Corona imekuja kuumbua uongo wa dini

Corona imekuja kuumbua uongo wa dini

Scars,
DINI ni mpango wa mwanadamu kumtafuta Mungu, imeumbua dini nyinginna ndio maana kua dini moja kubwa wakaamua kufunga misa zao, wakafuata wale wa MECCA sasa WOKOVU ambao uliletwa na YESU ndio umebaki na ndio mpango wa Mungu kuwakomboa wanadamu na dhaambi zao, hawa watu wa wokovu wanadamu
 
Na tatizo la watanzania mnapenda sana KUONGOPEWA KULIKO UKWELI.
viongozi wa dini NI watu kama sisi. Hawana mamlaka yoyote au nguvu zozote za kuzuia au kuponesha magonjwa.
Ila leo akitokea kiongozi wa dini anasema anatibu corona.
MTAKIMBILIA HUKO.
sababu mnapenda kudanganywa.
NA WAO WANAJUA. Scars,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
laiti kweli wangekua wanaroho mtakatifu anaewapa maono, nadhani wangekua msaada mkubwa sana yanapokuja majanga kama haya maana wangeomba kuoneshwa dawa watu wakapona bt na wao wamejawa na hofu na wanawasubiri madaktari kama waamuz wa hili na si mungu anaewapa maono
 
Kumekuwa na mbwembwe nyingi za wachungaji, mitume na manabii kukitokea matatizo yoyote katika jamii wakijinasibu kuyamaliza kwa uwezo waliopewa.

Mara nyingi wao hutunga vitu na kusisitiza wameoneshwa na Mungu na kutamka kuviondoa. Wakijinasibu wakati mwingine hata kusema wanawaponya watu walioathirika na virusi vya UKIMWI.

Naomba niseme kati ya watu wamekuwa wasanii ni hao manabii pamoja na waumini wao wasio na uelewa ambao huacha kufanya kazi na kuwaita baba zao.

Sasa nasema Corona hii hapa, iondosheni Tanzania. Au yatatueni machangamoto ya ndoa zenu huko nyumbani kwenu. Jihadharini na kudanganya watu kujifanya mnaponya kumbe mnatumia wasanii.

Nachukia wanaoigiza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hakuna nabii mkuu. hii corona ni real wakati wao ni fake
ni sawa na mafuta na maji havichangamani
 
nawachukia sana hawa wapumbavu mkuu, yaani wanazitumia changamoto za ulimwengu huu kujipatia kipato kwa njia nyepesi kweli....

haya wamuombe mungu awape maono yakutibu corona sasa kama kweli wanayotuaminishaga yanaukweli
 
Wakati wa janga la njaa miaka mitatu na nusu watu walipokula mavi ya njiwa vipi hapakuwa na nabii au wakati Israel wametekwa kwenda Babeli hapakuwa na nabii?
 
Baba Swalehe,
Wakati wewe unataka kujua Mungu yupi ni wa wakweli kuna wengine wanataka kujua kama huyo Mungu kweli yupo?

Wewe unaweza kujibu hilo swali kuwa kweli Mungu yupo?
 
Hizi biashara za dini inajulikana wazi kabisa kwamba zilikujaje hapa africa. Siku tukijikomboa kutoka kwenye janga la utumwa wa dini nadhani africa inaweza kuja kupiga hatua kubwa sana hapa duniani katika kila nyanja ili kutengeneza future nzuri kwa kizazi kijacho.
Kwani dini imemzuia muafrika asifanye maendeleo? Mbona haya malalamiko tunayo sisi tu waafrika na wakati hizi dini zimeenea sehemu nyingi tu duniani lakini hatuoni wakilalamika hivi?
 
Scars,
Kwa maana nyengine ni kwamba kumbe tunaweza kuaminishwa jambo la kisayansi na kumbe jambo hilo lisiwe kweli.

Kwenye sayansi tunaambiwa kunafanyika tafiti na sio imani,ila mbona kuna utata wengine wanasema kuna virusi vya ukimwi na wengine wanasema hakuna virusi vya ukimwi? Na wote ni wanasayansi wenye kutofautiana hivyo na wana ushahidi wao wa kisayansi.
 
Mambo ya imani ni magumu.

Usitegemee mara zote uombe na Mungu akujibu on the sport.

Hata Mfalme Daudi kuna wakati alikosea Mungu akawapiga tauni ya siku tatu taifa lilikaribia kuisha.

Hata wana wa Israeli walikuwa wakimkosea Mungu anawapiga au na vita au na maradhi hadi watubu.

