Chimbuko na Upotofu wa kanisa la Waadventista Wasabato

Chimbuko na Upotofu wa kanisa la Waadventista Wasabato

Walisema uongo wa hiyo tarehe ya mwisho wa Dunia/ kurudi kwa Bwana Yesu. Kwa maana hiyo alivunja ile amri "Usishuhudie Uongo." Na Biblia iko wazi kwamba nabii wa uongo utamjua akikutabiria na baadaye akikuambia fuata njia ya utabiri wake ambayo ni ya upotovu inayokutoa kwa Mungu. Kwa hiyo Wasabato wanafuata njia ya upotovu wa Ellen na wenzake, iliyosema siku ya mwisho wa dunia ni 31/10/1884 ambayo ilipita bila walichotabri kutimia.

Neno la Mungu linasema na liko wazi kuwa hatujui siku wala saa atakayorudi Bwana wa Majeshi. Sitaki kuamini Ellen na wenzslake walikuwa hawajui hili Neno, na rudia sitaki kuamini hivyo.
Sijui ni mangapi yamepotoshwa. Hilo moja ni dhahiri.
Hyo siku wengi waliitafsiri tofauti haikua siku ya mwisho duniani...
Na hakuna ajuaye siku siku ya mwisho hata malaika walioko mbinguni hawajui hilo
 
Walisema uongo wa hiyo tarehe ya mwisho wa Dunia/ kurudi kwa Bwana Yesu. Kwa maana hiyo alivunja ile amri "Usishuhudie Uongo." Na Biblia iko wazi kwamba nabii wa uongo utamjua akikutabiria na baadaye akikuambia fuata njia ya utabiri wake ambayo ni ya upotovu inayokutoa kwa Mungu. Kwa hiyo Wasabato wanafuata njia ya upotovu wa Ellen na wenzake, iliyosema siku ya mwisho wa dunia ni 31/10/1884 ambayo ilipita bila walichotabri kutimia.

Neno la Mungu linasema na liko wazi kuwa hatujui siku wala saa atakayorudi Bwana wa Majeshi. Sitaki kuamini Ellen na wenzslake walikuwa hawajui hili Neno, na rudia sitaki kuamini hivyo.
Sijui ni mangapi yamepotoshwa. Hilo moja ni dhahiri.
CHief nakukaribisha ujiunge na kanisa linaloamini katika misingi ya Biblia
 
PAPA AMERUHUSU USHOGA SO SIKUSHANGAI.

BADALA YA KUJIBU HOJA UNALETA UMEA WA KISH#O#GA
Siamini kumtusi mtu ni roho ya Kristo.
Kama unategemea akili zako kujibu hoja,huwezi kamwe kumshawishi hata muuaji akuelewe.

Si busara kumdhalilisha mtu kiasi hicho.Hii ni sawa na ugaidi.Unamtisha mtu ili akusikilize wewe na kukufuata.
 
Hyo siku wengi waliitafsiri tofauti haikua siku ya mwisho duniani...
Na hakuna ajuaye siku siku ya mwisho hata malaika walioko mbinguni hawajui hilo

Kanisa huanzia nyumbani chini ya maongozi ya Roho Mtakatifu. Asante kwa ukaribisho wewe endelea huko uliko na mimi na endelea huku maadamu wote tunayatenda yale yaliyo mapenzi ya Mungu wa Mbinguni.

Hata wanafunzzi wa Yesu walikuja kushitaki kwa Bwana Yesu pale walipowaona watu wengine huko wakikemea kwa jina la Yesu. Bwana Yesu akasema ni sawa as long as hawako kinyume na sisi. Kemea ushoga kanisani upinge na ukatae kwa nguvu zote kwa msaada wa Mungu. Kwani hiyo ni sawa kabisa sio kuhangaika kupiga vita kusali jumapili.
 
Yako mambo ukijitafakarisha kwa umakini unabaki huna majibu. Watu wanao mtaja Ellen White na kunukuu maandiko yake mara nyingi tu wakihubiri na kufundisha wanawashangaa na kupiga vita wenzao wanao mtaja Mariamu Mama wa Bwana Yesu. Hivi Ellen na Mariamu Mama wa Yesu ambaye Malaika alisema umebarikiwa kuliko wanawake wote atiliwe kweshi maki anapotajwa, kweli. Mariamu Mama wa,Yesu Kabarikiwa kuliko hata Ellen hili nalo halijulikani.

Kweli shetani ni muongo na ukicheza naye atakupepeta kama makapi ya ngano.
 
Wasabato mnasomea wapi hiyo theology 😂😂😂

Si Wasabato tu mambo ya Imani yamekuwa ya kifundishwa kwa kukaririsha wahusika huku wakiwa wanatishwa. Kwa hiyo wengi hawajiulizi wala kutafakari kile wanacho ambiwa wakifundishwa. Matokeo yake wanakuwa madodoki ya kufyonza kila kitu kasisi au kiongozi wake wa imani anachosema.

Kwa Ukristo si hivyo. Bwana Yesu alisema wazi kuhusu siku za mwisho na manabii wa uongo. Kuhusu kuzijaribu roho nk. Na alijua mwanadamu peke yake hawezi kushindana na shetani na hila zake. Ndiposa akatuletea msaidizi wa karibu, Roho Mtakatifu/Roho wa Mungu/ Roho wa Kristo/ Roho wa Kweli. Roho Mtakatifu anaishi ndani ya kila muumini aliye mpokea Bwana Yesu akabatizwa.
Na katika Neno lake akasema wazi Mungu ni Roho nao wamuabuduo humuabudu katka Roho na Kweli.
 
Yaani kama hili gazeti lote limekaa siku zote na watu 4 pekee ndo wame like maana yake hujaeleweka.. nilitegemea baada ya kueleza mapungufu na kasoro za kanisa la Waadventista wasabato, kuhusu Siku ya saba na Huduma ya Yesu katika Patakatifu pa mbinguni ungekuja sasa kutueleza ni Dini ipi au dhehebu gani sasa ambalo halina mapungufu na tunapaswa kuabudu huko kwa mjibu wa Maandiko matakatifu.

Badala yake umeishia tu kuponda misingi na mafundisho na kutuambia utakuja na Andiko linaloelezea siku gani tukusanyike, Jumamosi au jumapili, huku Ukisahau kuna watu wanakusanyika jumatatu, jumanne, jumatano, Alhamis, na ijumaa. Huku pia ukisahau hata kukusanyika baa au kwa ajili ya maandamano yote ni mikusanyiko..

SOMA VITABU UPATE MAARIFA YA KUMJUA MUNGU , Acha kuwa unadokoa dokoa mistari ili upate kinachokufurahisha..
 
Yaani kama hili gazeti lote limekaa siku zote na watu 4 pekee ndo wame like maana yake hujaeleweka.. nilitegemea baada ya kueleza mapungufu na kasoro za kanisa la Waadventista wasabato, kuhusu Siku ya saba na Huduma ya Yesu katika Patakatifu pa mbinguni ungekuja sasa kutueleza ni Dini ipi au dhehebu gani sasa ambalo halina mapungufu na tunapaswa kuabudu huko kwa mjibu wa Maandiko matakatifu.

Badala yake umeishia tu kuponda misingi na mafundisho na kutuambia utakuja na Andiko linaloelezea siku gani tukusanyike, Jumamosi au jumapili, huku Ukisahau kuna watu wanakusanyika jumatatu, jumanne, jumatano, Alhamis, na ijumaa. Huku pia ukisahau hata kukusanyika baa au kwa ajili ya maandamano yote ni mikusanyiko..

SOMA VITABU UPATE MAARIFA YA KUMJUA MUNGU , Acha kuwa unadokoa dokoa mistari ili upate kinachokufurahisha..
Nilishasoma na nimasoma sana mtoto wa ellen white
 
Yako mambo ukijitafakarisha kwa umakini unabaki huna majibu. Watu wanao mtaja Ellen White na kunukuu maandiko yake mara nyingi tu wakihubiri na kufundisha wanawashangaa na kupiga vita wenzao wanao mtaja Mariamu Mama wa Bwana Yesu. Hivi Ellen na Mariamu Mama wa Yesu ambaye Malaika alisema umebarikiwa kuliko wanawake wote atiliwe kweshi maki anapotajwa, kweli. Mariamu Mama wa,Yesu Kabarikiwa kuliko hata Ellen hili nalo halijulikani.

Kweli shetani ni muongo na ukicheza naye atakupepeta kama makapi ya ngano.
Ila wasabato wanakuambia ellen white ni bora kuliko mariamu
Yaan kama ulivyo sema
Kweli shetani ni muongo na ukicheza naye atakupepeta kama makapi ya ngano.
Nahisi ellen ni wakala wa shetani
 
PAPA AMERUHUSU USHOGA SO SIKUSHANGAI.

BADALA YA KUJIBU HOJA UNALETA UMEA WA KISH#O#GA
🤣🤣🤣
Papa amesema ushoga ni dhambi kama zambi nyingine
Kwa hiyo hatuwezi wazuia wasije kanisani eti kwa kuwa ni shoga
Je wewe ni mkamilifu huna zambi?

Usiwe unakurukupa kushutumu kwa chuki zako bila kutafakari

Wasabato mnamuona ellen white ni bora kuliko Mariamu

Kweli shetani ni muongo na ukicheza naye atakupepeta kama makapi ya ngano.
Ellen white ni wakala wa shetani sio bure
 
Yaani kama hili gazeti lote limekaa siku zote na watu 4 pekee ndo wame like maana yake hujaeleweka.. nilitegemea baada ya kueleza mapungufu na kasoro za kanisa la Waadventista wasabato, kuhusu Siku ya saba na Huduma ya Yesu katika Patakatifu pa mbinguni ungekuja sasa kutueleza ni Dini ipi au dhehebu gani sasa ambalo halina mapungufu na tunapaswa kuabudu huko kwa mjibu wa Maandiko matakatifu.

Badala yake umeishia tu kuponda misingi na mafundisho na kutuambia utakuja na Andiko linaloelezea siku gani tukusanyike, Jumamosi au jumapili, huku Ukisahau kuna watu wanakusanyika jumatatu, jumanne, jumatano, Alhamis, na ijumaa. Huku pia ukisahau hata kukusanyika baa au kwa ajili ya maandamano yote ni mikusanyiko..

SOMA VITABU UPATE MAARIFA YA KUMJUA MUNGU , Acha kuwa unadokoa dokoa mistari ili upate kinachokufurahisha..
Sawa kama umesoma wewe gazeti langu inatosha
 
KIXI nimesoma na nimeelewa kwamba unaelekea kuupata ukweli. Endelea kuyasoma maandiko, na utapona.

Yesu, Mitume wote waliitunza sabato. Bwana alienda kwenye masinagogi siku ya Bwana. Tena alikuwa anafundisha huko. Luka 6;6. .

Unataka watu wasishike amri za Mungu?

Ufunuo 14:12 "Hapo ndipo penye subira ya watakatifu hao wazishikao amri za Mungu na imani ya Yesu."

Hayo mengine unayaleta kutaka kujichanganya mwenyewe tu. Ila ukitulia utajua, bila amri za Mungu wnadamu wataanguka na hata hiyo Neema itapotea kabisa. Neema ndio intufanya hadi sasa tunaishi pamoja na zambi hili ila siku ya Mwisho hukumu inatoka kwa makosa uliyoyafanya. Makosa ni mambo unayoyafanya kinyume cha sheria.

Kuhusu kuingia patakatifu pa patakatifu.. Nitakuletea ndondo nyingine zaidi. Ila ukweli kila kitu kiko wazi.

Wasabato wanaamini yesu na huwa hawamuombi mtu wala binadamu yeyote isipokuwa Yesu mwokozi.
 
Yaani kama hili gazeti lote limekaa siku zote na watu 4 pekee ndo wame like maana yake hujaeleweka.. nilitegemea baada ya kueleza mapungufu na kasoro za kanisa la Waadventista wasabato, kuhusu Siku ya saba na Huduma ya Yesu katika Patakatifu pa mbinguni ungekuja sasa kutueleza ni Dini ipi au dhehebu gani sasa ambalo halina mapungufu na tunapaswa kuabudu huko kwa mjibu wa Maandiko matakatifu.

Badala yake umeishia tu kuponda misingi na mafundisho na kutuambia utakuja na Andiko linaloelezea siku gani tukusanyike, Jumamosi au jumapili, huku Ukisahau kuna watu wanakusanyika jumatatu, jumanne, jumatano, Alhamis, na ijumaa. Huku pia ukisahau hata kukusanyika baa au kwa ajili ya maandamano yote ni mikusanyiko..

SOMA VITABU UPATE MAARIFA YA KUMJUA MUNGU , Acha kuwa unadokoa dokoa mistari ili upate kinachokufurahisha..

Jamaa AMEANDIKA Pumba sana.

Kwakweli Huyu jamaa nimemdharau mno.

UZI WAKE NI TAKATAKA.
 
''The Great Disappointment'' 1844 ya Willium Miller ndio iliyomaliza sana imani za watu juu ya Usabato. Ni sawa tu na alichofanya Kibwetere na yule Mchungaji wa juzi hapo Kenya
Waadventista wasabato huipokea Biblia kama kanuni yao pekee na hushika baadhi ya misingi ya imani kuwa ndiyo mafundisho ya mabadiliko matakatifu. Imani hizi, kamazilivyoorodheshwa hapa, hufanya welekevu wa kanisa na udhihirisho wa mafundisho ya mabadiliko. Masahihisho ya kauli hizi yanaweza kutegemewa katika kikao cha Halmashaurikuu wakati kanisa likiongozwa na Roho Mtakatifu kwenye ufahamu ulio kamili zaidi ya ukweli wa Biblia au linapopata lugha iliyo bora zaidi ya kuelezea mafundisho ya Neno Takatifu la Mungu.

1.Maandiliko Matakatifu
Maandiko Matakatifu, yaani Agano la kale na Jipya ndiyo Neno la Mungu lililoandikwa,likatolewa kwa uvuvio wa Mungu, kupitia kwa watu watakatifu walionena na kuandika kamawalivyoagizwa na Roho Mtakatifu. Ndani ya neno hili, Mungu amemkabidhi mwanadamu maarifa yaliyo lazima kwa ajili ya wokovu. Maandiko matakatifu ni ufunuo usioweza kukosa wa mapenzi yake. Ndiyo upeo wa tabia, kipimo cha uzoefu, ufunuo thabiti wenye mamlaka wa mafundisho ya imani, na kumbukumbu aminifu ya matendo ya mungu katika historia. (2Petro 1:20,21. 2Timotheo 3:16,17. Zaburi 119: 105. Mithal 30: 5,6. Isaya 8:20. Yoh 17:17. 1Wathe 2:13. Waeb4:12.)

2.Utatu Mtakatifu
Kuna Mungu mmoja: Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, umoja wa nafsi tatu za milele. Mungu hapatikani na mauti, mwenye nguvu zote, ajuaye yote, zaidi ya yote, na aliyeko daima. Yeye hana mwisho na ni zaidi ya ufahamu wa kibinadamu, hata hivyo anafahamika kupitia kujifunua kwake binafsi. Milele zote yu astahili kuabudiwa, kusujudiwa, kutumikiwa na viumbe vyote. (kumb 6:4. Mith 28:19. 2kor 13:14. Waef 4:4-6. 1Petr 1:2 1Tim 1:17 Ufunuo 14:7)

3.Baba
Mungu Baba wa milele ndiye muumbaji, Chimbuko, Mtengenezaji, na Mfalme wa viumbe wote. Ni mwenye haki na Mtakatifu, Mwingi wa rehema,, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, na mwingi wa uthabiti wa upendo na uaminifu. Tabia na uwezo vilivyodhihirishwa ndani ya Mwana na Roho Mtakatifu pia ni ufunuo wa Baba. (Mwanzo 1:1 Ufu 4:11.
1wakor 15:28. Yoh 3:16. 1Yoh 4:8. 1Tim 1:17. Kut 34:6,7. Yoh 14:9).

4.Mwana
Mungu Mwana wa milele alifanya mwili katika Yesu Kristo. Kupitia kwake vitu vyote viliumbwa, tabia ya mungu imefunuliwa, wokovu wa wanadamu unakaribishwa na ulimwengu unahukumiwa. Milele zote Mungu kweli, Alifanyika mwanadamu kweli, Yesu aliye kristo. Alichukuliwa mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu na kuzaliwa na bikira Mariamu. Akaishi na kupitia uzoefu majaribu kama mwanadamu, lakini kwa ukamilifu alioonyesha kwa mfano wa haki na u[endo wa Mungu. Kwa miujiza yake alidhihirisha uwezo wa Mungu na alithibitishwa kama Masihi aliyeahidiwa. Aliteseka na kufa kwa hiari msalabani kwa ajili ya dhambi zetu, na kama mbadala wetu, Alifufuliwa kutoka kwa wafu, na akapaa kuhudumu katika hekalu la mbinguni kwa niaba yetu. Atakuja tena katika utukufu kwa ajili ya ukombozi wa mwisho wa watu wake na urejeshwaji wa vitu vyote. (Yoh 1: 1-3,14. Wakol 1: 15-19,. Wafil 2:5-11. Yoh 10:30, 14:9 Warum 6:23. 2Wakor 5:17-19.Yoh 5:22. 1Wakor 15:3,4. Luka 1:35. Yoh 14:1-3)

5.Roho Mtakatifu
Mungu Roho wa milele alikuwa mtendaji pamoja na Baba na Mwana katika uumbaji, kufanyika mwili, na katika ukombozi. Aliwavuvia waandishi wa mabadiliko matakatifu. Alijaza maisha ya kristo na uwezo. Huwavuta na kuwasadikisha wanadamu, na wale wanaoitikia huwafanya upya na kuwabadilisha katika sura ya Mungu. Akipelekwa na Baba na Mwana ili kuwa siku zote pamoja na watoto wake, hutoa karama za kiroho kwa kanisa, huliwezesha kumshuhudia kristo, na kwa upatano wa maandiko uliongoza kwenye ukweli wote. (Mwa 1,2. Luka 1:35, 4:18. Mdo 10:38. 2Petr 1:21. 2Wakor 3:18. Yoh 14:16-18,26, 15:26,27, 16:7-13)

6.Uumbaji
Mungu ni muumba wa vitu vyote, na amefunua katika maandiko uhalisi wa tukio la
shughuli zake za uumbaji. Katika siku sita Bwana alizifanya “Mbingu na Nchi” na vitu vyote
vilivyoko hai juu ya nchi, akastarehe siku ya saba ya juma lile la kwanza. Na hivyo
akaanzisha sabato kama kumbukumbu ya milele ya kukamilika kwa kazi yake ya uumbaji.
Mwanaume na Mwanamke wa kwanza walifanywa kwa mfano wa Mungu kama upeo wa
kazi yake ya Uumbaji, wakapewa utawala juu ya ulimwengu, na wakaagizwa kuajibika na
utunzaji wake. Wakati ulimwengu ulipomalizika kila kitu kilikuwa “ni chema sana”
ukitangaza utukufu wa Mungu. (Mwa 1,2. Kut20:8-11. Zab 19:1-6, 33:6-9, 104. Waebr
11:3)

7.Asili ya Mwanadamu
Mwanaume na Mwanamke walifanyawa kwa mfano wa Munguwakiwa kila mmoja na nafsi
yake, uwezo na uhuru wa kufikirina kutenda. Ingawa waliumbwa viumbe huru, kila mmoja
ni umoja wa nafsi isiyogawanyika ya mwili, akili na roho, akimtegemea Mungu kwa uhai na
pumzi na mengine yote. Wakati wazazi wetu wa kwanza walipomwasi Mungu, walikana
utegemezi wao kwa Mungu na wakaanguka kutoka hadhi yao ya juuchini ya Mungu. Sura
ya Mungu iliyopo ndani yao ikaharibika na wakawa chini ya mauti. Wazao wao hushiriki
asili hii ya kuanguka na matokeo yake. Wanazaliwa wakiwa na udhaifu na mivuto ya
kuelekea kwenye uovu. Lakini Mungu katika kristo aliupatanisha ulimwengu na nafsi yake,
na kwa Roho wake hurejesha ndani ya mwanadamuwatubuo sura ya muumba wao.
Wakiwa wameumbwa kwa ajili ya utukufu wa Mungu, wanaitwa kumpenda na kupendana
wao kwa wao na kutunza mazingira yao.(Mwa 1:26-28, 2:7. Zab 8:4-8. Mdo 17:24-28. Mwa
3. Zab 51:5 War 5:12:17. 1Yoh 4:7,8,11,20. Mwa 2:15

8.Pambano kuu
Jamii yote ya wanadamu sasa inahusika katika pambano kuu baina ya kristo na shetani
kuhusu tabia ya Mungu, sheria yake, na utawala wake juu ya ulimwengu. Ugomvi huu
ulianza mbinguni wakati kiumbe aliyeumbwa na kutunukiwa uhuru wa kuchagua, katika
kujiinua akawa shetani, mpinzani wa Mungu, na kupelekea sehemu ya Malaika kwenye uasi.
Akaiagiza Roho ya uasi katika ulimwengu huu pale alipowaongoza Adamu na Hawa
kingia dhambini. Dhambi hii ya mwanadamu ilileta matokeo ya upotoshaji ya sura ya
Mungukatika wanadamu, Uvurugaji wa ulimwengu ulioumbwa, na mwishowe kuteketea
wakati wa gharika iliyokumba ulimwengu wote. Ukitazamwa na viumbe wote ulimwengu
huu ukawa uwanja wa vita ya ulimwengu, ambao kutokana nao Mungu wa upendo
hatimaye akathibitika kuwa mwenye haki. Katika kuwasaidia watu wake katika pambano
hili, kristo anamtuma Roho Mtakatifu na malaika watiifu kuongoza, kulinda, na
kutegemeza katika njia ya wokovu. (Ufu 12:4-9, Isa 14:12-14, Eze 28:12-18, War 1:19-32,
5:12-21, 8:19-22, 1Wakor 4:9, Waeb 1:14)

