na wengi hujipa matumaini na hawataki kuusikia ni kwamba mwili hau hitaji kemikali ya alcohol na sivyo Mungu alivyokuumba.

Binafsi nilishawahi kua mtu miaji wa vilevi laini kama bia hadi gin na whisky.Ukweli ni kuwa wakati nimeshatumia mwili ulikua ukipata shida hasa mfumo wa upumuaji, ile hali kuhisi hewa kubanwa puani na kuvuta hewa kwa shida.

Athari nyinginezo ni pamoja na kua mjinga mfano kupoteza concentration na mambo yako binafsi huku ukijali na kupigania muda wa unywaji zaidi.

Athari ni nyingine ni kuponea chupuchupu kupata ajali.Mifano niliyoishihudia kwa macho yangu mawili ni vifo kwa upande wa ndugu,mtu aliyekua akisifika kwa kugida chupa za bapa na pombe laini alifariki dunia mwaka jana mwishoni kwa maradhi mabaya ya ini.

Inasikitisha sana wapendwa kuona jinsi jamii inavyoumia na kupoteza nguvu kazi ya taifa katika ulevi, sasa hivi ulevi umekua ni kitu cha kujivuna na kuongeza status yaani kama wewe sio mlevi basi utaonekana mjinga na mpumbavu katikati ya watu na marafiki.

Mimi binafsi nilikua mlevi wa bangi na sigara kwa miaka sita sasa na pombe karibia miaka mitatu,ukweli ni kua hakuna faida niliyopata au cv niliyojenga kutokana matumizi ya vilevi hivyo zaidi yake ni hasara,kupoteza heshima na uhusiano wangu na familia na jamii kwa ujumla.

Nakusihi mpendwa kama wewe sio mtumiaji mwombe sana Mungu kwa kunia usiingie katika mtego huu ni hatari mno mno na tena mno kwa maisha yako mazuri hadi uzeeni, na kwa wale watumiaji jitahidi uache mara moja maana inawezekana mtu asikudanye kua eti punguza kidogo kidogo huo ni uongo na ni ngumu kuacha kwa namna hiyo,mimi binafsi ni shahidi na niliacha vyote mara moja kirahisi tu.

View attachment 2591129

Nakaribisha maswali.
Usimpangie mtu matumizi na starehe zake.
 
Habari wapendwa,

Leo napenda tuzungumzie hili suala la ulevi na athari zake na jinsi linavyoumiza familia na jamii kwa ujumla.
Wapendwa ulevi ni tabia mbaya ambayo mtu hujijengea taratibu akizani ya kua yupo sawa kumbe anajimaliza siku hadi siku.

Kwa mfano ulevi wa pombe tuache bangi na sigara hivi pia nitavizungumzia mwishoni,sio siri madhara ni makubwa watu hujidangaya kunywa kwa kujilinda na kujipa matumaini kua mfano bia mbili tatu hazitanidhuru lakini ukweli ni kua unapokua katika utumwa huo jua fika unaharibu mwili wako mpendwa, akili zako utajidanganya kua zitakuwa salama zaidi unavyotumia pombe lakini ukweli wa kisayansi ni kua unapelekea kemikali aina ya dopamain kuzalishwa kwa wingi katika ubongo na kupelekea ubongo kuratibu matendo ya mwili vibaya, yaani kupungukiwa utimamu, huu ndio ukweli na uache ukuingie vizuri na uelewe na kubadilika wewe kama mtumiaji

Achilia mbali hizo athari za ubongo lakini ukweli ambao unauma na wengi hujipa matumaini na hawataki kuusikia ni kwamba mwili hau hitaji kemikali ya alcohol na sivyo Mungu alivyokuumba.

Binafsi nilishawahi kua mtu miaji wa vilevi laini kama bia hadi gin na whisky.Ukweli ni kuwa wakati nimeshatumia mwili ulikua ukipata shida hasa mfumo wa upumuaji, ile hali kuhisi hewa kubanwa puani na kuvuta hewa kwa shida.

Athari nyinginezo ni pamoja na kua mjinga mfano kupoteza concentration na mambo yako binafsi huku ukijali na kupigania muda wa unywaji zaidi.

Athari ni nyingine ni kuponea chupuchupu kupata ajali.Mifano niliyoishihudia kwa macho yangu mawili ni vifo kwa upande wa ndugu,mtu aliyekua akisifika kwa kugida chupa za bapa na pombe laini alifariki dunia mwaka jana mwishoni kwa maradhi mabaya ya ini.

Inasikitisha sana wapendwa kuona jinsi jamii inavyoumia na kupoteza nguvu kazi ya taifa katika ulevi, sasa hivi ulevi umekua ni kitu cha kujivuna na kuongeza status yaani kama wewe sio mlevi basi utaonekana mjinga na mpumbavu katikati ya watu na marafiki.

Mimi binafsi nilikua mlevi wa bangi na sigara kwa miaka sita sasa na pombe karibia miaka mitatu,ukweli ni kua hakuna faida niliyopata au cv niliyojenga kutokana matumizi ya vilevi hivyo zaidi yake ni hasara,kupoteza heshima na uhusiano wangu na familia na jamii kwa ujumla.

Nakusihi mpendwa kama wewe sio mtumiaji mwombe sana Mungu kwa kunia usiingie katika mtego huu ni hatari mno mno na tena mno kwa maisha yako mazuri hadi uzeeni, na kwa wale watumiaji jitahidi uache mara moja maana inawezekana mtu asikudanye kua eti punguza kidogo kidogo huo ni uongo na ni ngumu kuacha kwa namna hiyo,mimi binafsi ni shahidi na niliacha vyote mara moja kirahisi tu.

View attachment 2591129

Nakaribisha maswali.
Duu
 
Siku zote nasemaga pombe sio Tatizo Tatizo lipo Kwa mtu mwenyewe.......

Unafanya over drinking una stress una kunywa mpk unakua chronic....

Kunywa jua level yako ya alcohol usizidishe kipimo tena kunywa baada ya kazi...

Pombe sio Tatizo Tatizo ni mtu mwenyewe..
 
Back
Top Bottom