Dar es Salaam: Machinga wa Karume waandamana kuelekea ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wasema hawana imani na Viongozi. Mabomu ya machozi yarindima

Nakuunga mkono mkuu malipo ni hapa hapa duniani
 
Hivi ripoti ya uchunguzi wa kuungua kwa soko kuu la kariakoo ilishatoka?
Hizo kamati za uchunguzi na zenyewe zinapaswa zichunguzwe.
Wajinga waliwao tu hapo
 
Raha sana, malaika wa Magufuli leo wamegeuka mashetani 😃😃 kutesa kwa zamu .

Ningekuwa bilionea ningenunua hilo eneo kabisa.
 
Raha sana, malaika wa Magufuli leo wamegeuka mashetani 😃😃 kutesa kwa zamu .

Ningekuwa bilionea ningenunua hilo eneo kabisa.
Mabilionea huwa wanajielewa. Jitizame kwenye hicho kipengele kwanza kabla haujautaka huo
 
kule kaskazini mwa Afrika mmoja wenu alijiunguza kama ishara ya kupinga manyanyaso na mazingira magumu ya kufanyia kazi, na iliyobaki ni historia na yote ni kutokana na umoja wao. hapa Bongo utasota na ndugu zako tu akipigwa kirungu mmoja tu wote wanapotea, tuheshimu mamlaka lakini tujue kudai haki zetu.
 
wewe ni fisadi au??
 

Wafanyabiashara waandamana Dar​

Monday January 17 2022​

 
Uzi mzima umejaa makasiriko tu. Haya mje kula hapa break point ugali sangara kwa mboga za majani na mlenda unapata kwa 12,000 tu.

Huo muda mnaopoteza kupambana na serikali mngeutumia kutafuta suluhisho la life afterwards kuungua kwa mitaji yenu. Hapo wengine wanawapotezea muda hawana kitu chochote walichopoteza Ila uhuni tu.

Kama una mtaji wa maana huwezi kuona mtu anavurugana barabarani namna hiyo. Kaa utafakari unaanzaje upya hii ya kujivuruga mtapigwa uongeze machungu kwenye familia.

Hata mkifanya vurugu haifai. Jiulize kwa nini m ataka soko mapema hivyo?? Mmegeukana Kuna wenzenu wanataka maeneo mapema wayashike mapema .

Kuna mtu ana vizimba hata vitano alikamata hapo akavipangisha hao ndio wanaopiga kelele zaidi kuweni makini sana.
 
Wamepigwa ya machozi hapo, inawezekana wanahaki ila ujinga ni kuziba barabara na magogo na mawe.....huo ni ujinga
 
Ni kweli umefikiria hivi, waislamu wote, machinga wote dar ni ccm?
ndiyo maana yake hiyo, kama wasingekuwa ccm wangewakemea viongozi wao wanapojitmbulisha kama wawakilishi kwenye majukwaa ya siasa
 
Watachakazwa huwezi kuipelekesha serikali kizembe. Yaani kila mtu akitaka lake tu serikali ikubali? Kuna taratibu za kila jambo.
 
Wamepigwa ya machozi hapo, inawezekana wanahaki ila ujinga ni kuziba barabara na magogo na mawe.....huo ni ujinga
Safi kabisa haki hudaiwa kwa haki. Hata hivyo hilo soko ni la manispaa sio lap hata hiyo haki hawana.

Hii nchi Kuna group la watu wanahisi wao ndio was maana sana. Machinga wanajiona wao ni special group wasikilizwe kila matakwa yao.

Sijui wenye viwanda nao wagome halafu uone nani anasikilizwa?
 
We jamaa yangu wataikataa CCM waende chama kipi? Tupo sisi Ccm kibao tunataka kuhamia upinzani, tatizo upinzani haupo.

Hakuna chama cha upinzani chenye ahueni ambacho tunaweza kujiongeza kukipa nguvu kuiondoa CCM madarakani.

Mnatuonea bure wakati upinzani hauna mwelekeo wa maana na hii katiba kandamizi.
 
Mpaka hapo hao wamachinga na Watanzania hatujawajua waliochoma soko Hilo kweli na sababu zake......!

Mbona madishi yanajionesha dhahiri ukutani........!
 
We jamaa yangu wataikataa CCM waende chama kipi? Tupo sisi Ccm kibao tunataka kuhamia upinzani, tatizo upinzani haupo...
Hapo mwishoni umeeleza vizuri....."na hii katiba kandamizi"

Kudai katiba mpya haiitajiki chama cha upinzani.Sisi kama wananchi tuna wajibu wa kudai katiba mpya ili tupate vyama vya siasa vyenye nguvu.Je,sisi kama wananchi tunatimiza wajibu wetu wa kudai katiba mpya?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…