Nalinda heshima katika familia mkuu
Yawezekana unajibishana na malaya waliojazana humu Jf, usiumize kichwa na comments zao maana upo sahihi.
Sitaki kukuuliza kabila lako, kwa sababu makabila mengi Tz karibia yanafanana tamaduni zinazohusu ndoa.
Katika maelezo yako sijajua kama wazazi wako bado hai ama lah, pia wazazi wako kama wanaishi kwenye ndoa ama hapana.
Hakuna fedheha mbaya kama mtoto wa kike ambaye ndiye icon ya familia kuwa na akili za kijinga kuweza kulaghaiwa na wahuni na kuwaamini jumla kama anapendwa, hilo ni tatizo kubwa ambalo yeye analichukulia poa!
Mila za kwetu sisi, hata ingelitokea akadanganywa ama kutoroshwa, kosa hilo husamehewa kutokana na udhaifu wa jinsi yake ilimradi taratibu zifuatazo zitafuatwa:
Wakifika walikoamua kwenda kuishi ama kujificha, mwanaume yule lazima arudishe taarifa za where abouts zao na kisha wazazi wa mume ama mshenga huja mara moja na kuanza process za ndoa.
Asipojitokeza, ama taarifa za walipo zikichelewa, kaka zake huanza upelelezi kuwasaka popote walipo.
wakishafahamu walipo hutoa taarifa kwa baba, kisha baba huwatuma kaka zake hao wakamlete kwa fimbo za piga garagaza pamoja na huyo hawara yake.
Wakishakumrejesha nyumbani huwekwa kitimoto na wazazi.
Kama itakuwa katoroshewa karibu, kaka zake hufuata faini ya kumtorosha kabla ya mahari kuanza kupangwa na mahari ikishalipwa baraka za kuendelea na taratibu za ndoa na harusi hufanywa.
Kwa issue yako hii, kaka mtu una haki ya kughadhabika kwa sababu umeaibishwa na kaya yenu kuonekano hopeless kabisa.
Huyo bwana kama angelikuwa anampenda dada yako kweli, alitakiwa kuwa tayari alishafika nyumbani kwenu siku nyingi, mapema tu walipoanza kuishi pamoja bila ya idhini ya wazazi huko Dar.
Kitendo cha kuishi na mwanamke bila kufahamu kwao pamoja na ndugu zake ni dharau kubwa sana, pia ni upumbaf.
Jamaa anafurahia matokeo ya ushindi wa ulaghai wake kwa dada yako na kujiona kidume, lakini dunia ya Mungu hii, kuna uzima na umauti yeye hilo hajui, kuna watu wanaozeshwaga maiti na mahari kutolewa kabla ya mazishi.
Kwa hiyo tatizo likimtokea dada yako, jamaa kwa vyovyote hawajibiki kwa lolote.
Sheria za ndoa za '71 zinazotumika sasa, dada yako hana haki yoyote kwa bwana yule hata wangeishi maisha yote.
Kwa hiyo wazazi kama wapo hasa baba, washirikishe kuchukua maoni yao pamoja na hatua.
Adhabu zipo nyingi tu za kumchukulia msichana maruhuni na kichwa ngumu kama huyo zitakazofanya ajute maisha yake yote.