9.Maisha, Mauti na Ufufuo wa kristo
Katika maisha ya kristo ya utii mtakatifu kwa mapenzi ya Mungu, mateso yake, mauti na
ufufuo, Mungu alitoa njia pekee ya kafara kwa ajili ya dhambi ya mwanadamu, ili kwamba
wale ambao kwa imani wanapokea upatanisho huu waweza kuwa na uzima wa milele, na
ulimwengu wote uweze kuelewa vizuri upendo mtakatifu usio na kikomo wa muumba.
Kafara hii kamilifu huthibitisha haki ya sheria ya mungu na fadhili za tabia yake, kwa
sababu hufanya vyote viwili kuhukumu dhambi zetu na kutupatia msamaha. Kifo cha kristo
ni cha badala na cha kulipia, kupatanisha na chenye kubadilisha. Ufufuo wa Yesu kristo
hutangaza ushindi wa Mungu dhidi ya nguvu za uovu, na kwa wale wanaopokea kafara
huakikisha ushindi wao wa mwisho dhidi ya dhambi na mauti. Kinatangaza ukuu wa Yesu
Kristo, ambaye mbele zake kila goti mbinguni na duniani litapigwa.(Yoh3:16, Isa13:1,
1Petr 2:21, 22,1Wakor 15:3, 4, 20-22, 2Wakor 5:14, 19-21. War1:4, 3:25, 4:25, 8:3, 4,
Wafil2:6-11)

10.Uzoefu wa Wokovu
Katika upendo usio na mwisho na rehema zake Mungu alimfanya Kristo, asiyejua dhamdi
kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili kwambakatika yeye tuweze kufanywa haki ya Mungu.
Tukiongozwa na Roho mtakatifu tunatambua hitaji letu, tunakili hali yetu ya kuwa wenye
dhambi, tunatubu maasi yetu, na kuonyesha imani katika Yesu kama Bwana na Kristo,
kama mbadala na kielelezo. Imani hii inayopokea wokovu huja kupitia katika uwezo wa
kimbingu wan a ni karama ya neema ya Mungu. Kupitia kwa kristo tunahesabiwa haki,
tunafanywa kuwa wana wa binti za Mungu, na kukomesabiwa haki kutoka katika hali ya
kuwa chini ya dhambi. Kupitia kwa Roho tunazaliwa upyana kutakaswa, Roho hufanywa
upya nia zetu, huandika sheria ya Mungu ya upendo katika mioyo yetu, na tunapewa uwezo
wa kuishi maisha matakatifu. Tukikaa ndani yake tunakuwa washiriki wa asili ya uungu na
tuna hakika ya wokovu sasa na katika hukumu. (2Wakor 5:17-21, Yoh3:16, Wag1: 4, 4:4-
7, Tito3:3-7, Yoh16:8, Wag3:13,14. 1Petr 2:21,22. Warumi10:17, 3:21-26, 8:14-17, 12:2.
Warumi8:1-4,5:6-10, 2Petr 1:3,4)

11.Kukua katika kristo
Kwa kifo chake msalabani Yesu alizishinda nguvu za uovu. Yeye aliyewatiisha pepo
wachafu wakati wa huduma yake hapa duniani amezivunja nguvu zao na kuthibitisha
mwisho wao ni uangamivu usioepukika. Ushindi wa Yesu utupatia ushindi dhidi ya nguvu
za uovu ambazo bado zinatafuta kututawala, tunapo tembea naye kwa amani, fyraha, na
uhakika wa upendo wake.Sasa Roho Mtakatifu anakaa ndani yetu na kututia nguvu.
Tukidumu kujikabidhi kwa Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yetu tunawekwa
huru kutoka katika mzigo wa matendo yetu yaliyopita. Hatuishi tena gizani, katika hofu ya
nguvu za uovu, ujinga, na katika kukosa maana kwa namna ya maisha yetu ya awali,. Katika
uhuru huu mpya ndani ya kristo, tumeitwa kukua katika kufanana na tabia yake, tukiongea
naye kila siku katika sala, na kujilisha neno lake kikamilifu, tukikusanyika pamoja kwa ajili
ya ibada, na kushiriki katika utume wa kanisa. Tukijitoa katika kuwahudumia kwa upendo
wale wanaotuzunguka na kuwashuhudia wokovu wake, kuwepo kwake nasi daima kwa njia
ya Roho hugeuza kila wasaa na kazi kuwa uzoefu wa kiroho. (Zab.1:1,2. 23:4, 77:11,12,
Kol1:13-14, 2:6, 14-15, Luka10:17-20, Efe5:19-20, 6:12-18, 1Theo 5:23, 2Petr 2:9, 3:18.
Fil3:7-14, Math20:25-28, Yoh20:21, Gal5:22-25, Rum8: 38-39, 1Yoh4:4, Ebr10

12.Kanisa
Kanisa ni jamii ya waumini wanaomkiri Yesu kristo kuwa bwana na mwokozi katika
mfululizo wa kufungamana na watu wa Mungu katika nyakati za agano la kale, tunaitwa
kutoka katika ulimwengu, na tunajiunga pamoja kwa ajili ya ibada, kwa ajili ya ushirika, kwa
ajili ya mafundisho katika neno, na kwa ajili ya maadhimisho ya meza ya bwana, kwa ajili ya
huduma kwa wanadamu wote, na kwa ajili ya tangazo la injili ulimwenguni kote, kanisa
linapata mamlaka yake kutoka kwa kristo, aliye neno lililofanyika mwili, na kutoka katika
maandiko, ambayo ndiyo neno lililoandikwa. Kanisa ni jamaa ya Mungu, waliofanywa nay
eye kuwa watoto wake, washiriki wake huishi katika misingi ya agano jipya. Kanisa ni mwili
wa Kristo, jamii ya weny imani ambayo kristo mwenyewe ndiye kichwa. Kanisa ni bibi arusi
ambaye kwa ajili yake kristo apate kulisafisha na kulitakasa.Wakati wa kurudi kwake kwa
ushindi, ataliwasilisha kwake mwenyewew kanisa lenye utukufu, waaminifu wa karne zote,
walionunuliwa kwa damu yake, lisilo na waa au kunyanzi, lakini takatifu na lisilo na
ila.(Mwa12:3, Mdo:7:38, Waef4:11-15, 3:8-11, Math28:19,20, 16:13-20, 18:18,
Waef19:22,23, 5:23-27, Wakol1:17-18).

13.Masalio na Utume Wake
Kanisa la ulimwengu lijumuisha wale wote ambao kwa kweli wanamwamini kristo, lakini
katika siku za mwisho, kipindi cha kuenea kwa ukengeufu, masalio wameitwa kuzishika
amri za Mungu na imani ya Yesu kristo. Masalio hawa hutangaza kuwadia kwa saa ya
hukumu, hutangaza wokovu kupitia kristo, na hupiga mbiu ya kukarinia kwa marejeo yake.
Tangazo hili huwakilishwa katika mfano wa malaika watatu wa ufunuo 14, juambatana na
kazi ya hukumu mbinguni na kuwa na matokeo ya kazi ya toba na matengenezo duniani.
Kila muumini anatakiwa kuwa na sehemu binafsi katika ushuhuda huu wa ulimwenguni
kote. (Ufu12:17, 14:6-12, 18:1-4, 2Wakor 5:10, Yuda3,14, 1Petro1:16-19, 3:10-14,
Ufu21:1-14)

14.Umoja katika Mwili wa Kristo
Kanisa ni mwili mmoja ulio na washiriki wengi, walioitwa kutoka katika taifa, kabila, lugha,
na watu. Katika kristo tu viumbe wapya, ubainishi wa rangi, tamaduni, elimu, na taifa, na tofauti
kati ya tabaka ya juu nay a chini, tajiri na maskini, mwanaume na mwanamke,havipaswi kuleta mgawanyiko miongoni mwetu.Sote tu sawa katika kristo,
ambaye kwa roho mmoja ametufunga katika ushirika mmoja pamoja nay eye na sisi
wenyewe kwa wenyewe, tunapaswa kutumika na kutumikiwa pasipo kupendelea au kusita.
Kupitia kwa Yesu kristo katika maandiko tunashiriki imani na tumaini moja, na tunawafikia
wote kwa ushuhuda mmoja. Umoja huu una chimbuko lake katika umoja wa Mungu
mmoja mwenye nafsi tatu, ambaye ametufanya sisi tu watoto wake.(War12:4,5,
1Wakor12:12-14, Math28:19,20, Zabr133:1, 2Wakor5:16,17, Mdo17:26,27, Waef4:14-16,
4:1-6, Yoh17:20-23)

15.Ubatizo
Kwa njia ya ubatizo tunakiri imani yetu katika kifo na ufufuo wa Yesu kristo, na
kushuhudia kufia kwetu dhambi na kusudi letu la kuenenda katika upya wa maisha. Hivyo
tunamkubali kristo kuwa Bwana na Mwokozi, tunakuwa watu wake, na tunapokelewa kama
washiriki wa kanisa lake. Ubatizo ni mfano wa muungano wetu na kristo, msamaha wa
dhambi zetu na kupokea kwetu Roho Mtakatifu. Ni kwa kuzamishwa najini na unategemea
uthibitisho wa imani katika yesu na ushindi wa toba ya dhambi. Unafuata mafunzo katika
maandiko matakatifu na ukubali wa mafundisho yake. (Warum6:1-6, Wakol2:12,13,
Mdo16:30-33, 22:16, 2:38,Math28:19-20)

16.Meza ya Bwana
Meza ya Bwana ni ushiriki katika mfano wa mwili na damu ya Yesu kama udhihirisho wa
imani katika yeye, Bwana na mwokozi wetu. Katika ushirika huu kristo anakuwepo
kukutana na kuwaimarisha watu wake. Kadri tunavyoshiriki, kwa furaha tunatangaza mauti
ya Bwana mpaka arudipo tena. Maandalizi kwa ajili ya meza ya Bwana hujumuisha kujihoji
nafsi, toba na ungamo. Bwana aliamua huduma ya kutawadhana miguu kumaanisha
kutakaswa upya, kuonyesha nia ya kutumiana wenyewe kwa wenyewe katika unyenyekevu
ufananao na wa kristo, na kuungana mioyo yetu katika upendo. Huduma ya Meza ya
Bwana wazi kwa waumini wote wakristo. (1Wakor10:16,17. 11:23-30, Math 26:17-30,
Ufu3:20, Yoh6:48-63, 13:1-17)

17.Karama za Roho na Huduma
Mungu huwakirimia washiriki wote wa kanisa lake katika kila kizazi karama za kiroho
ambazo kila mshiriki atatumia katika huduma ya upendo kwa ajili ya mema ya kawaida ya
kanisa na wanadamu. Zikitolewa kwa wakala wa Roho Mtakatifu, ambaye humgawia kila
mshiriki kama apendavyo yeye, karama hizo hutoa uwezo wote na huduma zinazohitajiwa
na kanisa katika kuytekeleza shughuli zake zilizoamuriwa na Mungu. Kulingana na
maandiko huduma hizi hujumuisha huduma kama: Imani, uponyaji, unabii, mahubiri,
mafundisho, utawala, upatanisho, huruma, na huduma ya kujinyima na ufadhili kwa ajili ya
msaada na faraja kwa watu. Baadhi ya washiriki huitwa na mungu na kukirimiwa na Roho
kwa ajili ya shughuli zinazotambuliwa na kanisa katika uchungaji, uinjilisti, na utume, na
huduma za kufundisha zinahitajika hasa katika kuwapatia zana washiriki kwa ajili ya
huduma kulijenga kanisa hadi ukomavu wa kiroho, na kukuza umoja wa imani na maarifa
ya Mungu. Pale washiriki wanapozitumia karama hizi za kiroho kama mawakili waaminifu wa neema mbalimbali za Mungu, kanisa hulindwa dhidi ya mivuto miharibifu ya
mafundisho ya uwongo, na hukua kwa ukuaji unaotoka kwa Mungu, nakujengeka imara
katika imani na upendo.(Warumi12:4-8, 1Wakor12:9-11, 27,28. Waef4:8,11, Mdo6:1-7,
1Petr4:10-11)

18.Karama ya Unabii
Mojawapo ya karama za Roho Mtakatifu ni unabii, karama hii ni alama-kitambulisho cha
kanisa la masalio na ilidhihirishwa katika huduma ya Ellen G. White. Kama mjumbe wa
Bwana, maandishi yake ni chanzo kiendelezi na yenye mamlaka ya ukweli yanayolipatia
kanisa faraja, uongozi, mafundisho, na maonyo. Pia yanaweka wazi kuwa Biblia ndiyo
kanuni ambayo kwa hayo mafundisho yote na uzoefu lazima vipimwe. (Yoeli2:28,29,
Mdo2:14-21, Waeb1:1-3, Ufu12:17, 19:10)

19.Sheria ya Mungu
Kanuni kuu za sheria ya Mungu zimetiwa pamoja katika Amri kumi na mfano wake
ulidhihirishwa katika maisha ya kristo,. Nazo zinadhihirisha upendo wa Mungu, mapenzi
yake, na makusudi yake kuhusu mwenendo wa binadamu na mahusiano nazo ni sharti kwa
watu wote katika kila kizazi. Amri hizi ndiyo msingi wa agano la Mungu na watu wake na
kanuni katika hukumu ya Mungu. Kupitia uwakala wa Roho Mtakatifu zinasonda dhambi
na kuhamsha hisia za hitaji la mwokozi. Wokovu wote ni katika neema, na si kwa matendo,
lakini tunda lake ni utii wa amri kumi. Hutii huu hukuza tabia ya kikristo na huwa na
matokeo ya ustawi. Ni ushuhuda wa upendo wetu kwa Bwana na wajibu kwa ajili ya
wanadamu wenzetu. Utii wa imani udhihirisha uwezo wa kristokubadilisha maisha, na
hivyo huimarisha ushuhuda wa kristo. (Kut 20:1-17, Zab40:7,8 Math22:36-40 Kumb28:1-
14 Math5:17-20, War8:3,4 Zab 19:7-14)

20.Sabato
Muumbaji mkarimu, baada ya siku sita za uumbaji, alipumzika siku ya saba na kuanzisha
sabato kwa ajili ya watu wote kama kumbukumbu ya uumbaji. Amri ya nne ya sheria za
Mungu zisizobadilika inaagiza adhimisho la sabato hii ya siku ya saba kama siku ya
mapumziko, ibada, na huduma kulingana na mafundisho na uzoefu wa Yesu, Bwana wa
sabato. Sabato ni siku ya mawasiliano yenye furaha pamoja na Mungu na sisi kwa sisi. Ni
mfano wa ukombozi wetu katika kristo, ishara ya utakaso wetu, ishara ya utii wetu, na
mwonjo wa umilele wetu wa siku zijazo katika ufalme wa Mungu. Sabato na ishara ya daima
ya mungu ya agano la milele la Mungu kati yake na watu wake. Utunzaji wa furaha wa
wakati huu mtakatifu toka jioni hadi jioni, jua kuchwa hadi jua kuchwa, ni adhimishola
matendoya Mungu ya uumbaji na ukombozi. (Mwa 2:1-3, Kut20:8-11, Luka4:16, Isay56:5-
6, 58:13-14, Math12:1-12, Ezek20:12-20, Kumb5:12-15, Wal23:32, Marko1:32).

21.Uwakili
Sisi tu mawakili wa Mungu, tuliokabidhiwa nay eye wakati na fursa, uwezo na mali, na
mibaraka ya dunia na raslikamali zake. Tunawajibika kwake kwa matumizi yake sahihi.
Tunakiri umilikaji wa Mungu kwa huduma ya uaminifu kwake na kwa wanadamu wenzetu, na kwa kurudisha Dhaka na kutoa sadaka kwa ajili ya utangazaji wa injili yake na kwa
utegemezaji na ukuaji wa kanisa lake. Uwakili ni fursa iliyotolewa kwetu na Mungu kwa ajili
ya malezi katika upendo na ushindi dhidi yao choyo na tama. Wakili kufurahia mibaraka
inayowajia wengine kama matokeo ya uaminifu wake.(Mwa1:26-28, 2:15, 1Nyak29:14,
Hagai 1:3-11, Malak3:8-12, 1Wakor 9:9-14, Math23:23, 2Wakor8:1-15 Warumi15:26-27.).

22. Mwenendo wa kikristo
Tumeitwa kuwa watauwa wanaofikiri, kujisikia, na kutenda kutenda kulingana na kanuni za
mbinguni. Ili Roho aumba ndani upya ndini yetu tabia ya Bwana wetu tunajihusisha tu
katika mambo yale ambayo yatazaa katika maisha yetu usafi unaofanana na kristo, afya, na
furaha katika maisha yetu. Hii inamaanisha kwamba maraha na maburudisho yetu
yanapaswa kufikia viwango vikuu vya maonji na uzuri wa kikristo. Huku tukitambua tofauti
za kitamaduni, mavazi yetu yanapaswa yawe ya kawaida, si ya anasa, na safi, yanayostahili
wale ambao uzuri wao wa asili yake si mapambo ya nje, bali asili yake ni mapambo
yasiyoharibika, yenye roho ya upole na utulivu. Pia inamaanisha kwamba kwa kuwa miili
yetu ni maekalu ya Roho mtakatifu, tunapaswa kuitunza kwa akili. Pamoja na mazoezi
tosha na mapumziko, yatupasa kuchagua lishe yenye afya sana kadiri inavyowezekana na
kuepuka vyakula visivyo najisi, vilivyotajwa katika maandiko matakatifu. Kwa vile vinywaji
vya vileo, tumbaku na matumizi mabaya ya madawa hudhuru miili yetu, yatupasa
kuepukana nayo pia. Badala yake yatupasa kujishughulisha na chochote kile kitakacholeta
mawazo yetu na miili yetu yawe katika nidhamu ya kistro, ambaye hutamani uzima wetu,
furaha, na wema. (Warumi 12:1-2, 1Yoh 2:6, Waef5:1;21, Wafil 4:8, 2Wakor 10:5, 6:14,
7:1, 1Pet3:1-4, Walawi 11:1-47, 3Yoh. 2)

23. Ndoa na Familia
Ndoa ilianzishwa Edeni na Mungu na ikasibitishwa na Yesu kuwa muungano wa maisha
yote kati ya mwanaume na mwanamke katika wenzi wenye upendo. Kwa mkristo kifungo
cha ndoa ni kwa Mungu na pia kwa mwenzi, na kishirikiwe tu na wenzi wenye imani moja.
Upendo wa hiari, heshma, staha, na uwajibikaji ndizo fito za {kujenga}uhusiano huu,
ambao utaakisi upendo, utakatifu, ukaribu, uthabiti wa uhusiano kati ya kristo na kanisa
lake. Kuhusu talaka, Yesu alifundisha kwamba mtu anayemwacha mwenza, isipokuwa kwa
sababu ya uasherati, na akaoa {au kuolewa} na mwingine azini. Ingawa baadhi ya
mahusiano ya kifamilia huenda yakashindwa kufikia lengo, wenzi katika ndoa ambazo
wamejitoa kikamilifu kila mmoja kwa mwenzake katika kristo wanaweza kufaulu kufikilia
katika umoja wenye upendo kupitia uongozi wa Roho na malezi ya kanisa. Mungu hubariki
familia na anakusaidia kwamba washirika wake watasaidiana wao kwa wao kufikia upevu
kamili. Wazazi wawalee watoto wao katika kumpendeza na kumtii Bwana. Kwa kielelezo
chao na maneno yao wawafundishe kwamba kristo ni mtiishaji mwenye upendo, daima
mpole na mwenye kujali, anayetaka wawe kiungo katika mwili wake, familia ya Mungu.
Kukuza ukaribu wa mahusiano wa kifamilia ni moja wapo ya alama{ya kujulisha}ujumbe wa
mwisho wa injil. (Mwa 2:18-25, Math 19:3-9, Yoh 2:1-11, 2Wakor6:14, Waef5:21-33, Luka
16:18, 1Wakor7:10-11, Kut20:12, Kumb6:5-9, Mith22:6, Mal 4:5-6)

24. Huduma ya Kristo katika Hekalu la Mbinguni
Kuna hekalu mbinguni, hema la kweli lililosimamishwa na Bwana na siyo mwanadamu.
Ndani yake kristo anahudumu kwa niaba yetu, akiwezesha kupatikana kwa ajili ya waumini
fanaka za kafara yake ya upatanisho iliyotolewa mara moja msalabani kwa ajili ya wote.
Alizinduliwa kuwa kuhani wetu mkuu na akaanza huduma yake ya uombezi wakati wa
kupaa kwake mbinguni. Mnamo mwaka 1884, mwishoni mwa kipindi cha unabii wa siku
2300, aliingia katika awamu ya pili nay a mwisho katika huduma yake ya upatanisho. Ni
kazi ya hukumu ya upelelezi ambaya ni sehemu ya mwisho ambayo hatimaye itakomesha
dhambi yote, iliyokuwa mfano wa kutakaswa kwa hekalu la kale la waebrania katika siku ya
upatanisho. Katika huduma hiyo kielelezo hekalu lilitakaswa kwa damu ya wanyama wa
kafara, likini mambo ya mbinguni hutakaswa kwa kafara kamilifu ya damu ya Yesu.
Hukumu ya upelelezi kufunua kwa viumbe wa mbinguni ni nani miongoni mwa wafu
wamelala katika kristo na hivyo, katika yeye wanahesabiwa kustahili kuwa na sehemu katika
ufunuo wa kwanza. Pia inadhihirisha zazi ni nani miongoni mwa walio hai wanakaa ndani
ya kristo, wakishika amri za Mungu na imani ya Yesu, na katika yeye, hivyo basi, wako
tayari kwa ajili ya kuhamasishwa kuingia katika ufalme wa milele. Hukumu hii huthibitisha
haki ya Mungu, katika kuwokoa wale wanaomwamini Yesu. Hutangaza kwamba wale
waliohudumu kuwa watiifu kwa Mungu watapokea ufalme. Hitimisho ya huduma hii ya
kristo itakuwa ndiyo mwisho wa kufunga mlango wa rehema ya mwanadamu kabla ya
marejeo ya Yesu. (Waebr 8:1-5, 4:14-16, 9:11-28, 10:19-22, 1:3, 2:16-17. Dan 7:9-27, 8:13-
14, 9:24-27. Hes 14:34. Ezekl 4:6 Ufu 14:6-7, 20:12, 14:12, 22:12. )

25. Kuja kwa Kristo mara ya pili
Kuja kwa kristo mara ya pili ndilo tumaini lenye baraka la kanisa, hitimisho kuu la injili.
Kuja kwa mwokozi kutakuwa halisi, binafsi, kutaonekana kwa dunia mzima. Atakaporudi
wenye haki waliokufa watafufuliwa na pamoja na wenye haki walio hai watavikwa utukufu
na kuchukuliwa kwenda mbinguni, lakini waovu watakufa. Kutimizwa karibu kabisa kwa
sehemu nyingi za unabii, pamoja na hakli ya sasa ya ulimwengu, huonyeshe kwamba kuja
kwa kristo ku karibu sana. Wakati wa tukio hilo hakukufunuliwa, na hivyo basi
tunahimizwa kuwa tayari kwa nyakati zote. .(Tito 2:13, Math 24, Mdo1:9-11, Math24:14,
Ufu1:7, 14:14-20, Math24:43-43, Wakor15:51-50, 1Wathes1:7, 4:13-18, 5:1-6, Marko 13,
Luka 21:2, Tim 3:1-5).

