Corona imekuja kuumbua uongo wa dini

Corona imekuja kuumbua uongo wa dini

Pamoja yote uliyoandika, huwezi kuvunja watu moyo wa kuamini.

Inaonyesha hujui neno maombi maana yake.
Poleni na majukumu ya hapa na pale sasa na kale yanayowafanya msilale, niende moja kwa moja kwenye mada husika.

Kama kweli maombi yanafanya kazi kwa namna ambayo tunaaminishwa, kwanini viongozi wa dini wameungana kutekeleza agizo la kuvunja mirundamano ikiwemo mijumuiko ya kiibada ili kuikwepa korona?

Kama walifanya maombi kwa lengo la kuizuia corona isiingie nchini, lakini tunaona corona imeingia, nini kinachokufanya uwaamini kua maombi ya sasa wanayojipanga kuyafanya yataitokomeza corona mazima?

Haya mambo probably si magumu ila ugumu tunauweka sisi kwa kuweka mizaha kwa kutumia kivuli cha dini.

Hivi mfano hawa madaktari wetu na sekta ya afya kiujumla wangejumuika kwenye maombi kwa kuamini kwamba maombi ni njia madhubuti ya kutatua matatizo kama haya katika kila janga la ugonjwa. Kama ambavyo watu wa dini wamekua wakituhimiza kufanya, je tungefanikisha kutibu gonjwa lipi kwa maombi?

Ngoma inaingia tanzania wabongo tulijitia wachamungu sana kua tumepewa mamlaka ya kukanyaga nyoka na n'ge hivyo ukimwi kwetu sio tishio.

Lakini tunachokiona mpaka saizi mapasta na masheikh wanachukua vidonge kwa siri sana. Lakini pamoja na hayo hatuwaoni wakijisalimisha kua wameshindwa kudhibiti ukimwi kwa maombi yao.

Mungu ambaye tunamtolea sadaka kila siku halafu katika matatizo kama haya kajichimbia tu wala hatuoni juhudi zake, huyu si mungu wakuabudiwa. Ni sawa na rafiki mnafki ambaye kwenye matanuzi mkiwa viwanja mnakua naye karibu sana halafu ikatokea siku umeishiwa anakukimbia.

Wahubiri wanahubiri huku wamevaa face mask at the same time wanasema damu ya yesu ni tiba ya kila kitu. What a joke but i ain't laughing?

Tunaambiwa ukiwa na imani waweza kuamisha hadi milima lakini sikutegemea kuona vatican, mekka ziwe kipaumbele kukataza watu wasiende kwao kwa hofu ya korona.

Mungu muweza wa yote yuko wapi mbona kawasusia msala madaktari wetu halafu yeye amesizi tu eti mpaka aamshwe kwa maombi?

Kwanini mungu mjuzi wa yote na muweza wa yote ahitaji maombi?

Mbona kwenye zile hadithi za gharika na sodoma na gomora huyu mungu ali-respond haraka sana kwanini asifanye hivyo kwenye janga hili linalomaliza ndugu zetu na kudhoofisha hali ya uchumi wetu?

Hivi kweli mungu huyu yupo kweli? Maana viongozi wetu wa dini nao wanaathirika mpaka inafikia hatua italy makanisa yameshehena maiti inamaana yeye haoni?

Kwanini Mungu ahitaji maombi yetu ili aweze ku-solve matatizo yetu, ilihali anaelewa hitaji la moyo wetu hata kabla hatujasema?
=============================

Chukua tahadhari kwa kufuata angalizo lililotolewa na mamlaka ya afya Corona haidhibitiwi kwa maombi bali kwa kuepuka makatazo ambayo yameainishwa na shirika la afya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wote wako chaka wanaskilizia madaktari watoe jibu la hitimisho maana wao tayari wamejipanga na majibu yao mfukoni mwao

Ikitokea madaktari wametoa dawa, tutawaskia wakisema maombi yao ndio yamewezesha wanasayansi kupata dawa.

Na ikitokea hakuna dawa iliyotengenezwa na wanasayansi watasema kua mungu katupa corona ili kutujaribu na kutupima imani au watasema mungu hujibu maombi kwa wakati wake
Kwa kweli mkuu hii imekuwa kama danganya toto tuu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Best comment so far,naendelea kusoma nyingine...
Wewe jamaa bhana
Kama hii ndio hoja yako basi unaweza kusema kila jambo limekuja kuumbua uongo wa dini.

Kwa nini hukusema kutafuta riziki kumekuja kuumbua uongo wa dini,maana ingetosha tu mtu kukaandani na kuomba dua halafu chakula kikamshukia.
Au kwanini hukusema kusoma kumekuja kuumbua uongo wa dini,maana ingetosha tu mtu kwenda msikitini kuomba dua kisha tayari akawa professor. Na hivyo hivyo mambo mengine.

