Dar es Salaam: Machinga wa Karume waandamana kuelekea ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wasema hawana imani na Viongozi. Mabomu ya machozi yarindima

Dar es Salaam: Machinga wa Karume waandamana kuelekea ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wasema hawana imani na Viongozi. Mabomu ya machozi yarindima

Tuliolia kipindi cha mwendazake sasa ni wakati wa kucheka tu.

Tunataka mamalishe, machinga, wakulima & co wateseke kabisa maana ndiyo kubwa na hao ndiyo waliompa jeuri mwendazake.

Yako wapi sasa tuliwaambia wakashupaza shingo zao, acha sasa zivunjike.
Haikuhitaji kuwa mfuasi wa chama au dini Bali ubinadamu tu unatosha kujua kiwango cha unyama waliofanyiwa na wanaoendelea kufanyiwa......

Itikadi zao au mitazamo ya kisiasa hailalishi unyama waliofanyiwa........
 
Serikali ya CCM pamoja na madhila yote wanayo wafanyia wananchi bado wameona haitoshi Sasa wameona hata ugali wao pia wautie mchanga.......

Endeleeni tu watawala wa CCM hili bomu mnalolisuka likija kulipuka litaleta maafa makubwa sana sio kwa wananchi bali hata kwenu pia........

Ukandamizaji, unyanyasaji, na uonevu dhidi ya wenye haki ndio chimbuko la ugaidi na vita vya wenyewe kwa wenyewe......hatuna haja ya kufikia huko kama badala yake lakini watawala wanawasukuma wananchi wafikie huko.......Mungu aepushie mbali.......
 
Wafanyabiashara ndogondogo maarufu machinga wa soko la Karume (Mchikichini) wameandamana hadi kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla kushinikiza kiongozi huyo atoe tamko la kuwaruhusu waendelee kufanya shughuli zao kwenye soko hilo.

Wafanyabiashara hao wameandamana leo Jumatatu Januari 17, 2022 ambapo walikuwa wanaimba "Tunataka Soko letu" wakiwa wamezingira geti la ofisi hiyo, ikiwa ni siku moja imepita tangu soko hilo kuteketea kwa moto usiku wa kuamkia jana.

Wakizungumza katika tukio hilo, baadhi ya wafanyabishara hao wamesema wanafanya hivyo baada ya kukosa imani na maamuzi yaliyochukuliwa na viongozi hao huku wakionyesha kusikitishwa kwao na kitendo cha wenzao kuvunjiwa mabanda yao waliyojenga usiku wa kuamkia leo na jeshi la polisi.

Silvanus Mwakipesile amesema Mkuu wa Mkoa aliwaahidi leo saa 2:00 asubuhi angefika kwenye soko hilo kuwaona na kuwapa muongozo lakini wanashangaa kabla ya kiongozi huyo kwenda kuna watu wamevunjiwa mabanda yao na sehemu hiyo kuwekwa chini ya ulinzi mkali ukisimamiwa na Jeshi la Polisi.

"Tumekosa imani na viongozi jana alisema anakuja lakini hadi sasa hatujamuona na chakushangaza waliojenga vibanda vyao wamebomolewa, sisi hatuwezi kuwasubiri wao maisha yetu magumu watuache tujenge wenyewe ili tuendelee kufanya kazi zetu," amesema

"Siku zilizotolewa kwa ajili ya kufanya uchunguzi ni nyingi tunataka tuachwe tujenge mabanda wakati uchunguzi ukiendelea na si kubaki hivihivi tutakula Nini na tunawatoto wanatakiwa kwenda shule,"amesema Saida Mohamed


Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Ng'wilabuzu Ludigija amewaomba wafanyabishara hao kuwa wavumilivu na kufuata utaratibu uliotangazwa na Serikali kwamba waiachie kamati ifanye kazi kwa siku saba na kutoa ripoti badala ya kuandamana kutaka kushindana na Serikali.

"Mnatakiwa kujiongeza pamoja na kwamba mnadai haki lakini lazima mfuate utaratibu Jana Waziri tuiachie Kamati ifanye kazi na walete ripoti tunaomba kuweni na subira,"amesema.

Jana baada ya soko hilo kuungua Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Amos Makalla aliwataka wafanyabiasha wa soko hilo kuwa watulivu huku akiahidi kuundwa kamati ambayo itachunguza chanzo cha moto huo kwa siku 14 akipiga marufuku shughuli zozote kuendelea wakati wa uchunguzi huo.

Muda mfupi baada ya RC Makalla kutoa tamko hilo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Innocent Bashungwa aliagiza kamati hiyo kufanya uchunguzi kwa siku saba badala ya 14.

Chanzo;- Mwananchi
Wanaandamanaje wakati mkuu wa mkoa yuko pale pale
 
Wafanyabiashara ndogondogo maarufu machinga wa soko la Karume (Mchikichini) wameandamana hadi kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla kushinikiza kiongozi huyo atoe tamko la kuwaruhusu waendelee kufanya shughuli zao kwenye soko hilo.

