Corona imekuja kuumbua uongo wa dini

Corona imekuja kuumbua uongo wa dini

Naweza nikahojiana nawewe katika angle yeyote ile ambayo wewe kwako unaiona kama itakusaidia kupandikiza uzushi ulio aminishwa

Hapo nimekuonesha ni namna gani dini imekua ikikuongopea kupitia kichaka cha "roho mtakatifu"

Nawewe umeonesha niwazi kabisa umejua hilo thats why hujajisumbua kumjua baba yangu kwa njia ya kufikirika "roho mtakatifu"

Kama roho mtakatifu kashindwa kukuelekeza baba yangu alipo, unahakika gani kua huyo roho mtakatifu ataweza kukuongoza ukapata pepo ambayo umekua ukiaminishwa?



It's Scars
Kama majadiliano yapo serious twende huko ,kama yapo kwenye majadiliano ya kubishana bila hoja siko huko.

Sijakuuliza baba yako Nani?
Swali unaaminije huyo uliye naye kuwa ni baba yako.?

Nguvu ya Roho Mtakatifu nitakapoihitaji itakuja.
 
Kama hakuna aya inayotetea kuran ikijinasibisha kua ni kitabu cha kweli

Niambie unajuaje kuran imesema ukweli?



It's Scars
Sababu nzuri ni wewe. Maana mpaka sasa unababaika na kubwabwaja na kuhororoja bila mpango na kuleta usiyoulizwa. Sikushangai kwani wote tukiwawekea aya niliyokuwekea juu hapo, hali iliyokupata huwapata. Rudia kusoma, mpaka kieleweke...

Kumbe hata unachokisoma Hukielewi. Hakuna Aya hapo inayosema unayoyasema. Hiyo ni challenge. Kasome tena uelewe kilichoandikwa kabla hujakurupuka. Au challenge imekuwa nzito kwako unatafuta pakutokea?

Kuhusu "spider" na "Spiderman" yupi ni fictitious na yupi ni non fiction?

Hapo sasa.
 
Unamkataa spiderman kua hayupo kihalisia halafu unayakubali mapepo?

Unauliza maswali ya kitoto sana, athari ya "spiderman" unaipata wapi mpaka ujenge hoja juu yake ? Hakuna athari unayopata katika uhalisi,lakini athari ya mapepo/majini waouvu ipo na inaonekana. Tatizo la umithilishaji lina wasumbua sana wakana Mungu.
Kwanini matatizo ya akili yausishwe na mapepo wakati tayali ishajulikana kua ni matatizo ya akili?
Yameshajulikana, sasa kipi kilicho sababisha matatizo kuwepo ? Haihitaji nguvu kubwa kujua ya kuwa tatizo hutatuliwa kwa kujua chanzo cha tatizo hilo kwanza.
 
Kama hakuna aya inayotetea kuran ikijinasibisha kua ni kitabu cha kweli

Niambie unajuaje kuran imesema ukweli?



It's Scars
Tunajua Qur'aan imesema ukweli sababu haipingani na hali halisi yaani uhalisia.
 
Unajuaje kua dhana ya mungu sio kitu kilichobuniwa kwa ajili ya dini kutawala watu, huoni kwamba hakuna utofauti na spiderman ambaye amebuniwa kwa ajili ya ku entertaining watu?

Watu kuathirika na dhana ya mungu hakuthibitishi mungu yupo, kunathibitisha wajinga katika jamii bado wapo

Corona imetua watu wanakufa kizembe kwasabu ya ujinga walio athirika kupitia dhana ya mungu kuamini kua maombi ndio msaada wa kweli utaowaepusha na janga hilo

Athari ya dhana ya mungu katika jamii ni kubwa, watu wanajiua kwa kujitoa muhanga kwa ujinga walioathirika nao kuamini ukijitoa mhanga utakua rewarded ukifika peponi

Athari za mungu katika kijamii kiujumla ni athari za ujinga





It's Scars
Huyo aliyebuni habari za Mungu ili atawale ni nani na anatawala kvipi? Hebu elezea basi maana kila mtu anasema lake wengine wanasema watu walibuni habari za Mungu baada ya kukosa majibu yenye kuhusu ulimwengu, Yani ilimradi kila mtu anaongea lake tu,haya niambie habari za mungu zilibuniwa wapi na nani na hao watu/mtu anatawala vp?

Nimekwambia suala la spiderman linaishia kwenye movie tu hakuna mtu aliyewahi kudai uwepo wa spiderman nje ya movie,mtu akisikia spiderman moja kwa moja anajua panaongelewa movie. Na hakuna utata juu ya hilo,sasa nakushangaa unafananisha visivyofanana.

Nimekwambia habari za kweli Mungu yupo au hayupo ni jambo lenye kujadiliwa hadi sasa,ila hilo la spiderman halhitaji mjadala maana kila mmoja anajua spiderman kitu kilichobuniwa kwenye movie basi.
 
