Changamoto ya umeme nchini ilianza na Awamu ya Tatu, sasa ni mbaya zaidi. Kwanini maji ya Ziwa Victoria yasipelekwe hadi Mtera na JNHPP kupata suluhu?

Changamoto ya umeme nchini ilianza na Awamu ya Tatu, sasa ni mbaya zaidi. Kwanini maji ya Ziwa Victoria yasipelekwe hadi Mtera na JNHPP kupata suluhu?

Ungeijua Misri usingeleta huu utoporo wako hapa
 
Nilpofika hopo pa Ethiopia wanatumia maji ya Ziwa Victoria kupitia mto Nile... Siku endelea tena kusoma hiyo post yako.

Yaani unaonyesha unauelewa mdogo sana. Labda rudi darasani tena kasome Geography vizuri uuelewe mto Nile.
Wewe ndiye unaonesha hujasoma shule na kama ulisoma basi ulisoma ujinga. Hiyo geographia huijui. Kwa kukuelimisha kidogo ni kuwa kwa kawaida mito yote hupeleka maji aidha kwenye maziwa au baharini. Ziwa Victoria, ambalo ndiyo ziwa la maji baridi kubwa la tatu duniani, hupokea maji yake kutoka mito zaidi ya mia moja ya nchi za Tanzania, Kenya na Uganda. Tanzania ndiyo inayoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya mito inayopeleka maji hayo ziwa victoria ikiwemo Mto Mara, Mto Simiyu, Mto Mirongo, Mto Manonga na Mto Kagera - kwa kutaja michache.

Mto Nile ndiyo mto pekee duniani ambao badala ya kupeleka maji ziwani au baharini kama ilivyo mito mingine, mto huu hutoa maji Ziwa Victoria na kuyapeleka kwenye bahari la Mediterranean ukianzia kwenye Mto Kagera na kupitia Uganda, Sudan, Ethiopia na Egypt. Bila kuwepo kwa mto Nile kuyapeleka maji haya ya Ziwa Victoria barahirini, ziwa hili lingalifurika na kuifanya Tanzania yote kuwa bahari. Hii ndiyo design ya Muumba wetu wa dunia na anga. Mto huu pia unajulikana kama the Blue River. Ndiyo mto mrefu kuliko mito mingine yote duniani.

Ethiopia na Egypt wanategemea sana mto huu wa Nile kwa uhai wao kwani nchi hizo ni za ukame throughout. Hawa chanzo kingine cha maji. Wakichimba visima wanapata mafuta badala ya maji. Kwa kutumia mto Nile unaotoka kwetu wanazalisha umeme mwingi ambao wataanza kutuuzia sisi. Pia mafuta yao wanatuuzia kupitia OPEC.

NB: Jaribu basi angalao google: 'The Grand Ethiopean Renaissance Dam'. Utaona ujinga wako uliousoma shuleni uliokurukupa kuuleta hapa.
 
Sasa kama kwa shirika la umma faida sio monetary peke yake kwa nini mishipa inakotoka ukitaka TANESCO nayo i break-even??
Hivi unajua hata tunaongelea nini ? Ngoja ni-break it down simply...

Comment: Wewe umesema Hii Bei unataka iwe ndogo kiasi gani sababu huenda wengine yao ipo juu

Jibu: Huwezi kujilinganisha na kipofu kwenye mbio sababu yeye anatumia masaa basi wewe ukitumia dakika 50 inatosha (meaning kwamba tuna vyanzo vingi) pili bei hii tunayonunua sasa ni kwamba Tanesco ananunua units ili atuuzie na baada ya hayo yote hata break-even haipo which means kodi zetu bado zinalipa (sio kumlipa Tanesco bali dalali anayepata faida)

Comment: Shirika gani la UMMA lina break-even

Jibu: Apart kwamba kuna Mashirika ya UMMA China yanatengeneza faida lukuki pia Tanesco inaweza kutengeneza monetary profit lakini hata isipotengeneza hata sumni lakini umeme ukawa wa bei ndogo faida yake ni tosha sababu Nishati ni Huduma kama ilivyo Utilities nyingine

Comment: Sasa kama Shirika la UMMA faida sio Monetary Pekee mishipa inakutoka ya nini?