Wafanyabiashara hao wameandamana leo Jumatatu Januari 17, 2022 ambapo walikuwa wanaimba "Tunataka Soko letu" wakiwa wamezingira geti la ofisi hiyo, ikiwa ni siku moja imepita tangu soko hilo kuteketea kwa moto usiku wa kuamkia jana.

Wakizungumza katika tukio hilo, baadhi ya wafanyabishara hao wamesema wanafanya hivyo baada ya kukosa imani na maamuzi yaliyochukuliwa na viongozi hao huku wakionyesha kusikitishwa kwao na kitendo cha wenzao kuvunjiwa mabanda yao waliyojenga usiku wa kuamkia leo na jeshi la polisi.

Silvanus Mwakipesile amesema Mkuu wa Mkoa aliwaahidi leo saa 2:00 asubuhi angefika kwenye soko hilo kuwaona na kuwapa muongozo lakini wanashangaa kabla ya kiongozi huyo kwenda kuna watu wamevunjiwa mabanda yao na sehemu hiyo kuwekwa chini ya ulinzi mkali ukisimamiwa na Jeshi la Polisi.

"Tumekosa imani na viongozi jana alisema anakuja lakini hadi sasa hatujamuona na chakushangaza waliojenga vibanda vyao wamebomolewa, sisi hatuwezi kuwasubiri wao maisha yetu magumu watuache tujenge wenyewe ili tuendelee kufanya kazi zetu," amesema

"Siku zilizotolewa kwa ajili ya kufanya uchunguzi ni nyingi tunataka tuachwe tujenge mabanda wakati uchunguzi ukiendelea na si kubaki hivihivi tutakula Nini na tunawatoto wanatakiwa kwenda shule,"amesema Saida Mohamed


Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Ng'wilabuzu Ludigija amewaomba wafanyabishara hao kuwa wavumilivu na kufuata utaratibu uliotangazwa na Serikali kwamba waiachie kamati ifanye kazi kwa siku saba na kutoa ripoti badala ya kuandamana kutaka kushindana na Serikali.

"Mnatakiwa kujiongeza pamoja na kwamba mnadai haki lakini lazima mfuate utaratibu Jana Waziri tuiachie Kamati ifanye kazi na walete ripoti tunaomba kuweni na subira,"amesema.

Jana baada ya soko hilo kuungua Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Amos Makalla aliwataka wafanyabiasha wa soko hilo kuwa watulivu huku akiahidi kuundwa kamati ambayo itachunguza chanzo cha moto huo kwa siku 14 akipiga marufuku shughuli zozote kuendelea wakati wa uchunguzi huo.

Muda mfupi baada ya RC Makalla kutoa tamko hilo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Innocent Bashungwa aliagiza kamati hiyo kufanya uchunguzi kwa siku saba badala ya 14.

Chanzo;- Mwananchi
"Tunataka soko letu"..... hiyo ardhi ni yao?
 
Katika suala la soko kuungua hakuna kitu kinanisikitisha Kama mtu mtaji wake wote aliweka hapo kupotea ,hapo Kuna watu hawana kitu mfukoni then familia inamtegemea,Kodi, mikopo etc...Tuwaangalia watu kwa jicho la ubinadamu.. huwezi kuelewa Hadi yakukute..
Ni jambo la kawaida faida na hasara kwenye biashara.
 
Katika suala la soko kuungua hakuna kitu kinanisikitisha Kama mtu mtaji wake wote aliweka hapo kupotea ,hapo Kuna watu hawana kitu mfukoni then familia inamtegemea,Kodi, mikopo etc...Tuwaangalia watu kwa jicho la ubinadamu.. huwezi kuelewa Hadi yakukute..
Hio ndio ile moment unaweza kumtia mtu ngumi jabali ukamzimisha sababu una stress mbaya kmmmmke
 
Hakuna mmachinga mwenye ubavu wa kuandamana.
Tutamkanyaga mpaka atamtaja aliyemtuma.
Team Jiwe a.k.a Sukuma gang kwisha habari zenu
 
Wafanyabiashara ndogondogo maarufu machinga wa soko la Karume (Mchikichini) wameandamana hadi kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla kushinikiza kiongozi huyo atoe tamko la kuwaruhusu waendelee kufanya shughuli zao kwenye soko hilo.

Wafanyabiashara hao wameandamana leo Jumatatu Januari 17, 2022 ambapo walikuwa wanaimba "Tunataka Soko letu" wakiwa wamezingira geti la ofisi hiyo, ikiwa ni siku moja imepita tangu soko hilo kuteketea kwa moto usiku wa kuamkia jana.

Wakizungumza katika tukio hilo, baadhi ya wafanyabishara hao wamesema wanafanya hivyo baada ya kukosa imani na maamuzi yaliyochukuliwa na viongozi hao huku wakionyesha kusikitishwa kwao na kitendo cha wenzao kuvunjiwa mabanda yao waliyojenga usiku wa kuamkia leo na jeshi la polisi.

