Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wewe ndiye unaonesha hujasoma shule na kama ulisoma basi ulisoma ujinga. Hiyo geographia huijui. Kwa kukuelimisha kidogo ni kuwa kwa kawaida mito yote hupeleka maji aidha kwenye maziwa au baharini. Ziwa Victoria, ambalo ndiyo ziwa la maji baridi kubwa la tatu duniani, hupokea maji yake kutoka mito zaidi ya mia moja ya nchi za Tanzania, Kenya na Uganda. Tanzania ndiyo inayoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya mito inayopeleka maji hayo ziwa victoria ikiwemo Mto Mara, Mto Simiyu, Mto Mirongo, Mto Manonga na Mto Kagera - kwa kutaja michache.Nilpofika hopo pa Ethiopia wanatumia maji ya Ziwa Victoria kupitia mto Nile... Siku endelea tena kusoma hiyo post yako.
Yaani unaonyesha unauelewa mdogo sana. Labda rudi darasani tena kasome Geography vizuri uuelewe mto Nile.
Hivi unajua hata tunaongelea nini ? Ngoja ni-break it down simply...Sasa kama kwa shirika la umma faida sio monetary peke yake kwa nini mishipa inakotoka ukitaka TANESCO nayo i break-even??
Uganda wanajenga chanzo kipya cha umeme mto nile (mto kagera) kwenye mpaka wa uganda na tanzania kwa upande wa mrongo sijui sisi tunakwama wapi aisee wakati ni rasilimali ambayo iko upande wetu pia
sasa mgao unatoka wapi kama vyanzo vipo mkuu na maeneo mengi kagera yanatumia umeme kutoka grid ya UgandaMwingine huyu, Kwani Rusumo kuna nini
Ugumu uko wapi? Mbona tumepanga kupeleka gesi kutoka Mtwara hadi Mombasa kwa bomba? Mbona mafuta ya Uganda yatapelekwa hadi Tanga kwa bomba? Mbona crude oil inapelekwa kutoka Dar es Salaam hadiMZambia kwa bomba?How? Maji ya Ziwa Victoria yapelekwe Kidatu na Mtera! .Hivi somo la Geography lilifutwa?
Wewe bila shaka utakuwa unatokea tanesco. Umejitahidi kutetea masilahi yenu lakini wala haujaeweka unachokibishi.Harafu acha upotoshaji wa kipumbavu..
Awamu ya 3 ya Mkapa ulitaka kubinafsisha Tanesco so uamzi wa mwisho haukufikiwa ndani Baraza la Mawaziri baadae wakaja wakafuta huo mpango na kufanya modernisation ya management ya Tanesco ila kwa Miaka yote ile ya mchakato wa ubinafsishaji Hakuna uwekezaji mpya wa Serikali uliofanywa kwa sababu ya hiyo sintofahamu..
JK alirithi Nchi ikiwa Hakuna Tanesco yenye vyanzo vipya vya umeme na Uchumi unajua so tunrescue situation ndipo Sasa mitambo ya mafuta almaarufu majenereta ikakodiwa na kuketwa maana huwezi kaa bila umeme huku wakiendelea na uwekezaji wa umeme wa Gas..
So Hadi anaondoka Madarakani Umeme wa gas ndio ukawa na proportion kubwa kwenye energy mix ya 63%.
Mwendazake akaja akaishia kupuuza gas na kuanza mradi wa bwawa ambao haujulikani ungeisha lini,Miaka 5 ikapita bwawa liko 30%.
Amekuja Rais Samia akakutana na Hali Kama ya aliyoikuta JK, mvua zikapungua umeme wa maji ukapungua na gas ilipuuzwa , Sasa kaongeza Pesa Wizara ya Nishati ili kupata umeme wa gas wakati wanaendela na kukomaa na bwawa..
Naomba hapa muelewe awamu ya 4 haitaki.kuzima Moto inaenda na ufumbuzi wa kudumu,bwawa litakuwepo na gas na vyanzo vinginevyo vitaanzishwa ili kuanzia 2026 huko walau kazi ibaki ya mainatanance na sio generation.