26. Mauti na Ufunuo
Mshahara wa dhambi ni mauti. Lakini Mungu, ambaye peke yakehapatwi na mauti,
atawapa uzima wa milelewaliokombolewa wake. Mpaka siku hiyo mauti ni hali ya
kutokuwa na fahamukwa watu wote. Wakati kristo, aliye uzima wetu, atakapotokea, wenye
haki waliofufuliwa na walio hai watafikwa utukufu na kunyakuliwa juu ili kumlaki Bwana
wao. Ufufuo wa pili ambao ni ufufuo wa waovu, utatokea miaka elfu moja baadaye.
(Warum 6:23,1Tim 6:15-16, Mhu 9:5-6, Zab 149:3-4, Yoh 11:11-14, 1Wakor 15:51-54,
1Wathes 4:13-17, Ufu 20:1-10)
.
27. Milenia {Miaka Elfu} na Mwisho wa Dhambi
Milenia ni miaka elfu moja ya utawala wa kristo pamoja na watakatifu wake mbinguni kati
ya ufufuo wa kwanza na pili. Wakati huo waovu waliokufa watahukumiwa, dunia itakuwa
ukiwa na utupu, bila wanadamu wakazi walio hai, lakini ikikaliwa na shetani na malaika
zake. Mwishowe kristo na watakatifu wake na Mji Mtakatifu watashuka kutoka Mbinguni.
Ndipo waovu waliokufa watafufuliwa, nao pamoja na shetani na malika zake watauzingira
mji, Lakini moto kutoka mbinguni utawateketeza ili kuitakasa dunia. Na hivyo ulimwengu
utakuwa huru bila dhambi na wenye dhambi milele. (Ufu 20, 1Wakor 6:2-3, Yer 4:23-26,
Ufu 21:1-5,Mal 4:1, Ezekl 28:18-19)

28. Dunia Mpya
Katika dunia mpya, ambamo haki hukaa,Mungu ataweka tayari makao ya milele
waliokombolewa na mazingira makamilifu kwa maisha ya milele, upendo, furaha na
kujifunza mbele zake. Kwa hapa Mungu mwenyewe atakaa pamoja na watu wake, na taabu
na mauti vitakuwa vimepita. Pambano kuu litakuwa limemalizika, na dhambi haitakuwepo
tena. Vitu vyote vyenye uhai na visivyo na uhai vitatangaza kwamba Mungu ni pendo, naye
atatawala milele. Amina. (2Pet 3:13, Isa 35, 65:17-25, Math 5:5, Ufu 21 :1-7, 22:1-5, 11:5).

 
Kumekuwa na mijadala mingi na mawazo mengi yenye kukinzana katika Tanzania kuhusiana na mafundisho ya Kanisa la Waadventista Wasabato. Hivyo niliamua kuchunguza misingi ya imani ya Kanisa hili ili kupata picha kamili ya mafundisho yao. Ilikuwa dhahiri kuwa imani ya Waadventista Wasabato ni dini ya uongo yenye mafundisho ya kupotosha mafundisho hayo yanatokana na roho za udanganyifu, ambazo mtume Paulo alisema zitajitokeza katika siku za mwisho. “Basi roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watujitenga na Imani, wakisikiliza roho zindanganyazo, na mafundisho ya mashetani.” (1Tim. 4:1). Mafundisho ya Adventista Wasabato yanawakilisha ‘injili nyingine’, injili ya uongo ambayo Paulo anatuonya vikali kabisa katika Wagalatia 1:3-9 na 2 Wakorintho 11:1-4.

Kwangu mimi, ilikuwa muhimu kujifunza kitu kimoja tu kuhusu mafundisho yao ili kugundua kuwa mafundisho hayo yalikuwa uongo mtupu. Mmoja wapo wa waasisi muhimu wa kanisa la Waadventista Wasabato mnamo miaka ya 1800 alikuwa Ellen G. White. Alifundisha tarehe ya 22 Oktoba 1844 kuwa Yesu Kristo alitoka katika ‘patakatifu’ mbinguni naye akaingia “patakatifu pa patakatifu”. Hili wazo sio tu liko kinyume na Maandiko lakini pia halina mantiki. Ni nani anaweza kuamini katika upuuzi huu ambao haujaandikwa mahala popote katika Maandiko? Jibu la hili swali ni kwamba, hili ni kazi ya roho idanganyayo ifanyayo kazi kwa nguvu kwa wanaume na wanawake walio vipofu wa ukweli na uelewa wa Injili ya Yesu Kristo.

Neno la Mungu linatufundisha kwamba baada ya kufufuka kwake, Yesu Kristo aliingia Patakatifu pa Patakatifu (mbinguni) kwa damu yake (Waebrania 9:7,8-12; 10:19). Patakatifu pa Patakatifu ni ishara ya uwepo na utukufu wa Mungu pale anapoketi na kutawala; zaidi ya haya, Maandiko yanatufundisha kwamba watu wa Mungu waliokombolewa, wao wenyewe wana ujasiri wa Kuingia Patakatifu Pa Patakatifu kwa sababu ya damu na kafara ya Yesu Kristo (Waebrania 4:16; 6:19,20; 10:19-23). Kitabu cha Waebrania kinatudhihirisha kuwa ile Hema jangwani inawakilisha vitu vya kiroho vilivyopo mbinguni, na kwamba sasa Wakristo wanao uwezo wa kuingia uwepo kwenye Mungu kwa njia ya Roho Mtakatifu (Waefeso 2:18).

Kwa nini mtu anaweza kuachana na akili na kuamini kitu ambacho kinapinga dhahiri mafundisho ya Biblia? Jibu ni kama ifuatavyo: kulikuwa na watu katika miaka ya 1800 ambao walikuwa wanaamini kuwa Yesu atarudi duniani tarehe 22 Oktoba 1844. Hii ilitokana na tafsiri yao ya Danieli 8:14 na zile siku 2300 zilizotajwa humo. Mmoja ya waanzilishi wa kwanza wa mafundisho haya ni mwanaume aitwaye William Miller na wafuasi wake waliitwa “Millerites” (Wafuasi wa Miller) au ‘Waadventista’. Tayari hapa tunaona udanganyifu uliokuwa ukifanya kazi katika mioyo ya hawa watu kwa kufikiria kwanza wangeweza kuikokotoa siku ya kurudi kwake Bwana, wakati Bwana mwenye ameisha tuonya kabisa kuhusu mambo haya ( Mathayo 24:23-27,44; 25:13). Ni kweli kwamba Bwana hakurudi siku hiyo na kulikuwa na kukatishwa tama sana miongoni mwa ‘Waadventista’ – kwa ujumla waliitwa ‘Adventists’ kwa sababu walitazimia ‘Kuja’ (yaani, ‘Advent’) kwake Yesu kutatokea wakati ule. Badala ya kutubu wengine walizidi kujidanganya ili kuhararisha tafsiri zao za Danieli sura ya 8.

Hiram Edson alikuwa miongoni wa wale waliovunjwa moyo, lakini alisema siku iliofuata, alipokuwa akikatisha katika shamba fulani alipumzika ili kusali na ilikuwa kama mbingu zilifunguka mbele yake. Ansema kwamba “Iliwekwa dhahiri kwake” kwamba sio kuwa ilimbidi Yesu kurudi duniani Oktoba 22, 1884, lakini siku hiyo Kristo alitoka patakatifu mbinguni na kuingia patakatifu pa patakatifu ili kufanya kazi iliyo takatifu zaidi (F.D Nichol, The Midnight Cry p.458).

Edson bila kuchelewa alishirikisha tafsiri hii wafuasi wengine ambao wote waliiona kama habari njema! Hawa watu walikuwa wamepagawa sana na tafsiri yao kuhusu Daniel 8:14 kaisi cha kwamba ilikuwa rahisi kudanganywa na shetani kupitia ndoto mbalimbali na maono waliyokuwa wakipata. Walijaribu kutumia kitabu cha Waebrania sura za 8 na 9 ili kuhalalisha mawazo yao ya kuwa Yesu alihama kutoka patakatifu na kuingia patakatifu pa patakatifu tarehe hiyo ya 22 Oktoba 1884!

Edson alianza kujifunza Biblia pamoja na waamini wengineo wawili, O.R.L Crosier na Franklin B. Han, ambao walichapisha matokeo yao kwenye makala yao iitwayo “Day-Dawn”. Hivyo maono ya Edson ndiyo yakawa msingi wa “Mafundisho ya Patakatifu” (ambayo nitayaongelea hivi punde), na watu walioamini mafundisho haya ndiyo walikuwa kundi ambalo liliinuka kutoka kwenye makundi mengine ya Waadventista na kuwa kanisa la Waadventista Wasabato. Ufunuo huu wa uongo ulikuwa wenye kuhamasisha sana kwa Waadventista. Ellen White aliandika baadaye, “Maandiko ambayo kuliko chochote kile ndiyo yalikuwa msingi na nguzo kuu ya Imani ya Waadventista, yalitoa tamko kuwa ‘Itachukuwa siku 2,300 ndipo mahali patakatifu patawekwa wakfu tena.’ ’’ (Danieli 8:14).

Ellen White na Waadventista waliamini kuwa zile siku 2,300 zilizotajwa na Daniel ziliisha Oktoba 22, 1884, na kuanzia hapo Kristo alianza awamu mpya ya huduma yake! Na Ellen White aliita hii “msingi na nguzo kuu ya Imani ya Waadventista”! Na hii bado ni msingi wa Imani za dini ya Waadventista Wasabato hadi leo. (Sitajishughulisha na mambo ya majina ambayo makundi mbalimabli ya Waadventista wasabato waliyatumia kutofautiana na wengine mwanzoni mwa historia yao. Muhimu kwetu kwa ajili ya somo hili ni mwanzo wa msingi wa imani ya Waadventista Wasabato.)

Ellen White aliandika kitabu cha maono yake. Baadhi ya maono yake inawakilisha makufuru kwa kupotosha na kuchanganya kabisa maono na mifano ya Biblia (Early Writings p 54,55). Hiki kitabu kilikuwa ni kazi ya udanganyifu. Anadai kwamba alipata maono ya mbinguni na aliongea na malaika na Kristo. Haya maono na ufunuo ilibidi kuhalalisha mafundisho yao ya uongo kuhusu Yesu kuinga katika patakatifu pa patakatifu Oktoba 1844. Hii ilibidi itokee Oktoba 22, 1844! Anadai alipata maono mengi kama haya, ambayo kiukweli sio ongezeko la maandiko tu ila pia ni kuharibu thamani ya maandiko. Waadventista wanadai kuwa mafunuo haya ya Ellen White ni ‘yenye mamlaka’ kwa Waadventista Wasabato. Tunajua kuwa kitabu cha Ufunuo kinaongelea kuhusu watu watakaokiongezea! (Ufunuo 22:18).

Waadventista wanaweza wakasema kuwa Ellen White haongezei kwenye kitabu cha Ufunuo, lakini kwa sababu ya mambo mengi mapya na yenye kupotosha kwenye ‘maono yake’, na kwa sababu wafuasi wake wana amini kazi zake ni zenye ‘mamlaka’, hiki ndicho anachofanya. Kuhusu kazi zake Ellen White anasema, “Shuhuda hizi ni za Roho wa Mungu au shetani” (Testimonies for the Church, Vol. 4, p.230). Ni dhahiri kuwa shuhuda zake sio za Roho wa Mungu.

Kama nilivyosema, kama hii ndio mwanzo na chanzo cha mafundisho ya Waadventista, inatosha kwa mimi kutambua kuwa mafundisho haya yanatokana na uongo mtupu. Hata hivyo, sio ajabu kwamba kadiri tunavyoendelea kuyaangalia mafundisho yao tunaendela kukutana na udanganyifu na makosa mengine. Wakiendelea kushikilia tafsiri yao ya Danieli 8:14, Waadventista wanafundisha kuwa Yesu aliingia mahali patakatifu pa patakatifu Oktoba 22 1844 ili ‘kupasafisha mahali patakatifu’. Hivyo wanaamini Yesu amekuwa akipasafisha mahali patakatifu pa patakatifu kuanzia 1844 hadi leo! Hii iko wapi katika Bibla? Haipo. Inatokana ‘maono’ ya Edison Hiram na Ellen White tu! Basi!

Walitaka kutoa umuhimu wa tarehe walioichagua kama tafsiri ya Danieli 8:14. Lakini huu mstari unaongelea kuhusu kusafishwa kwa mahali ‘patakatifu’, na siku 2,300. Kwanza, kama tulivyoona, mwanzoni walidhani ‘kusafishwa kwa mahali patakatifu’ ni kurudi kwake Yesu duniani, lakini hii haikutokea, hivyo Waadventista walitunga tafsiri mpya kuhusu ‘kusafishwa kwa mahali patakatifu’ ambayo mstari wa 14 unaongelea. Hivyo walitunga kitu ambacho hakijafundishwa kwenye Maandiko, ambayo wanaiita “Hukumu ya Uchunguzi”. Kuhusu Yesu kuingia patakatifu pa patakatifu, Ellen White anaandika,

“Baada ya kupaa, mkombozi wetu akaanza kazi ya ukuhani mkuu… Huduma ya kuhani (katika Agano la Kale) katika mwaka mzima ndani ya sehemu ya kwanza ya patakatifu… inawakilisha kazi ya huduma ambayo Yesu aliianza baada ya kufufuka. Ilikuwa ni kazi ya kuhani wa kila siku kupeleka mbele za Mungu damu ya sadaka ya dhambi… Kwa hivyo Yesu akamsihi Mungu Baba kwa damu yake kwa ajili ya wakosefu na kuleta maombi ya toba ya waumini mbele yake. Hiyo ilikuwa kazi ya huduma katika sehemu ya kwanza ya patakatifu mbinguni”.

“Kwa karne kumi na nane, kazi hii ya ukuhani imendelea katika sehemu ya kwanza ya patakatifu. Damu ya Kristo inaombea kwa niaba ya waamini wajutao, ilileta msamaha na kukubaliwa na Baba ingawa bado dhambi zao zimebaki katika vitabu vya kumbukumbu. Kama ilivyokuwa kwa kila ibada, kulikuwa na kazi ya upatanisho katika kila mwisho wa mwaka. Kwa hiyo kabla ya kazi ya Yesu kwa ajili ya ukombozi wa wanadamu kukamilika kuna kazi ya upatanisho kwa ajili ya kuondoa dhambi patakatifu. Hii ni huduma iliyoanza siku 2,300 zilipoisha, yaani 1844. Katika muda huo kama ilivyotabiriwa na Nabii Danieli, Kuhani wetu mkuu aliingia patakatifu (pa takatifu) kufanya sehemu ya mwisho ya kazi yake ya pekee ili kutakasa madhabahu”

“Kama zamani za kale dhambi za watu kuipitia imani yao juu ya sadaka za dhambi zilizohamishiwa patakatifu pa duniani, hivyo katika Agano Jipya dhambi za waungamaji kupitia imani yao katika Kristo zinahamishiwa patakatifu pa mbinguni. Utakaso wa kidunia ulikamilishwa kwa ondoleo la dhambi zilizoichafua, hivyo utakaso halisi wa mbinguni unakamilishwa kwa ondoleo, kufutwa au kufichwa kwa dhambi zilizoandikwa pale. Lakini kabla ya hili kutimia, lazima kuwa na tathmini ya vitabu kujua nani, kupitia kutubu dhambi na imani kwa Kristo anastahili kupata faida ya upatanisho. Utakaso wa patakatifu unahusisha kuchunguza kazi ya hukumu. Na hii ni lazima ifanyike kabla ya Kristo kuja na kuwakomboa watu wake.” (Great Controversy p.421, 422).

Hii ni dhana ya udanganyifu ambayo Waadventista wanatembea. Kung’ang’ania kwao tafsiri ya Danieli 8:14, kunapotosha si maandiko tu bali pia hueleza mambo ambayo Biblia haijafundisha na pia hupingana na kazi ya ukombozi ya Kristo. Ellen White na Waadventista wanafundisha kuwa baada ya kupaa kwa Yesu Kristo, alikaa miaka 1800 katika kile kinachohusiana na sehemu ya kwanza ya hema huko mbinguni, akiingilia kati kwa niaba ya waaminio kuwatetea kupitia damu yake mbele ya Baba yake! Baada ya hii miaka 1800 anamaliza huduma yake na kuanza kazi ya ‘hukumu ya uchunguzi’ katika patakatifu pa patakatifu ili kusafisha mahali patakatifu! Wazo hili ni la kwao wenyewe. Ni jambo la kushangaza jinsi watu wanavyoweza kujidanganya!

Haikuishia hapo. Ellen White anasema kwamba ingawa maombezi ya Kristo yalitoa msamaha wa waaminii waliotubu, lakini dhambi zao zinabaki zimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu kilichopo patakatifu pa patakatifu! Hivyo anasema kabla kazi ya ondoleo la dhambi kuisha lazima kumbukumbu hizi ziondolewe! Waadventista wanafundisha kwamba mnamo 1844 Kristo akaingia patakatifu pa patakatifu ambako kumbukumbu zipo. Kumbukumbu hizi zimeandikwa dhambi na kila matendo ya mwamini, na kwamba Kristo ataanza kuchunguza vitabu hivi na kujua nani anafaa ondoleo la dhambi. Ellen White anaandika kwamba dhambi za waungamaji zimewekwa kwa Yesu na kupitia imani zimehamishiwa patakatifu pa patakatifu! Je dhambi hizi zinapelekwaje?

Maana hizi dhambi zimeandikwa katika vitabu vya kumbukumbu huko patakatifu pa patakatifu, na kwa kuwa huko zinachafua au unajisi patakatifu! Je patakatifu panapataje utakaso? Panasafishwa na Yesu kwa kuchunguza maisha ya waamini na kuamua ni nani anastahili kwa sababu ya kutubu kwake kwa kweli na kukua katika neema! Kufutwa kwa dhambi katika vitabu viliyopo patakatifu pa patakatifu kunaitwa “kutakasa patakatifu”. Hii imeanzishwa na Waadventista na wanasema baada ya kazi hii kuisha ndipo Yesu atakapokuja kuchukua walio wake. Mambo hayo yanawakilisha aina ya wazimu! Ni mbali sana sana na ukweli wa Biblia.

Nukuu zifuatazo zinaonyesha wazi kuwa Waadventista wanafikiri kuwa kazi ya upatanisho bado inaendelea, “Damu ya Yesu, wakati ikimuweka huru muungamaji kutoka katika hukumu za kisheria haikuwa ikifuta dhambi … dhambi itasimama patakatifu mpaka upatanisho wa mwisho,” (Patriarch’s and Prophets, p.357)…. “sasa wakati kuhani wetu mkuu anafanya upatanisho kw ajili yetu; yatubidi kuwa wakamilifu katika Kristo,” (The Great Controversy, p.623)… “badala ya kuja duniani katika mwisho wa siku 2300 ndani ya mwaka 1844, ikiisha Kristo aliingia patakatifu pa mbinguni, ikimalizika kazi ya upatanisho ndio maandilizi ya ujio wake.” (The Great Controversy, p.422). Watu wanawezaje kumfuata mwanamke anayesema kwamba baada ya ufufuo Yesu akafanya maombezi kwa ajili yetu, lakini damu yake haikutosha kufuta dhambi, na baada ya kama miaka 1800 ilikuwa lazima kazi ya hukumu yenye uchunguzi ianze ili dhambi ziweze kuondolewa? Hii ni kazi ya udanganyifu kwa wamfuatao!

Hakuna moja kati ya haya linalofundishwa katika Biblia, lakini yote ni katika kupinga au kukinzana na kazi ya Yesu Kristo pale Kalvari. Katika Kalvari mwana wa Mungu alilia kwa sauti kuu, “Yametimia!” Mara baada ya hapo, pazia la hekalu lililotenganisha pataatifu na patakatifu pa patakatifu lilipasuka. Hii ilimaanisha kwamba kupitia damu yake Yesu alifungua njia ya patakatifu pa patakatifu mbinguni, yaani kwenda kwenye uwepo wa Mungu! Waebrania 9:8 inasema, “Njia ya kupaingia patakatifu pa patakatifu mbinguni ( kwa maana ya Kigiriki) ilikuwa haijadhihilishwa bado, hapo hema ya kwanza ilipokuwa ingaliikisimama”.