Hao watumishi wa leo nao ni watu kama wewe wengi wao wana makandokando kibao. Mungu anawatazama kwanza watubu warejee kwake.

Hata hivyo tuamini tu kuwa wapo wachache wanaoomba na Mungu anasikia.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunao Amin timesha fundishwa before kua itafika wakat. Mtafanyiwa maajabu ambayo yatataka kuamin hamna mungu pia watafufuliwa watu walio kufa utaoneshwa ndugu zako walio kufa nyuma pia maisha yatakua magum na tutaulizwa unataka tukusaidie mkane MUNGU wako Kama hutaki bas angamia na mungu pia alituasa kua Makin na Zama hiz Kwan yeyote atae mkana muda huu basi

amelaaniwa.situation iliopo Sasa ivi Sina Shaka ndio nyakat zile za wanadam kufanya kitu na kutoa point kua wao wamefanya mbona MUNGU wetu hajafanya, soon wataanza kufufua WATU Kwan wamebakiza inshu moja tu how to restore ubongo Kwan moyo tayar pia wazungu wamesha Anza kutoa shuhuda kwamba baada ya muda kadhaa tutaweza kuongea na ndugu zetu ambayo tayar wamesha kufa
Ukitaka kuyaona haya fatilia kuja kwa masih dajal hiz hoja ni kwa Iman ya kiislam tu sijui wakristo Wana hoja Gani.

Ndugu zetu kwa upande wa Iman Ila niwashaur tu endelea kumuamin MUNGU wako
Pia Kaka nikujibu tu ni kwamba wazungu wamewafanya wajinga wengi kuamin kwamba ukitambua hakuna mungu Basi wewe unaakili umejitambua ndiomana wengi wanao jiita majinias hawajambui MUNGU kisa tu hoja zao hazijibiw like MUNGU ametokea wapi bila kujua hili ni swal la kijinga ok tuseme hamna MUNGU

bas na wao watujibu ulimwengu umetokea wap watakwambia ni big bang Yes tunaweza kukubal ni big hang but materio yalitoka wap Kama sisi tumeweza kutokea From no where kwann MUNGU ashindwe pia wanasanyan hawatak kuamin MUNGU yupo SABABU hawana ushaid Wala majibu ilo ndio kosa hawajui vitu vinamipaka yake

MUNGU katuumba ili tuje tumtukuze katika mazingira magum na mazuri Tena niwakumbushe waumin wenzangu ya kua huu ndio muda mzuri wa kumuabudu MUNGU wako sababu MUNGU anapenda kunyenyekewa kwa nyakat zozote zile Sasa Kaz ni kwako kukufuru au kuendelea kufanya ibada Kwan hii ni mitihan tu na tunatakiwa kuifaulu mungu awabariki. Scars,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dunia yote imesalander! Hakuna mwenye nguvu, hakuna mwenye utaalamu, hakuna tajiri, hakuna teknolojia, hakuna silaha kali, hakuna usalama wa taifa, hakuna hakuna hakuna chochote. Kila nchi inalilia hali yake. Kila nchi inafunga mipaka yake, haijulikani tena nani anamfungia nani. Hakuna nchi inayohurumia nchi nyengine, kila moja inapambana kivyake... yote yamesababishwa na kidudu kidogo-virus.. wala hakionekani kwa macho!!!! Unahitaji nini kukubali kuwa Mungu yupo? ambaye akitaka lake hakuna nguvu yeyote inayoweza kulizuia?!!
Ameleta corona akitaka ataiondoa hakutaka ataiacha iendelee kutia adabu watu. Hapangiwi ampe nani na nani ni maamuzi yake tu!!! Watu wa dini yeye ndo anawajua zaidi kuliko wewe kama ni wa kweli au waongo! Sisi tunaomuamini uwepo wake na nguvu zake tunamuomba atunusuru na hili lkn hatuna haki ya kumlazimisha. Tunaomba, anaweza akatukubalia au akatukatalia! Hakuna mwenye guarantee ya maamuzi ya Mungu!
[emoji91][emoji91][emoji91]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jana nimesikia Mch.mmoja akisisitiza watu watoto wasitoke nje kwa kutumia mfano wa Wanaisrael walivoelekezwa wasitoke nje huko Misri.

Hahaha kila hali wanayopitia watu wa dini hutafuta tumaini kwenye vitabu vyao ili kujiridhisha

Sasa hao waisrael wana relate vipi na hii corona?