Jibu: Hivi hapo Juu and as far as TANESCO is concerned kuna faida gani zaidi ya madalali kupiga Pesa na Serikali kuifanya TANESCO kama Kibubu chao.., Unaona faida yoyote ?, Na kama wewe unaridhika na hayo basi angalia upya na kama bado unaridhika, basi motives sio kwa faida ya Nchi
 
Uganda wanajenga chanzo kipya cha umeme mto nile (mto kagera) kwenye mpaka wa uganda na tanzania kwa upande wa mrongo sijui sisi tunakwama wapi aisee wakati ni rasilimali ambayo iko upande wetu pia

Mwingine huyu, Kwani Rusumo kuna nini
 
How? Maji ya Ziwa Victoria yapelekwe Kidatu na Mtera! .Hivi somo la Geography lilifutwa?
Ugumu uko wapi? Mbona tumepanga kupeleka gesi kutoka Mtwara hadi Mombasa kwa bomba? Mbona mafuta ya Uganda yatapelekwa hadi Tanga kwa bomba? Mbona crude oil inapelekwa kutoka Dar es Salaam hadiMZambia kwa bomba?

Mbona hadi sasa maji ya Ziwa Victoria yanapelekwa hadi Tabora kwa bomba? Mbona maji ya Ziwa Victoria tuna mpango ya kuyapeleka hadi Singida kwa Mwiguru Nchemba kwa bomba na hatimaye hadi Dodoma kwenye makao makuu ya nchi yetu? Kwani hilo bwawa la Mtera na la Nyerere liko umbali gani kutokea Tabora ambako maji haya yalishafika? Kwa nini tusiyapeleke huko kwanza kabla ya kuyapeleka Singida na Dodoma? Kwani gharama itakuwa trilioni ngapi? Mbona Tanesco wanakusanya karibu trilion 3 kwa mwezi kutoka kwa wateja wao millioni 3 wa sasa, kwa nini wasigharimie bomba hilo ambalo litawaonezea wateja na makusanyo ya pesa? Tunataka watanzania wote milioni 61 wawe wateja wa tanesco.
 
Harafu acha upotoshaji wa kipumbavu..

Awamu ya 3 ya Mkapa ulitaka kubinafsisha Tanesco so uamzi wa mwisho haukufikiwa ndani Baraza la Mawaziri baadae wakaja wakafuta huo mpango na kufanya modernisation ya management ya Tanesco ila kwa Miaka yote ile ya mchakato wa ubinafsishaji Hakuna uwekezaji mpya wa Serikali uliofanywa kwa sababu ya hiyo sintofahamu..

JK alirithi Nchi ikiwa Hakuna Tanesco yenye vyanzo vipya vya umeme na Uchumi unajua so tunrescue situation ndipo Sasa mitambo ya mafuta almaarufu majenereta ikakodiwa na kuketwa maana huwezi kaa bila umeme huku wakiendelea na uwekezaji wa umeme wa Gas..

So Hadi anaondoka Madarakani Umeme wa gas ndio ukawa na proportion kubwa kwenye energy mix ya 63%.

Mwendazake akaja akaishia kupuuza gas na kuanza mradi wa bwawa ambao haujulikani ungeisha lini,Miaka 5 ikapita bwawa liko 30%.

Amekuja Rais Samia akakutana na Hali Kama ya aliyoikuta JK, mvua zikapungua umeme wa maji ukapungua na gas ilipuuzwa , Sasa kaongeza Pesa Wizara ya Nishati ili kupata umeme wa gas wakati wanaendela na kukomaa na bwawa..

Naomba hapa muelewe awamu ya 4 haitaki.kuzima Moto inaenda na ufumbuzi wa kudumu,bwawa litakuwepo na gas na vyanzo vinginevyo vitaanzishwa ili kuanzia 2026 huko walau kazi ibaki ya mainatanance na sio generation.
Wewe bila shaka utakuwa unatokea tanesco. Umejitahidi kutetea masilahi yenu lakini wala haujaeweka unachokibishi.
 
