Chanjo ya COVID-19: Hivi wataalam hamjui ukweli au mmeamua kumpotosha Rais?

Chanjo ya COVID-19: Hivi wataalam hamjui ukweli au mmeamua kumpotosha Rais?

Kwani umelazimishwa mjomba mbona povu linakutoka, sigara imeandikwa hatari kwa afya yako na bado inauzwa na watu wanavuta si hiari yao sasa wewe povu la nini, hutaki acha sisi tunaotaka acha damu zigande 😅😅😅
Kamwambie Mama samia ambaye badala ya kuwaletea tu chanjo na kuja kuwadunga, yeye anataka kuchagua ipi salama wakati chanjo ni hiari tu.
 
unadhani kuna mtu yuko tayari!!!

wee waache wabongo tu,Mungu ndio anawajua vizuri.

kinachofata ni kulazimishana,zitadoda maabara nakwambia.subiri uone.
Mimi najiuliza hivi hawa wanaotaka chanjo humu ndio hawa hawa watu tuliyonao huku mitaani au hawa wengine? Hizo barakoa tu kuvaliwa huku mitaani ni issue halafu ndio watake kuchanjwa hawa watu?
 
Between the two evils, I go for the lesser. Hiyo ndiyo principle yetu. Maana yake ni kwamba;

1. COVID19 inaua kama huna kinga/ chanjo
Au
2. Ukiwa umechanja inaweza kukuletea complications zinazoweza kukusababisha kufa

Ni hivyo tu ndiyo Logic ya wanaotaka kuchanjwa, wamechagua a LESSER EVIL"
jamiiforums~p~CQqe4Z4t766~1.jpg
 
Zozote tutachoma tu kama wewe hutaki hama nchi ila chanjo lazima zije utake usitake, mambo ya kupangiana afya zetu iliisha 17 March
nashangaa corona iko nchini ila chanjo umeshindwa kuifata nje ya nchi,vipi huogopi kufa!!!
 
Marais waliopata chanjo msisanganyike kuwa ile ni chanjo, ni danganya toto mbele ta camera ili watu waamini haina madhara.

Hakuna raisi achome haya ma chanjo yasioeleweka.wanachoma dawa nyingine kuhamasisha watu wapate chanjo ili wao watimize mashart waliopewa.

Una uhakika au evidence ya unachoongea?
 
Habari ndugu wanaJF,

Jana kwenye mkutano wa rais na wanahabari nilimsikia akiongea confidently kuhusu kuagiza na kuanza kutumia chanjo za covid. Ieleweke kwamba hizo chanjo zilitolewa kwa dharura bila conclusive data za kitafiti na baadhi ya madhara ya muda mfupi yaliyokwishatokea ni kuganda kwa damu (blood clots), kushuka kwa kiwango cha chembechembe nyeupe za damu zinazohusika na kuganda kwa damu 'platelets' na kusababisha tatizo linalojulikana kitaalamu kama 'thrombocytopenia' matatizo ya mzio 'autoimmunity' ambapo chembe chembe za kinga zinashambulia viungo vya mwili na hii ikitokea kwenye viungo muhimu kama figo, ini na ubongo inaweza kupelekea vishindwe kabisa kufanya kazi 'organ failure'.

Hivi karibuni shirika la kuthibiti magonjwa la marekani CDC limeripoti kuongezeka kwa cases zinazoonyesha athari kwenye misuli ya moyo 'myocarditis' na hata kwenye kiwambo kinachozunguka moyo 'pericarditis' kwa vijana na watoto waliochanjwa chanjo ya korona inayotumia teknolojia ya mRNA. Pia, uchambuzi wa kitaalamu uliotolewa hivi karibuni umeonyesha ndani ya masaa 48 kibebeo cha chanjo inapodungwa mwilini 'lipid nanoparticles' kimeonekana hasa kwenye vifuko vya mayai kwa wanawake 'ovaries' na kwenye uboho wa mifupa 'bone marrow' jambo ambalo siyo la kawaida na linaweza kusababisha shida za uzazi kwa akina mama na matatizo ya kansa za damu 'leukemias' 'lymphomas' na ukizingatia hizi shida za kansa, madhara ya uzazi na hata mzio 'autoimmunity' zinaweza kuchukua muda mrefu hata miaka zaidi ya mitatu kudhihirika.

Je, wataalamu wamemshauri rais kwa kuzingatia utaalamu na up-to-date information zinazotolewa kuhusu madhara ya hizo chanjo? au wameamua tu kutoa ushauri unaoendeshwa na upepo wa ngoma inavyochezwa huko duniani kuhusiana na huu ugonjwa wa covid.