We jamaa mwenyezimungu aliweka nidhamu/kanuni katika ulimwengu na mambo hayaendi vile unavyo fikiri wewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe jamaa bhana
Kama hii ndio hoja yako basi unaweza kusema kila jambo limekuja kuumbua uongo wa dini.

Kwa nini hukusema kutafuta riziki kumekuja kuumbua uongo wa dini,maana ingetosha tu mtu kukaandani na kuomba dua halafu chakula kikamshukia.
Au kwanini hukusema kusoma kumekuja kuumbua uongo wa dini,maana ingetosha tu mtu kwenda msikitini kuomba dua kisha tayari akawa professor. Na hivyo hivyo mambo mengine.

We jamaa mwenyezimungu aliweka nidhamu/kanuni katika ulimwengu na mambo hayaendi vile unavyo fikiri wewe.
Kama Mungu aliweka nidhamu katika ulimwengu sasa kwanini corona inasumbua watu halafu tunaona wachamungu wakijihami kwa maombi wakati huu ugonjwa ni sehemu ya matokeo yanayotokana na nidhamu ya ulimwengu aliyoiweka mungu?
 
Pamoja yote uliyoandika, huwezi kuvunja watu moyo wa kuamini.

Inaonyesha hujui neno maombi maana yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
Na hakuna mahali nimeandika kua mvunjike moyo msiamini

Neno maombi muda wake sahihi wakujidhihirisha ilikua ni huu hatutaki maana ya maneno ambayo haisadifu vitendo
 
Dunia yote imesalander! Hakuna mwenye nguvu, hakuna mwenye utaalamu, hakuna tajiri, hakuna teknolojia, hakuna silaha kali, hakuna usalama wa taifa, hakuna hakuna hakuna chochote. Kila nchi inalilia hali yake. Kila nchi inafunga mipaka yake, haijulikani tena nani anamfungia nani. Hakuna nchi inayohurumia nchi nyengine, kila moja inapambana kivyake... yote yamesababishwa na kidudu kidogo-virus.. wala hakionekani kwa macho!!!! Unahitaji nini kukubali kuwa Mungu yupo? ambaye akitaka lake hakuna nguvu yeyote inayoweza kulizuia?!!
Ameleta corona akitaka ataiondoa hakutaka ataiacha iendelee kutia adabu watu. Hapangiwi ampe nani na nani ni maamuzi yake tu!!! Watu wa dini yeye ndo anawajua zaidi kuliko wewe kama ni wa kweli au waongo! Sisi tunaomuamini uwepo wake na nguvu zake tunamuomba atunusuru na hili lkn hatuna haki ya kumlazimisha. Tunaomba, anaweza akatukubalia au akatukatalia! Hakuna mwenye guarantee ya maamuzi ya Mungu!
Ona sasa mwingine huyu

Yani matatizo yanayoua ndugu zetu ikiwemo wachungaji na mashehe ndio njia madhubuti ya kuonesha ukuu wa mungu?
 
Ukweli ni kwamba
Huijui DINI vile ambavyo inatakiwa uijue
Usijidai unaijua dini kuliko wenzako wanao hubiri huku wamevaa mask

Na wala usijidai unaijua dini kuliko wale waliokuzuia usiende kwao kama ulivyozoea siku zote kuwafata ili kupata elimu ya dini

It's Scars
 
Mungu aliweka principles na anafanya Kazi kwa principles.

Huwezi kuwa na njaa halafu unaomba muujiza ushibe bila kula.Lazima kifanyike kitu ili chakula kionekane

Vivyo hivyo kwa magonjwa.Mungu amekupa akili uitumie na siyo mahali unapoweza kutumia akili ya kawaida uombe muujiza.Chumba choo, kitumie vizuri ili usipate kipindupindu.Sasa wewe unaenda kujichamba bila kunawa halafu unashika vyombo vya ndani ukiugua kipindu pindu unamlaumu nani?

Mwisho Mungu usimchukulie poa ndugu yangu unless wewe ni devil worshiper.Kama we ni mtu wa kawaida tu,ujue devil mwenyewe anamwogopa na kutetemeka.Anaweza kukushughulikia tu ili ajipendekeze kwa tabia yako ya kumdharau Mungu.

Tubu na nyenyekea kwa Mungu na acha kuangalia udhaifu wa watu wengine jiangalie wewe mwenyewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya sasa ndiyo madhara ya kuchanganya DINI, SIASA, UTAPELI, SAYANSI, HALF-KNOWLDGE na PREJUDICE.

Katika ukristu, sote tunajua kuna matepeli wengi, wanaotumia jina la Yesu kuishi mjini, kuwafanya wengine mazoba ili wao wapige dili, na hawa wameuumiza ukristu kwa sehem kubwa. Wanapaswa kulaumiwa sababu hawamuhubiri Yesu wa msalaba ila Yesu wa Harusini kana, wao ukristu ni kupata utajari, kupona magonjwa yote, kuishi kama uko peponi ilihali uko duniani.