Kwa hiyo pale ambapo pazia la hekalu liligawanyika mara mbili ilimaanisha kwamba Mungu alihitimisha na kusitisha kazi ya hema, na kwa sababu ya damu ya Yesu tunapata uwezo wa kuingia katika ufalme wa mbinguni, kama mwandishi anavyoelezea katika kitabu cha Waebrania 13:10-22. Kwa sababu ya kifo cha Yesu na ufufuko wake tuna uwezo mkubwa wa kuingia katika patakatifu pa patakatifu kwa damu ya Yesu, kama Waebrania 10:19 inavyoeleza kwa ufasaha. Lakini Wasabato wanataka kusema kuwa Kristo hakuingia patakatifu pa patakatifu hadi hapo mwaka 1844! Hili siyo fundisho la pembeni lao! Ni fundisho la msingi!

Siku ya upatanisho katika Agano la Kale ilitoa msamaha wa dhambi za Israeli kwa kutoa sadaka ya fahali na mbuzi. Kufanya upatanisho kwa watu mara mmoja kwa mwaka, damu ya wanyama hawa ilipelekwa patakatifu pa patakatifu na kuhani mkuu na ilinyunyuziwa kwenye kiti cha rehema (Walawi 16). Waebrania sura ya 9 na 10 inatueleza kwamba ni kuhani mkuu peke yake ndiye aliyeenda patakatifu pa patakatifu mara moja kwa mwaka na damu ya fahali na mbuzi, kwa hiyo Kristo kama kuhani wetu mkuu aliingia patakatifu pa patakatifu kupitia damu yake mwenyewe baada ya ufufuko wake na “na kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele” (Waebrania 9:12). Lengo moja kuu la kitabu cha Waebrania ni kutuonyesha kwamba Yesu Kristo ni kuhani wetu mkuu, ambaye baada ya kuteswa na kufa Kalvari, aliingia patakatifu pa patakatifu mbinguni kwa damu yake kwa msamaha wa dhambi na kwa wokovu wa watu. Ellen White anakinzana na mafundisho ya kitabu cha Waebrania kwa kudai kuwa Yesu hakuingia patakatifu pa patakatifu hadi mwaka 1844!

Zaidi ya hayo mafundisho ya Ellen White yanakinzana na maneno ya Mungu kwa kunena kuwa kazi ya ukombozi haijaisha bado kwa sababu kuna uhitaji wa “takaso la patakatifu”. Neno la Mungu linasema kwamba kwa sadaka moja ya Yesu tumepata uzima wa milele na ya kwamba hao katika Kristo wamekwisha kombolewa kwa damu ya mwana kondoo – 1Petro 1:18. Mwandishi kwa Waebrania anasema, “lakini huyu alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu… maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao watakaotakaswa.” (Waebrania 10:12-14).

Haya na maandiko mengine yanasema waziwazi kwamba ilikuwa sadaka moja ya Kristo iliyofanywa katika tukio moja la kifo chake msalabani ambalo liliimarisha ukombozi wetu na utakaso wa ndani wa roho zetu! Kristo hakusubiri miaka 1800 baada ya kufufuka kwake kabla ya kuingia patakatifu pa patakatifu! Je! Kuhani mkuu katika Agano la Kale alitumia miaka 1800 katika mahali pa hema kabla ya kuingia patakatifu pa patakatifu pamoja na damu ya fahali na mbuzi? Hayo ni jambo la wazimu tu.

Biblia haizungumzii zaidi juu ya kazi au huduma ambayo Kristo inabidi aibebe ili kuimaliza kazi ya ukombozi, utakaso na msamaha! Mafundisho ya Wasabato yanashambulia moyo wa Injili ya Yesu Kristo. Dini ya Wasabato ni adui ya Injili. Aina yoyote ya huduma aliyonayo Kristo kwa sasa inategemea na kumalizika kwa kazi yake ya ukombozi ambayo aliikamilisha kupitia kifo chake na kufufuka! Hata hivyo Ellen White na Waadventista wanataka tuamini ya kwamba kazi ya utakaso wa patakatifu kupitia ‘hukumu ya uchunguzi’ imekuwa ikiendelea toka 1884 na bado inaendelea.

Ellen White anaweka maneno yake mwenyewe kuwa “ni ujio huu (yaani, kuingia patakatifu pa patakatifu) na sio ule wa mara ya pili duniani ambao umetamkwa katika utabiri na utathibitika mwisho wa siku 2300 mnamo 1844. Ikihudhuriwa na malaika wa mbinguni, kuhani wetu mkuu anaingia patatifu pa patakatifu katika uwepo wa Mungu kuingia katika matendo yake ya kazi za wokovu kwa niaba ya mwanadamu – kufanya kazi ya ‘hukumu ya uchunguzi’ na kufanya upatanisho kwa wale ambao wameonyesha kustahili faida zake… wale tu waliokwenda mbele za Mungu kwa toba na ungamo, ambao dhambi zao kupitia damu ya sadaka ya dhambi, zilihamishiwa au zilipelekwa patakatifu na zilikuwa sehemu ya kazi ya siku ya upatanisho. Kwa hiyo katika siku ya upatanisho na hukumu ya uchunguzi, mada zitakazohusishwa ni zile za wale waliofanywa watu wa Mungu.” (The Great Controversy, p.480).

Mafundisho haya pia huhoji uungu wa Yesu Kristo. Je, Kristo ni mwanadamu mpaka atumie miaka mingi kupitia vitabu ili kuona ni nini watu wamefanya? Je, Kristo si Mungu? Je, Kristo si mwana wa Mungu? Je majina ya hao watakatifu hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima tangu kuumbwa kwa ulimwengu? (Ufunuo17:8). Je, hatukuchaguliwa katika Kristo kabla kuwekwa misingi ya ulimwengu kama inavyosema Efeso 1:4? Yesu alijua kwamba Petro atamkana mara tatu! Yesu Kristo aliwaambia makanisa kwenye kitabu cha ufunuo kwamba “Ninajua kazi yenu…” . Ukweli ni kwamba Mwana wa Mungu anatujua (kwa undani zaidi) zaidi ya tunavyofikiri na hahitaji kuchukua miaka 200 au zaidi kutuchunguza maisha yetu! Mafundisho yao ni jambo la uzushi.

Waadventista Wasabato wana jumla ya misingi 28 ya Imani (unaweza kusoma kwenye tovuti yao), na mafundisho hayo hapo juu ni moja ya misingi hiyo 28 ya kuamini kwao! Ellen White ameandika, “Suala la hekalu la Mungu takatifu na hukumu ya uchunguzi yapaswa yajulikane na watu wa Mungu. Wote wanahitaji kuwa na ufahamu juu ya nafasi na kazi ya makuhani wakuu. Vinginevyo itakuwa ni vigumu kuitendea kazi imani ambayo ni ya msingi sana kwa wakati huu au kuichukua nafasi ile ambayo Mungu amekwisha itayarisha kwa ajili yao kuijaza. Wote waliopokea nuru kutokana na masomo haya wanapaswa wabebe ushuhuda wa kweli kuu ambayo Mungu ametenda kwao.” (Great Controversy p.480). Kwa mujibu wa maneno yake mwandishi huyu anasema kwamba sio tu unapaswa kuelewa mafundisho haya ili kutimiza hatima yako katika mpango wa Mungu, lakini pia unapaswa kuwashirikisha na wengine!

Kwa habari ya hukumu maandiko yanasema wazi kwamba sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu (Rum.14:10; 2 WaKor. 5:10), na pia wale wote ambao majina yao hayapo kwenye kitabu cha uzima watateswa kwenye hukumu ya milele. Biblia pia ina maonyo makali sana kwa wale waamini walioigeukia dunia baadaya kumuamini Kristo. Lakini maandiko hayakubaliani kabisa hata kwa mstari mmoja wazo la Waadventista juu ya “Hukumu ya Uchunguzi”. Pia haikubaliani na dhana kwamba Kristo alisubiri miaka 1800 baada ya ufufuo kabla ya kuingia patakatifu pa patakatifu! Tuelezeje machanganyiko na udanganyifu huo? Kuamini mambo hayo ni jambo la kuacha akili ambayo Mungu alitupa, na kuwaruhusu pepo kukuongoza na kukufanya kipofu juu ya mambo yale yaliyo wazi kabisa!

Kutokana na msingi huu wa uongo hii imepelekea makosa na uongo mwingi kuendelea, kwa mfano Ellen White alisema kwamba mwisho wa nyakati dhambi zote zitawekwa juu ya shetani, ameandika:

“Ilionekana kwamba kama vile Kristo alifanyika dhabihu ya sadaka ya dhambi, kuhani mkuu alimuwakilisha Kristo kama kiunganishi na kondoo wa dhabihu kama shetani, mwanzilishi wa dhambi, ambaye juu yake dhambi zote za waliotubu zitawekwa juu yake.” (The Great Controversy p.422). “Dhambi zao zina hamishiwa kwa mwanzilishi wa hizo dhambi.” (Testimonies for the Church Vol. 5, p.475).

Hii ni dhana potofu na inapingana kabisa na maandiko ambayo yanamuelezea mwana wa Mungu kama mwana kondoo wa Mungu aondoaye dhambi za ulimwengu. Isaya anasema, “Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote.” (Isaya 53:6). Na mwandishi kwa Waebrania anasema, “lakini sasa, mara moja tu, katika utimilifu wa nyakati, amefunuliwa, azitangue dhambi kwa dhabihu ya nafsi yake.” (Waebrania 9:26). Kristo Yesu aliihukumu dhambi katika mwili (Rumi 8:3). Tena inasema, “Yeye asiyejua dhambi alifanyika kuwa dhambi kwa ajili yetu ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika yeye (2 Wakorintho 5:21). Na Petro anatuambia, “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti…” (1 Petro 2:24). Sura ya 9 na 10 Waebrania inaeleza wazi kwamba Kristo anawakilisha ile dhabihu ambayo ilitolewa kwenye Agano la Kale kufanya upatanisho kwa ajili ya watu na sio shetani. “Kristo naye, akiisha kutolewa sadaka mara moja azichukue dhambi za watu wengi…” (Waebr.9:28). Wazo kwamba dhambi zetu zitabebeshwa na shetani ni uongo na la kuchanganya, na linaonyesha upungufu wa uelewa wa kile Mungu alichofanya kwetu kupitia Kristo pale Calvary.

Ellen White alichukia dhana ya hukumu ya milele, hakutaka kukubaliana kwamba Mungu atatuma watu kwenye hukumu ya milele. Aliukataa huu ukweli kabisa, katika hili anakubaliana na mafundisho ya Mashahidi wa Yehova. Alifundisha kwamba wasioamini na wenye dhambi wataangamizwa kabisa na kumbukumbu lao litapotea kabisa. Aliandika,

“Haikubaliani kabisa na kila hisia za upendo na huruma au hata za utashi wetu wa haki, dhana kwamba waliokufa katika hali ya dhambi au uovu wapo wanateseka milele kwenye moto jehanamu.” (The Great Controversy,p.535). “Lakini niliona kwamba Mungu hatawaacha wateseke jehanam wala hata wapeleka mbinguni. Bali atawaangamiza na kuwafanya kama vile hawakuwahi kuwapo hapo awali.” (Early Writings p.221).

Bado dhana hii inaendelea kufundishwa kwa upana na bado imejengeka kwenye mabaraza ya kiimani. Ni wapi kwenye kurasa za neno la Mungu mafundisho kama hayo yanapatikana? Anandika haya kana kwamba hajawahi kusoma Biblia! Anajiinua juu ya neno la Mungu na huruma ya Mungu! Maandiko yanaeleza wazi kabisa juu ya hukumu ya milele. Katika sura ya 25 Matayo, Yesu alisema wasio haki wataiendea ile hukumu ya milele lakini wenye haki watapata uzima wa milele (Mathayo 25:46). Katika tafsiri ya Kigiriki ya Agano Jipya, neno ‘milele’ ni sawa na ndilo linalozungumziwa sehemu hizo mbili, yaani ‘adhabu’ na ‘maisha’; kwa maneno mengine, kama adhabu sio ya milele vivyo hivyo na maisha ya milele kwa waamini sio ya milele! Kwenye mstari 41 wa sura hii Yesu anawaambia wasio wa haki au wenye dhambi waondoke kwenda moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya shetani na malaika zake. Kuna maandiko mengi yanauthibitisha ukwelii huu na kuuweka dhahiri – Daniel 12:2; Mathayo 18:8, Marko 9:43,44; 2 Wathess. 1:9; Ufunuo 14:11; 19:3; 20:10; 21:8. Kwa akili ya kibinadamu jambo la hukumu ya milele linaonekana ni jambo kubwa na lisilokuwa la kawaida lakini siku ya hukumu, Hukumu ya Mungu itaonekana ni jambo la haki kabisa na wala hakuta kuwa na mtu wa kumlaumu au kumshitaki Mungu kwa kukosa huruma na rehema. Binadamu katika kujivuna kwao wanatukuza kujiona kwao wenye huruma na rehema kinyume na Mungu.

Waadventista Wasabato na Mashahidi wa Yehova bado wanaamini kwamba malaika mkuu Michael ndiye YESU KRISTO, hata hivyo, Waadventista bado wanaamini Kristo ni mwana wa Mungu na yu na utukufu wa Mungu.

Tukielekezea macho yetu kwenye kiini cha somo letu juu ya “siku ya saba ya Wadventista”, yaani fundisho lao juu ya siku ya sabato. Somo hili zaidi ya vitu vingine linaonyesha Uadventista sio Ukristo, sio kwa asili wala kwa tafsiri ya maandiko. Mwaka 1847 Ellen White alidai kwamba alipata maono juu ya mji mtakatifu huko mbinguni na alipelekwa sehemu takatifu. Alidai kwamba Kristo alifungua pazia na akaingia patakatifu pa patakatifu na akaona kopo la dhahabu lenye ile mana, na ile fimbo ya Haruni iliyochipuka, na vile vibao vya agano. Anasema kwamba aliona amri kumi zimeandikwa kwenye mbao mbili na zilikuwa ziking’aa sana, na moja ilikuwa iking’aa zaidi, na ndio inayozungumzia Sabato, yaani, amri ya nne. (Early Writings of Ellen G. White, p.32,33).

Hebu tukae na tufikiri mambo hayo. Mengi yaliyoamuriwa na Mungu kipindi cha Agano la Kale yalikuwa ni udhihirisho wa Kristo ambaye angekuja baadaye. Ni Yesu Kristo ambaye sasa ni mkate wa uzima aliyekuja ulimwenguni kutoka mbinguni (Yoh.6:32, 33); chaguo la Mungu kwa habari ya kuhani mkuu sio Haruni wala uzao wa kabila la LAWI bali chaguo la Mungu ni YESU KRISTO! Je Ellen White hakuelewa kwamba tunaye Kristo badala ya Manna siku za leo? Je, hakutambua kwamba Kristo amechukua nafasi au Mungu amebadili ukuhani wa kilawi (Waebrania7;11-22)? Unaona vipi Ellen White alivyotukuza mambo ya Agano la Kale na hakujali Mwana wa Mungu Yesu Kristo?

Mungu ameweka Agano Jipya ambapo YESU ndiye nuru; YESU ndiye mkate wa Mbinguni na chaguo la Mungu la milele kama kuhani wetu mkuu! YESU amejawa na utukufu unaong’aa kwa njia ya pekee sana kiasi kwamba sio Mussa (torati) wala Elia (nabii) anaweza kulinganishwa naye kwa njia yoyote! (Mathayo17:4-8; 2 Wakor. 3:10). Ellen White alisema katika patakatifu pa patakatifu amri ya nne iling’aa kuliko zote – kana kwamba Yesu si kitu! Hapa ndipo tunaona udanganyifu wa kiasi kikubwa wa Ellen na Waadventista. Inaonyesha hawaelewi sio tu juu ya Agano Jipya la kweli bali pia juu ya Injili ya kweli, na hawaelewi kazi ya YESU msalabani na yale aliyoyafanya kwa niaba yetu!

Neno la Mungu linatufundisha kwamba Torati ililetwa na Musa lakini neema na kweli imekuja kupitia Kristo Yesu, “Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki.” (Warumi 10:4), na kwamba hatuko tena chini ya sheria (Rum.6:14). Je, hii inamaanisha kwamba tudumu katika dhambi? La hasha! Mungu ametuosha kwa damu ya mwanakondoo na ametupa Roho na kuweka sheria yake ndani ya mioyo yetu (Waebrania 8). Sasa tunaishi kwa imani na kwa ‘sheria ya Roho na Uzima ulio katika Kristo Yesu’ sawasawa na Warumi 8:4. Na katika dhana ile ya kwamba Kristo alikuja kuitimiza torati – hii ni juu ya yale ambayo sheria ama Torati haikuweza kutufanya wenye haki. Mungu amefanya hayo kupitia kifo na ufufuo wa Mwanae kwa kuyaweka maisha Yake kwetu ili tuweze kuzaa matunda ya haki kupitia Kristo (Wafilipi 1:11)! Paulo anatumia sura nzima ya tatu ya Wakorintho wa Pili kuzungumzia jinsi Torati inavyoleta hukumu ya kifo, na jinsi utukufu wa Kristo na maisha yake yanavyoizidi torati na sheria ya Musa. Sura ya kwanza ya Waebrania inamdhihirisha Kristo kama ndio nuru ya Mungu na anaonyesha sura ya Mungu halisi! Lakini maono ya Ellen White yanamtazama Kristo kama mtu aliyemsindikiza hekaluni tu, na anatilia mkazo zaidi kwenye mambo ya Agano la Kale la zamani kama “kopo la dhahabu lenye ile mana, na ile fimbo ya Haruni iliyochipuka”! Na kwake katika hili ni amri kumi ndizo zilizong’aa sana na amri ya nne ndio iliyong’aa zaidi kuliko zingine zote. Mafundisho ya Wasabato yanatokana na maono hayo ya uongo.

Katika 2 Wakorintho sura ya 3, Paulo anasema Mungu amewafanya mawakili wa Agano Jipya, na sio wa andiko (kwa maneno mengine, sio katika vibao vya mawe, kama anavyosema katika mstari wa tatu) bali kwa Roho wa Mungu aliye hai. Paulo anatufundisha kwamba, “andiko huua, bali Roho huhuisha.” Kwa maneno mengine, wale wanaohubiri na kutilia mkazo katika kutunza amri zilizoandikwa kwenye vibao mawe sio mawakili wa Agano Jipya, sio mawakili wa YESU. Sio hivyo tu bali ni mawakili wa kifo kwa wasikilizaji wao, sio uhai. Kwa maneno mengine, ni huduma ya Roho Mtakatifu tu inayotupa uzima, uzima uliobeba tunda la haki. Wale wanaosisitiza sheria zilizoandikwa kwenye vibao za mawe, wanasisitiza mauti, kwa sababu sheria iliyoandikwa kwenye vibao vya mawe hazina nguvu kutufanya tuwe hai wala kutufanya tuwe wenye haki!

Paulo anaendelea kusema kwamba “huduma ya kifo” iliyoandikwa kwenye jiwe ilikuwa na aina ya utukufu katika ule muda ambao Musa alipewa. Lakini Paulo anaelezea kwamba ‘utukufu wa Roho Mtakatifu” – ambao Paulo sasa anauita “huduma ya haki” – ni mkubwa zaidi kuliko “utukufu wa andiko”, ambao Paulo sasa anauita “huduma ya hukumu”. Anatufundisha kwamba utukufu wa Roho (kwenye Agano Jipya) ni mkubwa kuliko wa utukufu wa amri ulioandikwa kwenye vibao vya mawe, ni kama vile utukufu wa amri ulioandikwa kwenye mawe hauna utukufu sasa (mstari wa 10). Kiuhalisia anatuambia kwamba utukufu wa huduma ya Roho na wa haki ni mkubwa sana kiasi kwamba Mungu ameacha utukufu wa huduma ya maandishi ya kwenye vibao iliyoandikwa kwenye jiwe (mstari wa 11). Waadiventista hawaelewi neno la Mungu katika sura hii, na katika mafundisho yao wanafufua au wanarudisha ‘huduma ya andiko iliyoandikwa kwenye vibao vya mawe’ ambayo inawafanya watu waendelee kubaki katika kifo cha kiroho na hukumu. Wanaitukuza huduma hii kinyume na Agano Jipya la Mungu ambalo linaweka sheria zake ndani ya mioyo yetu kwa Roho wake. Waadventista wanafuata haki, ila katika kutilia mkazo katika sheria ya Musa, wanasababisha kifo na hukumu. Na ni haki ambayo Waadventista wanasema wanaishi kwayo, ambayo kabisa wanakosa na kushindwa kuipata kwa mafundisho yao kuhusu sheria. (Warumi 10:2,3).