Silvanus Mwakipesile amesema Mkuu wa Mkoa aliwaahidi leo saa 2:00 asubuhi angefika kwenye soko hilo kuwaona na kuwapa muongozo lakini wanashangaa kabla ya kiongozi huyo kwenda kuna watu wamevunjiwa mabanda yao na sehemu hiyo kuwekwa chini ya ulinzi mkali ukisimamiwa na Jeshi la Polisi.

"Tumekosa imani na viongozi jana alisema anakuja lakini hadi sasa hatujamuona na chakushangaza waliojenga vibanda vyao wamebomolewa, sisi hatuwezi kuwasubiri wao maisha yetu magumu watuache tujenge wenyewe ili tuendelee kufanya kazi zetu," amesema

"Siku zilizotolewa kwa ajili ya kufanya uchunguzi ni nyingi tunataka tuachwe tujenge mabanda wakati uchunguzi ukiendelea na si kubaki hivihivi tutakula Nini na tunawatoto wanatakiwa kwenda shule,"amesema Saida Mohamed


Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Ng'wilabuzu Ludigija amewaomba wafanyabishara hao kuwa wavumilivu na kufuata utaratibu uliotangazwa na Serikali kwamba waiachie kamati ifanye kazi kwa siku saba na kutoa ripoti badala ya kuandamana kutaka kushindana na Serikali.

"Mnatakiwa kujiongeza pamoja na kwamba mnadai haki lakini lazima mfuate utaratibu Jana Waziri tuiachie Kamati ifanye kazi na walete ripoti tunaomba kuweni na subira,"amesema.

Jana baada ya soko hilo kuungua Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Amos Makalla aliwataka wafanyabiasha wa soko hilo kuwa watulivu huku akiahidi kuundwa kamati ambayo itachunguza chanzo cha moto huo kwa siku 14 akipiga marufuku shughuli zozote kuendelea wakati wa uchunguzi huo.

Muda mfupi baada ya RC Makalla kutoa tamko hilo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Innocent Bashungwa aliagiza kamati hiyo kufanya uchunguzi kwa siku saba badala ya 14.

Chanzo;- Mwananchi
Ccm ni chaka la maadui wa watanzania.
 
Wamachinga wa nchi hii tunapata tabu sana. Nafikiri wanataka kuweka STAND ya DALADALA pale maana mpaka sasa hivi stendi za daladala zimekuwa adimu sana.
Wacha wawafukuze ili wajue kuwa ccm ni sawa na jini mahaba wakati wa uchaguzi
 
Tuliolia kipindi cha mwendazake sasa ni wakati wa kucheka tu.

Tunataka mamalishe, machinga, wakulima & co wateseke kabisa maana ndiyo kubwa na hao ndiyo waliompa jeuri mwendazake.

Yako wapi sasa tuliwaambia wakashupaza shingo zao, acha sasa zivunjike.
Wewe endelea kuwacheka kwa kuchekeshwa na vilio vya watu uliowataja mamalishe, machinga, wakulima

Ila utambue ndo kundi la walio wengi nchi hii kama si wazazi wako ni ndugu zako pia wamo humo sasa endelea tu kuwacheka Mkuu bilionea.
 
Mwenyekiti wa machinga kuambatana na CCM, haimaanishi machinga wote Ni CCM
Mfano sheikh wa Dar muda wote yupo na CCM, hii maana yake waislamu wote wa dar Ni CCM?
Ndio maana yake hiyo kwa kuwa alikuwa anasema katumwa kuwawakilisha machinga wote
 
Hii serikali imepoteza uaminifu kwa wananchi mapema sana, serikali haina huruma kabisa, watu wameunguliwa vibanda vyao wanajenga upya bado wanawavunjia tena?!

Na huyu Mkuu wa wilaya Ilala anaendeleza tamaduni ya kijinga, wasubiri nini wakati hawajui kula yao itatoka wapi? basi wagawieni mishahara yenu na marupurupu sio hizo ahadi hewa mnazowapa. Watu wanaungua Dsm jua kali nyie mko ofisi zenye AC mnawaambia wawe na subira?

Sasa naamini kuna uwezekano mkubwa serikali ikawa inahusika na haya matukio ya moto unaounguza masoko ya nchi hii usiku tu, hawa hawawezi kujichunguza ndio maana huwa hawatoi majibu ya ripoti za tume wanazounda, hawa ni corrupt.

Nawaunga mkono machinga kwa hatua walizochukua kudai haki yao sababu zote walizotoa ni za msingi kabisa, kama makundi mengine yangekuwa na uthubutu huo, nina hakika CCM ingebaki historia nchi hii.
Machinga hawawezi kuiondoa ccm maana ndiyo chama chao.

Hao hao walitumika na ccm chini ya mwenyekiti wao kuwatukana viongozi wa upinzani na wapinzani kwa ujumla wao.

Mungu huwa analipa hapa hapa duniani na ukisha kufa ni mahesabu tu.
 
Back
Top Bottom