Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru chamtunuku Rais Samia Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa), leo Oktoba 10, 2023

Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru chamtunuku Rais Samia Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa), leo Oktoba 10, 2023

Hongera kwake.

Kwa wivu wa machadomo na Sukuma gang watasema ameuza Bandari 😂😂😂

Nawakumbusha tuu Samia ameungana na Putin , Shinzo Abe Kuwahi kupata hiyo degree.

Aliyepewa na Mungu kapewa tuu ,mapovu mengine wayapeleke kupambania familia zao.
---
Chuo Kikuu maarufu nchini India cha Jawaharlal Nehru, leo Oktoba 10, 2023 kimemtunuku Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa), Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa mwanamke wa kwanza kutunukiwa shahada hiyo na chuo hicho.

Rais Samia anapokea shahada hiyo ikiwa ni takribani mwaka mmoja tangu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kumtunuku Shahada ya Heshima ya Udaktari kutambua mchango wake katika kuboresha sekta ya elimu, uchumi, demokrasia, na usawa wa kijinsia nchini.

Chuo hicho kilianzishwa Aprili 22, 1969 na kupewa jina la Waziri Mkuu wa kwanza wa India, Jawaharlal Nehru, na kuwa moja ya vyuo vikuu bora nchini India na duniani kwa ujumla kikijivunia kuwa taasisi ya elimu ya juu ambapo watu maarufu wa India walipata elimu yao ya juu.

Baadhi ya majina maarufu yaliyoandikishwa katika chuo hicho ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa India, Bw. Subrahmanyam Jaishankar, na Waziri wa Fedha, Bi. Nirmala Sitharaman, huku kikitoa Shahada ya Heshima kwa viongozi wawili pekee akiwemo Rais wa Urusi, Vladmir Putin pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Japan, Hayati Shinzo Abe.

Shahada hiyo ya heshima imetolewa kwa kutambua juhudi za Rais Samia katika kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na India, kutokana na mafanikio yake katika uwanja wa kidiplomasia, haswa diplomasia ya kiuchumi, na mafanikio katika kuchochea maendeleo yanayojikita kwa watu nchini Tanzania.
 
[emoji736]Kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na India

[emoji736]Diplomasia ya Uchumi

[emoji736]Mchango wake katika maisha ya kila siku ya Wananchi wa Tanzania
03c46a96-1272-4325-a628-9c9994a4962a.jpg


[emoji736]Mafanikio yake Kikanda na Kimataifa
 
Jawaharlal Nehru was an Indian anti-colonial nationalist, secular humanist, social democrat, and author who was a central figure in India during the middle of the 20th century. Nehru was a principal leader of the Indian nationalist movement in the 1930s and 1940s. Wikipedia

Huyu bwana historia yake alikuwa mzalendo, mwana demokrasia na mpingaji wa ukoloni, inasikitisha chuo chenye jina lake kutumika vizuri kwa kutambua mchango wa Rais wetu kipenzi, hakika mama anaupiga mwingi kuanzia Dubai hadi India ..
Jamaa wajanja
 
LUKUVI! Kama nimemuona Lukuvi, au macho yangu yana ukungu? Nijulisheni wakuu.
 
Hongera Mheshimiwa Rais. Hongera sana Mama Yetu Mpendwa. Msukuma na Babu Tale sijui walihudhuria?
 
Vyeti vya kijinga ile mbaya. Akiwa huko wanamuuliza anataka cheti Cha aina gani kisha wanampa kama anavyotaka. Halafu bila aibu utasikia chawa wananza kumtaja kwa hicho cheo bortion.
Wala usijali watamuuliza Mbowe 🤣🤣
 
Sidhani kama Mbowe ana muda wa na hivyo vyeti vya kiduwanzi. Na ikitokea na yeye akashobokea vyeti vya aina hiyo, na yeye atakuwa mshamba fulani tu.
Angekuwa hana.mda nyie chawa wake msingekuwa mnahangaika
 
haya majamaa ni kama wameshajua weakness yetu!
Unaonekana wanampamba kama walivyofanya wale waarabu wa depi wedi ila nao watupige na kitu kizito kichwani.
Hata watu unaondamana nao dunia inajua hawa watu hawako serious!
Kweli tunatumia pesa za walipa kodi kwa watu kama steve nyerere! hapana!
 