Naelezea zaidi kuhusu hili katika makala yangu nyingine (Je, Tukusanyike Siku Gani Kati ya Jumamosi na Jumapili?), ila acha nioneshe hapa kwamba wale wanaohubiri kutunza/kufuata sheria ya Musa wapo kinyume na huduma ya Roho, wala hawajui huduma ya Roho katika maisha yao inayozaa matunda ya haki. Kwa kupitia huduma ya Roho tu ndio tunapata ubatizo katika Roho anayetupa uzima, uzima wa Yesu ndani yetu ambao kwa huo tunaishi maisha ya kitakatifu na kuzaa matunda ya haki. Kwa kutilia mkazo katika kufuata amri kumi, Waadventista wanazuia neema ya Kristo (Wagal. 1:6) na kujaribu utakatifu uliokamilika “katika mwili” badala ya katika imani na katika Roho ya Kristo (Gal 3:2,3). Waadventista hawaelewi nguvu ya Injili kama ilivyotangazwa katika Warumi 8:1-4. Kwa mantiki hii wale wanaofuata mafundisho ya Waadventista wamewekwa nje katika kujua nguvu ya ukombozi wa Kristo katika kuwafanya wenye haki na watakatifu, na katika mantiki hii, Uadventista sio Ukristo; zaidi ya hili, kiuhalisia, unapinga Injili kama Paulo alivyoweka wazi katika barua yake yote kwa Wagalatia.

Katika maono yake, tunaona kwamba Ellen White na Waadventista kwa kupitia upotefu huu wamebadilisha sehemu sahihi ambayo Mungu amempa Kristo Yesu, na badala yake, Sheria, na hasa sheria ya Sabato! Wanataka wawapeleke watu kwenye Agano la Kale na waishi huko! Ni udanganyifu gani huu, hii ni kuinua sheria juu ya Yesu Kristo!

Ellen White alisema kwamba amri ya nne iling’aa juu ya zote na kuzungukwa na duara linalong’aa na ilitengwa kutunza heshima ya jina la Mungu! Anaendelea kusema kwamba kama amri ya nne inaweza kuvunjwa basi amri nyngine zote zinaweza kuvunjwa! (Early Writings of Ellen G. White, p.32,35). Labda hii inaweza kukusaidia kuelewa kwa nini Waadventista wengi wanasema kwamba kama tusipotunza sabato ni sawa na kusema tunaweza kufanya dhambi za kuvunja amri nyingine tisa! Hawaelewi kabisa Agano Jipya wanaposema “kama tunaweza kuvunja sabato ni sawa na kusema tunaweza kuzini!” (Haishangazi Waadventista hawawezi kusikia au kuelewa tunayosema wakati akili zao zimepofushwa na roho hii ya udanganyifu). Akili za Waadventista yamepotoshwa na mafundisho haya, na matokeo kwamba kushika sheria ni sehemu muhimu ya dini yao na ni aina hii ya dini ambayo Paulo alihubiri dhidi yake katika barua yake kwa Wagalatia. Tunaona kuwa mafundisho ya Wasabato juu ya siku ya saba hayatokani na maandiko bali yanatokana moja kwa moja na maono ya Ellen White ambayo yaliipa sheria nafasi ya kwanza badala ya Yesu Kristo. Nao Waadventista walitafsiri maandiko kufuatana na maono yake, na kwa kufanya hivyo wanapotosha maandiko yote!

Waadventista wana orodha ya imani 28 za msingi (unaweza kusoma mwenyewe kwenye tovuti yao ya rasmi). Namba 20 inahusu sabato, na inasema, “amri ya nne ya sheria ya Mungu isiyobadilika inahitaji kushikwa kwa siku hii ya saba ya sabato…. Ni ishara ya ukombozi wetu katika Kristo, ishara ya utakaso wetu, ishara ya utii wetu.” (“The fourth commandment of God’s unchangeable law requires the observance of this seventh-day Sabbath… It is a symbol of our redemption in Christ, a sign of our sanctification, a token of our allegiance.”) Kwa hiyo wanasema kwamba kushika sabato ni ishara ya ukombozi wako na utakaso! Watu hawa wamezua dini mpya lakini hakika sio Ukristo! Sisi tunakombolewa kwa damu ya Yesu Kristo; sisi tunatakaswa dhambi zetu kwa damu yake na kwa Roho wa Mungu. Hili limeshatimizwa kwa ajili yetu na Yesu Kristo, na utakaso wetu umeonyeshwa kwa kupitia maisha yaliyobadilishwa kwa imani katika Kristo na si kwa utunzaji wa sheria ya sabato!

Namba 19 ya sheria ya msingi ya imani ya Waadventista (inayoitwa “Sheria ya Mungu”) inasema, “Kanuni kuu za sheria ya Mungu ni ilivyo katika amri kumi, na imeonyeshwa kwa mfano katika maisha ya Kristo. Maagizo haya ni msingi wa Agano la Mungu na watu wake na kiwango katika hukumu ya Mungu.” (“The great principles of God’s law are embodied in the Ten Commandments and exemplified in the life of Christ… These precepts are the basis of God’s covenant with His people and the standard in God’s judgment.”)

Ni wazi kuwa kwa sentensi hizi Waadventista wamekataa ukweli wa Injili na hawana uelewa wa Agano Jipya. Msingi wa Agano Jipya la Mungu na watu wake ni damu ya mwanae Yesu Kristo – sio amri kumi! (Luka 22:20, Waebrania 9;14-20;12:24; 13:20). Ukamilifu wa Mungu umewekwa katika Yesu Kristo – na sio katika amri 10! (Wakolosai 2:9). Mungu sio maandiko yaliyoandikwa kwenye vibao vya mawe; Yeye ni uzima wenyewe, na kutimiza haki ya sheria tunahitaji maisha yake ndani yetu na kuishi kwa imani ndani yake. Yesu Kristo alisema yeye ni njia ya ukweli na uzima! Kristo anayeishi ndani yetu ni njia ya kutimiza haki – na sio kutunza sheria (warumi 8:2-4). Msingi wa Agano la Mungu na sisi ni kifo na ufufuo wa mwanawe! Kama mafarisayo, ndivyo wasabato hao wanashika kwa makini sheria. Wanaabudu maadhimisho ya mambo ya sheria na kukataa njia ya Mungu katika uzima na haki kwa njia ya imani katika mwana wake Yesu Kristo. Kupitia bidii yao katika sheria wanakosa kabisa haki ya sheria; wanashindwa kutimiza haki kwa mujibu wa sheria hata kama inasemwa katika Warumi 10:2-4. Je, hawajasoma, “hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya sheria.” (Warumi 3:20)? Kiwango katika hukumu ya Mungu siyo amri kumi kama Wasabato wanadai katika udanganyifu wao, bali ni Yesu Kristo mwenyewe,

“Katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na Injili yangu, kwa Kristo Yesu.” (Warumi 2:16).

“Yeye asemaye ya kuwa anakaa ndani yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama yeye alivyoenenda… Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama Yeye alivyo mtakatifu… Katika hili pendo limekamilishwa kwetu, ili tuwe na ujasiri katika siku ya hukumu; kwa kuwa, kama yeye alivyo, ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu.” (1 Yoh. 2:6; 3:2,3; 4:17.)

Ingawa mengi zaidi yanaweza kuongelewa kuhusu sheria na imani, nimeandika kikamilifu kuhusu hili katika makala nyingine inayoitwa “Tukusanyike siku gani kati ya jumamosi na jumapili?” Kwa hiyo tafadhali soma makala hiyo ambapo nimeenda katika maandiko mengi ambayo yanahusiana na tofauti kati ya kuishi kwa imani na kuwa chini ya sheria.

Maria alikuwa mama wa Yesu duniani, lakini wale wakatoliki wanaoomba kwake hufanya ibada ya sanamu. Mungu alitoa sheria kupitia Musa, lakini katika Agano Jipya Mungu ametupa Yesu Kristo ili tupate kutimiza haki kwa njia ya “imani ndani yake” – si kwa “kushika sheria ya Musa”. Kwa mafundisho yao Waadventista hufanya ibada ya sanamu na kuinua sheria juu ya Yesu Kristo. Kwa kuitukuza sheria, hasa ya amri ya nne, wamepotoshwa kuhusu maana ya Agano Jipya na wametolewa nje ya wokovu kutoka kwa Mwana wa Mungu.

Ibada hii ya sanamu inajionyesha yenyewe katika udanganyifu zaidi na Ellen White katika habari za siku ya sabato. Yeye hufundisha kwamba utunzaji wa sabato utakuwa upimaji mkubwa wa uaminifu miongoni mwa Waristo – itawatofautisha kati ya wale wanaomtumikia Mungu na wale wasiomtumikia! Alisema wale waumini wanaokutana jumapili huonesha ‘uhaini’ wao kwa Mungu kwa kuiinamia “sheria ya nchi”, na katika nyakati za mwisho wao ndio watakaokuwa na chapa ya Mnyama! ‘Waumini’ wanaotunza sabato wanaonyesha uaminifu kwa mamlaka ya Mungu na wao atawapa “muhuri ya Mungu” uliotajwa katika kitabu cha Ufunuo. Wengine wote (pamoja na wale wanaokiri Kristo) watapokea chapa ya Mnyama! Waadventista mara nyingi huwaita Wakristo wasiotunza sabato na sheria ya Musa “kanisa potofu” , “makanisa yaliyoanguka” au “babeli”. Na wanafanya hivyo pia kwa Wakristo wasiokubaliana nao kwenye vikao kama vile vikundi vya facebook. Hiki ndo ambacho Ellen White aliandika,

“Niliona kwamba sabato ni, na itakuwa, ukuta utakaotenganisha Waisraeli wa kweli wa Mungu (yaani, wale wanaoshika siku ya sabato) na wasioamini (yaani, wote wasioshika siku ya sabato).” Early writings p.32,33.

“Alama au muhuri ya Mungu ni sabato yake, na muhuri au alama ya Mnyama na kupinga sabato.” (The Great Controversy page 691, 1888 edition.)

“Niliona kwamba Mungu ana wana waaminifu miongoni mwa makanisa yalioanguka na kabla mapatilizo hayajaachiwa, wahubiri na watu wataitwa kutoka katika makanisa haya na kwa furaha watapokea ile kweli… Wote walio waaminifu wataondoka katika makanisa yaliyoanguka, na kusimama na masalia.” (Early Writings p.261.)

Hivyo fundisho hili linafikia kiwango cha uongo kamili. Linasema kuwa, si tu kwamba tunatakiwa kutunza sheria ya Musa kwa ujumla wake, lakini iwapo hatutatunza hii sabato ya nje tutakuwa ni sehemu ya haya makanisa yaliyoanguka (au Babeli) na tutakuwa ni sehemu ya wale wanaopokea chapa ya mnyama! Je, hapo unaweza kuona kanisa la Wasabato linavyotuingiza kwenye mtego wa kanisa la vifungo na hofu?

Kanisa la Wasabato lina mfumo wa kuamini ambao sio tu kwamba unawaweka nje ya Injili ya kikiristo, bali hata katika upinzani dhidi ya injili! Katika maana hii kanisa la Sabato ni kama kanisa la Mormons na kanisa la Mashahidi wa Jehova. Joseph Smith, aliyeanzisha kanisa la Mormons alidai kuwa aliona maono na kusema kuwa malaika alimsaidia kutafsiri kwa Kiingereza kitabu cha sahani za dhahabu. Vivyo hivo usabato hutegemea kwa wingi maono na mafundisho ya Ellen White kwa ajili ya kuelewa na tafsiri ya maandiko. Kanisa la Sabato hujitahidi sana kukataa dhana hii, wakisema kuwa Biblia iko juu zaidi katika mafundisho na matendo. Na kwa wazi kabisa husema,

“Hatuamini kuwa maandiko ya Ellen White yanaweza kutumika kama msingi wa mafundisho… Hatuamini kuwa Biblia inaweza tu kueleweka kupitia maandiko ya Ellen White” (“We do not believe that the writings of Ellen White may be used as the basis of doctrine… We do not believe that Scripture can be understood only through the writings of Ellen White.”)

Hii sio kweli; hebu angalia matumizi ya neno “tu” katika sentensi iliyotangulia! Wanachomaanisha ni kuwa tafsiri yao ni inafanana na ya Ellen White na hivyo hawamtegemei yeye (lakini ni tafsiri inayofanana na ya kwake kwa sababu waliathiriwa na yeye!). Hii ni hoja inaendelea katika mzunguko! Tunakaribia ukweli halisi tunapoangalia kauli nyingine wanazotoa kuhusu maandiko ya Ellen White:

“Hatuamini kuwa ubora au kiwango cha uvuvio (inspiration) katika maandiko ya Ellen White ni tofauti na maadiko ya biblia… Tunaamini kuwa Ellen White alivuviwa na Roho Mtakatifu na kuwa maandiko yake, yatokanayo na uvuvio huo, yanahusu na yana mamlaka, na hasa kwa Waadventista Wasabato” (“We do not believe that the quality or degree of inspiration in the writings of Ellen White is different from that of scripture… We believe that Ellen White was inspired by the Holy Spirit and that her writings, the product of that inspiration, are applicable and authoritative, especially to Seventh-day Adventists.” The Adventist Review, December 23, 1982, The Inspiration and Authority of the Ellen G. White Writings, Ten Affirmations and Ten Denials on Ellen White’s Authority).

Hivyo hapa wanaeleza kwa uwazi kabisa kuwa ubora au kiwango cha uvuvio cha Ellen White ni sawa na cha Biblia (hata kama siku hizi wanajaribu kuzikana), na kuwa maandiko yake yanaendana na yana mamlaka. Wasabato wanaamini kuwa maono na mafundisho ya Ellen White nilioorodhesha hapo juu yamevuviwa na Mungu! Hii inaonesha jinsi kanisa zima la Wasababto lilivyodanganyika. Hakuna kanisa la kikristo linaloweza kueleza hivi juu ya mwandishi wao yeyote yule, hata kama wanamwamini au kufuata mafudisho yake kiasi kwa gani.

Tuliwahi kuwa na semina Morogoro na nilikuwa na majadiliano na muumini wa kanisa la sabato. Baada ya kumwonyesha maandiko toka Wagalatia na Wakolosai hatimaye alikubali kuwa ni makosa kuwaeleza watu kuwa wanatakiwa kukusanyika siku ya sabato. Shauku yangu ni kuwa watu wasizuiwe kupata wokovu kamili ambao upo katika Yesu Kristo na ndio sababu nimeandika makala haya. Ni kwa ajili ya watu wale ambao hawana uhakika na wanahitaji wa maelezo ya kimaandiko na ufafanuzi, na kwa hao ambao ijapokuwa ni wasabato, hawajaarithiriwa na kupofushwa na mafundisho ya namna hiyo. Mungu huangalia mioyo yetu na ninafikri inawezekana kwamba mtu akisikia kwa mara ya kwanza kupitia kanisa la sabato habari za Yesu kufa kwa ajili ya dhambi zao na kuamini, Mungu aweza kutenda katika maisha yao. Iwapo moyo wa mtu huyu ni wazi na kweli mbele za Mungu, basi kusoma kwake neno la Biblia kutamwongoza kutoka katika uongo huu wa kanisa la Sabato. Na hivyo, makala hii imeandikwa katika matumaini hayo, kwa sehemu, ili kuwafikia watu kama hao. Lakini kwa wale ambao tayari wameshaathriwa kwa kina sana na mafundisho haya Wasabato na ambao wana bidii sana katika Sheria, upofu na uongo ambao hutenda kazi mioyoni mwao hufanya vigumu kwao kukiri ukweli na kuelewa kile ambacho kiko wazi kabisa katika maandiko ya Biblia. Kama mafarisayo watapinga na kupambana na ukweli wa Injili.

Baadhi ya watu hubishana na Wasabato kana kwamba wasabato ni Wakristo ambao hushika mafundisho yaliyo tofauti na Wakristo wengine. Watu wanaofanya hivyo wanakuwa hawawatendei haki Wasabato! Kushindana na Wasabato kana kwamba ni Wakristo wenzao ni kuwadanganya! Iwapo unataka kuwa rafiki wa kweli na iwapo unataka kuwapenda upendo ule wa Injili, inakubidi kuwaasa kuwa wanafundisha “injili nyingine” (Gal 1:8) na kwamba wanajiweka chini ya laana (Wagal. 3:10), kwamba dini yao ni bure (Gal 4:11), kwa Yesu hana faida yoyote kwao na kuwa wameanguka kutoka kwenye neema (Gal 5:4)! Hii sio kuwahukumu; hii sio kuwakashifu wala sio kuwa katili kwao. Bali huu ni uhalisia ambao pendo letu kwa Bwana Yesu na ukweli wake vinatakiwa kutuongoza katika kutangaza.
Umepotosha sana kwa ulichoandika, sijui ni kwa makusudi au bahati mbaya. ninaweka hapa chini misingi ya kanisa la wasabato ambayo imekuwa derived kutoka kwenye biblia na biblia tu, na tupo tayari kujifunza

Waadventista wasabato huipokea Biblia kama kanuni yao pekee na hushika baadhi ya misingi ya imani kuwa ndiyo mafundisho ya mabadiliko matakatifu. Imani hizi, kamazilivyoorodheshwa hapa, hufanya welekevu wa kanisa na udhihirisho wa mafundisho ya mabadiliko. Masahihisho ya kauli hizi yanaweza kutegemewa katika kikao cha Halmashaurikuu wakati kanisa likiongozwa na Roho Mtakatifu kwenye ufahamu ulio kamili zaidi ya ukweli wa Biblia au linapopata lugha iliyo bora zaidi ya kuelezea mafundisho ya Neno Takatifu la Mungu.

1.Maandiliko Matakatifu
Maandiko Matakatifu, yaani Agano la kale na Jipya ndiyo Neno la Mungu lililoandikwa,likatolewa kwa uvuvio wa Mungu, kupitia kwa watu watakatifu walionena na kuandika kamawalivyoagizwa na Roho Mtakatifu. Ndani ya neno hili, Mungu amemkabidhi mwanadamu maarifa yaliyo lazima kwa ajili ya wokovu. Maandiko matakatifu ni ufunuo usioweza kukosa wa mapenzi yake. Ndiyo upeo wa tabia, kipimo cha uzoefu, ufunuo thabiti wenye mamlaka wa mafundisho ya imani, na kumbukumbu aminifu ya matendo ya mungu katika historia. (2Petro 1:20,21. 2Timotheo 3:16,17. Zaburi 119: 105. Mithal 30: 5,6. Isaya 8:20. Yoh 17:17. 1Wathe 2:13. Waeb4:12.)

2.Utatu Mtakatifu
Kuna Mungu mmoja: Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, umoja wa nafsi tatu za milele. Mungu hapatikani na mauti, mwenye nguvu zote, ajuaye yote, zaidi ya yote, na aliyeko daima. Yeye hana mwisho na ni zaidi ya ufahamu wa kibinadamu, hata hivyo anafahamika kupitia kujifunua kwake binafsi. Milele zote yu astahili kuabudiwa, kusujudiwa, kutumikiwa na viumbe vyote. (kumb 6:4. Mith 28:19. 2kor 13:14. Waef 4:4-6. 1Petr 1:2 1Tim 1:17 Ufunuo 14:7)

3.Baba
Mungu Baba wa milele ndiye muumbaji, Chimbuko, Mtengenezaji, na Mfalme wa viumbe wote. Ni mwenye haki na Mtakatifu, Mwingi wa rehema,, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, na mwingi wa uthabiti wa upendo na uaminifu. Tabia na uwezo vilivyodhihirishwa ndani ya Mwana na Roho Mtakatifu pia ni ufunuo wa Baba. (Mwanzo 1:1 Ufu 4:11.
1wakor 15:28. Yoh 3:16. 1Yoh 4:8. 1Tim 1:17. Kut 34:6,7. Yoh 14:9).

