Hili la Mug* aya na chanjo za corona limenikumbusha mapropesa Lypumber na sakata la kutengua barua, propesa Muongo na sakata la pesa la escrow!! Wote hao waliweka elimu mfukoni kwa maslahi ya aibu ya tumbo!! Kwa uchungu tukubali ukweli kuwa tutasubiri sana kupata maprofesa hasa wanaozingatia taaluma na kuachana na kitu kidogo!! Sina muda wa kutosha kuleta habari ya propesa Kapuyer na helkopta ya jeshi kuitumia kutembelea washkaji wake kwa gharama ya mlipa kodi wa Tanzania!, propesa Kawermbwer na mdororo wa elimu!! Hebu tuongezee orodha ya mapropesa wetu! Mug*ya huyu huyu wakati wa awamu ya 5 alisema kwenye mhadhara na wasomi wenzake kuwa chanjo huandaliwa na kuhakikiwa usalama wake kwa miaka 10 hadi 15!! Alikuwa anaziponda chanjo hizi hizi anazipigia debe leo!! Ni aibu yake itakayomfuata kwenye historia!