Congo: Wachawi wafanya tamasha la hadhara kuonyesha nguvu walizo nazo za kufanya miujiza. Waazimia kuutumia uchawi kukuza uchumi na maendeleo

Congo: Wachawi wafanya tamasha la hadhara kuonyesha nguvu walizo nazo za kufanya miujiza. Waazimia kuutumia uchawi kukuza uchumi na maendeleo

Haya yalitosha kuwathibitishia Waafrika wa leo kuwa hakuna uchawi bali ghilba ya watu waovu tu.

Ilikuwaje Waafrika washindwe kuwaloga hao wazungu washenzi waliowatendea ufedhuli kiwango hicho?
Wachawi konki ndio walikiwa machifu, na machifu walikuwa upande wa wazungu na si upande wa watu wao
 
Si kweli, umedanganywa mambo mengi na mkoloni.
  • Huyu mtu mweusi ndiye mgunduzi wa zana za mawe.
  • Ndiye mgunduzi wa moto
  • Ndiye mgunduzi wa zana za muziki
  • Ndiye mgunduzi wa chuma na ndiye mtumiaji wa awali kabisa wa zana za chuma.
Alipokuja mzungu wahunzi wote na uzao wao aliwauawa na wengine kuwakata viganja vya mikono yao.

Walieneza dini yao kwa makali ya upanga.

Unaeleza contradiction kubwa. Kama mwafrika ndiye aliyegundua hizo teknolojia za awali ilikuwaje mzungu awe vizuri zaidi aweze kusafiri maelfu ya kilomita hadi Afrika halafu awadhibiti na kuwaua Waafrika kirahisi hivyo?

Lazima atakuwa alikuwa zaidi. Ana vyombo vya usafiri advanced na vifaa kama navigation aids. Ana vitabu vya dini. Ana zana za kuua za hali ya juu. Ana elimu kubwa ya dunia, n.k.
 
Tuombe Rais ampe wizara ya michezo na utamaduni Msukuma... na sisi tutapewa hilo fursa tukapae bila mbawa
 
Huwa najiuliza Sana jibu sipati. Hivi kwann mwafrika hakutumia uchawi Ili asichukuliwe utumwani au kutawaliwa na mkoloni.
Akili zao zinaishia kwenye kurogana tu na kuoneana wivu vilikuwa vinapigwa na wakoloni badala hata kujibadilisha wote wawe nyau lakini wanatandikwa makalio tu na ndivyo hayakuwa na nguo yalikuwa magumu kama magome ya miti.
 
Halafu walikuwa wanachongeana kwa wakoloni, ila waafrika sie kama tuna kaujinga fulani ikiwemo laana ya akili.
 
Ngozi nyeusi ni laana. Mpaka wakajipeleka utumwani wenyewe kwa wenyewe.... duh
Ufunuo wa Yohana 1


13 na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa Mwanadamu, amevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini.
14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji; na macho yake kama mwali wa moto;
15 na miguu yake kama shaba iliyosuguliwa sana, kana kwamba imesafishwa katika tanuru; na sauti yake kama sauti ya maji mengi.
16 Naye alikuwa na nyota saba katika mkono wake wa kuume; na upanga mkali, wenye makali kuwili, ukitoka katika kinywa chake; na uso wake kama jua liking'aa kwa nguvu zake.
17 Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,
 
Kibingu Yesu hakuwa mzungu
1643509291014.png

1643509344537.png
 
Wachawi nchini Congo 🇨🇩 DR wamefanya tamasha la wazi lenye nia ya kuonyesha nguvu na uwezo waluo nao.

Wachawi hao kutoka majimbo 12 walikuwa wamevalia mavazi yenye rangi kali na waliweza kuonyesha shughuli zao mbalimbali ambapo waliiomba serikali ya nchi hiyo iwapatoe leseni ili waweze kuzifanya kazi zao kibiashara na kukuza uchumi.

Mshana Jr, wenzetu wameanza kuutumia uchawi kimaendeleo, sisi tunakwama wapi?

Naunga mkono mapinduzi ya teknolojia, kamwe hatuwezi kufanikiwa kwa kutegemea teknolojoa mtumba.

Uchawi ukitumika vyema utakuwa chachu ya mabadiliko ya kisayansi na teknolojoa.

Ili nchi iendelee, inahitaji teknolojia yake yenyewe tofauti na sass ambapo tuna teknolojia mtumba na elimu wanayosoma vijana wetu imeshindwa kutoa matokeo chanya ndio maana hata waliosoma sayansi wanataka wawe wanasiasa

IP Man wa kikongo.
 
Back
Top Bottom