Ndiyo, hiyo biology ya fomu foo mnayofundishwa platelets hazipo kwenye kundi la chembe nyeupe za damu, ukisoma zaidi utapata maarifa kiundani dogo, kwa sasa kalili hivyo hivyo ulivyofundishwa.......Hahahahahah.....biology ya form foo tena?
Atakuwa anasubiria ya jero...nashangaa corona iko nchini ila chanjo umeshindwa kuifata nje ya nchi,vipi huogopi kufa!!!
Sawa tumekusoma lakini kumbuka Mama aliteua jopo la wataalam kupitia yote hayo na kumshauri nini la kufanya na technology ya mRNA katika Corona vaccine inatumika na vaccines za Pfizer na Moderna ambazo ni chanjo za USA na mpaka sasa watu karibi 70% ambao ni 200 millions kati ya 300 millions ya wamerekani wamepata chanjo ya kwanza.Habari ndugu wanaJF,
Jana kwenye mkutano wa rais na wanahabari nilimsikia akiongea confidently kuhusu kuagiza na kuanza kutumia chanjo za covid. Ieleweke kwamba hizo chanjo zilitolewa kwa dharura bila conclusive data za kitafiti na baadhi ya madhara ya muda mfupi yaliyokwishatokea ni kuganda kwa damu (blood clots), kushuka kwa kiwango cha chembechembe nyeupe za damu zinazohusika na kuganda kwa damu 'platelets' na kusababisha tatizo linalojulikana kitaalamu kama 'thrombocytopenia' matatizo ya mzio 'autoimmunity' ambapo chembe chembe za kinga zinashambulia viungo vya mwili na hii ikitokea kwenye viungo muhimu kama figo, ini na ubongo inaweza kupelekea vishindwe kabisa kufanya kazi 'organ failure'.
Hivi karibuni shirika la kuthibiti magonjwa la marekani CDC limeripoti kuongezeka kwa cases zinazoonyesha athari kwenye misuli ya moyo 'myocarditis' na hata kwenye kiwambo kinachozunguka moyo 'pericarditis' kwa vijana na watoto waliochanjwa chanjo ya korona inayotumia teknolojia ya mRNA. Pia, uchambuzi wa kitaalamu uliotolewa hivi karibuni umeonyesha ndani ya masaa 48 kibebeo cha chanjo inapodungwa mwilini 'lipid nanoparticles' kimeonekana hasa kwenye vifuko vya mayai kwa wanawake 'ovaries' na kwenye uboho wa mifupa 'bone marrow' jambo ambalo siyo la kawaida na linaweza kusababisha shida za uzazi kwa akina mama na matatizo ya kansa za damu 'leukemias' 'lymphomas' na ukizingatia hizi shida za kansa, madhara ya uzazi na hata mzio 'autoimmunity' zinaweza kuchukua muda mrefu hata miaka zaidi ya mitatu kudhihirika.
Je, wataalamu wamemshauri rais kwa kuzingatia utaalamu na up-to-date information zinazotolewa kuhusu madhara ya hizo chanjo? au wameamua tu kutoa ushauri unaoendeshwa na upepo wa ngoma inavyochezwa huko duniani kuhusiana na huu ugonjwa wa covid.
Mimi ningeshauri zitumike zaidi njia za kujikinga badala ya kuhimiza kampeni za chanjo ambayo ipo kwenye utafiti, kwa sababu ukishachanja hakuna namna ya kuondoa hiyo chanjo mwilini, kinachobaki inakuwa ni kupambana na madhara yanayoweza kutokea ndani ya muda mfupi, muda wa kati au muda mrefu.
Nawasilisha.
Tunashukuru kwa kushiriki, ngoja wataalamu hasa waje....Sawa tumekusoma lakini kumbuka Mama aliteua jopo la wataalam kupitia yote hayo na kumshauri nini la kufanya na technology ya mRNA katika Corona vaccine inatumika na vaccines za Pfizer na Moderna ambazo ni chanjo za USA na mpaka sasa watu karibi 70% ambao ni 200 millions kati ya 300 millions ya wamerekani wamepata chanjo ya kwanza.
Kuna chanjo nyingine za Corona ambazo hazitumii
mRNA technology haujacomment lolote kwenye hizo chanjo.
Madhara kwa vaccines ya aina yoyote yapo lakini inaweza kuwa ni margin ndogo sana, katika hao 200 Millions ya wamarekani ni wachache sana ndio wanapata hizo athari.
Sasa ulitaka chanjo zisitumike na ugonjwa uenee na kuzidi kuuwa watu duniani
sababu ya hizo athari kwa watu wachache sana.
Mambo ya wataalam waachie wataalam usituletee over generalization za conclusions zako ambazo hazina utafiti kamili.
Nimeipenda avatar yako...Hujalazimishwa kuchanja,nyie endeleeni kumuenzi dikteta.
Mimi sinaga ubishi wa kijinga.Mimi na familia yangu tutachanja kama tulivyochanja chanjo ya pepo punda na kifaduro na suruaWewe utafanya kipi, usiwasemee wengine....
