Corona imekuja kuumbua uongo wa dini

Corona imekuja kuumbua uongo wa dini

Sasa kama umemsoma humo kwenye hivyo vitabu, kipi kilicho kufanya ujue kwamba hayupo ?. Kijana hili swali ni swali jumla jamala, yaani halikwepeki mzee.

Jibu swali nililo kuuliza.
Kwani kuna relation gani kati ya kusoma kitu nauwepo wa hicho kitu kihalisia?

Nikikupa kitabu cha spiderman hapa ukisome utasema yupo kwasababu umemsoma?
 
Kwani wapi nimesema kua hiyo ni post yako?

Hiyo post mimi nimeiandika na kwangu haina utata, sasa wewe ambaye umejenga swali kupitia hiyo post unabidi uniambie umeielewaje
Hakuna alie sema ina utata, nimekurudisha huko ili uone ya kuwa maswali yangu yanahusu hicho ulichokiandika katika hiyo post, na huwezi kuyatoa humo kama unavyodai.
 
Hakuna alie sema ina utata, nimekurudisha huko ili uone ya kuwa maswali yangu yanahusu hicho ulichokiandika katika hiyo post, na huwezi kuyatoa humo kama unavyodai.
Nimejua kua maswali yako yanahusu hapo na ndio maana nimekutaka unijuze wewe uliielewaje hiyo post?
 
Nilikuvua nguo kwa uongo wako kama huu uliosema sijibu maswali kama haitoshi nilikuwekea screenshot ya maswali ambayo nilikuuliza na hujayajibu mpaka muda huu

Twende moja kwa moja kwenye mada

Kwanza hapa unatakiwa kuelewa nilikua namkusudia mungu ambaye hana sifa ya ubaya, sasa huyu wako mwenye sifa ya ubaya hadi kufikia anaumba ubaya sijawahi kuzisikia habari zake nimekuomba umthibitishe kwanza ili tuendelee
Mungu asiye na sifa za ubaya unakusudia ubaya kama upi ?

Na huyo Mungu asiyekuwa na sifa ya ubaya(uliokusudia) sifa hizo kazisema mwenyewe kuwa hana ama unamuongezea wewe ilhali yeye mwenyewe hajasema kuhusu hizo sifa ?



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani kuna relation gani kati ya kusoma kitu nauwepo wa hicho kitu kihalisia?

Nikikupa kitabu cha spiderman hapa ukisome utasema yupo kwasababu umemsoma?
Ona ulivyo kuwa kilaza, jifunze kusoma hoja kisha uelewe, nilikupa angalizo huko mwanzo kwamba, usihoji au kuuliza swali kabla hujaelewa, matokeo yake ndio haya.

Umesema umemsoma katika hivyo vitabu, haijalishi yupo au hayupo, nikakuuliza, umejuaje kama hayupo ?.Hili ndio swali la msingi.

Unaleta habari za spiderman naona unaishi mule mule katika mtindo dhaifu wa logic, ulianza lini kumsikia spider man ? Yeye kwa dhati yake anajidhihirishaje ?.Haya maswali watu wa logic na falsafa hamuwezi kujiuliza au kuyauliza sababu mnaishi katika fikra na uhojaji wakina Aristotle yaani mpo kwenye chumba kidogo, nje ya chumba hicho hamuwezi kufikiria.

Sasa jibu maswali niliyo kuuliza.

1. Umejuaje Mola hayupo ?
2. Kwa vipi kuwepo kwa mabaya kuthibitishe kutokuwepo kwa Mola ?
3. Lil kinachosababisha mabaya yawepo ?

Ahsante.
 
Nimejua kua maswali yako yanahusu hapo na ndio maana nimekutaka unijuze wewe uliielewaje hiyo post?
Sasa, kwanini umekana kwa kudai hayahusu hoja yako ? Sasa ongeza umakimi kijana, utazidi kuumia.
 
Mungu asiye na sifa za ubaya unakusudia ubaya kama upi ?

