#COVID19 Chanjo ni Lazima: Hoja ya Mbowe ina Mashiko

unataka kuniambia kwamba mwendazake alituongopea kuwa hakukuwa na korona

Asiyejua kuwa mwendazake alituongopea kuwa hakuna Corona na watu hawafi kwa Corona, bila shaka atakuwa pia kaaminishwa chanjo haina sababu na kaamini hivyo.

Bila shaka aliyeamini hivyo angali pia anaamini kwenye nyungu, michai chai, mikaratusi, malimao na matango pori mengine.

Hiiiiii bagosha!
 

Na huku ulaya Nani katudanganya. Acha Siasa. Hakuna chanjo ya lazima hasa kwa hizi za corona. Wengi tu hawataki. So sio huko kwenu tu.
 
Uko sahihi, Mbowe ameweka mbele maslahi ya watu wengi, anaamini kwa dhati ili kunusuru uhai wa watu wengi basi wachanjwe
Na Mbowe Mwenyewe kaonyesha mfano kuwa hayuko kimanenomaneno tu yeye keshapokea chanjo tayari

Mbowe angaliweza kuchagua kunyamaza kwa maslahi yake binafsi kisiasa.

Nani asiyejua kuwa pana watu wanaoufanyia siasa ugonjwa huu kwa maslahi yao binafsi bila kujali maisha ya watu?


Kwani haijulikani kuwa vigogo wengi tayari wameshachanjwa na kwa ubinafsi wao ni faida kwao (au haiwahusu) hata kama tukiaminishwa kuwa ugonjwa huu haupo sasa hata kama upo?

Mbowe ni wa kupigiwa mfano.
 
It's a waste of space same topic, six threads

Why come come here then? Why don't you stick to those to save yourself of some space?

Hiiiiii bagosha!
 
Kama watu wote hawatachanjwa hii chanjo yao itakuwa ni kupoteza muda. Chanzo iwe lazima ili kuokoa maisha ya wengi
 
Kama watu wote hawatachanjwa hii chanjo yao itakuwa ni kupoteza muda. Chanzo iwe lazima ili kuokoa maisha ya wengi

Hamna haja ya kuwalazimisha watu wasioelewa umuhimu wa kuchanjwa kama idadi inayotakiwa inaweza kufikiwa kwa uelewa wa wengine au kwa kuwaelimisha au kuwashawishi tu wasioelewa.

Hata hivyo kama threshold hiyo haiwezi kufikiwa, kujifunza mbinu mbadala tokea kwa ma quarter pin (Kagame na Museveni) ni halali.

Wajinga na wapumbavu wengi au wachache hawawezi kuachiwa ku dictate "fate" za wengine na hasa zihusuzo maisha au vifo.

"Fate" za maisha au vifo ni kwa walio na dhamana wala si vinginevyo.

Huo ndiyo ulio ukweli mchungu.
 

Asante Mkuu ni kweli najua ni suala la Mda tu chanjo itakua lazima. Tena naamini itakubalika iwe chanjo moja tu.

Ila Mimi Hapana.
 
Maudhui hayafanani japo ni same topic.

Ndiyo maana tumelazimika kujitambulisha mwanzo kabisa wa uzi ili kuhakikisha tunafahamiana kwanza, kwa maudhui na lugha.
 
Pale MACHAGA wanavyorukia hoja ya makengeza Mbowe 🀣🀣

 
Hivi hii nchi mbona watu hawajitambui? eti chanjo ni lazima! kachanje wewe siyo uwaamulie watu afya zao. Eti mbowe kasema yeye ni daktari? anajua nini kuhusu huo ugonjwa? harafu nyie mlikuwa wapi awamu ya 5? maana awamu hii mna kihere2 kweli! lazima muwe na mipaka ya kusema, serikali iwadhibiti maana mmekuwa wajinga kupitiliza sasa!
 
Asante Mkuu ni kweli najua ni suala la Mda tu chanjo itakua lazima. Tena naamini itakubalika iwe chanjo moja tu.

Ila Mimi Hapana.

Inahitaji ujasiri mkubwa kama wako, Mbowe, mimi na yule kuusema ukweli hata kama ni mchungu kama huu:

"Asante Mkuu ni kweli najua ni suala la Mda tu chanjo itakua lazima. Tena naamini itakubalika iwe chanjo moja tu."

Heshima kwako mkuu.

Hata hivyo kuwa na amani. Safari itakuwa hivi:

1. Wapo wanaouelewa muhimu wa chanjo. Wanaisubiri na kwa hakika, kwao imechelewa mno. Hao pia si wachache.
2. Wapo watakao elewa kirahisi kwenye elimu na uhamasishaji. Hasa hasa Mama Samia, Kabudi, Mbowe, Lissu, Jaffo, Msukuma, Kibajaji, Kishimba, Gwajima, na binamu zao watakapochukua jukwaa moja kuhamasisha.
3. Wapo watakao shawishika kirahisi ili kusafiri, fursa, nk

Inshallah, kwa hao tu threshold itakuwa imefikiwa na kiboko kitakuwa kimekuepuka wewe kama wewe.

Yote kheri, Mungu ni mwema. Tena ni mwema sana.

Niweke wazi: "Mimi na nyumba yangu tutachanjwa mwanzoni tu."
 
Mawazo ya hovyo sana kusema chanjo iwe ya lazima katika hili mbowe amefail kabisa chanjwa wewe na familia yako tu ya watu wengine yaache waamue wenyewe wala halihitaji kampeni
 
Mbowe aache upumbavu, ni ujinga kama nchi kuanza kuangaika na vijimafua visivyoweza kuua hata kifaranga cha kuku.
 
Pale MACHAGA wanavyorukia hoja ya makengeza Mbowe 🀣🀣

View attachment 1860492

Yego Masika. Wasiba Mo?

Uliuona utambulisho mwanzoni lakini?

!! πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ !!

Hii siyo zile ngoma mlizozowea kule Ukara zisizokesha.

Hiiiiii bagosha!
 
Yego Masika. Wasiba Mo?

Uliuona utambulisho mwanzoni lakini?

!! πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ !!

Hii siyo zile ngoma mlizozowea kule Ukara zisizokesha.

Hiiiiii bagosha!
Mimi ni Mzanaki zungumza kizanaki nikuelewe. Usiruke ruke kama umepakwa pili pili huko chuma.

 
Mawazo ya hovyo sana kusema chanjo iwe ya lazima katika hili mbowe amefail kabisa chanjwa wewe na familia yako tu ya watu wengine yaache waamue wenyewe wala halihitaji kampeni

Unayasoma wapi hayo uliyoyaandika jombi? Tulia kunywa maji soma. Elimu haina mwisho:



Hiiiiii bagosha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…