Tangu Jakaya Kikwete atunukiwe PhD ya mashaka na kuanza kujiita daktari wakati hata master's hakuwa nayo, umeibuka mchezo mchafu wa kuwapa shahada za heshima honoris causa marais wetu ambao elimu zao kama si za kuunga au kughushi, zinatia shaka. J

e hii kama siyo kuwafanya vijana wetu wakose motisha wa kuzihenyekea mbali na kudhalilisha shahada hizi ni nini? Je wanazistahiki?

Je wanapaswa kujiita madaktari wakati wengi ni vihiyo? Je ni kwanini hawaoni aibu hii au ni kwa vile ni vihiyo? Je kuna namna wanafanya nyuma ya pazia ili kupewa shahada hizi chafu? Je kwanini tusitunge sheria za kuzuia jinai hii ya kiakili na kimaadili?
 

Attachments

  • PhD ZA AIBU NA AJABU.jpg
    PhD ZA AIBU NA AJABU.jpg
    26.2 KB · Views: 2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiendelea na ziara yake ya kitaifa nchini India tarehe 10 Oktoba, 2023.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru kwenye hafla iliyofanyika New Delhi nchini India tarehe 10 Oktoba, 2023. Rais Samia ni Mwanamke wa Kwanza kutunukiwa Shahada hiyo ya Heshima na Chuo hicho Nchini India.

Ni Viongozi wawili tu ambao wametunukiwa Shahada hiyo ya Heshima akiwemo Rais wa Urusi, Vladmir Putin pamoja na Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Japan Hayati Shinzo Abe.

===
Rais Samia ameshukuru kwa heshima hii aliyopewa ya kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa) kutoka chuo cha Jawaharlal Nehru, India, na amesema hii ni mara ya kwanza kwake kupatiwa heshima hii nje ya nchi baada ya kupatiwa na Chuo Kikuu cha Dar es salaam.

Amewashukuru wazazi wake kwa kuona umuhimu wa kuwekeza kwa mtoto wa kike, CCM, ndugu zake pamoja na watu wote waliomshika mkono kuhakikisha anafikia sehemu alipo hivi leo.
View attachment 2777575
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi pamoja na wageni mbalimbali mara baada ya kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru kwenye hafla iliyofanyika New Delhi nchini India tarehe 10 Oktoba, 2023.
Tuzo hii ameitoa kwa watoto wa kike wa kitanzania wanaoishi kwenye mazingira magumu, amewatia moyo kuwa hakuna kisichowezekana.

Kwa Tanzania, India sio nchi tu bali ni sehemu ya familia iliyotenganishwa na mwambao wa bahari, pia ni rafiki wa majira yote. Urafiki huu ulianza zamani, tangu enzi za ukoloni ambapo wananchi wengi wa India wapo nchini Tanzania, hata baadhi ya vyakula vya kihindi vinapatikana Tanzania.

Sherehe ya diwali husherekewa pia Tanzania, pia mahekalu ya Kihindu yapo Tanzania na hata kwenye ziara hii imejumlisha Watanzania wenye asili ya Kihindi.

Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru (Javāharalala Neharū Viśvavidyālaya) ni chuo kikuu cha utafiti wa umma kilichoko Kusini Magharibi mwa Delhi , India. Kilianzishwa mwaka 1969 na kupewa jina la Jawaharlal Nehru, Waziri Mkuu wa kwanza wa India.
View attachment 2777616
View attachment 2777617
Wanafunzi wa Vyuo Vikuu mbalimbali nchini India wakiwa kwenye hafla ambayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alitunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru, New Delhi nchini humo tarehe 10 Oktoba, 2023.

View attachment 2777618
View attachment 2777619
View attachment 2777620
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye hafla ambayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alitunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru, New Delhi nchini India tarehe 10 Oktoba, 2023.





Swali la msingi kwanini hicho chuo hakika mpa heshima hyo waziri mkuu Wai ndugu naendra mondi hyo heshima
 
Back
Top Bottom