Na huyo Mungu asiyekuwa na sifa ya ubaya(uliokusudia) sifa hizo kazisema mwenyewe kuwa hana ama unamuongezea wewe ilhali yeye mwenyewe hajasema kuhusu hizo sifa ?



Sent using Jamii Forums mobile app
Nakusudia Ubaya wowote ule

Vitabu ndio vimeandika hivyo kua yeye ni mungu mwenye upendo wote, na mimi nimejenga hoja kupitia refer hiyo
 
Nakusudia Ubaya wowote ule

Vitabu ndio vimeandika hivyo kua yeye ni mungu mwenye upendo wote, na mimi nimejenga hoja kupitia refer hiyo

Sasa kipi hasa kilicho kujulisha hayupo ? Au umekurupuka tu kuandika unavyojisikia ?
 
Sasa, kwanini umekana kwa kudai hayahusu hoja yako ? Sasa ongeza umakimi kijana, utazidi kuumia.
Wakuongeza umakini niwewe uliye quote jambo ambalo huwezi kuliezelea umelielewaje na sio mimi.

Inaonekana hata hichi ulichokijibu hujakielewa, hujajua ulichokijibu kililenga nini mimi kukuambia kua Nimejua kua maswali yako yanahusu hapo na ndio maana nimekutaka unijuze wewe uliielewaje hiyo post? Inaonekana hata hapo hukuelewa shabaha ya hiyo post ililenga nini

Nakuuliza tena hiyo post wewe umeielewaje?
 
Wakuongeza umakini niwewe uliye quote jambo ambalo huwezi kuliezelea umelielewaje na sio mimi.

Inaonekana hata hichi ulichokijibu hujakielewa, hujajua ulichokijibu kililenga nini mimi kukuambia kua Nimejua kua maswali yako yanahusu hapo na ndio maana nimekutaka unijuze wewe uliielewaje hiyo post? Inaonekana hata hapo hukuelewa shabaha ya hiyo post ililenga nini

Nakuuliza tena hiyo post wewe umeielewaje?
Kijana maswali yangu yameonyesha nilichokielewa mzee, sasa kama hutaki kujibu maswali yangu kwa kisingizio hicho,tunasea hivi hatulei ujinga.
 
Sasa kipi hasa kilicho kujulisha hayupo ? Au umekurupuka tu kuandika unavyojisikia ?
Hiyo hoja nimemjibu huyo mwenzako ambaye imemlenga Mungu ambaye hana sifa ya ubaya, sasa wewe umeidandia juu wakati wewe una mungu wako ambaye anawaumbia watu ubaya.

Kwaiyo kwanza kabisa nataka nijue unakubaliana na mungu huyo ambaye hana sifa ya ubaya wala kuumba ubaya?
 
Kijana maswali yangu yameonyesha nilichokielewa mzee, sasa kama hutaki kujibu maswali yangu kwa kisingizio hicho,tunasea hivi hatulei ujinga.
Kama maswali yako yameonesha ulichokielewa unashindwa nini kutuambia hapa ulichokielewa ili tujenge hoja kupitia uelewa wako juu ya hilo jambo?

yani unataka tuanze kuweka mlolongo usio wa lazima wakati tunaweza ku-simplify mjadala kwa wepesi tu, mimi sina uwezo wa kuingia kichwani mwako kujua umeelewaje nakuuliza uniambie ili nijue

Umeelewaje ile post?
 
Hiyo hoja nimemjibu huyo mwenzako ambaye imemlenga Mungu ambaye hana sifa ya ubaya, sasa wewe umeidandia juu wakati wewe una mungu wako ambaye anawaumbia watu ubaya.

Kwaiyo kwanza kabisa nataka nijue unakubaliana na mungu huyo ambaye hana sifa ya ubaya wala kuumba ubaya?

Kijana naona uoga umezidi, sijasema kama umenijibu mimi, na hujamjibu ndio maana nimetilia mkazo tena swali la msingi. Unaruka ruka tu.
 
