Dalili za mwanamke asiyekupenda kwa dhati

Dalili za mwanamke asiyekupenda kwa dhati

Kuna nakala takriban 100,000 nilizosoma zilizoelezea namna ya kumjua mwanamke anayekupenda. Na kila nayosoma nikifika mwisho inasema kwa maelezo zaidi tafuta kitabu fulani uelewe zaidi

Nimesoma vitabu vya wanafalsafa wengi na historia zao, wapo ambao walikufa katikati ya research ikiwa bado haijakamilika wakiendelea kutafuta majibu ya kumjua mwanamke

Yupo mwanafalsama mmoja alikua na hoja nzito sana ambayo ilionekana kupigiwa kura nyingi za ndio. Huyo ndo mwanafalsafa aliyesema ili mwanamke akupende unatakiwa umiliki pesa

Lakini tangu billgate na jef bozess ndoa zao ziparanguke imebidi aingie chaka tena kufanya research upya
Kumjua mwanamke ni jambo dogo sana,na kusoma kwako nakala 100,000 (Japo si kweli),jalia ingekuwa kweli basi hukujua wapi pakuchukua maalumati juu ya mwanamke.

Ukitaka kuwajua wanawake soma habari za mitume. Bali unaweza kusoma kusoma kurasa moja ukamjua mwanamke.

Mwanamke yeyote yule katika uso wa dunia na mgongo wa ardhi hii anataka haya :

1. Heshima
2. Upendo/Mapenzi
4. Uhuru
5. Matunzo

Mwanamke hapendi haya :

1. Manyanyaso
2. Dharau

Aliyesema mwanamke akupende umiliki pesa,huyo alikosea sana,wapo wanawake waume zao walikuwa watawala yaani wanaongoza dola na anaishi katika kasri na kila kitu anapata,ila furaha yake haikuwa humo wala maisha yale,akawa anayakumbuka maisha ya kwao aliko toka,na akaja kuachwa na huyo mume wake,wala hakujutia.

Kisha mwalimu wangu akasema ya kuwa "Ukiweza kumsimamia mwanamke basi utaweza kusimamia mambo mengine mengi kwa ufanisi mkubwa sana".

Kuna kisa kimoja kinaelezea mkusanyiko wa Wanawake kumi na moja,mkusanyiko huo wakawekeana masharti ya kuwa kila mmoja amuelezee mume wake kinaga ubaga. Uzuri wa kisa kile umepambika kwa lugha tamu fasaha na yenye mafumbo na uwazi wa kustaajabisha,muhusika mkuu ambaye ni mwanamke wa kumi na moja aliitwa "Ummu Zari'i". Na kisa hicho kikapewa jina lake.
 
Alafu haya matatizo ya kujikojolea mara nyingi huwakuta wanawake..huyu financial services ana mdogo wake yupo high school ndy ana Hilo tatizo Kwa mujibu wa maelezo yake..so mtafutie dawa maana yeye anambwela Tu Hadi Leo hajachukua hatua yoyote,kuna mtu kajitokeza Ampe dawa lkn Hadi Leo mwezi wa pili Hadi namkumbusha alafu anasema alisahau
Mwambie aniambie nina dawa....mficha maradhi...
 
Kwa mwanamke hakuna kitu kupenda.
Japo sisi wanaume ndiyo tunapenda sana ndiyo maana majukumu ya kuwatunza na kuwasimamia yapo kwetu,ila wanawake nao wanapenda mno. Hili liko wazi.
 
Akiwa na zote au mojawapo
akiwa na moja wapo kati ya hizo jaribu tu kumrekebisha ama ongea nae t atakuelewa na natumain atapenda ku change ila km atakuwa na zaid mybe 3 thats how its start
 
Aisee na mwanaume asiyekupenda anakuaje mkuu maana....🤔
1.HAPIGI SIMU, BALI HUTUMIA SMS
2.ANA SABABU ZA KUCHELEWA
3.ANAWASILIANA NA MPENZI WA ZAMANI
4.HAKUTAMBULISHI KWA MARAFIKI
5.HUEPUKA WATU KUWAONA PAMOJA
6.HAZUNGUMZII MIPANGO YA BAADAYE
7.HAKUNA MATENDO YA MAHABA
8.MIPANGO UNAPANGA WEWE
9.HANA MPANGO NA WATU WAKO
10.HAKUMBUKI LOLOTE LA MAANA
 
Kuna nakala takriban 100,000 nilizosoma zilizoelezea namna ya kumjua mwanamke anayekupenda. Na kila nayosoma nikifika mwisho inasema kwa maelezo zaidi tafuta kitabu fulani uelewe zaidi

Nimesoma vitabu vya wanafalsafa wengi na historia zao, wapo ambao walikufa katikati ya research ikiwa bado haijakamilika wakiendelea kutafuta majibu ya kumjua mwanamke

Yupo mwanafalsama mmoja alikua na hoja nzito sana ambayo ilionekana kupigiwa kura nyingi za ndio. Huyo ndo mwanafalsafa aliyesema ili mwanamke akupende unatakiwa umiliki pesa

Lakini tangu billgate na jef bozess ndoa zao ziparanguke imebidi aingie chaka tena kufanya research upya
pesa sabuni ya roho.....ila si kila kitu!......hii inanikumbusha wana waisraeli walipokuwa jangwani kutoka Misri kuelekea nchi ya ahadi Mwenyezi mungu aliwalisha Manna ambayo ilikuwa bora kuliko vyakula vya duniani ila watu hawa hawakutosheka au waliboreka wakata vyakula vyao dhalili vya kidunia.

hivyohivyo watu wa Saba/yemen...walipewa nchi ya neema na safari zao zilifupishwa kimiujiza na mwenyezi mungu ila waliboreka wakaomba mambo yawe tofauti ,ili mradi walikufuru.

Hivyo binadamu hana wema....hata umpe vyote, neema ikimzidi atakufuru
 
Ukiweka za mwanaume naomba unitag!
1.HAPIGI SIMU, BALI HUTUMIA SMS
2.ANA SABABU ZA KUCHELEWA
3.ANAWASILIANA NA MPENZI WA ZAMANI
4.HAKUTAMBULISHI KWA MARAFIKI
5.HUEPUKA WATU KUWAONA PAMOJA
6.HAZUNGUMZII MIPANGO YA BAADAYE
7.HAKUNA MATENDO YA MAHABA
8.MIPANGO UNAPANGA WEWE
9.HANA MPANGO NA WATU WAKO
10.HAKUMBUKI LOLOTE LA MAANA
 
ZIJUE DALILI 10 ZA MWANAUME MPITA NJIA KATIKA MAHUSIANO YENU, NAAMANISHA HATAKI NDOA NI (CHAPA TWENDE, A.K.A MUONGO)

1.HAPIGI SIMU, BALI HUTUMIA SMS
2.ANA SABABU ZA KUCHELEWA
3.ANAWASILIANA NA MPENZI WA ZAMANI
4.HAKUTAMBULISHI KWA MARAFIKI
5.HUEPUKA WATU KUWAONA PAMOJA
6.HAZUNGUMZII MIPANGO YA BAADAYE
7.HAKUNA MATENDO YA MAHABA
8.MIPANGO UNAPANGA WEWE
9.HANA MPANGO NA WATU WAKO
10.HAKUMBUKI LOLOTE LA MAANA

USIPOTEZE MUDA

Hakuna Mtu Mwenye Lengo La Kukuvunja Moyo, Lakini Ujumbe Ulio Dhahiri Ni Kwamba, Kama Unafikiria Uhusiano Wa Kudumu Na Mtu Kisha Akawa Anaonesha Ishara Zilizobainishwa Hapa, Basi Tambua Tu Kuwa Huyo Si Wako Na Atakupotezea Muda Wako Bure. Wala Usijaribu Kumlazimisha, Maana Mambo Ya Kulazimisha Huwa Hayadumu.

Ni Muhimu Sana Kuhakikisha Kuwa Mtu Unayetaka Kujenga Naye Uhusiano Wa Kudumu Anakupenda Kwa Dhati. Wala Haipendezi Kumng’ang’ania Mtu Ambaye Mapenzi Yake Kwako Ni Nusu Nusu. Hakikisha Kuwa Mtu Unayempenda Na Unayetaka Kuwa Naye Ni Yule Ambaye Amekuzimikia Na Atamani Sana Kuwa Nawe. Mtu Huyu Utampata, Hususan Kama Wewe Mwenyewe Utaweka Jitihada Za Makusudi Na Kujiweka Katika Hali Ya Kupendwa Na Kupendeka.
 
Unapokuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi mwanamke ambaye hakupendi kwa dhati basi utamgundua kwa dalili zifuatazo;

  1. Hataki kuambata na wewe katika matembezi na ikitokea anakuwa mtu wa masharti mara akuambie tangulia nakuja au pengine kutembea nawe kwa umbali.
  2. Anapata kigugumizi kukutambulisha kwa rafiki zake na ndugu na inapotokea amebanwa hafikishi ujumbe kwa kiwango timilifu.
  3. Haoneshi kubana matumizi kwa ajili ya maendeleao, kwake ni kufuja mali na anapokosa kupewa pesa ni mwepesi kulalamika na wakati mwingine kununa kabisa.
  4. Anaahilisha mara kwa mara kukutana na wewe tena bila kukueleza sababu za msingi Au kukutungia uongo wa dhahili na kuusisitiza bila kuona aibu.
  5. Anapokuwa akitoa maelezo ya mwanaume amtakaye sifa zake zinakuwa hayalingani na wewe. Anaweza kukuambia napenda kuishi na mwanaume mwenye gari au mwenye mwili mkubwa, sifa ambazo wewe huna!
  6. Hacheki kwa furaha hata kama ukimchekesha haoneshi furaha ya moyoni. Tena mara nyingine anakuwa mkimya na mshiwishi mkubwa wa kuachana kutoka kwenye matembezi yenu ya jioni. “Aaah, mi nimechoka narudi nyumbani”
  7. Anajaribu kukuunganisha na wanawake wengine na haoni vibaya anaposikia unamfukuzia mwingine badala yake anakutia moyo wa kuendelea na usaliti wako. Hana wivu kabisa.
  8. Hajuti anapokukosea, mwepesi wa kujitenga, kutokuzungumza nawe na mwingi wa kukusukumia makosa hata kama yeye ndiye aliyekukosea.
  9. Msambazaji wa habari za udhaifu wako na mtu asiyekusifia mbele za wenzake. Si balozi mwema kwa familia yake, haishi kukuponda mbele ya wazazi na ndugu zake.
  10. Mwepesi wa kupokea na si wa kutoa mmiliki wa mali zako na mkumbatiaji wa mali zake pia. Msiri wa mipango yake na mtu anayependa kujua zaidi ya kwako kuliko wewe kujua yake.
Nitarud
 
Back
Top Bottom