Mimi ningeshauri zitumike zaidi njia za kujikinga badala ya kuhimiza kampeni za chanjo ambayo ipo kwenye utafiti, kwa sababu ukishachanja hakuna namna ya kuondoa hiyo chanjo mwilini, kinachobaki inakuwa ni kupambana na madhara yanayoweza kutokea ndani ya muda mfupi, muda wa kati au muda mrefu.

Nawasilisha.​
mkuu hakuna aliyekuwekea bastola mdomoni ili uchanjwe.Chanjp ikija waache wenzako wajichannje wewe jifukize
 
Wewe ni Dr. Wa masuala gani? Isije ikawa ni mataga alielishwa tango na mwendazake
Huyu anayeita chembe sahani za damu (platelets) kuwa chembe nyeupe za damu (white blood cells) ni Daktari pori kutoka Kolomije. Hakuna kitu hapo.
 
Habari ndugu wanaJF,

Jana kwenye mkutano wa rais na wanahabari nilimsikia akiongea confidently kuhusu kuagiza na kuanza kutumia chanjo za covid. Ieleweke kwamba hizo chanjo zilitolewa kwa dharura bila conclusive data za kitafiti na baadhi ya madhara ya muda mfupi yaliyokwishatokea ni kuganda kwa damu (blood clots), kushuka kwa kiwango cha chembechembe nyeupe za damu zinazohusika na kuganda kwa damu 'platelets' na kusababisha tatizo linalojulikana kitaalamu kama 'thrombocytopenia' matatizo ya mzio 'autoimmunity' ambapo chembe chembe za kinga zinashambulia viungo vya mwili na hii ikitokea kwenye viungo muhimu kama figo, ini na ubongo inaweza kupelekea vishindwe kabisa kufanya kazi 'organ failure'.

Hivi karibuni shirika la kuthibiti magonjwa la marekani CDC limeripoti kuongezeka kwa cases zinazoonyesha athari kwenye misuli ya moyo 'myocarditis' na hata kwenye kiwambo kinachozunguka moyo 'pericarditis' kwa vijana na watoto waliochanjwa chanjo ya korona inayotumia teknolojia ya mRNA. Pia, uchambuzi wa kitaalamu uliotolewa hivi karibuni umeonyesha ndani ya masaa 48 kibebeo cha chanjo inapodungwa mwilini 'lipid nanoparticles' kimeonekana hasa kwenye vifuko vya mayai kwa wanawake 'ovaries' na kwenye uboho wa mifupa 'bone marrow' jambo ambalo siyo la kawaida na linaweza kusababisha shida za uzazi kwa akina mama na matatizo ya kansa za damu 'leukemias' 'lymphomas' na ukizingatia hizi shida za kansa, madhara ya uzazi na hata mzio 'autoimmunity' zinaweza kuchukua muda mrefu hata miaka zaidi ya mitatu kudhihirika.

Je, wataalamu wamemshauri rais kwa kuzingatia utaalamu na up-to-date information zinazotolewa kuhusu madhara ya hizo chanjo? au wameamua tu kutoa ushauri unaoendeshwa na upepo wa ngoma inavyochezwa huko duniani kuhusiana na huu ugonjwa wa covid.

Mimi ningeshauri zitumike zaidi njia za kujikinga badala ya kuhimiza kampeni za chanjo ambayo ipo kwenye utafiti, kwa sababu ukishachanja hakuna namna ya kuondoa hiyo chanjo mwilini, kinachobaki inakuwa ni kupambana na madhara yanayoweza kutokea ndani ya muda mfupi, muda wa kati au muda mrefu.

Nawasilisha.​
Mkuu


Hatuna watalaamu walio tayari kusimamia ukweli na kujitoa mhanga hata wakitishiwa maisha au kufukuzwa kazi wanapelekeshwa na wanasiasa ambao huwa ndio chanzo cha maangamizi ya binadamu. Kuna unafiki uliotopea miongoni mwao wakitenda kumfurahisha mwenye bakuli la chakula na huduma muhimu kwa ajili yao
 
unadhani kuna mtu yuko tayari!!!

wee waache wabongo tu,Mungu ndio anawajua vizuri.

kinachofata ni kulazimishana,zitadoda maabara nakwambia.subiri uone.
Mimi niko tayari, usifanye conclusion kwa niaba ya wote
 
Huyu anayeita chembe sahani za damu (platelets) kuwa chembe nyeupe za damu (white blood cells) ni Daktari pori kutoka Kolomije. Hakuna kitu hapo.
Nimekwambia mimi ni mtaalamu wa kutohoa maneno ya kiingereza kwenda kiswahili au unataka kujipima na biology yako ya fomu foo.
 
Back
Top Bottom