Kila la heri...Mimi sinaga ubishi wa kijinga.Mimi na familia yangu tutachanja kama tulivyochanja chanjo ya pepo punda na kifaduro na surua
Nyie endeleeni kujifukiza
Naomba tusisambaze habari ambazo hatujachungulia, Ulaya hawakukataa Covishield (=Astrazeneca kutoka Uhindi). Inaonekana kiwanda cha Uhindi wamesahau hadi sasa kuomba kibali kwa dawa kwa nchi za Ulaya (jinsi ilivyo kwa kila chanjo, ipate kibali cha Mamlaka ya Tiba Ulaya)
Its not free of charge!! The government pays for it by using tax payers money!Pigweni tu chanjo its free of charge!
Mbona afrika waliochanjwa ni kidogo sana lakini maambukizi yamepungua sana ukilinganisha na 2020? Kilichopunguza maambukizi ni natural immunity wala siyo chanjo!Wewe una uhakika gani kuwa wanachoma kitu kingine na siyo chanjo ya covid? Wewe ndiye unayewacoma Marais wote hizo chanjo feki? Chanjo zimepunguza kwa kiasi kikubwa maambukizi ya Covid huko USA na maeneo mengine Duniani. Acha uongo wa kishamba wewe.
Kumbe umefanya utafiti? Kinachokinga Waafrika hadi sasa ni 1) idadi ndogo ya wazee (maana watoto halafu vijana mara nyingi hawana matatizo makubwa). Halafu 2) tabia ya watu wengi kuishi vijijini na kutosafiri sana. Halafu 3) hali ya watu wengi ambao wanakaa mazingira ambako hewa inapita; wengi hukalia nyumba bila madirisha yenye kioo hivyo hewa inapita.Mbona afrika waliochanjwa ni kidogo sana lakini maambukizi yamepungua sana ukilinganisha na 2020? Kilichopunguza maambukizi ni natural immunity wala siyo chanjo!
Waambie hao...Hali ni tete ndugu zanguni. Watu wanapoteza life, hili gonjwa msilichukulie poa. Tujihadhari, kumbi za harusi, sherehe za aina yoyote tuepukane nayo bandugu. Mkitaka kujua ukweri nendeni hospitalini mukajionee hali inatisha bandugu.
Waambie hao...
Nenda gengeni ukale kama hujala mchana huu wewe haya mambo yamekuzidi kimo acha kutoa mawazo fyongo hapa. Dunia nzima wanachanja, kuanzia Western countries mpaka Asia bial kusahau warusi nk na soon robo tatu ta dunia itakuwa imechanjwa halafu wewe ambaye upeo wako hauna tofauti na kima unaleta bla bla bla zako hapa. Acha chanjo ije kama wewe hutaki kuchanja achia wenye akili wachanje.
Unaweza kujenga hoja kwa namba?
Weka chanjo gani ina matatizo gani, hususan blood clots.
Weka wangapi wamepata hizo chanjo.
Wangapi wamepata blood clots.
Wangapi wamefariki kwa blood clots.
Halafu, linganisha na vifo vitakavyotokea kwa watu wa idadi hiyohiyo ambao hawatachanjwa kwa kuogopa blood clots.
Kuzungumzia chanjo bila kunyambulisha chanjo gani ni uvivu, kwa sababu, si chanjo zote ziko sawa.Kwani mkuu wamekwambia ukichanjwa hautaugua tena Corona...
Ukipata maambukizi utaugua na hio chanjo yako inaweza ikawa tatizo kwako vile vile madhara yapo ya papo kwa papo na mengine ni ya muda mrefu ndio maana nchi zingine wataalamu wameomba zistop kwanza nasisitiza sio Magufuli alioomba chanjo istop kwanza ni wanasayansi wa nchi za ulaya...ila tofauti ni kwamba Magufuli aliwatangulia kusema na wao wakafuata
Takwimu za watu waliopatwa na madhara ya chanjo inasemekana ni nyingi kuliko zinazotangazwa ...
Ushasema BBC....Kuzungumzia chanjo bila kunyambulisha chanjo gani ni uvivu, kwa sababu, si chanjo zote ziko sawa.
Leo nilikuwa nasikiliza BBC World Service wanasema Indonesia kuna madaktari wamechanjwa chanjo mbili za Mchina na bado wanaambukizwa Coronavirus na kufa.
Sasa hapo watu wamekuwa specific kutaja chanjo za China, hata kama kuna kuchunguza wanaanza kuchunguza za China.
Sasa chanjo haziwezi kukosa matatizo, huu ugonjwa mpya.
Lakini, chanjo gani? Zina matatizo gani? Hatari ikoje? Hatari ya kuchanjwa na kutochanjwa ipi ni kubwa?
Maana kama kuna chanjo ina nafasi ya kukuua mtu mmoja kwa kila watu laki moja wanaochanjwa, halafu ukipata ugonjwa unakufa kati ya watu 100 watakaougua, na una nafasi kubwa ya kuambukizwa, hapo unaweza kuwa justified kupiga chanjo.
Wewe ukiongelea chanjo hata hujaitaja chanjo gani nakuona unaongea vitu usivyovijua.
Sawa. Usichanje. Wanaotaka waache wachanje.Ushasema BBC....
Mkuu jiongeze chanjo ni biashara za wenye power they control everything mpaka hizo media..takwimu utazisubiria sana..
Ushaambiwa na baadhi ya wanasayansi madhara yanayotokana na hio chanjo...inatosha