Changamoto ya umeme nchini ilianza na Awamu ya Tatu, sasa ni mbaya zaidi. Kwanini maji ya Ziwa Victoria yasipelekwe hadi Mtera na JNHPP kupata suluhu?

Kwa nini basi yasiendelezwe haya mabwawa yaliyopo, mfano Kihansi, Mtera hata na Hale?

Capacity ya Kihansi ni 300 MW lakini sasa imewekewa mitambo ya 180, nimewahi kutembelea Hale na Mtera mitambo yake duh! ya mwaka 47! Imechoka hatari.
 
Ama kweli CCM ni janga kubwa kwa taifa hili. Na mnakiri kabisa utopolo wenu 🙆🙆🙆
 
Huu Ni ukweli mchungu,Ni ujinga tuu wa yule jamaa yenu.
Tena ili kukwepa usafirishaji wa gesi kutumia bomba.
Tungejenga station ya kuzalisha umeme huko huko Mtwara, afu transmission line zilete umeme huku. Hii ingesababisha bei kuwa ndogo maana tungekwepa tumia bomba.
Au tungelipa mkopo wote wa bomba tulimiliki liwe letu

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Kwa nini basi yasiendelezwe haya mabwawa yaliyopo, mfano Kihansi, Mtera hata na Hale?

Capacity ya Kihansi ni 300 MW lakini sasa imewekewa mitambo ya 180, nimewahi kutembelea Hale na Mtera mitambo yake duh! ya mwaka 47! Imechoka hatari.
Hayo bado hayawezi kuzalisha megawatt nyingi. Kumbuka mahitaji yetu hadi kufikia 2030 yaatakua zaidi ya megawatt 2000. Hivyo hakuna namna bwawa jipya ilikua lazima
 
Kwa nini basi yasiendelezwe haya mabwawa yaliyopo, mfano Kihansi, Mtera hata na Hale?

Capacity ya Kihansi ni 300 MW lakini sasa imewekewa mitambo ya 180, nimewahi kutembelea Hale na Mtera mitambo yake duh! ya mwaka 47! Imechoka hatari.
Kuendelezwa kwake maana yake waondoe tope lote kwa kufunga maji yasitiririke kwa muda fulani.

Waweke turbines mpya, generators mpya.
Hiyo ni gharama kuliko kununua generators za gas

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Kulipia bomba liwe letu alafu gesi unaendelea kununua kwa mwekezaji bado ni kazi bure. Wengi hadi sasa hamuelewi vizuri, kutegemea chanzo Cha umeme Cha kununua kwa mwekezaji ni jambo la ajabu. Labda ungesema tutafute pesa zaidi alqfu hiyo gesi tuanze kuchimba wenyewe
 
Ili uchimbe inabidi ufanye utafiti utafiti ni bahati nasibu.

Bomba twalipia dollar kadhaa kwa kila cbm 1, na bado hatuitumii gesi hata kwa asilimia 20 ya uwezo wa bomba, hivyo hii husababisha muda wa kulipa kuwa mrefu ukijumlisha mfumko wa bei twajikuta twalipa hela nyingi sana

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Hayo bado hayawezi kuzalisha megawatt nyingi. Kumbuka mahitaji yetu hadi kufikia 2030 yaatakua zaidi ya megawatt 2000. Hivyo hakuna namna bwawa jipya ilikua lazima
Mimi sikatai kwamba bwawa jipya ilikuwa lazima, lakini lilihitaji proper planning na hesabu hasa za matumizi ya maji, kwani mto rufiji unategemewa na viumbehai wengi sana kwa hivyo impacts za kuzuia maji kwenye bwawa zilitakiwa zifanyiwe kazi vizuri. Sisi kama wananchi tunataka kitu sustainable siyo bwawa limejengwa halafu hakuna maji ya kujaza.
 
Endapo hela zilizotumika Mwalimu Nyerere zingewekezwa kwenye gas turbines hakika tungepata umeme mwingi sana

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Gesi sio renewable, kuwekeza pekee huko ni hasara kubwa mno. Kwa nchi yetu hii ambayo tuna renewable sources nyingi ni ajabu sana kuziacha na kutumia nguvu kwenye gesi. Hata hivyo gesi bado tunainunua kwa gharama kubwa toka kwa mwekezaji
 
Hizi story za bwawa hupotoshwa na wale ambao walikuwa hawataki ni Kama story za gesi pia wale walikua hawataki walipotosha.

Mradi ni 2% tu ya eneo lote. Sasa hao viumbe wanakosaje kutumia hayo maji?
 
Gharama za uzalishaji usifikiri gesi ni bure, inanunuliwa kutoka kwa mwekezaji
Ni kweli. Hiyo gesi si yetu tena. Tulishanyang'anywa kitambo na mabepari aka wawekezaji kupitia mikataba mibovu ya miaka mia kama walivyotaka
kufanya kwenye bandari yetu ya Bagamoyo. Wanaimiliki kwa asilimia 100% (by JPM), wao ndiyo wanatuuzia kwa bei wanayoitaka wao. Mtungi wa gesi wa kilo 15 ambao unatosha siku 7 tu za kupikia maharage ya familia ya watu saba, unauzwa TSH 60,000. Unit moja ya umeme majumbani tunauziwa TSH 400 na wanania ya kuipandisha. Yaani maharage ya Sh 1,000 unayapika kwa Sh 2,000 (bei ya Kilowatt-hour 5). Jumla inakuwa Sh 3,000 ambayo ingalitosha mboga ya nusu kilo iliyopikwa kwa kutumia kuni ulizokata mti bure.
Huko kwa mabepari bei ya umeme ni sawa na bure yaani Kilowatt-hour moja bei yake haizidi TSH 30!
 
Mie nawaza tu ikiwa sa hivi ni msimu wa mvua lakini maji ya kuzalisha umeme bwawani tunaambiwa hakuna je ikifika kiangazi itakuwaje?
Si ndo itakuwa mgao wa week kwa week
 
Mie nawaza tu ikiwa sa hivi ni msimu wa mvua lakini maji ya kuzalisha umeme bwawani tunaambiwa hakuna je ikifika kiangazi itakuwaje?
Si ndo itakuwa mgao wa week kwa week
Sababu zao ni kigeugeu tu. Kiangazi utaambiwa kuna ukame, sijui ni kiangazi gani ambacho huwa hakina ukame, au definition ya kiangazi kwa tanesco siyo ile tunayoijua sisi. Wakati wa masika na mvua zikileta mafuriko maeneo mbali mbali ya nchi, tanesco watasema mabwawa yao hayana maji kwa sababu ya shughuli za kibinadamu kwenye vyanzo vyake vya maji. Utadhani hizo shughuli za kibinadamu zimeanza leo. Kwa nini hizi shughuli za kibinadamu hazizuii haya mafuriko bali zinazuia tu maji kutoingia kwenye mabwawa ya tanesco. JPM alituambia kuwa mabwawa haya huwa yanafunguliwa kuchepusha maji yasijae.

Mara tunaambiwa miundo mbinu yote ya transmission inahitaji overhaul yote. Trilioni takriban 60 za pesa zitahitajika kwa zoezi hili ambalo litakamilika mwaka 2026. Yote haya yanaweza kuwa hujuma tu zenye malengo fulani fulani yakiwemo ya kisiasa. Yanahitaji ufumbuzi wa haraka. Hata kama maji ya Victoria yakipelekwa kule bado mabwawa hayo hayatajaa kama hujuma hizo bado zitakuwepo.
 
Duh, sijaelewa
 
Akili hizi we ukipewa nchi, lazima tuingie kwenye vita na wamisri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…