Niwakati was kusimamisha miradi yote na kuhamia kwenye hili la umeme na majiAwamu ya baba wa taifa na ile ya mzee ruhusa hakukuwa na changamoto la katika katika kwa umeme maeneo ambayo huduma hii ilikuwa imeyafikia. Ni kweli kwamba maeneo hayo yalikuwa hasa kwenye miji mikubwa ya nchi. Shughuli za kiuchumi wa viwanda hazikuwa nyingi kama ilivyo sasa ambapo tumesambaza huduma hii ya umeme hadi kwenye karibu kila kijiji.
Jinsi uchumi wa viwanda ulivyozidi kukua na idadi ya watu kuongezeka, ndivyo changamoto ya umeme ilivyojitokeza na kukua kila kukicha. Zilianza hasa katika kipindi cha awamu ya tatu ya Mzee Mkapa ambaye suluhisho lake lilikuwa ni kuwapa kampuni ya makaburu wa South Africa kutuendeshea Tanesco yetu. Matokeo yake hatutayasahau. Tulipigwa tukapigika.
Ikaja awamu ya nne ya Mzee Kikwete. Wao wakaona suluhisho lake ni kukodi majenereta ya kuzalisha umeme wa dharura kutoka makampuni ya nje ya nchi kama yale ya Richmond, Dowans, Symbion na IPTL. Tukapigwa na kupigika hadi Waziri mkuu akatimuliwa na bunge la Mzee Sitta.
Ikaja awamu ya tano ya Mzee Magufuli. Nayo ikahangaika kwa kubana mafisadi na kuanzisha mahakama ya mafisadi kama suluhisho la changamoto hili la umeme. Kwa kiasi fulani kukawa na ahueni ya kuonesha kuwa ile ndoto ya Tanzania ya viwanda ifikapo 2025 labda ingaliweza kutimia.
Sasa imekuja awamu ya sita ya Mama yetu Mzee Salmia inayopenda kushirikisha wananchi wote kupata suluhisho la changamoto mbali mbali ya wananchi kidemokrasia. Kwa kuwa umeme wa bei rahisi kuliko wote ni ule unaotokana na maji. Na kwa kuwa nchi yetu imejariwa mito mingi na kuzungukwa na maziwa makubwa makubwa mengi: kwa nini maji ya ziwa kama lile la Victoria yasipekwe kwa mabomba huko kwenye bwawa la Mtera na lile la Nyerere ili wakati wa ukame kwenye mabwawa hayo, yakafunguliwa kuyajaza? Ethiopia wanatumia maji ya ziwa Victoria kupitia mto Nile kuzalisha maelfu ya maelfu ya MW za umeme hadi kuwauzia Wakenya.
Kwanini sisi tusitumie Ziwa hili ambalo liko kwetu? Kwani ni shilingi ngapi kupeleka maji ya ziwa letu huko? Kama hatuna hizo hela, tutafute pa kukopa kwani manufaa ya mkopo huu ni mkubwa sana. Hili litakuwa ni suluhisho la once and for all ya changamoto hili la umeme.
Tutaweza hata kuuza umeme nje ya nchi na kuachana na kuuza mahindi na mchele nje ya nchi wakati tukiwa tuna njaa. Tutaweza kupunguza sana bei ya umeme ili wananchi wote waweze kuitumia kama nishati rahisi ya kupikia na hivyo kuachana na ukataji wa miti wakitafuta kuni na mkaa. Mwananchi ataweza kutumia shilingi zisizozidi elfu tano tu kwa mwezi kwa nishati ya kupikia ya umeme.
Tanesco nao wataweza kukusanya matrilioni ya pesa kwani kila mwananchi atakuwa mteja wao. Viwanda vingi vitajengwa na kuzalisha bidhaa nyingi kwa bei nafuu. Kwa muda mfupi nchi yetu itakuwa upper middle income country chini ya uangalizi wa mama!
