Corona Virus: Tanzania yathibitisha kuwa na mgonjwa wa kwanza, ni raia wa Tanzania, aliwasili kutoka Ubelgiji

Corona Virus: Tanzania yathibitisha kuwa na mgonjwa wa kwanza, ni raia wa Tanzania, aliwasili kutoka Ubelgiji

Vp kasha nyongwa au ..maana uyu ni mjinga katuletea kabsa
Screenshot_20200316-191243_GBInsta.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu atunusuru. Sidhani kama tuna uwezo Wa kupima na kujua hali ya mgonjwa kwa haraka. Hata Trump alipopimwa alisubiri hadi Siku mbili ndo matokeo yakatoka rasmi.

Huko Marekani gharama ya kipimo kimoja kwa mwenye BIMA ya afya ni dola 1,000. Kama huna BIMA ya afya in dola 2,500. Hapo unazungumzia zaidi ya sh 2,300,000/=

kwa mwenye BIMA na sh 5,800,000/= kwa asiyekuwa na BIMA. Hapa Bongo tutaweza?? Isije tukàishia kupima joto tu kwa wageni.
 
Sema na sisi watanzania wajuaji sana. Dalili za corona sio mtu akiipata saa nne basi saa 5 zinaonekana,sio hivyo. Wanasema mpaka siku 14. Ingekuwa kama unavyosema basi hata huu ugonjwa usingefika hata US na Europe
 
Ivi jamani ukijihisi mfano una dalili za Corona na kuchukuliwa na kuwekwa karantini inamaana mahitaji yote ya malazi unapewa na serikali ama ukitengwa kivyako vyako.......Hii hali ilivyokuwa ngumu uku mtaani nyie mnaonaje
 
Hawa c ndo wale wanaojiita wapinzani hata wakiambiwa kila raia atapewa kiwanja bure bado watapinga tu kwasababu wao wanajiita wapinzani , upumbavu katika ubora wake ndo mana sikuhiz raia wenyewe upinzani hatuuelewi unapoteza radh kwa upuuz Kama huu
wewe nawe siasa imekukaa hadi kwenye mambo ya kuogofya bure kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kilichotokea kwa mgonjwa wa kwanza kugundulika Tanzania ndio kimetokea kwa nchi zote duniani zilizopata wagonjwa wa Corona Virus.

Tatizo pale uwanja wa ndege hawapimi vipimo vingi vya kimaabara. Nadhani wana angalia joto, muonekano n.k.

Sasa dalili za nje zinazo pimika au kuonekana kirahisi zinatokea siku zaidi ya 4 tangu mtu apate maambukizi.
Zikishatokea wakaenda kupima maabara sampuli kutoka mwilini mwake ndio ugonjwa unaothibitika kirahisi.

Wakisema wapime damu na mate au mkojo au machozi kabla mgonjwa hajaruhusiwa kutoka uwanja wa ndege basi kutakuwa na vurugu kubwa na foleni kama hospital au kambiya magonjwa ya mlipuko, hata wzima watapatia maambukizi hapo hapo uwanja wa ndege.

Jambo la msingi kama tuko tayari kujitenga na dunia inabidi wasiruhusu ndege na mabasi yote ya kutoka nje ya nchi.
 
Hebu tusihamishe magoli hapa, kuna watu wanapaswa wawajibike, huyo mgonjwa aliingia na hakuwekwa karantini, kama angekaa karantini tusingekuwa tunamzungumzia leo. Watu wanafanya kazi kwa mazoea, uongozi wa airport uwajibike, waziri wa afya awajibike.

Nchi zenye tawala za kipumbavu, lazima wananchi waumie tu
 
Nadhani pia wawafuatilie wafanyakazi wote wa airports na mipakni ambao hawako kazini kwa sababu wanaumwa.nahisi wengi watakuwa wameambukizwa
 
Kumbe alipimwa kaachiwa akaamua kujiweka karantin mwenyewe? Serikali mbona mnatoa taarifa za uongo? Hamjali kabisa shenziii
 
Back
Top Bottom