Kama maswali yako yameonesha ulichokielewa unashindwa nini kutuambia hapa ulichokielewa ili tujenge hoja kupitia uelewa wako juu ya hilo jambo?

yani unataka tuanze kuweka mlolongo usio wa lazima wakati tunaweza ku-simplify mjadala kwa wepesi tu, mimi sina uwezo wa kuingia kichwani mwako kujua umeelewaje nakuuliza uniambie ili nijue

Umeelewaje ile post?
Maswali niliyouliza inabidi ukiri hujayaelewa mzee, kama hujayaelewa kwanini una dai umeyajibu ? Hili tatizo.

Maswali niliyo uliza yanaakisi nilichokielewa na maswali yako wazi, na nimekusaidia kuyapa namba.
 
Nakusudia Ubaya wowote ule

Vitabu ndio vimeandika hivyo kua yeye ni mungu mwenye upendo wote, na mimi nimejenga hoja kupitia refer hiyo
Hujafafanua.

Sitaki unavyokusudia wewe,nataka anavyokusudia Mungu mwenyewe ambae unamsemea sifa zake hizo kasemaje.

Kusema ubaya wowote ule hapo inaonesha unataka kuingiza mpaka mambo yako uyatie katika mabaya,kila ulitakalo utalitia katika ubaya kwa malengo yako wewe.

Ubaya unaousema ni upi kwa mujibu wa Mungu mwenyewe ?

Nataka uniambie kwa Mujibu wa huyo MUNGU ubaya ni nini na amekusudia nini kusema ubaya ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Poleni na majukumu ya hapa na pale sasa na kale yanayowafanya msilale, niende moja kwa moja kwenye mada husika.

Kama kweli maombi yanafanya kazi kwa namna ambayo tunaaminishwa, kwanini viongozi wa dini wameungana kutekeleza agizo la kuvunja mirundamano ikiwemo mijumuiko ya kiibada ili kuikwepa korona?

Kama walifanya maombi kwa lengo la kuizuia corona isiingie nchini, lakini tunaona corona imeingia, nini kinachokufanya uwaamini kua maombi ya sasa wanayojipanga kuyafanya yataitokomeza corona mazima?

Haya mambo probably si magumu ila ugumu tunauweka sisi kwa kuweka mizaha kwa kutumia kivuli cha dini.

Hivi mfano hawa madaktari wetu na sekta ya afya kiujumla wangejumuika kwenye maombi kwa kuamini kwamba maombi ni njia madhubuti ya kutatua matatizo kama haya katika kila janga la ugonjwa. Kama ambavyo watu wa dini wamekua wakituhimiza kufanya, je tungefanikisha kutibu gonjwa lipi kwa maombi?

Ngoma inaingia tanzania wabongo tulijitia wachamungu sana kua tumepewa mamlaka ya kukanyaga nyoka na n'ge hivyo ukimwi kwetu sio tishio.

Lakini tunachokiona mpaka saizi mapasta na masheikh wanachukua vidonge kwa siri sana. Lakini pamoja na hayo hatuwaoni wakijisalimisha kua wameshindwa kudhibiti ukimwi kwa maombi yao.

Mungu ambaye tunamtolea sadaka kila siku halafu katika matatizo kama haya kajichimbia tu wala hatuoni juhudi zake, huyu si mungu wakuabudiwa. Ni sawa na rafiki mnafki ambaye kwenye matanuzi mkiwa viwanja mnakua naye karibu sana halafu ikatokea siku umeishiwa anakukimbia.

Wahubiri wanahubiri huku wamevaa face mask at the same time wanasema damu ya Yesu ni tiba ya kila kitu. What a joke but I ain't laughing?

Tunaambiwa ukiwa na imani waweza kuamisha hadi milima lakini sikutegemea kuona vatican, mekka ziwe kipaumbele kukataza watu wasiende kwao kwa hofu ya korona.