It's Scars
 
Kama huna din ni bora ukae kimya tambua kuna watu nigeria wameombewa na wamepona kama huna imani kufanikiwa ni shughuri,wewe huna din so kaa kimya
Namna pekee ya kumfanya jamaa akae kimya we jaribu kumthibitishia mungu yupo

It's Scars
 
Kwa hiyo ukimwi, kansa, ebola, presha etc yalikuja ili kuthibitisha MUNGU hayupo? Utasema vilema viwete vipofu kn wapo kwasababu Mungu /nguvu ya maombi imeshindwa?......
Kina ayubu walipigwa magonjwa mazito pamoja na kuwa alikua mcha Mungu sana lkn yote ili idhihirike kua Mungu yupo.....
ndugu acha kukufulu haya yote yapo ili wanadamu mkumbuke ukuu wa Mungu.....
Kwanza hayo maandishi ya biblia unahakika gani kwamba yamezungumza ukweli?

It's Scars
 
Poleni na majukumu ya hapa na pale sasa na kale yanayowafanya msilale, niende moja kwa moja kwenye mada husika.

Kama kweli maombi yanafanya kazi kwa namna ambayo tunaaminishwa, kwanini viongozi wa dini wameungana kutekeleza agizo la kuvunja mirundamano ikiwemo mijumuiko ya kiibada ili kuikwepa korona?

Kama walifanya maombi kwa lengo la kuizuia corona isiingie nchini, lakini tunaona corona imeingia, nini kinachokufanya uwaamini kua maombi ya sasa wanayojipanga kuyafanya yataitokomeza corona mazima?

Haya mambo probably si magumu ila ugumu tunauweka sisi kwa kuweka mizaha kwa kutumia kivuli cha dini.

Hivi mfano hawa madaktari wetu na sekta ya afya kiujumla wangejumuika kwenye maombi kwa kuamini kwamba maombi ni njia madhubuti ya kutatua matatizo kama haya katika kila janga la ugonjwa. Kama ambavyo watu wa dini wamekua wakituhimiza kufanya, je tungefanikisha kutibu gonjwa lipi kwa maombi?

Ngoma inaingia tanzania wabongo tulijitia wachamungu sana kua tumepewa mamlaka ya kukanyaga nyoka na n'ge hivyo ukimwi kwetu sio tishio.

Lakini tunachokiona mpaka saizi mapasta na masheikh wanachukua vidonge kwa siri sana. Lakini pamoja na hayo hatuwaoni wakijisalimisha kua wameshindwa kudhibiti ukimwi kwa maombi yao.

Mungu ambaye tunamtolea sadaka kila siku halafu katika matatizo kama haya kajichimbia tu wala hatuoni juhudi zake, huyu si mungu wakuabudiwa. Ni sawa na rafiki mnafki ambaye kwenye matanuzi mkiwa viwanja mnakua naye karibu sana halafu ikatokea siku umeishiwa anakukimbia.

Wahubiri wanahubiri huku wamevaa face mask at the same time wanasema damu ya yesu ni tiba ya kila kitu. What a joke but i ain't laughing?

Tunaambiwa ukiwa na imani waweza kuamisha hadi milima lakini sikutegemea kuona vatican, mekka ziwe kipaumbele kukataza watu wasiende kwao kwa hofu ya korona.

Mungu muweza wa yote yuko wapi mbona kawasusia msala madaktari wetu halafu yeye amesizi tu eti mpaka aamshwe kwa maombi?

Kwanini mungu mjuzi wa yote na muweza wa yote ahitaji maombi?

Mbona kwenye zile hadithi za gharika na sodoma na gomora huyu mungu ali-respond haraka sana kwanini asifanye hivyo kwenye janga hili linalomaliza ndugu zetu na kudhoofisha hali ya uchumi wetu?

Hivi kweli mungu huyu yupo kweli? Maana viongozi wetu wa dini nao wanaathirika mpaka inafikia hatua italy makanisa yameshehena maiti inamaana yeye haoni?

Kwanini Mungu ahitaji maombi yetu ili aweze ku-solve matatizo yetu, ilihali anaelewa hitaji la moyo wetu hata kabla hatujasema?

====

Chukua tahadhari kwa kufuata angalizo lililotolewa na mamlaka ya afya Corona haidhibitiwi kwa maombi bali kwa kuepuka makatazo ambayo yameainishwa na shirika la afya
Mswali mepesi sana. Sijakna hoja inayohitaji majibu ya kufikirisha kwa sababu vyote ulivyondika ni lugha za kawaida za wapofu wa imani. Jifunze kwanza imani ni nini na inatendaje kazi ndipo uje na hoja za kueleweka. Pole sana mkuu

Sent from my SM-T355Y using Tapatalk
 
Back
Top Bottom