Jibu rahisi tu ni kwamba hata Yesu mwenyewe, hakuponya wagonjwa wote aliokutana nao, aliponya wale tu ambao uponyaji wao unahusika moja kwa moja na lengo lake kuja duniani, ambalo ni kuokoa roho (na mwili akitaka Yesu, ila sio kwa kuamrishwa na mwanadamu)

Lengo la Yesu na Ukristu, sio kumfanya mwanadamu astarehe duniani, bali mwanadamu atambue maisha ya duniani kama matayarisho ya maisha ya umilele, hili ndilo lililomleta Yesu duniani, na ndiyo kwa mfano kanisa katoliki linafundisha.

Unadhani kwa nini wamisionari walikuja na dini mkono wa kulia na shule/hospitali mkono wa kushoto? je kuna wamisonari wa kikatoliki walikuja na kusema acheni hospitali njooni tuwaombee mpone?

Mungu anasikia kilio chetu na anaweza kutuponya kwa muujiza Corona endapo akitaka, sisi tunafunga na kusali kumuonesha haja na hitaji letu, japo analijua lakini ameshasema OMBENI NANYI MTAPEWA, BISHENI NANYI MTAFUNGULIWA....hakusema simama mlangoni, nitafungua kwa kuwa ninajua unataka kuingia!!!!

Tutumie utashi wetu wa kibinadamu, ambao ni zawadi ya Mungu, kukwepa corona, na tumuombe Mungu atuepushe na Corona kwa namna zile ambazo ziko nje ya uwezo wetu kama wanadamu, ila tusatake kumfanya Mungu shemeji yetu kuwa aje sasa aponeshe Corona ndo awe Mungu kweli.

Nawaambia hivi, hata Mungu akishuka leo hii akaponesha Corona dunia nzima, hamtamwamini, sababu Corona sio kipimo cha uwezo na mamlaka ya Mungu, Mungu hapimwi kwa uwezo wake wa kuponya Corona
 
Una hoja dhaifu sana.mbona yashawahi kupita magonjwa makubwa corona cha mtoto.watu walikufa na dawa ikapatikana,maisha yakaendelea..corona ni ugonjwa kama magonjwa mengine..sioni sababu yakukashifu dini.
corona ipo na itaondoka itabaki story.corona iuwe iwezavyo haiwezi fikia maleria na ambayo dawa zake zipo zakila aina na zinajulikana na inauwa kila siku.mbona hamzisemi dini?.corona ni gonjwa la mlipuko limekuja litaondoka maisha yataendelea.
 
Sasa nani amekwambia amewaachia Madaktari,wakati yeye ndio ameruhusu ugonjwa huo uwepo na uwadhuru watu.

Yeye ndio ameuleta na yeye ndio wakuuondoa,hakuna mwanadamu mwenye kuweza kuuondoa ugonjwa wala kuleta ugonjwa.

Maelezo yako yote yanaonyesha ni kwa namna gani humjui Mola muumba wa mbingu na ardhi.

Kama hili linajulikana kiujumla inamaana unataka kutuaminisha kua watu wadini ni wanafki?

Kama mungu yeye ndio ameamua watu wafe kwa korona na jambo hilo linatambulika kidini kwanini watu wadini wanafanya maombi ili wasalimike?


Halafu kama point ya mungu ni kuwadhuru watu kwa corona kwanini vatican na mekka wakataze watu wasiende kuhiji makwao kwa kuogopa kudhurika na ugonjwa?

Huoni kwa kuwazuia watu wasiende huko maana yake ni kuzuia watu wasidhurike jambo ambalo wanakua wanaenda kinyume na matakwa ya mungu?

Unaelewa kwa mujibu wako hao waliozuia nyinyi msiende huko wamefanya dhambi maana wanawanyima haki ya kusambaza ugonjwa ili watu wadhurike kama alivyokusudia mungu wenu??



It's Scars
 
Hso waebrania ulio wanukuu unahakika gani kama wamesema ukweli?

Unafikiri mapadre huko vatican hawajaona kua kuna nukuu za waebrania mpaka wameamua kupiga marufuku msiende?
Inafurahisha mtu ambaye humwamin Mungu kutaka kuhakikishiwa kama yupo .hicho ni kituko kwa sababu step ya kwanza unatakiwa umwamin Mungu yupo nje ya hapo huwez kumwamin wala kumwelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sahihi "ajabu" sio "hajabu" .

Sikujui kweli ila najadili ujinga wako juu ya jambo hili, kwa vile umeudhihirisha.
Kutokua sahihi wakati nikizungumzia mungu ambaye si sahihi ni sahihi pia

Hunijui ila umeweza kunijadili, hivyo umeonesha ujinga wako wa awali kua sio lazima kitu ukijue ndipo uweze kukijadili. Sasa ulipokua unasema simjui mungu ajabu namjadili nadhani umejiona ujinga wako ulipo

It's Scars
 
Back
Top Bottom