Chongolo: Mbowe ana wajomba zake Nyeri na Zitto baadhi ya baba zake wanakaa Bukavu

Chongolo: Mbowe ana wajomba zake Nyeri na Zitto baadhi ya baba zake wanakaa Bukavu

Chongolo ndio anakuza mambo,kwani mtu kuwa na ndugu zake Elsewhere ni shida?
Uliza Nape na Membe na hao wanaojiita wenye chama wazalendo ndio walikuza hayo mambo kumhusu magufuli

What goes around comes around
Wakajisahau kuwa wao nao ni wa kuja
 
Namsikiliza hapa Katibu wangu redioni anasema suala la Mama Samia kuwa na wajomba sehemu nyingine ya dunia sio kubwa Kama linavyotaka kuaminishwa.

Ameenda mbali na kusema mababu zake Zitto wakati wanahamia Kigoma wakitokea Bukavu DRC baadhi ya ndugu zao walibaki huko na wanatembeleana mara kadhaa.

Kwa Upande wa Mbowe amedai pia ujombani kwake Wana asili ya Nyeri nchini Kenya na hata akiwa Kenya huwa hakai hotelini, huwa anakaa nyumba za familia lakini bado alipata nafasi ya kuombea urais.

Amedai wapinzani wafanye kazi waache kutweet vitu vidogo vidogo.
Sawa
 
Wapinzani wako sahihi kuhamasisha umma wa watanzania kudai katiba mpya. Anachokisema Chongolo ni kutapatapa tu kwa kuwa Hangaya ni Rais tayari ambaye alipaswa kufanyiwa vetting hata kabla ya kuwa makamo wa Rais. Kama anachotetea ni habari ndogo, atueleze kwa nini Salim Ahmed Salim alizuiwa kuwa Rais wa JMT pamoja na kuwa na sifa lukuki zilizomuwezesha kuigawa Dunia kwenye Umoja wa Mataifa? Watu wengi hasa mkoa wa Kigoma wamenyanyaswa kwa miaka mingi na idara ya uhamiaji kwa hizi siasa za maji taka. Nadhani uraia pacha uhalalishwe tu, isiwe haki ya upendeleo kwa baadhi ya watu tu..... Chongolo na CCM yake amechemsha tena sana.
 
Mwambieni chongolo hiyo sio ishu !ishu ni ngoro ngoro kupewa wajomba KWA kumwaga Damu za Masai hapo ndio ishu hapo!!


Akome kabisa kupindisha UKWELI!!
 
Siasa za ubaguzi ni rahisi kuzianzisha, mwisho wake zinamtafuna kila mtu, inakuwa kushutumiana tu. Hazina afya kwa hakika.
 
Mnaosakama Magufuli kuwa ana ndugu zake Burundi na jumuiya mrundi mumesikia? Benard Membe umesikia? Huna nduguzo Msumbiji? Unajitia mtanzania mzalendo wakati na wewe kwenu asili yenu Msumbiji
Kwani mtu mwenye asili ya Msumbiji hawezi kuwa Mtanzania mzalendo wewe kilaza??
 
Ukaburu umesharudi tena tangu Nyerere afe? Hapa tukitafuta asili ya kila mtu tutajikuta hatuko wamoja.
Tutaanza kuwamaliza Wahindi kwanza harafu baadaye Wapare,Wachaga,Waha,Wamakonde,Wahaya,Wakurya,Wangoni,nk
 
Mbona Mnyika Babu zake wanatokea Angola 🇦🇴.
 
Namsikiliza hapa Katibu wangu redioni anasema suala la Mama Samia kuwa na wajomba sehemu nyingine ya dunia sio kubwa Kama linavyotaka kuaminishwa.

Ameenda mbali na kusema mababu zake Zitto wakati wanahamia Kigoma wakitokea Bukavu DRC baadhi ya ndugu zao walibaki huko na wanatembeleana mara kadhaa.

Kwa Upande wa Mbowe amedai pia ujombani kwake Wana asili ya Nyeri nchini Kenya na hata akiwa Kenya huwa hakai hotelini, huwa anakaa nyumba za familia lakini bado alipata nafasi ya kuombea urais.

Amedai wapinzani wafanye kazi waache kutweet vitu vidogo vidogo.
Chogolo anababayake huko Comoro.
 
Chongolo aseme je hao ndugu Zitto huko kongo na Mbowe huko kenya je wanataka mbuga zetu?Hao ndugu zao wanazitolea macho Mali zetu tna kwa garama ya maisha ya wananchi wetu?
 
Namsikiliza hapa Katibu wangu redioni anasema suala la Mama Samia kuwa na wajomba sehemu nyingine ya dunia sio kubwa Kama linavyotaka kuaminishwa.

Ameenda mbali na kusema mababu zake Zitto wakati wanahamia Kigoma wakitokea Bukavu DRC baadhi ya ndugu zao walibaki huko na wanatembeleana mara kadhaa.

Kwa Upande wa Mbowe amedai pia ujombani kwake Wana asili ya Nyeri nchini Kenya na hata akiwa Kenya huwa hakai hotelini, huwa anakaa nyumba za familia lakini bado alipata nafasi ya kuombea urais.

Amedai wapinzani wafanye kazi waache kutweet vitu vidogo vidogo.
Kuna watu wana akili kama za Jiwe kwa kweli.
Yaani juyo Chongolo ana deal na vitu kama hivi [emoji848][emoji848][emoji848]
 
Back
Top Bottom