4.Mwana
Mungu Mwana wa milele alifanya mwili katika Yesu Kristo. Kupitia kwake vitu vyote viliumbwa, tabia ya mungu imefunuliwa, wokovu wa wanadamu unakaribishwa na ulimwengu unahukumiwa. Milele zote Mungu kweli, Alifanyika mwanadamu kweli, Yesu aliye kristo. Alichukuliwa mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu na kuzaliwa na bikira Mariamu. Akaishi na kupitia uzoefu majaribu kama mwanadamu, lakini kwa ukamilifu alioonyesha kwa mfano wa haki na u[endo wa Mungu. Kwa miujiza yake alidhihirisha uwezo wa Mungu na alithibitishwa kama Masihi aliyeahidiwa. Aliteseka na kufa kwa hiari msalabani kwa ajili ya dhambi zetu, na kama mbadala wetu, Alifufuliwa kutoka kwa wafu, na akapaa kuhudumu katika hekalu la mbinguni kwa niaba yetu. Atakuja tena katika utukufu kwa ajili ya ukombozi wa mwisho wa watu wake na urejeshwaji wa vitu vyote. (Yoh 1: 1-3,14. Wakol 1: 15-19,. Wafil 2:5-11. Yoh 10:30, 14:9 Warum 6:23. 2Wakor 5:17-19.Yoh 5:22. 1Wakor 15:3,4. Luka 1:35. Yoh 14:1-3)

5.Roho Mtakatifu
Mungu Roho wa milele alikuwa mtendaji pamoja na Baba na Mwana katika uumbaji, kufanyika mwili, na katika ukombozi. Aliwavuvia waandishi wa mabadiliko matakatifu. Alijaza maisha ya kristo na uwezo. Huwavuta na kuwasadikisha wanadamu, na wale wanaoitikia huwafanya upya na kuwabadilisha katika sura ya Mungu. Akipelekwa na Baba na Mwana ili kuwa siku zote pamoja na watoto wake, hutoa karama za kiroho kwa kanisa, huliwezesha kumshuhudia kristo, na kwa upatano wa maandiko uliongoza kwenye ukweli wote. (Mwa 1,2. Luka 1:35, 4:18. Mdo 10:38. 2Petr 1:21. 2Wakor 3:18. Yoh 14:16-18,26, 15:26,27, 16:7-13)

6.Uumbaji
Mungu ni muumba wa vitu vyote, na amefunua katika maandiko uhalisi wa tukio la
shughuli zake za uumbaji. Katika siku sita Bwana alizifanya “Mbingu na Nchi” na vitu vyote
vilivyoko hai juu ya nchi, akastarehe siku ya saba ya juma lile la kwanza. Na hivyo
akaanzisha sabato kama kumbukumbu ya milele ya kukamilika kwa kazi yake ya uumbaji.
Mwanaume na Mwanamke wa kwanza walifanywa kwa mfano wa Mungu kama upeo wa
kazi yake ya Uumbaji, wakapewa utawala juu ya ulimwengu, na wakaagizwa kuajibika na
utunzaji wake. Wakati ulimwengu ulipomalizika kila kitu kilikuwa “ni chema sana”
ukitangaza utukufu wa Mungu. (Mwa 1,2. Kut20:8-11. Zab 19:1-6, 33:6-9, 104. Waebr
11:3)

7.Asili ya Mwanadamu
Mwanaume na Mwanamke walifanyawa kwa mfano wa Munguwakiwa kila mmoja na nafsi
yake, uwezo na uhuru wa kufikirina kutenda. Ingawa waliumbwa viumbe huru, kila mmoja
ni umoja wa nafsi isiyogawanyika ya mwili, akili na roho, akimtegemea Mungu kwa uhai na
pumzi na mengine yote. Wakati wazazi wetu wa kwanza walipomwasi Mungu, walikana
utegemezi wao kwa Mungu na wakaanguka kutoka hadhi yao ya juuchini ya Mungu. Sura
ya Mungu iliyopo ndani yao ikaharibika na wakawa chini ya mauti. Wazao wao hushiriki
asili hii ya kuanguka na matokeo yake. Wanazaliwa wakiwa na udhaifu na mivuto ya
kuelekea kwenye uovu. Lakini Mungu katika kristo aliupatanisha ulimwengu na nafsi yake,
na kwa Roho wake hurejesha ndani ya mwanadamuwatubuo sura ya muumba wao.
Wakiwa wameumbwa kwa ajili ya utukufu wa Mungu, wanaitwa kumpenda na kupendana
wao kwa wao na kutunza mazingira yao.(Mwa 1:26-28, 2:7. Zab 8:4-8. Mdo 17:24-28. Mwa
3. Zab 51:5 War 5:12:17. 1Yoh 4:7,8,11,20. Mwa 2:15

8.Pambano kuu
Jamii yote ya wanadamu sasa inahusika katika pambano kuu baina ya kristo na shetani
kuhusu tabia ya Mungu, sheria yake, na utawala wake juu ya ulimwengu. Ugomvi huu
ulianza mbinguni wakati kiumbe aliyeumbwa na kutunukiwa uhuru wa kuchagua, katika
kujiinua akawa shetani, mpinzani wa Mungu, na kupelekea sehemu ya Malaika kwenye uasi.
Akaiagiza Roho ya uasi katika ulimwengu huu pale alipowaongoza Adamu na Hawa
kingia dhambini. Dhambi hii ya mwanadamu ilileta matokeo ya upotoshaji ya sura ya
Mungukatika wanadamu, Uvurugaji wa ulimwengu ulioumbwa, na mwishowe kuteketea
wakati wa gharika iliyokumba ulimwengu wote. Ukitazamwa na viumbe wote ulimwengu
huu ukawa uwanja wa vita ya ulimwengu, ambao kutokana nao Mungu wa upendo
hatimaye akathibitika kuwa mwenye haki. Katika kuwasaidia watu wake katika pambano
hili, kristo anamtuma Roho Mtakatifu na malaika watiifu kuongoza, kulinda, na
kutegemeza katika njia ya wokovu. (Ufu 12:4-9, Isa 14:12-14, Eze 28:12-18, War 1:19-32,
5:12-21, 8:19-22, 1Wakor 4:9, Waeb 1:14)

9.Maisha, Mauti na Ufufuo wa kristo
Katika maisha ya kristo ya utii mtakatifu kwa mapenzi ya Mungu, mateso yake, mauti na
ufufuo, Mungu alitoa njia pekee ya kafara kwa ajili ya dhambi ya mwanadamu, ili kwamba
wale ambao kwa imani wanapokea upatanisho huu waweza kuwa na uzima wa milele, na
ulimwengu wote uweze kuelewa vizuri upendo mtakatifu usio na kikomo wa muumba.
Kafara hii kamilifu huthibitisha haki ya sheria ya mungu na fadhili za tabia yake, kwa
sababu hufanya vyote viwili kuhukumu dhambi zetu na kutupatia msamaha. Kifo cha kristo
ni cha badala na cha kulipia, kupatanisha na chenye kubadilisha. Ufufuo wa Yesu kristo
hutangaza ushindi wa Mungu dhidi ya nguvu za uovu, na kwa wale wanaopokea kafara
huakikisha ushindi wao wa mwisho dhidi ya dhambi na mauti. Kinatangaza ukuu wa Yesu
Kristo, ambaye mbele zake kila goti mbinguni na duniani litapigwa.(Yoh3:16, Isa13:1,
1Petr 2:21, 22,1Wakor 15:3, 4, 20-22, 2Wakor 5:14, 19-21. War1:4, 3:25, 4:25, 8:3, 4,
Wafil2:6-11)

10.Uzoefu wa Wokovu
Katika upendo usio na mwisho na rehema zake Mungu alimfanya Kristo, asiyejua dhamdi
kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili kwambakatika yeye tuweze kufanywa haki ya Mungu.
Tukiongozwa na Roho mtakatifu tunatambua hitaji letu, tunakili hali yetu ya kuwa wenye
dhambi, tunatubu maasi yetu, na kuonyesha imani katika Yesu kama Bwana na Kristo,
kama mbadala na kielelezo. Imani hii inayopokea wokovu huja kupitia katika uwezo wa
kimbingu wan a ni karama ya neema ya Mungu. Kupitia kwa kristo tunahesabiwa haki,
tunafanywa kuwa wana wa binti za Mungu, na kukomesabiwa haki kutoka katika hali ya
kuwa chini ya dhambi. Kupitia kwa Roho tunazaliwa upyana kutakaswa, Roho hufanywa
upya nia zetu, huandika sheria ya Mungu ya upendo katika mioyo yetu, na tunapewa uwezo
wa kuishi maisha matakatifu. Tukikaa ndani yake tunakuwa washiriki wa asili ya uungu na
tuna hakika ya wokovu sasa na katika hukumu. (2Wakor 5:17-21, Yoh3:16, Wag1: 4, 4:4-
7, Tito3:3-7, Yoh16:8, Wag3:13,14. 1Petr 2:21,22. Warumi10:17, 3:21-26, 8:14-17, 12:2.
Warumi8:1-4,5:6-10, 2Petr 1:3,4)

11.Kukua katika kristo
Kwa kifo chake msalabani Yesu alizishinda nguvu za uovu. Yeye aliyewatiisha pepo
wachafu wakati wa huduma yake hapa duniani amezivunja nguvu zao na kuthibitisha
mwisho wao ni uangamivu usioepukika. Ushindi wa Yesu utupatia ushindi dhidi ya nguvu
za uovu ambazo bado zinatafuta kututawala, tunapo tembea naye kwa amani, fyraha, na
uhakika wa upendo wake.Sasa Roho Mtakatifu anakaa ndani yetu na kututia nguvu.
Tukidumu kujikabidhi kwa Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yetu tunawekwa
huru kutoka katika mzigo wa matendo yetu yaliyopita. Hatuishi tena gizani, katika hofu ya
nguvu za uovu, ujinga, na katika kukosa maana kwa namna ya maisha yetu ya awali,. Katika
uhuru huu mpya ndani ya kristo, tumeitwa kukua katika kufanana na tabia yake, tukiongea
naye kila siku katika sala, na kujilisha neno lake kikamilifu, tukikusanyika pamoja kwa ajili
ya ibada, na kushiriki katika utume wa kanisa. Tukijitoa katika kuwahudumia kwa upendo
wale wanaotuzunguka na kuwashuhudia wokovu wake, kuwepo kwake nasi daima kwa njia
ya Roho hugeuza kila wasaa na kazi kuwa uzoefu wa kiroho. (Zab.1:1,2. 23:4, 77:11,12,
Kol1:13-14, 2:6, 14-15, Luka10:17-20, Efe5:19-20, 6:12-18, 1Theo 5:23, 2Petr 2:9, 3:18.
Fil3:7-14, Math20:25-28, Yoh20:21, Gal5:22-25, Rum8: 38-39, 1Yoh4:4, Ebr10

12.Kanisa
Kanisa ni jamii ya waumini wanaomkiri Yesu kristo kuwa bwana na mwokozi katika
mfululizo wa kufungamana na watu wa Mungu katika nyakati za agano la kale, tunaitwa
kutoka katika ulimwengu, na tunajiunga pamoja kwa ajili ya ibada, kwa ajili ya ushirika, kwa
ajili ya mafundisho katika neno, na kwa ajili ya maadhimisho ya meza ya bwana, kwa ajili ya
huduma kwa wanadamu wote, na kwa ajili ya tangazo la injili ulimwenguni kote, kanisa
linapata mamlaka yake kutoka kwa kristo, aliye neno lililofanyika mwili, na kutoka katika
maandiko, ambayo ndiyo neno lililoandikwa. Kanisa ni jamaa ya Mungu, waliofanywa nay
eye kuwa watoto wake, washiriki wake huishi katika misingi ya agano jipya. Kanisa ni mwili
wa Kristo, jamii ya weny imani ambayo kristo mwenyewe ndiye kichwa. Kanisa ni bibi arusi
ambaye kwa ajili yake kristo apate kulisafisha na kulitakasa.Wakati wa kurudi kwake kwa
ushindi, ataliwasilisha kwake mwenyewew kanisa lenye utukufu, waaminifu wa karne zote,
walionunuliwa kwa damu yake, lisilo na waa au kunyanzi, lakini takatifu na lisilo na
ila.(Mwa12:3, Mdo:7:38, Waef4:11-15, 3:8-11, Math28:19,20, 16:13-20, 18:18,
Waef19:22,23, 5:23-27, Wakol1:17-18).

13.Masalio na Utume Wake
Kanisa la ulimwengu lijumuisha wale wote ambao kwa kweli wanamwamini kristo, lakini
katika siku za mwisho, kipindi cha kuenea kwa ukengeufu, masalio wameitwa kuzishika
amri za Mungu na imani ya Yesu kristo. Masalio hawa hutangaza kuwadia kwa saa ya
hukumu, hutangaza wokovu kupitia kristo, na hupiga mbiu ya kukarinia kwa marejeo yake.
Tangazo hili huwakilishwa katika mfano wa malaika watatu wa ufunuo 14, juambatana na
kazi ya hukumu mbinguni na kuwa na matokeo ya kazi ya toba na matengenezo duniani.
Kila muumini anatakiwa kuwa na sehemu binafsi katika ushuhuda huu wa ulimwenguni
kote. (Ufu12:17, 14:6-12, 18:1-4, 2Wakor 5:10, Yuda3,14, 1Petro1:16-19, 3:10-14,
Ufu21:1-14)

14.Umoja katika Mwili wa Kristo
Kanisa ni mwili mmoja ulio na washiriki wengi, walioitwa kutoka katika taifa, kabila, lugha,
na watu. Katika kristo tu viumbe wapya, ubainishi wa rangi, tamaduni, elimu, na taifa, na tofauti
kati ya tabaka ya juu nay a chini, tajiri na maskini, mwanaume na mwanamke,havipaswi kuleta mgawanyiko miongoni mwetu.Sote tu sawa katika kristo,
ambaye kwa roho mmoja ametufunga katika ushirika mmoja pamoja nay eye na sisi
wenyewe kwa wenyewe, tunapaswa kutumika na kutumikiwa pasipo kupendelea au kusita.
Kupitia kwa Yesu kristo katika maandiko tunashiriki imani na tumaini moja, na tunawafikia
wote kwa ushuhuda mmoja. Umoja huu una chimbuko lake katika umoja wa Mungu
mmoja mwenye nafsi tatu, ambaye ametufanya sisi tu watoto wake.(War12:4,5,
1Wakor12:12-14, Math28:19,20, Zabr133:1, 2Wakor5:16,17, Mdo17:26,27, Waef4:14-16,
4:1-6, Yoh17:20-23)

15.Ubatizo
Kwa njia ya ubatizo tunakiri imani yetu katika kifo na ufufuo wa Yesu kristo, na
kushuhudia kufia kwetu dhambi na kusudi letu la kuenenda katika upya wa maisha. Hivyo
tunamkubali kristo kuwa Bwana na Mwokozi, tunakuwa watu wake, na tunapokelewa kama
washiriki wa kanisa lake. Ubatizo ni mfano wa muungano wetu na kristo, msamaha wa
dhambi zetu na kupokea kwetu Roho Mtakatifu. Ni kwa kuzamishwa najini na unategemea
uthibitisho wa imani katika yesu na ushindi wa toba ya dhambi. Unafuata mafunzo katika
maandiko matakatifu na ukubali wa mafundisho yake. (Warum6:1-6, Wakol2:12,13,
Mdo16:30-33, 22:16, 2:38,Math28:19-20)

16.Meza ya Bwana
Meza ya Bwana ni ushiriki katika mfano wa mwili na damu ya Yesu kama udhihirisho wa
imani katika yeye, Bwana na mwokozi wetu. Katika ushirika huu kristo anakuwepo
kukutana na kuwaimarisha watu wake. Kadri tunavyoshiriki, kwa furaha tunatangaza mauti
ya Bwana mpaka arudipo tena. Maandalizi kwa ajili ya meza ya Bwana hujumuisha kujihoji
nafsi, toba na ungamo. Bwana aliamua huduma ya kutawadhana miguu kumaanisha
kutakaswa upya, kuonyesha nia ya kutumiana wenyewe kwa wenyewe katika unyenyekevu
ufananao na wa kristo, na kuungana mioyo yetu katika upendo. Huduma ya Meza ya
Bwana wazi kwa waumini wote wakristo. (1Wakor10:16,17. 11:23-30, Math 26:17-30,
Ufu3:20, Yoh6:48-63, 13:1-17)

17.Karamu za Roho na Huduma
Mungu huwakirimia washiriki wote wa kanisa lake katika kila kizazi karama za kiroho
ambazo kila mshiriki atatumia katika huduma ya upendo kwa ajili ya mema ya kawaida ya
kanisa na wanadamu. Zikitolewa kwa wakala wa Roho Mtakatifu, ambaye humgawia kila
mshiriki kama apendavyo yeye, karama hizo hutoa uwezo wote na huduma zinazohitajiwa
na kanisa katika kuytekeleza shughuli zake zilizoamuriwa na Mungu. Kulingana na
maandiko huduma hizi hujumuisha huduma kama: Imani, uponyaji, unabii, mahubiri,
mafundisho, utawala, upatanisho, huruma, na huduma ya kujinyima na ufadhili kwa ajili ya
msaada na faraja kwa watu. Baadhi ya washiriki huitwa na mungu na kukirimiwa na Roho
kwa ajili ya shughuli zinazotambuliwa na kanisa katika uchungaji, uinjilisti, na utume, na
huduma za kufundisha zinahitajika hasa katika kuwapatia zana washiriki kwa ajili ya
huduma kulijenga kanisa hadi ukomavu wa kiroho, na kukuza umoja wa imani na maarifa
ya Mungu. Pale washiriki wanapozitumia karama hizi za kiroho kama mawakili waaminifu wa neema mbalimbali za Mungu, kanisa hulindwa dhidi ya mivuto miharibifu ya
mafundisho ya uwongo, na hukua kwa ukuaji unaotoka kwa Mungu, nakujengeka imara
katika imani na upendo.(Warumi12:4-8, 1Wakor12:9-11, 27,28. Waef4:8,11, Mdo6:1-7,
1Petr4:10-11)

18.Karama ya Unabii
Mojawapo ya karama za Roho Mtakatifu ni unabii, karama hii ni alama-kitambulisho cha
kanisa la masalio na ilidhihirishwa katika huduma ya Ellen G. White. Kama mjumbe wa
Bwana, maandishi yake ni chanzo kiendelezi na yenye mamlaka ya ukweli yanayolipatia
kanisa faraja, uongozi, mafundisho, na maonyo. Pia yanaweka wazi kuwa Biblia ndiyo
kanuni ambayo kwa hayo mafundisho yote na uzoefu lazima vipimwe. (Yoeli2:28,29,
Mdo2:14-21, Waeb1:1-3, Ufu12:17, 19:10)

19.Sheria ya Mungu
Kanuni kuu za sheria ya Mungu zimetiwa pamoja katika Amri kumi na mfano wake
ulidhihirishwa katika maisha ya kristo,. Nazo zinadhihirisha upendo wa Mungu, mapenzi
yake, na makusudi yake kuhusu mwenendo wa binadamu na mahusiano nazo ni sharti kwa
watu wote katika kila kizazi. Amri hizi ndiyo msingi wa agano la Mungu na watu wake na
kanuni katika hukumu ya Mungu. Kupitia uwakala wa Roho Mtakatifu zinasonda dhambi
na kuhamsha hisia za hitaji la mwokozi. Wokovu wote ni katika neema, na si kwa matendo,
lakini tunda lake ni utii wa amri kumi. Hutii huu hukuza tabia ya kikristo na huwa na
matokeo ya ustawi. Ni ushuhuda wa upendo wetu kwa Bwana na wajibu kwa ajili ya
wanadamu wenzetu. Utii wa imani udhihirisha uwezo wa kristokubadilisha maisha, na
hivyo huimarisha ushuhuda wa kristo. (Kut 20:1-17, Zab40:7,8 Math22:36-40 Kumb28:1-
14 Math5:17-20, War8:3,4 Zab 19:7-14)

20.Sabato
Muumbaji mkarimu, baada ya siku sita za uumbaji, alipumzika siku ya saba na kuanzisha
sabato kwa ajili ya watu wote kama kumbukumbu ya uumbaji. Amri ya nne ya sheria za
Mungu zisizobadilika inaagiza adhimisho la sabato hii ya siku ya saba kama siku ya
mapumziko, ibada, na huduma kulingana na mafundisho na uzoefu wa Yesu, Bwana wa
sabato. Sabato ni siku ya mawasiliano yenye furaha pamoja na Mungu na sisi kwa sisi. Ni
mfano wa ukombozi wetu katika kristo, ishara ya utakaso wetu, ishara ya utii wetu, na
mwonjo wa umilele wetu wa siku zijazo katika ufalme wa Mungu. Sabato na ishara ya daima
ya mungu ya agano la milele la Mungu kati yake na watu wake. Utunzaji wa furaha wa
wakati huu mtakatifu toka jioni hadi jioni, jua kuchwa hadi jua kuchwa, ni adhimishola
matendoya Mungu ya uumbaji na ukombozi. (Mwa 2:1-3, Kut20:8-11, Luka4:16, Isay56:5-
6, 58:13-14, Math12:1-12, Ezek20:12-20, Kumb5:12-15, Wal23:32, Marko1:32).

21.Uwakili
Sisi tu mawakili wa Mungu, tuliokabidhiwa nay eye wakati na fursa, uwezo na mali, na
mibaraka ya dunia na raslikamali zake. Tunawajibika kwake kwa matumizi yake sahihi.
Tunakiri umilikaji wa Mungu kwa huduma ya uaminifu kwake na kwa wanadamu wenzetu, na kwa kurudisha Dhaka na kutoa sadaka kwa ajili ya utangazaji wa injili yake na kwa
utegemezaji na ukuaji wa kanisa lake. Uwakili ni fursa iliyotolewa kwetu na Mungu kwa ajili
ya malezi katika upendo na ushindi dhidi yao choyo na tama. Wakili kufurahia mibaraka
inayowajia wengine kama matokeo ya uaminifu wake.(Mwa1:26-28, 2:15, 1Nyak29:14,
Hagai 1:3-11, Malak3:8-12, 1Wakor 9:9-14, Math23:23, 2Wakor8:1-15 Warumi15:26-27.).