Mungu muweza wa yote yuko wapi mbona kawasusia msala madaktari wetu halafu yeye amesizi tu eti mpaka aamshwe kwa maombi?

Kwanini Mungu mjuzi wa yote na muweza wa yote ahitaji maombi?

Mbona kwenye zile hadithi za gharika na sodoma na gomora huyu mungu ali-respond haraka sana kwanini asifanye hivyo kwenye janga hili linalomaliza ndugu zetu na kudhoofisha hali ya uchumi wetu?

Hivi kweli Mungu huyu yupo kweli? Maana viongozi wetu wa dini nao wanaathirika mpaka inafikia hatua italy makanisa yameshehena maiti inamaana yeye haoni?

Kwanini Mungu ahitaji maombi yetu ili aweze ku-solve matatizo yetu, ilihali anaelewa hitaji la moyo wetu hata kabla hatujasema?

====

Chukua tahadhari kwa kufuata angalizo lililotolewa na mamlaka ya afya Corona haidhibitiwi kwa maombi bali kwa kuepuka makatazo ambayo yameainishwa na shirika la afya
Watu wameasi sheria,wameibadili amri.Ndiyo sababu laana imeila hii dunia(Isaya 24:3-6).Chunguza vizuri ktk kutoka 20:3-17 uzisome amri za MUNGU,kisha uchunguze sheria ya MUNGU yenye amri kumi,ni amri ipi wanaadamu wameibadili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ona ulivyo kuwa kilaza, jifunze kusoma hoja kisha uelewe, nilikupa angalizo huko mwanzo kwamba, usihoji au kuuliza swali kabla hujaelewa, matokeo yake ndio haya.

Umesema umemsoma katika hivyo vitabu, haijalishi yupo au hayupo, nikakuuliza, umejuaje kama hayupo ?.Hili ndio swali la msingi.

Unaleta habari za spiderman naona unaishi mule mule katika mtindo dhaifu wa logic, ulianza lini kumsikia spider man ? Yeye kwa dhati yake anajidhihirishaje ?.Haya maswali watu wa logic na falsafa hamuwezi kujiuliza au kuyauliza sababu mnaishi katika fikra na uhojaji wakina Aristotle yaani mpo kwenye chumba kidogo, nje ya chumba hicho hamuwezi kufikiria.

Sasa jibu maswali niliyo kuuliza.

1. Umejuaje Mola hayupo ?
2. Kwa vipi kuwepo kwa mabaya kuthibitishe kutokuwepo kwa Mola ?
3. Lil kinachosababisha mabaya yawepo ?

Ahsante.
Hapo nilikua nakuonesha kwamba chochote kile cha kufikirika kinawezwa kuandikwa vitabuni na kujadilika lakini hakufanyi kitu hicho kuwepo.

Huo mfano wa spiderman nimeutumia kuvuruga hoja yako iliyojikita katika msingi potofu, kudhani kwamba kila kinachosomwa vitabuni lazima kiwepo.

Miongoni mwa hoja za kipumbavu kwenye uzi huu, hii pumba niliyoinukuu hapo chini kutoka kwenye post yako ndio kinara

"Sasa kama umemsoma humo kwenye hivyo vitabu, kipi kilicho kufanya ujue kwamba hayupo"

Kama unaweza kumuelezea spiderman hayupo basi jua katika hizo hizo njia ulizotumia pia zinauwezo wa kumuelezea mungu kua hayupo

Hayo maswali uliyoyauliza kuhusu mola yamemlenga mola mwenye sifa ya ubaya ambaye ulikua unamzungumzia mwanzo?
 
Watu wameasi sheria,wameibadili amri.Ndiyo sababu laana imeila hii dunia(Isaya 24:3-6).Chunguza vizuri ktk kutoka 20:3-17 uzisome amri za MUNGU,kisha uchunguze sheria ya MUNGU yenye amri kumi,ni amri ipi wanaadamu wameibadili

Sent using Jamii Forums mobile app
Thibitisha Mungu yupo
 
Back
Top Bottom