Awamu ya baba wa taifa na ile ya mzee ruhusa hakukuwa na changamoto la katika katika kwa umeme maeneo ambayo huduma hii ilikuwa imeyafikia. Ni kweli kwamba maeneo hayo yalikuwa hasa kwenye miji mikubwa ya nchi. Shughuli za kiuchumi wa viwanda hazikuwa nyingi kama ilivyo sasa ambapo tumesambaza huduma hii ya umeme hadi kwenye karibu kila kijiji.

Jinsi uchumi wa viwanda ulivyozidi kukua na idadi ya watu kuongezeka, ndivyo changamoto ya umeme ilivyojitokeza na kukua kila kukicha. Zilianza hasa katika kipindi cha awamu ya tatu ya Mzee Mkapa ambaye suluhisho lake lilikuwa ni kuwapa kampuni ya makaburu wa South Africa kutuendeshea Tanesco yetu. Matokeo yake hatutayasahau. Tulipigwa tukapigika.

Ikaja awamu ya nne ya Mzee Kikwete. Wao wakaona suluhisho lake ni kukodi majenereta ya kuzalisha umeme wa dharura kutoka makampuni ya nje ya nchi kama yale ya Richmond, Dowans, Symbion na IPTL. Tukapigwa na kupigika hadi Waziri mkuu akatimuliwa na bunge la Mzee Sitta.

Ikaja awamu ya tano ya Mzee Magufuli. Nayo ikahangaika kwa kubana mafisadi na kuanzisha mahakama ya mafisadi kama suluhisho la changamoto hili la umeme. Kwa kiasi fulani kukawa na ahueni ya kuonesha kuwa ile ndoto ya Tanzania ya viwanda ifikapo 2025 labda ingaliweza kutimia.

Sasa imekuja awamu ya sita ya Mama yetu Mzee Salmia inayopenda kushirikisha wananchi wote kupata suluhisho la changamoto mbali mbali ya wananchi kidemokrasia. Kwa kuwa umeme wa bei rahisi kuliko wote ni ule unaotokana na maji. Na kwa kuwa nchi yetu imejariwa mito mingi na kuzungukwa na maziwa makubwa makubwa mengi: kwa nini maji ya ziwa kama lile la Victoria yasipekwe kwa mabomba huko kwenye bwawa la Mtera na lile la Nyerere ili wakati wa ukame kwenye mabwawa hayo, yakafunguliwa kuyajaza? Ethiopia wanatumia maji ya ziwa Victoria kupitia mto Nile kuzalisha maelfu ya maelfu ya MW za umeme hadi kuwauzia Wakenya.

Kwanini sisi tusitumie Ziwa hili ambalo liko kwetu? Kwani ni shilingi ngapi kupeleka maji ya ziwa letu huko? Kama hatuna hizo hela, tutafute pa kukopa kwani manufaa ya mkopo huu ni mkubwa sana. Hili litakuwa ni suluhisho la once and for all ya changamoto hili la umeme.

Tutaweza hata kuuza umeme nje ya nchi na kuachana na kuuza mahindi na mchele nje ya nchi wakati tukiwa tuna njaa. Tutaweza kupunguza sana bei ya umeme ili wananchi wote waweze kuitumia kama nishati rahisi ya kupikia na hivyo kuachana na ukataji wa miti wakitafuta kuni na mkaa. Mwananchi ataweza kutumia shilingi zisizozidi elfu tano tu kwa mwezi kwa nishati ya kupikia ya umeme.

Tanesco nao wataweza kukusanya matrilioni ya pesa kwani kila mwananchi atakuwa mteja wao. Viwanda vingi vitajengwa na kuzalisha bidhaa nyingi kwa bei nafuu. Kwa muda mfupi nchi yetu itakuwa upper middle income country chini ya uangalizi wa mama!