22. Mwenendo wa kikristo
Tumeitwa kuwa watauwa wanaofikiri, kujisikia, na kutenda kutenda kulingana na kanuni za
mbinguni. Ili Roho aumba ndani upya ndini yetu tabia ya Bwana wetu tunajihusisha tu
katika mambo yale ambayo yatazaa katika maisha yetu usafi unaofanana na kristo, afya, na
furaha katika maisha yetu. Hii inamaanisha kwamba maraha na maburudisho yetu
yanapaswa kufikia viwango vikuu vya maonji na uzuri wa kikristo. Huku tukitambua tofauti
za kitamaduni, mavazi yetu yanapaswa yawe ya kawaida, si ya anasa, na safi, yanayostahili
wale ambao uzuri wao wa asili yake si mapambo ya nje, bali asili yake ni mapambo
yasiyoharibika, yenye roho ya upole na utulivu. Pia inamaanisha kwamba kwa kuwa miili
yetu ni maekalu ya Roho mtakatifu, tunapaswa kuitunza kwa akili. Pamoja na mazoezi
tosha na mapumziko, yatupasa kuchagua lishe yenye afya sana kadiri inavyowezekana na
kuepuka vyakula visivyo najisi, vilivyotajwa katika maandiko matakatifu. Kwa vile vinywaji
vya vileo, tumbaku na matumizi mabaya ya madawa hudhuru miili yetu, yatupasa
kuepukana nayo pia. Badala yake yatupasa kujishughulisha na chochote kile kitakacholeta
mawazo yetu na miili yetu yawe katika nidhamu ya kistro, ambaye hutamani uzima wetu,
furaha, na wema. (Warumi 12:1-2, 1Yoh 2:6, Waef5:1;21, Wafil 4:8, 2Wakor 10:5, 6:14,
7:1, 1Pet3:1-4, Walawi 11:1-47, 3Yoh. 2)

23. Ndoa na Familia
Ndoa ilianzishwa Edeni na Mungu na ikasibitishwa na Yesu kuwa muungano wa maisha
yote kati ya mwanaume na mwanamke katika wenzi wenye upendo. Kwa mkristo kifungo
cha ndoa ni kwa Mungu na pia kwa mwenzi, na kishirikiwe tu na wenzi wenye imani moja.
Upendo wa hiari, heshma, staha, na uwajibikaji ndizo fito za {kujenga}uhusiano huu,
ambao utaakisi upendo, utakatifu, ukaribu, uthabiti wa uhusiano kati ya kristo na kanisa
lake. Kuhusu talaka, Yesu alifundisha kwamba mtu anayemwacha mwenza, isipokuwa kwa
sababu ya uasherati, na akaoa {au kuolewa} na mwingine azini. Ingawa baadhi ya
mahusiano ya kifamilia huenda yakashindwa kufikia lengo, wenzi katika ndoa ambazo
wamejitoa kikamilifu kila mmoja kwa mwenzake katika kristo wanaweza kufaulu kufikilia
katika umoja wenye upendo kupitia uongozi wa Roho na malezi ya kanisa. Mungu hubariki
familia na anakusaidia kwamba washirika wake watasaidiana wao kwa wao kufikia upevu
kamili. Wazazi wawalee watoto wao katika kumpendeza na kumtii Bwana. Kwa kielelezo
chao na maneno yao wawafundishe kwamba kristo ni mtiishaji mwenye upendo, daima
mpole na mwenye kujali, anayetaka wawe kiungo katika mwili wake, familia ya Mungu.
Kukuza ukaribu wa mahusiano wa kifamilia ni moja wapo ya alama{ya kujulisha}ujumbe wa
mwisho wa injil. (Mwa 2:18-25, Math 19:3-9, Yoh 2:1-11, 2Wakor6:14, Waef5:21-33, Luka
16:18, 1Wakor7:10-11, Kut20:12, Kumb6:5-9, Mith22:6, Mal 4:5-6)

24. Huduma ya Kristo katika Hekalu la Mbinguni
Kuna hekalu mbinguni, hema la kweli lililosimamishwa na Bwana na siyo mwanadamu.
Ndani yake kristo anahudumu kwa niaba yetu, akiwezesha kupatikana kwa ajili ya waumini
fanaka za kafara yake ya upatanisho iliyotolewa mara moja msalabani kwa ajili ya wote.
Alizinduliwa kuwa kuhani wetu mkuu na akaanza huduma yake ya uombezi wakati wa
kupaa kwake mbinguni. Mnamo mwaka 1884, mwishoni mwa kipindi cha unabii wa siku
2300, aliingia katika awamu ya pili nay a mwisho katika huduma yake ya upatanisho. Ni
kazi ya hukumu ya upelelezi ambaya ni sehemu ya mwisho ambayo hatimaye itakomesha
dhambi yote, iliyokuwa mfano wa kutakaswa kwa hekalu la kale la waebrania katika siku ya
upatanisho. Katika huduma hiyo kielelezo hekalu lilitakaswa kwa damu ya wanyama wa
kafara, likini mambo ya mbinguni hutakaswa kwa kafara kamilifu ya damu ya Yesu.
Hukumu ya upelelezi kufunua kwa viumbe wa mbinguni ni nani miongoni mwa wafu
wamelala katika kristo na hivyo, katika yeye wanahesabiwa kustahili kuwa na sehemu katika
ufunuo wa kwanza. Pia inadhihirisha zazi ni nani miongoni mwa walio hai wanakaa ndani
ya kristo, wakishika amri za Mungu na imani ya Yesu, na katika yeye, hivyo basi, wako
tayari kwa ajili ya kuhamasishwa kuingia katika ufalme wa milele. Hukumu hii huthibitisha
haki ya Mungu, katika kuwokoa wale wanaomwamini Yesu. Hutangaza kwamba wale
waliohudumu kuwa watiifu kwa Mungu watapokea ufalme. Hitimisho ya huduma hii ya
kristo itakuwa ndiyo mwisho wa kufunga mlango wa rehema ya mwanadamu kabla ya
marejeo ya Yesu. (Waebr 8:1-5, 4:14-16, 9:11-28, 10:19-22, 1:3, 2:16-17. Dan 7:9-27, 8:13-
14, 9:24-27. Hes 14:34. Ezekl 4:6 Ufu 14:6-7, 20:12, 14:12, 22:12. )

25. Kuja kwa Kristo mara ya pili
Kuja kwa kristo mara ya pili ndilo tumaini lenye baraka la kanisa, hitimisho kuu la injili.
Kuja kwa mwokozi kutakuwa halisi, binafsi, kutaonekana kwa dunia mzima. Atakaporudi
wenye haki waliokufa watafufuliwa na pamoja na wenye haki walio hai watavikwa utukufu
na kuchukuliwa kwenda mbinguni, lakini waovu watakufa. Kutimizwa karibu kabisa kwa
sehemu nyingi za unabii, pamoja na hakli ya sasa ya ulimwengu, huonyeshe kwamba kuja
kwa kristo ku karibu sana. Wakati wa tukio hilo hakukufunuliwa, na hivyo basi
tunahimizwa kuwa tayari kwa nyakati zote. .(Tito 2:13, Math 24, Mdo1:9-11, Math24:14,
Ufu1:7, 14:14-20, Math24:43-43, Wakor15:51-50, 1Wathes1:7, 4:13-18, 5:1-6, Marko 13,
Luka 21:2, Tim 3:1-5).

26. Mauti na Ufunuo
Mshahara wa dhambi ni mauti. Lakini Mungu, ambaye peke yakehapatwi na mauti,
atawapa uzima wa milelewaliokombolewa wake. Mpaka siku hiyo mauti ni hali ya
kutokuwa na fahamukwa watu wote. Wakati kristo, aliye uzima wetu, atakapotokea, wenye
haki waliofufuliwa na walio hai watafikwa utukufu na kunyakuliwa juu ili kumlaki Bwana
wao. Ufufuo wa pili ambao ni ufufuo wa waovu, utatokea miaka elfu moja baadaye.
(Warum 6:23,1Tim 6:15-16, Mhu 9:5-6, Zab 149:3-4, Yoh 11:11-14, 1Wakor 15:51-54,
1Wathes 4:13-17, Ufu 20:1-10)
.
27. Milenia {Miaka Elfu} na Mwisho wa Dhambi
Milenia ni miaka elfu moja ya utawala wa kristo pamoja na watakatifu wake mbinguni kati
ya ufufuo wa kwanza na pili. Wakati huo waovu waliokufa watahukumiwa, dunia itakuwa
ukiwa na utupu, bila wanadamu wakazi walio hai, lakini ikikaliwa na shetani na malaika
zake. Mwishowe kristo na watakatifu wake na Mji Mtakatifu watashuka kutoka Mbinguni.
Ndipo waovu waliokufa watafufuliwa, nao pamoja na shetani na malika zake watauzingira
mji, Lakini moto kutoka mbinguni utawateketeza ili kuitakasa dunia. Na hivyo ulimwengu
utakuwa huru bila dhambi na wenye dhambi milele. (Ufu 20, 1Wakor 6:2-3, Yer 4:23-26,
Ufu 21:1-5,Mal 4:1, Ezekl 28:18-19)

28. Dunia Mpya
Katika dunia mpya, ambamo haki hukaa,Mungu ataweka tayari makao ya milele
waliokombolewa na mazingira makamilifu kwa maisha ya milele, upendo, furaha na
kujifunza mbele zake. Kwa hapa Mungu mwenyewe atakaa pamoja na watu wake, na taabu
na mauti vitakuwa vimepita. Pambano kuu litakuwa limemalizika, na dhambi haitakuwepo
tena. Vitu vyote vyenye uhai na visivyo na uhai vitatangaza kwamba Mungu ni pendo, naye
atatawala milele. Amina. (2Pet 3:13, Isa 35, 65:17-25, Math 5:5, Ufu 21 :1-7, 22:1-5, 11:5).

SABBATH TIME | MUDA WA SABATO​

 
Unaweza kunisamaraizia japo kwa ufupi…mimi ni msabato
Na hicho ndicho kinachowaponza! Mnapenda mno kusamaraiziwa! Hamtaki kusoma Biblia mmesamaraiziwa na Ellen matokeo yake ni rahisi sana kudanganywa! Soma andiko mwanzo mwisho uelewe acha uvivu! Samahani lakini!
 
Umepotosha sana kwa ulichoandika, sijui ni kwa makusudi au bahati mbaya. ninaweka hapa chini misingi ya kanisa la wasabato ambayo imekuwa derived kutoka kwenye biblia na biblia tu, na tupo tayari kujifunza

Waadventista wasabato huipokea Biblia kama kanuni yao pekee na hushika baadhi ya misingi ya imani kuwa ndiyo mafundisho ya mabadiliko matakatifu. Imani hizi, kamazilivyoorodheshwa hapa, hufanya welekevu wa kanisa na udhihirisho wa mafundisho ya mabadiliko. Masahihisho ya kauli hizi yanaweza kutegemewa katika kikao cha Halmashaurikuu wakati kanisa likiongozwa na Roho Mtakatifu kwenye ufahamu ulio kamili zaidi ya ukweli wa Biblia au linapopata lugha iliyo bora zaidi ya kuelezea mafundisho ya Neno Takatifu la Mungu.

1.Maandiliko Matakatifu
Maandiko Matakatifu, yaani Agano la kale na Jipya ndiyo Neno la Mungu lililoandikwa,likatolewa kwa uvuvio wa Mungu, kupitia kwa watu watakatifu walionena na kuandika kamawalivyoagizwa na Roho Mtakatifu. Ndani ya neno hili, Mungu amemkabidhi mwanadamu maarifa yaliyo lazima kwa ajili ya wokovu. Maandiko matakatifu ni ufunuo usioweza kukosa wa mapenzi yake. Ndiyo upeo wa tabia, kipimo cha uzoefu, ufunuo thabiti wenye mamlaka wa mafundisho ya imani, na kumbukumbu aminifu ya matendo ya mungu katika historia. (2Petro 1:20,21. 2Timotheo 3:16,17. Zaburi 119: 105. Mithal 30: 5,6. Isaya 8:20. Yoh 17:17. 1Wathe 2:13. Waeb4:12.)

2.Utatu Mtakatifu
Kuna Mungu mmoja: Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, umoja wa nafsi tatu za milele. Mungu hapatikani na mauti, mwenye nguvu zote, ajuaye yote, zaidi ya yote, na aliyeko daima. Yeye hana mwisho na ni zaidi ya ufahamu wa kibinadamu, hata hivyo anafahamika kupitia kujifunua kwake binafsi. Milele zote yu astahili kuabudiwa, kusujudiwa, kutumikiwa na viumbe vyote. (kumb 6:4. Mith 28:19. 2kor 13:14. Waef 4:4-6. 1Petr 1:2 1Tim 1:17 Ufunuo 14:7)

3.Baba
Mungu Baba wa milele ndiye muumbaji, Chimbuko, Mtengenezaji, na Mfalme wa viumbe wote. Ni mwenye haki na Mtakatifu, Mwingi wa rehema,, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, na mwingi wa uthabiti wa upendo na uaminifu. Tabia na uwezo vilivyodhihirishwa ndani ya Mwana na Roho Mtakatifu pia ni ufunuo wa Baba. (Mwanzo 1:1 Ufu 4:11.
1wakor 15:28. Yoh 3:16. 1Yoh 4:8. 1Tim 1:17. Kut 34:6,7. Yoh 14:9).

4.Mwana
Mungu Mwana wa milele alifanya mwili katika Yesu Kristo. Kupitia kwake vitu vyote viliumbwa, tabia ya mungu imefunuliwa, wokovu wa wanadamu unakaribishwa na ulimwengu unahukumiwa. Milele zote Mungu kweli, Alifanyika mwanadamu kweli, Yesu aliye kristo. Alichukuliwa mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu na kuzaliwa na bikira Mariamu. Akaishi na kupitia uzoefu majaribu kama mwanadamu, lakini kwa ukamilifu alioonyesha kwa mfano wa haki na u[endo wa Mungu. Kwa miujiza yake alidhihirisha uwezo wa Mungu na alithibitishwa kama Masihi aliyeahidiwa. Aliteseka na kufa kwa hiari msalabani kwa ajili ya dhambi zetu, na kama mbadala wetu, Alifufuliwa kutoka kwa wafu, na akapaa kuhudumu katika hekalu la mbinguni kwa niaba yetu. Atakuja tena katika utukufu kwa ajili ya ukombozi wa mwisho wa watu wake na urejeshwaji wa vitu vyote. (Yoh 1: 1-3,14. Wakol 1: 15-19,. Wafil 2:5-11. Yoh 10:30, 14:9 Warum 6:23. 2Wakor 5:17-19.Yoh 5:22. 1Wakor 15:3,4. Luka 1:35. Yoh 14:1-3)

5.Roho Mtakatifu
Mungu Roho wa milele alikuwa mtendaji pamoja na Baba na Mwana katika uumbaji, kufanyika mwili, na katika ukombozi. Aliwavuvia waandishi wa mabadiliko matakatifu. Alijaza maisha ya kristo na uwezo. Huwavuta na kuwasadikisha wanadamu, na wale wanaoitikia huwafanya upya na kuwabadilisha katika sura ya Mungu. Akipelekwa na Baba na Mwana ili kuwa siku zote pamoja na watoto wake, hutoa karama za kiroho kwa kanisa, huliwezesha kumshuhudia kristo, na kwa upatano wa maandiko uliongoza kwenye ukweli wote. (Mwa 1,2. Luka 1:35, 4:18. Mdo 10:38. 2Petr 1:21. 2Wakor 3:18. Yoh 14:16-18,26, 15:26,27, 16:7-13)

6.Uumbaji
Mungu ni muumba wa vitu vyote, na amefunua katika maandiko uhalisi wa tukio la
shughuli zake za uumbaji. Katika siku sita Bwana alizifanya “Mbingu na Nchi” na vitu vyote
vilivyoko hai juu ya nchi, akastarehe siku ya saba ya juma lile la kwanza. Na hivyo
akaanzisha sabato kama kumbukumbu ya milele ya kukamilika kwa kazi yake ya uumbaji.
Mwanaume na Mwanamke wa kwanza walifanywa kwa mfano wa Mungu kama upeo wa
kazi yake ya Uumbaji, wakapewa utawala juu ya ulimwengu, na wakaagizwa kuajibika na
utunzaji wake. Wakati ulimwengu ulipomalizika kila kitu kilikuwa “ni chema sana”
ukitangaza utukufu wa Mungu. (Mwa 1,2. Kut20:8-11. Zab 19:1-6, 33:6-9, 104. Waebr
11:3)

7.Asili ya Mwanadamu
Mwanaume na Mwanamke walifanyawa kwa mfano wa Munguwakiwa kila mmoja na nafsi
yake, uwezo na uhuru wa kufikirina kutenda. Ingawa waliumbwa viumbe huru, kila mmoja
ni umoja wa nafsi isiyogawanyika ya mwili, akili na roho, akimtegemea Mungu kwa uhai na
pumzi na mengine yote. Wakati wazazi wetu wa kwanza walipomwasi Mungu, walikana
utegemezi wao kwa Mungu na wakaanguka kutoka hadhi yao ya juuchini ya Mungu. Sura
ya Mungu iliyopo ndani yao ikaharibika na wakawa chini ya mauti. Wazao wao hushiriki
asili hii ya kuanguka na matokeo yake. Wanazaliwa wakiwa na udhaifu na mivuto ya
kuelekea kwenye uovu. Lakini Mungu katika kristo aliupatanisha ulimwengu na nafsi yake,
na kwa Roho wake hurejesha ndani ya mwanadamuwatubuo sura ya muumba wao.
Wakiwa wameumbwa kwa ajili ya utukufu wa Mungu, wanaitwa kumpenda na kupendana
wao kwa wao na kutunza mazingira yao.(Mwa 1:26-28, 2:7. Zab 8:4-8. Mdo 17:24-28. Mwa
3. Zab 51:5 War 5:12:17. 1Yoh 4:7,8,11,20. Mwa 2:15

8.Pambano kuu
Jamii yote ya wanadamu sasa inahusika katika pambano kuu baina ya kristo na shetani
kuhusu tabia ya Mungu, sheria yake, na utawala wake juu ya ulimwengu. Ugomvi huu
ulianza mbinguni wakati kiumbe aliyeumbwa na kutunukiwa uhuru wa kuchagua, katika
kujiinua akawa shetani, mpinzani wa Mungu, na kupelekea sehemu ya Malaika kwenye uasi.
Akaiagiza Roho ya uasi katika ulimwengu huu pale alipowaongoza Adamu na Hawa
kingia dhambini. Dhambi hii ya mwanadamu ilileta matokeo ya upotoshaji ya sura ya
Mungukatika wanadamu, Uvurugaji wa ulimwengu ulioumbwa, na mwishowe kuteketea
wakati wa gharika iliyokumba ulimwengu wote. Ukitazamwa na viumbe wote ulimwengu
huu ukawa uwanja wa vita ya ulimwengu, ambao kutokana nao Mungu wa upendo
hatimaye akathibitika kuwa mwenye haki. Katika kuwasaidia watu wake katika pambano
hili, kristo anamtuma Roho Mtakatifu na malaika watiifu kuongoza, kulinda, na
kutegemeza katika njia ya wokovu. (Ufu 12:4-9, Isa 14:12-14, Eze 28:12-18, War 1:19-32,
5:12-21, 8:19-22, 1Wakor 4:9, Waeb 1:14)

9.Maisha, Mauti na Ufufuo wa kristo
Katika maisha ya kristo ya utii mtakatifu kwa mapenzi ya Mungu, mateso yake, mauti na
ufufuo, Mungu alitoa njia pekee ya kafara kwa ajili ya dhambi ya mwanadamu, ili kwamba
wale ambao kwa imani wanapokea upatanisho huu waweza kuwa na uzima wa milele, na
ulimwengu wote uweze kuelewa vizuri upendo mtakatifu usio na kikomo wa muumba.
Kafara hii kamilifu huthibitisha haki ya sheria ya mungu na fadhili za tabia yake, kwa
sababu hufanya vyote viwili kuhukumu dhambi zetu na kutupatia msamaha. Kifo cha kristo
ni cha badala na cha kulipia, kupatanisha na chenye kubadilisha. Ufufuo wa Yesu kristo
hutangaza ushindi wa Mungu dhidi ya nguvu za uovu, na kwa wale wanaopokea kafara
huakikisha ushindi wao wa mwisho dhidi ya dhambi na mauti. Kinatangaza ukuu wa Yesu
Kristo, ambaye mbele zake kila goti mbinguni na duniani litapigwa.(Yoh3:16, Isa13:1,
1Petr 2:21, 22,1Wakor 15:3, 4, 20-22, 2Wakor 5:14, 19-21. War1:4, 3:25, 4:25, 8:3, 4,
Wafil2:6-11)

10.Uzoefu wa Wokovu
Katika upendo usio na mwisho na rehema zake Mungu alimfanya Kristo, asiyejua dhamdi
kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili kwambakatika yeye tuweze kufanywa haki ya Mungu.
Tukiongozwa na Roho mtakatifu tunatambua hitaji letu, tunakili hali yetu ya kuwa wenye
dhambi, tunatubu maasi yetu, na kuonyesha imani katika Yesu kama Bwana na Kristo,
kama mbadala na kielelezo. Imani hii inayopokea wokovu huja kupitia katika uwezo wa
kimbingu wan a ni karama ya neema ya Mungu. Kupitia kwa kristo tunahesabiwa haki,
tunafanywa kuwa wana wa binti za Mungu, na kukomesabiwa haki kutoka katika hali ya
kuwa chini ya dhambi. Kupitia kwa Roho tunazaliwa upyana kutakaswa, Roho hufanywa
upya nia zetu, huandika sheria ya Mungu ya upendo katika mioyo yetu, na tunapewa uwezo
wa kuishi maisha matakatifu. Tukikaa ndani yake tunakuwa washiriki wa asili ya uungu na
tuna hakika ya wokovu sasa na katika hukumu. (2Wakor 5:17-21, Yoh3:16, Wag1: 4, 4:4-
7, Tito3:3-7, Yoh16:8, Wag3:13,14. 1Petr 2:21,22. Warumi10:17, 3:21-26, 8:14-17, 12:2.
Warumi8:1-4,5:6-10, 2Petr 1:3,4)

11.Kukua katika kristo
Kwa kifo chake msalabani Yesu alizishinda nguvu za uovu. Yeye aliyewatiisha pepo
wachafu wakati wa huduma yake hapa duniani amezivunja nguvu zao na kuthibitisha
mwisho wao ni uangamivu usioepukika. Ushindi wa Yesu utupatia ushindi dhidi ya nguvu
za uovu ambazo bado zinatafuta kututawala, tunapo tembea naye kwa amani, fyraha, na
uhakika wa upendo wake.Sasa Roho Mtakatifu anakaa ndani yetu na kututia nguvu.
Tukidumu kujikabidhi kwa Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yetu tunawekwa
huru kutoka katika mzigo wa matendo yetu yaliyopita. Hatuishi tena gizani, katika hofu ya
nguvu za uovu, ujinga, na katika kukosa maana kwa namna ya maisha yetu ya awali,. Katika
uhuru huu mpya ndani ya kristo, tumeitwa kukua katika kufanana na tabia yake, tukiongea
naye kila siku katika sala, na kujilisha neno lake kikamilifu, tukikusanyika pamoja kwa ajili
ya ibada, na kushiriki katika utume wa kanisa. Tukijitoa katika kuwahudumia kwa upendo
wale wanaotuzunguka na kuwashuhudia wokovu wake, kuwepo kwake nasi daima kwa njia
ya Roho hugeuza kila wasaa na kazi kuwa uzoefu wa kiroho. (Zab.1:1,2. 23:4, 77:11,12,
Kol1:13-14, 2:6, 14-15, Luka10:17-20, Efe5:19-20, 6:12-18, 1Theo 5:23, 2Petr 2:9, 3:18.
Fil3:7-14, Math20:25-28, Yoh20:21, Gal5:22-25, Rum8: 38-39, 1Yoh4:4, Ebr10

12.Kanisa
Kanisa ni jamii ya waumini wanaomkiri Yesu kristo kuwa bwana na mwokozi katika
mfululizo wa kufungamana na watu wa Mungu katika nyakati za agano la kale, tunaitwa
kutoka katika ulimwengu, na tunajiunga pamoja kwa ajili ya ibada, kwa ajili ya ushirika, kwa
ajili ya mafundisho katika neno, na kwa ajili ya maadhimisho ya meza ya bwana, kwa ajili ya
huduma kwa wanadamu wote, na kwa ajili ya tangazo la injili ulimwenguni kote, kanisa
linapata mamlaka yake kutoka kwa kristo, aliye neno lililofanyika mwili, na kutoka katika
maandiko, ambayo ndiyo neno lililoandikwa. Kanisa ni jamaa ya Mungu, waliofanywa nay
eye kuwa watoto wake, washiriki wake huishi katika misingi ya agano jipya. Kanisa ni mwili
wa Kristo, jamii ya weny imani ambayo kristo mwenyewe ndiye kichwa. Kanisa ni bibi arusi
ambaye kwa ajili yake kristo apate kulisafisha na kulitakasa.Wakati wa kurudi kwake kwa
ushindi, ataliwasilisha kwake mwenyewew kanisa lenye utukufu, waaminifu wa karne zote,
walionunuliwa kwa damu yake, lisilo na waa au kunyanzi, lakini takatifu na lisilo na
ila.(Mwa12:3, Mdo:7:38, Waef4:11-15, 3:8-11, Math28:19,20, 16:13-20, 18:18,
Waef19:22,23, 5:23-27, Wakol1:17-18).

13.Masalio na Utume Wake
Kanisa la ulimwengu lijumuisha wale wote ambao kwa kweli wanamwamini kristo, lakini
katika siku za mwisho, kipindi cha kuenea kwa ukengeufu, masalio wameitwa kuzishika
amri za Mungu na imani ya Yesu kristo. Masalio hawa hutangaza kuwadia kwa saa ya
hukumu, hutangaza wokovu kupitia kristo, na hupiga mbiu ya kukarinia kwa marejeo yake.
Tangazo hili huwakilishwa katika mfano wa malaika watatu wa ufunuo 14, juambatana na
kazi ya hukumu mbinguni na kuwa na matokeo ya kazi ya toba na matengenezo duniani.
Kila muumini anatakiwa kuwa na sehemu binafsi katika ushuhuda huu wa ulimwenguni
kote. (Ufu12:17, 14:6-12, 18:1-4, 2Wakor 5:10, Yuda3,14, 1Petro1:16-19, 3:10-14,
Ufu21:1-14)

14.Umoja katika Mwili wa Kristo
Kanisa ni mwili mmoja ulio na washiriki wengi, walioitwa kutoka katika taifa, kabila, lugha,
na watu. Katika kristo tu viumbe wapya, ubainishi wa rangi, tamaduni, elimu, na taifa, na tofauti
kati ya tabaka ya juu nay a chini, tajiri na maskini, mwanaume na mwanamke,havipaswi kuleta mgawanyiko miongoni mwetu.Sote tu sawa katika kristo,
ambaye kwa roho mmoja ametufunga katika ushirika mmoja pamoja nay eye na sisi
wenyewe kwa wenyewe, tunapaswa kutumika na kutumikiwa pasipo kupendelea au kusita.
Kupitia kwa Yesu kristo katika maandiko tunashiriki imani na tumaini moja, na tunawafikia
wote kwa ushuhuda mmoja. Umoja huu una chimbuko lake katika umoja wa Mungu
mmoja mwenye nafsi tatu, ambaye ametufanya sisi tu watoto wake.(War12:4,5,
1Wakor12:12-14, Math28:19,20, Zabr133:1, 2Wakor5:16,17, Mdo17:26,27, Waef4:14-16,
4:1-6, Yoh17:20-23)

15.Ubatizo
Kwa njia ya ubatizo tunakiri imani yetu katika kifo na ufufuo wa Yesu kristo, na
kushuhudia kufia kwetu dhambi na kusudi letu la kuenenda katika upya wa maisha. Hivyo
tunamkubali kristo kuwa Bwana na Mwokozi, tunakuwa watu wake, na tunapokelewa kama
washiriki wa kanisa lake. Ubatizo ni mfano wa muungano wetu na kristo, msamaha wa
dhambi zetu na kupokea kwetu Roho Mtakatifu. Ni kwa kuzamishwa najini na unategemea
uthibitisho wa imani katika yesu na ushindi wa toba ya dhambi. Unafuata mafunzo katika
maandiko matakatifu na ukubali wa mafundisho yake. (Warum6:1-6, Wakol2:12,13,
Mdo16:30-33, 22:16, 2:38,Math28:19-20)

16.Meza ya Bwana
Meza ya Bwana ni ushiriki katika mfano wa mwili na damu ya Yesu kama udhihirisho wa
imani katika yeye, Bwana na mwokozi wetu. Katika ushirika huu kristo anakuwepo
kukutana na kuwaimarisha watu wake. Kadri tunavyoshiriki, kwa furaha tunatangaza mauti
ya Bwana mpaka arudipo tena. Maandalizi kwa ajili ya meza ya Bwana hujumuisha kujihoji
nafsi, toba na ungamo. Bwana aliamua huduma ya kutawadhana miguu kumaanisha
kutakaswa upya, kuonyesha nia ya kutumiana wenyewe kwa wenyewe katika unyenyekevu
ufananao na wa kristo, na kuungana mioyo yetu katika upendo. Huduma ya Meza ya
Bwana wazi kwa waumini wote wakristo. (1Wakor10:16,17. 11:23-30, Math 26:17-30,
Ufu3:20, Yoh6:48-63, 13:1-17)

17.Karamu za Roho na Huduma
Mungu huwakirimia washiriki wote wa kanisa lake katika kila kizazi karama za kiroho
ambazo kila mshiriki atatumia katika huduma ya upendo kwa ajili ya mema ya kawaida ya
kanisa na wanadamu. Zikitolewa kwa wakala wa Roho Mtakatifu, ambaye humgawia kila
mshiriki kama apendavyo yeye, karama hizo hutoa uwezo wote na huduma zinazohitajiwa
na kanisa katika kuytekeleza shughuli zake zilizoamuriwa na Mungu. Kulingana na
maandiko huduma hizi hujumuisha huduma kama: Imani, uponyaji, unabii, mahubiri,
mafundisho, utawala, upatanisho, huruma, na huduma ya kujinyima na ufadhili kwa ajili ya
msaada na faraja kwa watu. Baadhi ya washiriki huitwa na mungu na kukirimiwa na Roho
kwa ajili ya shughuli zinazotambuliwa na kanisa katika uchungaji, uinjilisti, na utume, na
huduma za kufundisha zinahitajika hasa katika kuwapatia zana washiriki kwa ajili ya
huduma kulijenga kanisa hadi ukomavu wa kiroho, na kukuza umoja wa imani na maarifa
ya Mungu. Pale washiriki wanapozitumia karama hizi za kiroho kama mawakili waaminifu wa neema mbalimbali za Mungu, kanisa hulindwa dhidi ya mivuto miharibifu ya
mafundisho ya uwongo, na hukua kwa ukuaji unaotoka kwa Mungu, nakujengeka imara
katika imani na upendo.(Warumi12:4-8, 1Wakor12:9-11, 27,28. Waef4:8,11, Mdo6:1-7,
1Petr4:10-11)

18.Karama ya Unabii
Mojawapo ya karama za Roho Mtakatifu ni unabii, karama hii ni alama-kitambulisho cha
kanisa la masalio na ilidhihirishwa katika huduma ya Ellen G. White. Kama mjumbe wa
Bwana, maandishi yake ni chanzo kiendelezi na yenye mamlaka ya ukweli yanayolipatia
kanisa faraja, uongozi, mafundisho, na maonyo. Pia yanaweka wazi kuwa Biblia ndiyo
kanuni ambayo kwa hayo mafundisho yote na uzoefu lazima vipimwe. (Yoeli2:28,29,
Mdo2:14-21, Waeb1:1-3, Ufu12:17, 19:10)

19.Sheria ya Mungu
Kanuni kuu za sheria ya Mungu zimetiwa pamoja katika Amri kumi na mfano wake
ulidhihirishwa katika maisha ya kristo,. Nazo zinadhihirisha upendo wa Mungu, mapenzi
yake, na makusudi yake kuhusu mwenendo wa binadamu na mahusiano nazo ni sharti kwa
watu wote katika kila kizazi. Amri hizi ndiyo msingi wa agano la Mungu na watu wake na
kanuni katika hukumu ya Mungu. Kupitia uwakala wa Roho Mtakatifu zinasonda dhambi
na kuhamsha hisia za hitaji la mwokozi. Wokovu wote ni katika neema, na si kwa matendo,
lakini tunda lake ni utii wa amri kumi. Hutii huu hukuza tabia ya kikristo na huwa na
matokeo ya ustawi. Ni ushuhuda wa upendo wetu kwa Bwana na wajibu kwa ajili ya
wanadamu wenzetu. Utii wa imani udhihirisha uwezo wa kristokubadilisha maisha, na
hivyo huimarisha ushuhuda wa kristo. (Kut 20:1-17, Zab40:7,8 Math22:36-40 Kumb28:1-
14 Math5:17-20, War8:3,4 Zab 19:7-14)

20.Sabato
Muumbaji mkarimu, baada ya siku sita za uumbaji, alipumzika siku ya saba na kuanzisha
sabato kwa ajili ya watu wote kama kumbukumbu ya uumbaji. Amri ya nne ya sheria za
Mungu zisizobadilika inaagiza adhimisho la sabato hii ya siku ya saba kama siku ya
mapumziko, ibada, na huduma kulingana na mafundisho na uzoefu wa Yesu, Bwana wa
sabato. Sabato ni siku ya mawasiliano yenye furaha pamoja na Mungu na sisi kwa sisi. Ni
mfano wa ukombozi wetu katika kristo, ishara ya utakaso wetu, ishara ya utii wetu, na
mwonjo wa umilele wetu wa siku zijazo katika ufalme wa Mungu. Sabato na ishara ya daima
ya mungu ya agano la milele la Mungu kati yake na watu wake. Utunzaji wa furaha wa
wakati huu mtakatifu toka jioni hadi jioni, jua kuchwa hadi jua kuchwa, ni adhimishola
matendoya Mungu ya uumbaji na ukombozi. (Mwa 2:1-3, Kut20:8-11, Luka4:16, Isay56:5-
6, 58:13-14, Math12:1-12, Ezek20:12-20, Kumb5:12-15, Wal23:32, Marko1:32).

21.Uwakili
Sisi tu mawakili wa Mungu, tuliokabidhiwa nay eye wakati na fursa, uwezo na mali, na
mibaraka ya dunia na raslikamali zake. Tunawajibika kwake kwa matumizi yake sahihi.
Tunakiri umilikaji wa Mungu kwa huduma ya uaminifu kwake na kwa wanadamu wenzetu, na kwa kurudisha Dhaka na kutoa sadaka kwa ajili ya utangazaji wa injili yake na kwa
utegemezaji na ukuaji wa kanisa lake. Uwakili ni fursa iliyotolewa kwetu na Mungu kwa ajili
ya malezi katika upendo na ushindi dhidi yao choyo na tama. Wakili kufurahia mibaraka
inayowajia wengine kama matokeo ya uaminifu wake.(Mwa1:26-28, 2:15, 1Nyak29:14,
Hagai 1:3-11, Malak3:8-12, 1Wakor 9:9-14, Math23:23, 2Wakor8:1-15 Warumi15:26-27.).

22. Mwenendo wa kikristo
Tumeitwa kuwa watauwa wanaofikiri, kujisikia, na kutenda kutenda kulingana na kanuni za
mbinguni. Ili Roho aumba ndani upya ndini yetu tabia ya Bwana wetu tunajihusisha tu
katika mambo yale ambayo yatazaa katika maisha yetu usafi unaofanana na kristo, afya, na
furaha katika maisha yetu. Hii inamaanisha kwamba maraha na maburudisho yetu
yanapaswa kufikia viwango vikuu vya maonji na uzuri wa kikristo. Huku tukitambua tofauti
za kitamaduni, mavazi yetu yanapaswa yawe ya kawaida, si ya anasa, na safi, yanayostahili
wale ambao uzuri wao wa asili yake si mapambo ya nje, bali asili yake ni mapambo
yasiyoharibika, yenye roho ya upole na utulivu. Pia inamaanisha kwamba kwa kuwa miili
yetu ni maekalu ya Roho mtakatifu, tunapaswa kuitunza kwa akili. Pamoja na mazoezi
tosha na mapumziko, yatupasa kuchagua lishe yenye afya sana kadiri inavyowezekana na
kuepuka vyakula visivyo najisi, vilivyotajwa katika maandiko matakatifu. Kwa vile vinywaji
vya vileo, tumbaku na matumizi mabaya ya madawa hudhuru miili yetu, yatupasa
kuepukana nayo pia. Badala yake yatupasa kujishughulisha na chochote kile kitakacholeta
mawazo yetu na miili yetu yawe katika nidhamu ya kistro, ambaye hutamani uzima wetu,
furaha, na wema. (Warumi 12:1-2, 1Yoh 2:6, Waef5:1;21, Wafil 4:8, 2Wakor 10:5, 6:14,
7:1, 1Pet3:1-4, Walawi 11:1-47, 3Yoh. 2)

23. Ndoa na Familia
Ndoa ilianzishwa Edeni na Mungu na ikasibitishwa na Yesu kuwa muungano wa maisha
yote kati ya mwanaume na mwanamke katika wenzi wenye upendo. Kwa mkristo kifungo
cha ndoa ni kwa Mungu na pia kwa mwenzi, na kishirikiwe tu na wenzi wenye imani moja.
Upendo wa hiari, heshma, staha, na uwajibikaji ndizo fito za {kujenga}uhusiano huu,
ambao utaakisi upendo, utakatifu, ukaribu, uthabiti wa uhusiano kati ya kristo na kanisa
lake. Kuhusu talaka, Yesu alifundisha kwamba mtu anayemwacha mwenza, isipokuwa kwa
sababu ya uasherati, na akaoa {au kuolewa} na mwingine azini. Ingawa baadhi ya
mahusiano ya kifamilia huenda yakashindwa kufikia lengo, wenzi katika ndoa ambazo
wamejitoa kikamilifu kila mmoja kwa mwenzake katika kristo wanaweza kufaulu kufikilia
katika umoja wenye upendo kupitia uongozi wa Roho na malezi ya kanisa. Mungu hubariki
familia na anakusaidia kwamba washirika wake watasaidiana wao kwa wao kufikia upevu
kamili. Wazazi wawalee watoto wao katika kumpendeza na kumtii Bwana. Kwa kielelezo
chao na maneno yao wawafundishe kwamba kristo ni mtiishaji mwenye upendo, daima
mpole na mwenye kujali, anayetaka wawe kiungo katika mwili wake, familia ya Mungu.
Kukuza ukaribu wa mahusiano wa kifamilia ni moja wapo ya alama{ya kujulisha}ujumbe wa
mwisho wa injil. (Mwa 2:18-25, Math 19:3-9, Yoh 2:1-11, 2Wakor6:14, Waef5:21-33, Luka
16:18, 1Wakor7:10-11, Kut20:12, Kumb6:5-9, Mith22:6, Mal 4:5-6)

24. Huduma ya Kristo katika Hekalu la Mbinguni
Kuna hekalu mbinguni, hema la kweli lililosimamishwa na Bwana na siyo mwanadamu.
Ndani yake kristo anahudumu kwa niaba yetu, akiwezesha kupatikana kwa ajili ya waumini
fanaka za kafara yake ya upatanisho iliyotolewa mara moja msalabani kwa ajili ya wote.
Alizinduliwa kuwa kuhani wetu mkuu na akaanza huduma yake ya uombezi wakati wa
kupaa kwake mbinguni. Mnamo mwaka 1884, mwishoni mwa kipindi cha unabii wa siku
2300, aliingia katika awamu ya pili nay a mwisho katika huduma yake ya upatanisho. Ni
kazi ya hukumu ya upelelezi ambaya ni sehemu ya mwisho ambayo hatimaye itakomesha
dhambi yote, iliyokuwa mfano wa kutakaswa kwa hekalu la kale la waebrania katika siku ya
upatanisho. Katika huduma hiyo kielelezo hekalu lilitakaswa kwa damu ya wanyama wa
kafara, likini mambo ya mbinguni hutakaswa kwa kafara kamilifu ya damu ya Yesu.
Hukumu ya upelelezi kufunua kwa viumbe wa mbinguni ni nani miongoni mwa wafu
wamelala katika kristo na hivyo, katika yeye wanahesabiwa kustahili kuwa na sehemu katika
ufunuo wa kwanza. Pia inadhihirisha zazi ni nani miongoni mwa walio hai wanakaa ndani
ya kristo, wakishika amri za Mungu na imani ya Yesu, na katika yeye, hivyo basi, wako
tayari kwa ajili ya kuhamasishwa kuingia katika ufalme wa milele. Hukumu hii huthibitisha
haki ya Mungu, katika kuwokoa wale wanaomwamini Yesu. Hutangaza kwamba wale
waliohudumu kuwa watiifu kwa Mungu watapokea ufalme. Hitimisho ya huduma hii ya
kristo itakuwa ndiyo mwisho wa kufunga mlango wa rehema ya mwanadamu kabla ya
marejeo ya Yesu. (Waebr 8:1-5, 4:14-16, 9:11-28, 10:19-22, 1:3, 2:16-17. Dan 7:9-27, 8:13-
14, 9:24-27. Hes 14:34. Ezekl 4:6 Ufu 14:6-7, 20:12, 14:12, 22:12. )

25. Kuja kwa Kristo mara ya pili
Kuja kwa kristo mara ya pili ndilo tumaini lenye baraka la kanisa, hitimisho kuu la injili.
Kuja kwa mwokozi kutakuwa halisi, binafsi, kutaonekana kwa dunia mzima. Atakaporudi
wenye haki waliokufa watafufuliwa na pamoja na wenye haki walio hai watavikwa utukufu
na kuchukuliwa kwenda mbinguni, lakini waovu watakufa. Kutimizwa karibu kabisa kwa
sehemu nyingi za unabii, pamoja na hakli ya sasa ya ulimwengu, huonyeshe kwamba kuja
kwa kristo ku karibu sana. Wakati wa tukio hilo hakukufunuliwa, na hivyo basi
tunahimizwa kuwa tayari kwa nyakati zote. .(Tito 2:13, Math 24, Mdo1:9-11, Math24:14,
Ufu1:7, 14:14-20, Math24:43-43, Wakor15:51-50, 1Wathes1:7, 4:13-18, 5:1-6, Marko 13,
Luka 21:2, Tim 3:1-5).

26. Mauti na Ufunuo
Mshahara wa dhambi ni mauti. Lakini Mungu, ambaye peke yakehapatwi na mauti,
atawapa uzima wa milelewaliokombolewa wake. Mpaka siku hiyo mauti ni hali ya
kutokuwa na fahamukwa watu wote. Wakati kristo, aliye uzima wetu, atakapotokea, wenye
haki waliofufuliwa na walio hai watafikwa utukufu na kunyakuliwa juu ili kumlaki Bwana
wao. Ufufuo wa pili ambao ni ufufuo wa waovu, utatokea miaka elfu moja baadaye.
(Warum 6:23,1Tim 6:15-16, Mhu 9:5-6, Zab 149:3-4, Yoh 11:11-14, 1Wakor 15:51-54,
1Wathes 4:13-17, Ufu 20:1-10)
.
27. Milenia {Miaka Elfu} na Mwisho wa Dhambi
Milenia ni miaka elfu moja ya utawala wa kristo pamoja na watakatifu wake mbinguni kati
ya ufufuo wa kwanza na pili. Wakati huo waovu waliokufa watahukumiwa, dunia itakuwa
ukiwa na utupu, bila wanadamu wakazi walio hai, lakini ikikaliwa na shetani na malaika
zake. Mwishowe kristo na watakatifu wake na Mji Mtakatifu watashuka kutoka Mbinguni.
Ndipo waovu waliokufa watafufuliwa, nao pamoja na shetani na malika zake watauzingira
mji, Lakini moto kutoka mbinguni utawateketeza ili kuitakasa dunia. Na hivyo ulimwengu
utakuwa huru bila dhambi na wenye dhambi milele. (Ufu 20, 1Wakor 6:2-3, Yer 4:23-26,
Ufu 21:1-5,Mal 4:1, Ezekl 28:18-19)

28. Dunia Mpya
Katika dunia mpya, ambamo haki hukaa,Mungu ataweka tayari makao ya milele
waliokombolewa na mazingira makamilifu kwa maisha ya milele, upendo, furaha na
kujifunza mbele zake. Kwa hapa Mungu mwenyewe atakaa pamoja na watu wake, na taabu
na mauti vitakuwa vimepita. Pambano kuu litakuwa limemalizika, na dhambi haitakuwepo
tena. Vitu vyote vyenye uhai na visivyo na uhai vitatangaza kwamba Mungu ni pendo, naye
atatawala milele. Amina. (2Pet 3:13, Isa 35, 65:17-25, Math 5:5, Ufu 21 :1-7, 22:1-5, 11:5).

SABBATH TIME | MUDA WA SABATO​



ASANTE KWA ANDIKO MKUU.

HUYO KIJANA AMETUMWA NA ILE PEMBE NDOGO YA MNYAMA (VATCAN.)
 
Back
Top Bottom