NB: Umeme utokanao na gesi mara zote bei yake ni ya juu sana (unaffordable to many of our people) ukilinganishwa na ule unaotokanq na maji. Umeme wa gesi ni kwa wakati wa dharura tu au kwa kuuza nje.
Gharama za uzalishaji usifikiri gesi ni bure, inanunuliwa kutoka kwa mwekezajiWakati gesi ipo Tele ...ni swala la kuongeza Tu generator za gesi baasi
Tusiwazie katokea tanesko au danida chamsingi nacho kitetea kinafaa au hakifai kwa masrahi ya taifaWewe bila shaka utakuwa unatokea tanesco. Umejitahidi kutetea masilahi yenu lakini wala haujaeweka unachokibishi.
Umeme wa gesi haujawahi kuachwa, tuliebdelea kutumia kwa wungi Sana 62% ya umeme wote ulikua wa gesiMiundombinu ya gesi ya mtwara ilikuwa tayari, kilichotakiw ni kuongeza tu uzalishaji - mwendazake naye akaja ya yake kwamba eti gesi yote ishauzwa kwamba tulipigwa vibaya sana - hivyo CCM wakamshauri aachane na huo mradi na hilo bomba lao kisha aanzishwa mradi wake wa Rufiji ili ajizolee misifa kwamba ametengeneza umeme wa uhakika kwa bei nafuu, sasa mradi wenyewe umedoda.
Tanzania hatujui tunachokitaka !!
Mnaongea kitu hamjui, umeme wa gesi sio renewable. Gesi hii inaunuliwa ukitegemea kwa asilimia kubwa kuzalisha umeme huko mbeleni kutaakua na shida. Hizo sources zingine ni gharama sana kuzalisha umemePesa zinazotumika kujenga mradi wa Nyerere ndio zilibidi ziende kufanya iyo miradi ya gesi, solar na makaa ya mawe.
Hii nchi inahitaji mipango endelevu siyo leo amekuja kiongozi huyu na mipango yake na baada ya miaka kumi anakuja mwingine na kufuta yote yale ya awali na kuanzisha ya kwake.Hii Nchi naona inahitaji Rais dikiteka zaidi ya Magufuli,maana hata historian inaonesha Marais madikiteta ndio sana uchungu na Nchi na huwa wanabadilisha mambo.
Kufumba macho sio njia ya kuzuia ngumi ya usoHizi kelele za mgao sijui zinatokea wapi, Nipo Dom kijijini umeme full time.
Jpm hakuendelea na gesi? Katika kipindi chake matumizi ya gesi kuzalisha umeme yaliongezeka kuliko vyanzo vingine.Hii nchi inahitaji mipango endelevu siyo leo amekuja kiongozi huyu na mipango yake na baada ya miaka kumi anakuja mwingine na kufuta yote yale ya awali na kuanzisha ya kwake.
Laiti kama JPM angeendeleza hiyo ya gesi wakati inatayarishwa hiyo ya Rufiji hydropower kwa uangalifu zaidi basi tungekuwa angalau na mipango inayoeleweka. Leo hii gesi ndiyo hivyo, hydropower haieleweki - yaani tupo tupo tu.
Awamu ya 6 ikiisha akija mwingine ataanza na mengine mapya na kutupa haya ambayo tayari yapo kwenye pipeline.
Hapo umenena maana huko kwenye vyanzo (upstream) tunaharibu kama hatuna akili halafu tunategemea maji hayo hayo yafike mpaka rufiji.Unajua prediction ya miaka 30 ijayo unadhani iyo mito na mabwawa yataendelea kuwepo. Hapa ndio kwanza umeanza.
Unajua kwamba kuna blue nile na white nile na vyanzo vyao ni tafauti?Ethiopia na Egypt wanategemea sana mto huu wa Nile kwa uhai wao kwani nchi hizo ni za ukame throughout. Hawa chanzo kingine cha maji.