Mambo ya imani si ya kuyakurupukia angalia bwana usije ukawa mfano tunaoamini hata sasa tunaona Mungu ametusaidia angalia idadi ya waliopona vs Waliokufa utaona ukuu wa Mungu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ukweli ni mmoja tu either Mungu yupo, au hayupo. Ikiwa hayupo, wale wanaoamini uwepo wake hawatopata hasara yoyote. Ila kama yupo na yale anayoahidi baada ya kufa yapo , wasioamini watakuwaje? It is just a matter of thinking, ila Mungu yupo haijalishi watu wanakubali au wanapinga!!!
Point hapa sio mungu yupo au hayupo, ila ni hizi dini zinazojinasibu na kutumia kivuli cha mungu kutapeli na kupotosha
 
Mambo ya imani si ya kuyakurupukia angalia bwana usije ukawa mfano tunaoamini hata sasa tunaona Mungu ametusaidia angalia idadi ya waliopona vs Waliokufa utaona ukuu wa Mungu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote angekuwepo, kungekuwa hakuna kifo.

Kifo kuwepo kunaonesha Mungu huyo hayupo.

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Hakuna mahali nimekataa mwanasayansi kua na dini au yeyote yule

Mtu anaweza kujua kua mungu hayupo na dini ni utapeli lakini bado ukamuona msikitini au kanisani kwa kukwepa kutengwa na jamii

Na ndio maana nimekuonesha ni jinsi gani matatizo yakitokea watu hawatafuti suluhu kwa njia ya maombi kama walivyokua wakiaminishwa na dini.



It's Scars
Mimi nakuelezea kuhusu mtu kuwa muumini wa dini au anaamini Mungu ila wewe unaleta habari za kuingia msikitini na kanisani,wangapi hawaingia huko na jamii inawatambua dini zao?

Nenda majumba ya ibada utaona watu hufanya maombi kwa hili janga la corona,sijui unakwama wapi? Hata hawa matajiri pamoja na kupiga kazi kwa bidii ila bado hufanya maombi kama kawaida.
 
Mada siyo kuhusu uwepo wa Mungu,ama nguvu za Mungu,
Mada ni DINI
Mungu yupo na ana nguvu juu ya yote hili siyo la kujadili,kataa kubali,
Ishu ni hizi Dini,ndo anachomaanisha mleta mada,
NB namna dini zinashindwa kutukonektisha na majibu toka kwa Mungu,nadhani ndo maana kasema dini zimeumbuka,
Hajasema Mungu,kasema Dini,
Japo binafsi nadhani angeangazia viongozi wa dini zaidi kuliko dini maana wao ndo wafanya dini ziwe bandia ama halisi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote angekuwepo, kungekuwa hakuna kifo.

Kifo kuwepo kunaonesha Mungu huyo hayupo.

Sent from my typewriter using Tapatalk
Hakuna mungu Ila Allah, ambae ndiye muumba wako na wa vyote na umauti ni haki kwako.
 
Mada siyo kuhisu uwepo wa Mungu,ama nguvu za Mungu,
Mada ni DINI
Mungu yupo na ana nguvu juu ya yote hili siyo la kujadili,kataa kubali,
Ishu ni hizi Dini,ndo anachomaanisha mleta mada,

Sent using Jamii Forums mobile app
Dini zinatoa mafunzo yake kwenye vitabu vya dini ambako huko ndio tunapata maelezo yenye kuhusu Mungu.
 
Mimi simuongelei mungu
Namuongelea Mungu,
We endelea kumuongelea mungu
Kwanini mungu ahitaji maombi?

Wewe unaomba ili iweje? Na kwanini uombe kama mungu anajua kuisoma akili yako hata kabla hujamuomba?

Mbona yeye anauwezo wa kujua dhambi zako ulizozifanya kwa kufikiri tu kichwani mwako, na akazihesabu kua ni makosa?

Kwanini ashindwe kusoma hitaji lako la moyo wako bila kusubiria maombi yako?

It's Scars

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna kuamini Mungu na kuna kuigiza kumuamini Mungu
Kuna watu wauaji wanaua watu na ndiyo dhambi kubwa kwenye dini ila bado ni muumini wa dini na anaamini Mungu,sasa huyo mtu utasema anaamini dini kwa sababu katishwa atachomwa moto?

Hoja zengine za kuchekesha kweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unadhani ni kwa nini binadamu kaumbiwa akili na utashi na maarifa makubwa zaidi ya viumbe wote
Hili swala lingekua linatambulika kweli na ikawa linauhalisia, tusingeona nguvu kubwa ikitumika mekka na vatican kupiga marufuku watu wasiende kwa uoga wa kufa, wakati wakifa watapata maisha maziluri ya milele..

It's Scars

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom