Daniel Chongolo wa CCM: Watu Wanataka Katiba Mpya Kwa Maslahi Binafsi

Daniel Chongolo wa CCM: Watu Wanataka Katiba Mpya Kwa Maslahi Binafsi

Hayo aliyoyasema Chongolo kama agenda muhimu ndizo wanazotumia CCM kufubaza uwezo wa wananchi kufikiri.

Chongolo atuelezee kuanzia uhuru hadi leo suala la pembejeo lipoje? CCM imetekelezaje?
 
Maslahi binafsi kama yapi? Hivi Chongolo anajua anachokiongea? Hivi unaweza ukaweka maslahi binafsi kwenye katiba?

Labda angeigeuza na kuiambia serikali yake kwamba wasipeleke miswada ya kubadili katika kwa maslahi binafsi eg viongozi kutoshitakiwa ,kuongeza malupupulu kwa viongozi ,kuleta PPP ili makampuni yao yapate tenda ,hayo ndiyo maslahi binafsi.

Chongolo alivyokuwa Iringa hajamkemea kada mwenzake akiongopea umma kwamba kadi ya CCM itakuwa inafanya kazi ya kulink huduma zaidi ya 11 kama ATM ,Kadi ya NSSF ,Bima ya Afya etc bora Lukuvi alionyesha kwa lugha ya picha ni UONGO hadi alikuwa anasikitika na kama kutaka kucheka.
 
Siyo kweli kuna vitu vinatokea unasema hapa mmmhh panaitaji marekebisho ukichek katiba inakubana.
 
Leo kwa mara ya kwanza na mimi namwagika kumpongeza comrade Chongolo kwa kauli hiyo. Nimesema sana na nitasema zaidi ,CCM ndio isimamie suala la mchakato mpya kwa maslahi mapana ya Taifa.

Kama tukiacha wakina Mbowe na wengine kututengenezea katiba wanayotaka basi miaka 2 mingi kabla hatujaanza kuziba matobo makubwa ya katiba.

Nitasema tena jambo hili na ninaishauri CCM, Profesa Kabudi awe Mwenyekiti wa bunge la Katiba ni mzalendo na mwenye uwezo mkubwa, anafaa na anaweza kutupatia katiba mpya iliyo bora sana.
UKIAMBIWA TANZANIA KUNA MAAJABU USISHANGAE. KAULI NA MAONI KAMA YA HUYU MCHANGIAJI!!!!!!!. PATHETIC
 
Peleka huko ujinga wako, kwa hiyo sisi hatujui maana ya tume huru wewe na mumeo ndiyo mnajua?
Punguza makasiriko, mnalishwa mataputapu mnashindwa kujiongeza. Nilishiriki uchaguzi mkuu wa 2020 kuanzia kwenye kuandikisha wapiga kura kwenye daftari la kudumu, kusimamia uchaguzi mkuu na kuhesabu kura na kutangazwa matokeo, nikiri kusema ni moja ya uchaguzi fair sana kila box la kura lilifunguliwa kwa uwazi, uhesabuji ulifanyika kwa uwazi na matokeo yalitangazwa kwa uwazi. Ninaposikia stori humu za tume kutokuwa huru, nashangaa sana:

Nilichobaini baada ya kila zoezi:

i. Upinzani hauna nguvu kubwa mtaani ila mitandaoni tunadanganywa.
ii. Upinzani hautumii nguvu kuelimisha na kushawishi kujiandikisha.
iii. Upinzani hawaamini kwenye kushindwa na hapa wameweka kusudi la kushinda kupita kiasi.
iv. Wanadanganyika kwenye mikutano kwa wingi wa watu lakini wengi wa wanaohudhuria mikutano ya CHADEMA ni watoto wadogo ndio maana ni rahisi kusikia mama kapotezana na watoto wake watatu
 
Daniel Chongolo Katibu Mkuu wa CCM ametoa tahadhari wa Wananchi dhidi ya Matapeli wanaojifanya kutaka Katiba Mpya kumbe ni Kwa maslahi Yao binafsi ya Kisiasa..


My Take
Naunga mkono hii hoja maana suwaoni asasi za kijamii kupigania Wananchi badala yake ni Vyama vya siasa ndio wako mbele mbele Kwa mgongo wa Wananchi ila ni maslahi Binafsi..
Kwani wao CCM wana hofu gani na tume huru. CCM ndio wanufaika wa hii katiba mbovu so hana haki ya kutusemea ndio maana wanaiba na kutufanyia kila ujinga wakiwa na uhakika wa kukaa madarakani milele.
 
Kwani wao CCM wana hofu gani na tume huru. CCM ndio wanufaika wa hii katibu mbovu so hana haki ya kutusemea ndio maana wanaiba na kutufanyia kila ujinga wakiwa na uhakika wa kukaa madarakani milele.
Hakuna mtu ana hofu ila sio busara ku rash Kwa sababu tunataka Katiba Bora ambayo ni matakwa ya Wananchi so haraka haraka Haina baraka.
 
Hata Upande wa Pili ni hivyo hivyo! Watu hawataki Katiba mpya kwa Maslahi yao binafsi! Wanawaza tukitoka madarakaniu tutakula wapi?
 
Daniel Chongolo Katibu Mkuu wa CCM ametoa tahadhari wa Wananchi dhidi ya Matapeli wanaojifanya kutaka Katiba Mpya kumbe ni Kwa maslahi Yao binafsi ya Kisiasa..


My Take
Naunga mkono hii hoja maana suwaoni asasi za kijamii kupigania Wananchi badala yake ni Vyama vya siasa ndio wako mbele mbele Kwa mgongo wa Wananchi ila ni maslahi Binafsi..
Na kuna wale ambao hawataki katiba mpya kwa maslahi yao binafsi maana wanajua katiba mpya itawaondolea madaraka
 
Maccm mnajiona kama mna hati miliki vile ya hii nchi. Hovyo kabisa.
 
Pia kuna watu hawataki katiba mpya kwa ajili ya maslahi yao binafsi.
Kumbe tatizo wanahofia madaraka?.
Amini usiamini, kabla Rais SAMIA hajamaliza utawala wake 2030, tutakuwa na katiba mpya.
 
IF WE CANT CHANGE WE CANT MOVE FOWARD, KATIBA NI MABADILIKO MUHIMU KWA TAIFA KUPIGA HATUA,
"IF YOU CANT CHANGE ON TIME THE CHANGE WILL CHANGE YOU"
 
Hata wasiotaka Katiba mpya, wanaikataa kwa maslahi yao binafsi
 
Hakuna umuhimu wa kuwa na katiba mpya ni ujanja na utapeli tuu. Hii katiba ya 1977 ndiyo nzuri na ni urithi kutoka kwa mwalimu nyerere. Katiba hii ni nzuri sana endapo tutapata raisi mwenye hekima kama nyerere.

Hawa viongozi wa sasa hivi hawana maarifa ya kutengeneza katiba ona muswada wa sheria ya usalama wa taifa. Watanzania wangekuwa na akili wangeachana na mambo ya katiba kwani. Sheria kibao sasa hivi zina kinzana kipengele cha conflicts of law.

Katiba watakayo lazimisha kuiletea watanzania hawata iunga mkono.

Hakuna kiongozi mwenye akili ya kutengeneza katiba kwa sasa hivi wala msidanganywe.
Asante nabii tito kachukue buku saba zako Lumumba
 
Back
Top Bottom