NB: Umeme utokanao na gesi mara zote bei yake ni ya juu sana (unaffordable to many of our people) ukilinganishwa na ule unaotokanq na maji. Umeme wa gesi ni kwa wakati wa dharura tu au kwa kuuza nje.
Niwakati was kusimamisha miradi yote na kuhamia kwenye hili la umeme na maji

siTU yaende Mtera bali pia kwakutumia vyanzo vilivyo karibu yaingie mbugani pia kuepusha vifo vya wanwanyama ili tuwe na utarii endelevu
 
Miundombinu ya gesi ya mtwara ilikuwa tayari, kilichotakiw ni kuongeza tu uzalishaji - mwendazake naye akaja ya yake kwamba eti gesi yote ishauzwa kwamba tulipigwa vibaya sana - hivyo CCM wakamshauri aachane na huo mradi na hilo bomba lao kisha aanzishwa mradi wake wa Rufiji ili ajizolee misifa kwamba ametengeneza umeme wa uhakika kwa bei nafuu, sasa mradi wenyewe umedoda.

Tanzania hatujui tunachokitaka !!
Umeme wa gesi haujawahi kuachwa, tuliebdelea kutumia kwa wungi Sana 62% ya umeme wote ulikua wa gesi
 
Pesa zinazotumika kujenga mradi wa Nyerere ndio zilibidi ziende kufanya iyo miradi ya gesi, solar na makaa ya mawe.
Mnaongea kitu hamjui, umeme wa gesi sio renewable. Gesi hii inaunuliwa ukitegemea kwa asilimia kubwa kuzalisha umeme huko mbeleni kutaakua na shida. Hizo sources zingine ni gharama sana kuzalisha umeme

Hataa hivyo kwa sasa tunategemea sana umeme wa gesi kwa asilimia kubwa, Ila ndio Kuna bwawa nalo linakuja kama backup
 
Hii Nchi naona inahitaji Rais dikiteka zaidi ya Magufuli,maana hata historian inaonesha Marais madikiteta ndio sana uchungu na Nchi na huwa wanabadilisha mambo.
Hii nchi inahitaji mipango endelevu siyo leo amekuja kiongozi huyu na mipango yake na baada ya miaka kumi anakuja mwingine na kufuta yote yale ya awali na kuanzisha ya kwake.

Laiti kama JPM angeendeleza hiyo ya gesi wakati inatayarishwa hiyo ya Rufiji hydropower kwa uangalifu zaidi basi tungekuwa angalau na mipango inayoeleweka. Leo hii gesi ndiyo hivyo, hydropower haieleweki - yaani tupo tupo tu.

Awamu ya 6 ikiisha akija mwingine ataanza na mengine mapya na kutupa haya ambayo tayari yapo kwenye pipeline.
 
Hii nchi inahitaji mipango endelevu siyo leo amekuja kiongozi huyu na mipango yake na baada ya miaka kumi anakuja mwingine na kufuta yote yale ya awali na kuanzisha ya kwake.

Laiti kama JPM angeendeleza hiyo ya gesi wakati inatayarishwa hiyo ya Rufiji hydropower kwa uangalifu zaidi basi tungekuwa angalau na mipango inayoeleweka. Leo hii gesi ndiyo hivyo, hydropower haieleweki - yaani tupo tupo tu.

Awamu ya 6 ikiisha akija mwingine ataanza na mengine mapya na kutupa haya ambayo tayari yapo kwenye pipeline.
Jpm hakuendelea na gesi? Katika kipindi chake matumizi ya gesi kuzalisha umeme yaliongezeka kuliko vyanzo vingine.

Alichofanya ni kuongeza sources tu za umeme Kama hilo bwawa. Kutegemea gesi tu bila kuwa na mbadala ni hatari sana. Gesi sio renewable. Maji ni renewable. Hivyo alifanya sawa.
 
Unajua prediction ya miaka 30 ijayo unadhani iyo mito na mabwawa yataendelea kuwepo. Hapa ndio kwanza umeanza.
Hapo umenena maana huko kwenye vyanzo (upstream) tunaharibu kama hatuna akili halafu tunategemea maji hayo hayo yafike mpaka rufiji.
 
Gesi ya mtwara nini kilikwamisha huo mradi au huwa ni madili ya wakubwa mambo mengine hadi kichefuchefu kuyasikia au ndiyo miradi ya Kijani kuombea kura?😎😎
 
Ethiopia na Egypt wanategemea sana mto huu wa Nile kwa uhai wao kwani nchi hizo ni za ukame throughout. Hawa chanzo kingine cha maji.
Unajua kwamba kuna blue nile na white nile na vyanzo vyao ni tafauti?
 
Back
Top Bottom